Si washalipwa tayari, wakale hizo kwanza hadi ziishe kwanza tamaa ya nini? Kula ni kwa zamu ukishashiba unakaa pembeni na wenzio wapige tonge eeee..
Kama alivyofanya Mnyika!

Mbowe amekomaa!
 
Ilikuwa ni mwaka 2005. The same year Frederick Mwakalebelea alikatwa, akapewa Monica Mbega Iringa mjini. Nape alikatwa akapewa Hawa Ng'humbi Ubungo
Hawa Ng'umbi alimshinda Nape vibaya sana kwenye kura za maoni. Na ilikua 2010 si 2005!!

Mwakalebela alimshinda Monica Mbega 2010 Iringa
 
Richar Paul maarufu Marcas ameomba Ridhaa ya kuwa Mbunge wa jimbo la Arusha mjini kutokana na utendaji kazi alioufanya katika jamii

Alisema alishawahi kufanya mambo malimbali ikiwemo uanzilishi wa kukusanya mapato ya maegesho ya nagari (parking )Mkoa wa Arusha mbali na kazi hiyo pia kazi ingine aliyoifanya ni pamoja na kushauri Twiga bank kuwa bank ya posta Mara baada ya kuona bank hiyo kuwa na matawi manne na kukusanya Madeni na baadae kuwa moja ya bank kubwa nchini

Pia alisema ni mkusanyaji wamadeni sugu mamlaka ya usimamizi wa bandari zote Tanzania pamoja na mdai ya madeni sugu ya wanafunzi wa chuo cha bandari

Alisema endapo hata chaguliwa kuwa Mbunge wa Arusha hatasaidia wakina mama wanao panga bithaa bara barani eneo la frence cona wanapata maeneo ya kufanyia biashara zao mahali salama zaidi

Katika Sera yake amehaidi ataongea na watu wa national housing pamoja na viongozi wa chama na serikali hili kupata jengo katikati ya mji hili aweze kujenga city market

Amewaomba wajumbe kumpa ridhaa kwani jimbo la Arusha linaitaji MTU mwenye maono kama ya kwakwe aweze kusaidiana na Mh John Pombe Magufuli kuendeleza Tanzania ya uchumi wa kati
 
Hapo hapo Ujiji inaonekana 2005 Peter Serukamba(mkristo) alimuangusha Dr Warid (Muislamu) , vile vile 2010 huyu huyu Peter Serukamba Mkristo alimuangusha tena Ally Khalfan(Muislamu), vip wakati huo wazee wa Ujiji waislamu walikuwa wapi ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…