Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,559
- 19,101
Utaratibu wa ulivyo ni kwamba kura za maoni za leo ni mwanzo na wala sio mwisho wa mchakato. Hayakatwi majina, hayachujwi majina bali baada ya wagombea wote kupigiwa kura na wajumbe, Kamati ya Siasa ya Wilaya inapeleka matokeo na mapendekezo yao (rating and ranking) kutegemea nidhamu, uzalendo kwa nchi, utii kwa Chama na Serikali, kiwango cha elimu na uzowefu na usafi wa maadili kwa vikao vya juu kwa maamuzi ya mwisho
Jina moja linapitishwa kutokea juu na wengine wote waliogombea watalazimika kumuunga mkono mteule wa CC tena bila kinyongo wala fikra za kumuhujumu kwani adhabu yake ni kufukuzwa uanachama!
Maelezo yangu ni ya jumla, yamezingatia taratibu za kwenye kanuni za Chama na miongozo kuhusu chaguzi za teuzi, sina taarifa za ndani kama Mzee Gentamycine mwenyewe
Jina moja linapitishwa kutokea juu na wengine wote waliogombea watalazimika kumuunga mkono mteule wa CC tena bila kinyongo wala fikra za kumuhujumu kwani adhabu yake ni kufukuzwa uanachama!
Maelezo yangu ni ya jumla, yamezingatia taratibu za kwenye kanuni za Chama na miongozo kuhusu chaguzi za teuzi, sina taarifa za ndani kama Mzee Gentamycine mwenyewe