Uchaguzi 2020 Yaliyojiri upigaji kura za maoni za wagombea wa Ubunge na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia CCM - Julai 20-21, 2020
Mambo sasa hadharani. Siyo rocket science wala brain surgery. Ni hesabu rahisi tu za logic.

Ni hivi...

Kwa siasa za ndani na nje ya CCM, Makonda ni taswira ya JPM.

Huko Kigamboni, Makonda kaambulia 34.76% ya kura.
Hiyo ndiyo opinion ya wana CCM wa Kigamboni dhidi ya Makonda (mirroring JPM).

Hapana shaka kuwa huo ndiyo pia mtizamo miongoni mwa wana CCM walio wengi, wakiwamo wajumbe wa mkutano mkuu wao uliofanyika hivi karibuni kule Dodoma.... kwamba ndani ya mioyo ya wana CCM, JPM atakuwa anakubalika kwa 34.76% tu na siyo ile 100% ya maigizo.

Jee, ni nini tafsiri ya yote haya kuelekea uchaguzi mkuu October 2020?
Jibu ni rahisi.... kwamba kama uchaguzi mkuu ungekuwa unafanyika katika mazingira huru na haki, JPM asingeweza kuambulia hata 30% ya kura za Watanzania.

Makonda amekuwa ni barometer kuelekea October 2020.

Ni logic rahisi tu.
Hoja yako imekaa kihisia siyo kiuhalisia.
 
Makonda hakufanya reseach vizuri. angeweza kugombea Kibamba au Ukonga ambako kulikuwa na nafasi kubwa zaidi ya kushinda kuliko kwenda kupimana ubavu na Mbunge anayemaliza muda wake huku akiwa bado anakubalika na wana ccm wenzake.

Halafu, alichokifanya siyo afya kwa chama.

Kama Shuleni tu alikuwa hana Akili na hapo hapo tena Cheti alifoji, hivi hiyo Akili ya Kufanya ' Research ' ulitegemea iwemo ' Ubongoni ' mwake?
 
Jerry Slaa Usoni na katika Meno yake akitabasamu muda wote alikuwa ni mwana CCM, ila Moyoni hadi Rohoni kabisa alikuwa ni CHADEMA tupu!
Hapana. Alikuwa team Lowassa kabisa akiwa CCM. Yaani mtiifu. Hivyo ni kati ya wale aliyo na kinyongo nao. Jerry hajawahi kuwaza hata kuhamiachadema sema alijiingia Siasa za utimu au makundi ya wana CCM hatari
 
Kwa mara kwanza Nchini tunashuhudia uwazi nchini ya Mwenyekiti Taifa CCM Dr John Pombe Magufuli kwa jinsi Uchaguzi wa kura za maoni ndani ya CCM ulivyokuwa huru na uwazi tofauti na zamani



Kwa mara kwanza ile dhana Kwamba mwenye pesa ndo anapewa chapuo imeanza kukosa mashiko baada ya Takukuru kupewa Meno hasa kupitia mchakato ndani ya Chama chake


Kingine upigaji kuwa tumeshuhudia ukiwa ni wa Uwazi na karibu wagombea wote wameridhika na mchakato mzima wa kupiga kura na hili limeepusha mgogoro kwa wagombea wote


Kwa hili tunampongeza Mwenyekiti wa Chama Taifa Dr John Pombe Magufuli,Katibu Mkuu Dr Bashiru Ally pamoja Secretariet nzima kwa kazi nzuri kupitia mchakato huu wa kutafuta wagombea ndani ya Chama Mapinduzi


Natumai hata Uchaguzi wa mwezi kumi utaenda kuwa huru na wa haki kwa ustawi wa Taifa letu

Mungu Ibariki Tanzania

Alex Fredrick
Dar es salaam
afredrick59@gmail.com











FB_IMG_1595241614322.jpeg
 
20 Julai 2020
Mbeya, Tanzania

Dkt. Tulia Aongoza kwa 96% Kura za Maoni Mbeya Mjini
Kivumbi kuchanika nguo ndani ya ukumbe, wajumbe 885 wa CCM mkutano mkuu wa wilaya wapagawa na matumaini...


Dr. Tulia akiwa amekumbatia karatasi za kura 843 huku akitoa machozi, zilizomchagua ktk kura za maoni akimuwaza mgombea wa CHADEMA oktoba 2020

Source: MbeysYetuOnlineTV


Anatoa / Anatokwa Machozi ya nini sasa wakati inajulikana wazi wazi kuwa Kura hizo ni za Maagizo Maalum na kutoka Kwake Mtu Maalum nchini?
 
Kinje(Kilwa) ni vipi au kesho?
Munduli kwa familia ya Lowassa ni vipi?
 
Sijui Nani aliyemshauri kwenda huko wakati Jimbo la Kibamba lilikuwa wazi,
Kibamba kwa Mako ilikuwa haina dili....
sema ule upandet wa pili wa bahari jamaa alikuwa na maproject kinoma
 
Back
Top Bottom