Uwanja wa Ndege Dar: Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu - Julai 27, 2020
Hao ni kama kuni na vidole mkuu. Vidole vinasogeza/vinasukuma kuni kuingia kwenye mafiga/jiko ili kuni ziteketee lakini kamwe vidole havigusi moto.

Hawa nao wanachochea wenzao waingie kwenye matatizo wao wakiwa kwenye masofa wanachezea cm.
Yani kwenda kumpokea mpendwa wako unaingiaje!? Kwenye matatizo
 
Mkung'utwe kwa kosa gani? Lisu sio gaidi bali ni mwanasiasa anayerejea nchini baada ya matibabu. Hao mnaowatuma kupiga raia wema kwanini hamjawatuma kuwakamata na kuwapeleka mahakamani watoa rushwa wa ccm kwenye kura za maoni? Au hao polisi ni robots wa kupokea maelezo ya wanasiasa wa ccm, kuwapiga wafuasi wa Cdm bila kosa, lakini wakifumbia macho watoa rushwa wa ccm?
Nyie si ndiyo mliyokuwa mking'ang'ania lock down!! Au covid19 imeisha!!

Polisi wamezuia hiyo mikusanyiko isiyo na kibali. Mkikusanyika ni kutotii amri ya polisi hivyo kipigo cha mbwa mwizi ni halali yenu
 
Nasie tunajiandaa hapa na zana zetu..kila mtu anapata maelekezo lakin mioyoni mwetu hatuna ugomvi nae
Safari hii nani anataka kuwatuma kuja KUDHULUMU Raia wema haki zao za kuishi? Kule Pemba "Marehemu" alihusika kwa 100%, na kwa kweli leo hii Wapemba wote WANASHEREHEKEA kufuatia kifo cha ghafla cha MFITINI WAO huyo.
 
Asante sana mkuu, mimi ndio najongea hapo nikitokea Kibaha, InshaAllah kwa uwezo wa Mwenyezimungu tutampokea salama Jemedali wetu. Kibaha-Mbezi Mwisho-Kinyerezi-Segerea naibukia hapo AIRPORT.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787] kuna wabongo hamna cha kufanya hapa nchini,mnamaliza hewa tu ndo maana wakati mwingine hewa inakua nzito

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Tuna mkaribisha kiongozi wetu mbeba maono mh Lissu, tupo hapa kibaha kutokea Kakonko ili tumpokee kiongozi wetu mpendwa.
Salaam Wakuu,

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tanzania Bara Tundu Lissu anatarajiwa kuwasili nchini leo saa saba na dakika ishirini saa za afrika Mashariki.

Lissu amekaa nje ya nchi miaka mitatu sasa baada ya kuondoka kwa shambulio la risasi lililotokea mjini Dodoma ,Septemba 7, mwaka 2017, saa 7 mchana, Area ‘D’, kwenye nyumba ya makazi ya viongozi wa Serikali mjini Dodoma.

“Lissu kwa sasa anatimiza mwaka wa tatu na anarejea hapa nchini baada ya kupona kikamilifu. Watanzania na wanachama wa Chadema wanakutana hapa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), kwa lengo la kumpokea makamu mwenyekiti wa chama chao Lissu.

Hivyo timu nzima tupo hapa kukuletea kile kitakachojiri kwenye mapokezi haya.

Stay tuned.

======

UPDATES;

1105HRS: Hapa uwanjani pametulia, hakuna fujo wala dalili za fujo, Wanachama wachache wa CHADEMA wanaonekana wakipita pita huku na kule. Bado sijabahatika kuona gari la Polisi Wala Gari la CHADEMA.
View attachment 1518228
View attachment 1518224View attachment 1518225View attachment 1518226
Ratiba inaonesha muda wa ndege kufika ni saa saba na dakika Ishirini. Angalia kwenye chati
View attachment 1518258
1121hrs: Saa moja iliyoisha Tundu Lissu ndo amepanda ndege ya Ethiopian Airlines ET 805 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Bole Addis Ababa kuja hapa Dar Julius Kambarage Nyerere International Airport.

Safari inatazamiwa kuchukua masaa yasiyozidi Matatu kufika hapa tulipo.
View attachment 1518257
1140hrs: Mwenyekiti Mkoa wa Iringa CHADEMA William Mungai, aliyekuwa Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi(Sugu) Wakiwa Wamefika hapa Uwanja wa ndege kumpokea Lissu
View attachment 1518269
1156HRS: Kutoka kushoto: Hekima Mwasipu, Wakili wa Chadema, Sugu, Catherine Ruge Viti Maalum Mara na Mgombea wa Jimbo la Segerea CHADEMA
 
Naona tumefuatana sisi ndio tupo hapa picha ya ndege kibaha
Asante sana mkuu, mimi ndio najongea hapo nikitokea Kibaha, InshaAllah kwa uwezo wa Mwenyezimungu tutampokea salama Jemedali wetu. Kibaha-Mbezi Mwisho-Kinyerezi-Segerea naibukia hapo AIRPORT.
 
Back
Top Bottom