Uchaguzi 2020 Yaliyojiri upigaji kura za maoni za wagombea wa Ubunge na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia CCM - Julai 20-21, 2020
Uchaguzi huru ndani ya chama

Breaking News !


Dr. Faustine Engelbert Ndugulile ashinda kura za maoni za ndani ya chama cha CCM jimbo la Kigamboni jijini Dar es Sakaam.

Kura za maoni za wajumbe halali zilikuwa 399 hakuna kura iliyoharibika na Dr. Faustine Engelbert Ndugulile amefanikiwa kupata kura 190 za wajumbe hao wa mkutano wa wilaya ya Kigamboni..

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kutumbuliwa kwa kilichoitwa 'tamaa' isiyokubalika ndani ya CCM Mpya Bw. Paul Christian Makonda amepata kura 122.
 
Magufuli hawezi kumtosa Makonda, kuhusu tofauti ya kura ni kubwa sana, hata kama ingekuwa moja, Ndugulile anastahili kupewa hiyo nafasi.

Ila nikikumbuka Magufuli alivyomponda Ndugulile wakati akimtumbua u Naibu Waziri wa Afya, kuwa hospitali zake hazina dawa pamoja na cheo chake, bora Ndugulile asubiri tu kupewa cheo kingine.
 
20200721_020439.jpg
20200721_020439.jpg
 
Ukitathimni matokeo ya uchaguzi wa jimbo la kigamboni ,Nzega mjini,Mtama utaona wakongwe waliotetea majimbo yao , Bashe na Nape Nauye wamewaacha mbali sana wapinzani wao ,mfano Nape anakura Mia nne na ushee anayemfatia Ana kura miambili na Bashe kapiga kura miatatu na ushee, anaemfatia ana kura kumi na mbili .

Kwa kigamboni Ndugulile alitakiwa amuaache mbali sana Makonda ,kwa sababu ni mbunge jimbo hilo kwa miaka 10,halafu anatofautiana na mgeni kwa kura 68, hii si nzuri kwake. Kama ilivyoada kwa ccm kuongoza kura za maoni sio tiketi ya jina kurudi.


Safari ndio imeanza kuhusu hili jimbo la kigamboni,wagombea wakapitishwe kwenye kamati ya wilaya ya siasa ,kamati ya mkoa ya siasa kisha yapelekwe Dodoma kwa wazee cardinal rule ndio jina lirudi. Wale mnaompinga Makonda msishangilie kwa sasa, baadae msije kujikuta mnasonya

Hivi akili huwa mnakodisha au zenu?
 
Ndugulile to hell with him huyu vita ya corona alitaka watanzania tufe hata angepata kura zote mimi ningempinga anaamini dawa za kizungu alimpinga hadi Magufu;i tusijifukizie wakati anajua hakuna tiba ya CORONA KAMATI ZA UTEUZI MPENI YEYOTE sio Ndugulile mimi napinga wazi nikiwa CCM damu I SAY NDUGULILE NO NO NO NO kAMANDA MZURI HUONEKANA KWENYE VITA MAGUFULI KAPIGANA VITA nzuri ya corona sio ndugulile .hwezi zawadia ubunge mtu aliyeshindwa kupigana vita nampinga .Na CCM wa take note kuwa mimi nikiwa mmojawapo wa mpambanaji huria wa mitandaoni wa kujitolea mitandaoni wa CCM SIMTAKI NDUGULILE
 
Back
Top Bottom