Tunashukuru zoezi zima leo limewadia mbali na mawaa yanayoendelea kila mmoja kati ya vyama maarufu CCM na CDM kila mmoja akivutia kwake kuwa ataibuka kidedea.

Lakini mimi kama mfuasi/ mpenzi wa sera ya UHURU, HAKI NA MAENDELEO YA WATU nimejikuta natumia gharama kidogo kuhakikisha kura yangu inakua kama tone moja kati ya mamilioni ya matone ya mvua yanaweza kuleta madhara.

Mimi imenigharimu shilingi elfu tano kutoka sehem nayoishi sasa hadi sehemu niliyojiandikishia.

Imani yangu LISSU ni raisi mtarajiwa wa awamu ya sita.

Embu na wewe uliechangia kura kwa lissu tiririka gharama ulizotumia kumpa kura.
 
Lugha ngumu hii
 
CCM sasa ni dhahiri imechokwa na kila mtanzania wakiwemo wanaccm wenyewe.

Wapoga kura wa ccm wamemtupa mgombea urais wao na kuamua kutafuta Uhuru, Haki na Maendeleo.

 
Duh havijaisha, vipo sehemu kwaajili ya kazi ya kujazia.

Sent from my FIG-LX2 using JamiiForums mobile app
 
Na bila shaka utakuwa na kumbukumbu ya watu hao "makatili wanaoshabikia magufuli"; utawasahauje watu ka a Bashite, au hata Jingalao, na "wenye njaa"!
Hiyo ndiyo maana yangu.
 
Majizi yanasema yanakubalika halafu yana kura zilizopigwa tayari na wapigaji hawajulikani
Nafikili hapa ndo mchezo unaenda kuwa mgum,maana huu ni ushaidi tosha kwamba zipo Kura za wizi, NEC tokeni hadhalani mjibu, Nini kinatokea mpaka watu wanakamata Kura ambazo tiyari zimepigwa.

Na je Kuna umuhim gani wa kuendelea na uchaguzi huu? Nani atawaelewa mpaka mda huu kuanzia dunia ,SIONI UCHAGUZI HAPA ,ILI USITULETEHE FUJO UFUTEN TU, Rais aliyepo aendelee tukajipange upya
 
Sijalemba yani sijahangaika kusoma Kwingine
Nimemuona Jiwe nika tia Tick ya Maana sana Nadhani NEC wataniita Kuwa mtia tick bora Tanzania bara

Sahivi kuna Maandalizi ya Tafrija Fupi ya kupokea ushindi wa JPM
Hiyo haiwezi kukosa ndio cha maana
 
Kila mtu anaenda kupiga kura kwa mudawake, weukiondoka wengine wanakuja nahutajua sasaivi wapo wangapi kituoni.
Na vituo vingi vina sehemu zaidi ya mbili za kukagua vitambulisho majina na mwisho unapigakura na kuondoka zako.

Sasa kwenye hizo dakia 3 unazotolea mfano kama kwenye kituo nilicho pigia mimi unaongelea watu 9 wanakuwa wamesha piga kura na kuondoka zao.

Hapo sasa foleni itaanzaje.

Alafu kusema watu wamesusa eti kupiga kura niutoto, huko nikutokujielewa kwao.

Hata ivyo, usipo chagua mtu wa kukuongoza watu wengine watakuchagulia kiongozi na huna sababu ya kulalamika mbele ya safari.
 
Watanzania tutekeleze haki na wajibu wetu wa msingi kwa kupiga kura na kuipa nafasi Tume ya uchaguzi kuchakata na kutangaza matokeo kulingana na ratiba iliyowekwa. Mmi nishatekeleza wajibu wangu na sasa nipo nyumbani nikifuatilia mchakato mzima katika maeneo mengine ya Nchi kupitia luninga.

Kwa Ujumla mchakato unakwenda vizuri sana na naamini utaisha kwa amani na usalama hadi itakapofika saa 10 jioni. Kwangu naamini mchakato wa kidemokrasia na nimeshashiriki kutekeleza wajibu wangu. Kiongozi atakayeshinda na kutangazwa na Tume ya Uchaguzi ndiye niliyemchagua na ndiye atakayekuwa kiongozi wangu kwa ngazi husika. #Tanzania kwanza!!! God be with us.

 
Kiuhalisia hali imekua tofauti na mwaka 2015 hasa katika jiji la Dar es salaam , nakumbuka mwaka 2015 nilenda kituoni nikakuta misururu mirefu ya watu wakiwa kwenye foleni zaidi ya moja wakisubiri kupiga kura.

Yaani leo nimeenda kituoni kwangu ambapo ndipo hapo hapo nilipopigia kura 2015 yaani hakuna watu kabisa nimefika na kupiga kura na kuondoka na hakuna hata MTU yeyote aliyekua ananifuata nyuma yaani wasimamizi na mawakala wanapiga story tu hiyo naongelea kituoni kwangu, baada ya kupiga kura niakenda zangu kariakoo nikakuta hali ni ile ile vituoni hakuna watu kabisa, sijui ndio watu wamekata tamaa na kupiga kura kabisa.

Sasa sijajua Kama na mikoani hali ni hii hii au vip huko mlipo hali ipoje .
 
Ungekuwa na akili timamu usingemchagua huyu fedhuli atuongoze mamilioni ya Watanzania.
Haijalishi uko katika level gani ya maisha
Mkuu sio sawa kimtoa mtu akili wakati anapo tumia hakiyake ya kuchagua kiongozi anae mtaka, situnasemaga haki huinua taifa ama nihakigani inayo zungumzwa.
 
Leo nilipoingia kupiga kura nimekutana na makarani ambao walikuwa wakinakili namba za KITAMBULISHO CHANGU CHA MPIGA KURA kwenye Karatasi ya kupigia kura.

Hizi taarifa zikiingizwa kwenye system basi itakuwa ni shughuli nyepesi kujua mimi nimepigia kura chama gani.

Sasa endapo zitaanza itikadi mfano, kazi wapewe wa vyama fulani tu au mikopo wapewe watu fulani tu basi hii itachochea sana mpasuko mpya,
 

Uchaguzi wa 2015 idadi ya wapiga kura ilikuwa ndogo kuliko hii, na vituo vingi pia, lakini mpaka kufika mchana hivi mistari ilikuwa mingi. Siongei hili kwa kubahatisha. Watu wameacha kupiga kura maana wamechoka kugeuzwa mandondocha.

Na kwa taarifa yako kupiga kura ni njia ya kistaarabu kupita viongozi wenye uhalali wa wengi. Unapooanza kuwa na viongozi wanaoingia bila ridhaa ya wengi kwa sababu ya hujuma sio sifa. Hujaonekana hujui madhara ya kuwa na viongozi wasio na uhalali wa umma.
 

Hali ni hiyo hiyo nchi nzima, watu hawajakata tamaa, pale wamepuuza huo utoto uitwao uchaguzi ulioanza baada ya hii awamu ya 5 gani kuingia madarakani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…