Wanajeshi kwa waliohusika na tukio hili wawajibishwe
Hata kama kuna evidence kuwa picha uliyopiga ina element za jinai?
Ndo sababu katiba mpya ni muhimu sana kuna vitu vikewekwa ili ukihoji ujikute upo matatizoni , just kwa ajili ya nterst za viongozi.
Kuna mbunge aliwahi kuhoji inakuwaje mikataba mingi mibovu ya serikali ilikuwa na muhuri wa 'confidential'
Hiyo Katiba mpya sijui itakuwa na page ngapi maana kama mpaka mambo ya kupiga picha itakuwa humo!!
 
Huvunjiki popote yani, kuepuka un-neccessary fights ni hekima ambayo tumejaaliwa watu wachache mno.

Tunawajua jamaa ni wapenda sifa na katika mizania tu dogo yupo katika risk kubwa kuliko alivyokuwa anadhania. Yani hapo angeweza kufanywa jambo baya tu style ya Akwelina ile sababu ya kuvimba tu kusiko na maana. Nobody cares this time around.
Mi askari yoyote huwa simletei ubishi, najifanya mkosaji namuomba msamaha maisha yanasonga, hawa jamaa wa inferior complex....ile mizoezi yao afu mishahara kidogo wanaweza kutolea wewe hasira
 
Kichekesho. Ndiyo maana "ujui" ni msamiati rasmi kwako.

Ulibahatika kufika hata shule ya kata kweli mjomba?

Kwamba hata majeshi ya polisi, magereza, zimamoto, na binamu zao ndiyo unasikia leo?
Hakuna polisi anajiita mjeshi mjomba. Japo wanatamani kuwa wanajehi, pili wanajeshi, hizo ni porojo tu za kisiasa. Wanajeshi wote wapo kwenye wizara ya ulinzi. Hakuna nchi ambayo ina wizara zaidi ya moja yenye majeshi duniani kote.
 
Wewe umejuaje hizo ni ofisi na premises za Usalama wa Taifa?
Kuna kibao, bango, alama au maneno gani yanayopatambulisha hapo kama eneo la Usalama wa Taifa?
Majengo yao tunayajua kupitia watoto wao
 
Kweli kiswahili kigumu, ulishasema Mgambo Mimi nikuambie kuwa kuwa Mgambo ni Mwanajeshi tena?

Kwa taarifa yako kwa vile ujui kama ujui leo sasa nakufahamisha kuwa Kuna wanajeshi, Kuna polisi, Kuna TISS, Kuna magereza, zimamoto, uhamiaji, wanyama pori na wengine.

Hacha kubabaishwa na maneno ya kisiasa hayo., Wote hao wakisimama pamoja akatokea mtu akasema wanajeshi wasimame kulia, hakuna polisi wala TISS atakaechomoa pua yake kwenda kulia. Wewe kama polisi utabaki kuwa polisi tu.
Aisee Achikoyo safi sana umempa za uso, mimi hivyo hivyo kuna muda tulizinguana akitaka kulazimisha kwamba mgambo, Polisi, Magereza na vyombo vingine kwamba wote ni Wanajeshi. Haiwezi kuwa hivyo hata siku moja Mwanajeshi atabaki kuwa Mwanajeshi, Mgambo kama Mgambo vivyo hivyo na wengine.
 
Najua hawapendi nzi.....
Najua hawawezi shoot yeye sio muhalifu.
Ni bora usababishe jam, ila sio uingie Ndani kwao.
Japo inaonekana Huyu Dogo ( nahisi ni kijana mdogo) alikuwa na makosa.....
Na ana kiburi chake binafsi cha hadi ya familia aliyotoka.
Hakuwa na makosa! SI amesema Hapo kabisa Jamaa kamchomekea kwenye Traffic light!
Ndio maana wakataka kuchukua simu yake! Wanajijua wametokota...!
 
Hakuna polisi anajiita mjeshi mjomba. Japo wanatamani kuwa wanajehi, pili wanajeshi, hizo ni porojo tu za kisiasa. Wanajeshi wote wapo kwenye wizara ya ulinzi. Hakuna nchi ambayo ina wizara zaidi ya moja yenye majeshi duniani kote.

Kutokujua kwako maana ya neno "jeshi" should that be our problem?

Pole lakini. Neno "jeshi" ni kiswahili. Google au tafuta kamusi.
 
Kutokujua kwako maana ya neno "jeshi" should that be our problem?

Pole lakini. Neno "jeshi" ni kiswahili. Google au tafuta kamusi.
Bora warudishe JKT na mgambo ndio Watanzania wataelewa maana ya Jeshi, wengi wanadharau mgambo Polisi,TISS, Magereza, wakati ndio kikosi cha Askari wa miguu (infantryman)
 
Wapuuzi saaanaaa
Kuna miaka fulani ya nyuma kipindi natumia sana kinywaji tupo bar fulani hapo dar hao maraia yalikuwa 6 yalitaka kuleta mzozo sisi tulikua 2 tuliyadhibiti sana ila uharibifu ulitokea kidogo kwenye ile bar
 
Unaambiwa ingiza gari na wewe unaingiza gari unaakili wewe.
 
Kuna nidhamu ya maisha! Jambo dogo unaweza kulizungumza kistaarabu likaisha. Huyu anayelalamika ukimsikiliza unaona mwenyewe si mstaarabu. Maneno mengi, sauti ya juu mara uncle wake mbunge! Hivi angemwambia tu yule bro tusameheane ni mambo ya barabarani angepoteza nini? Na huyo bro wala hakutoa kitisho chochote kuhusiana na kazi yake #knowledge brings wisdom.🙏🙏🙏
 
Dogo kakubali kuingia kibra mwenyewe, angebaki njia kuu bora jam, au aunge moja kwa moja hawawezi mpiga risasi. Yaani Mimi unitoe main road uniforce niiingie mwenyewe getini aisee.
 
Back
Top Bottom