Kuna watu hawatakubali ila Magufuli kaleta mwamko mkubwa sana wa kisiasa ndani ya CCM. Yaani wana CCM wamechangamka sana.
Sema unatania!! Kafanya lipi huko CCM la kuleta huo mwamko?! Let me assume ningekuwa ndo Steve Nyerere kwa mfano:-
Siku ya kwanza nasikiliza Bunge namsikia Kibajaji anaongea... kila nikipima, naona "kama ubunge ndo vile mbona hata mimi naweza!!"
Siku ya pili, mara namsikia Lijuakali anaongea... na kila hatua anayoongea ni full kupigiwa makofi hadi na spika; lakini Steve kila nikimsikiliza Lijuakali, naona kabisa hata mimi kama kuchangia kwenyewe bungeni ndo vile, hata nami naweza kabisa!!
Steve Nyerere siku nyingine nimepotelea YouTube, nakuta mtu mzima, kashiba na kajazia hasa, anaanza kukata maono hadharani, halafu naambiwa yule nae ni mbunge na waziri!!
Hujakaa vizuri siku nyingine unamsikia Spika mwenyewe akitoa "speech" huku akimchana Mbowe live, na makofi anapigiwa kama yote!! Steve Nyerere mimi, kila nikimsikiliza Spika, naona hata ningeamshwa usingizini nikiwa bwax, kuongea kwenyewe ndo kama kwa Ndugai, nami naweza kabisa!!
Kwa staili hiyo nani ataogopa kuchukua fomu?!
Alertnatively, assume sasa pale bungeni kungekuwa na wajenga hoja kama Zito, Lissu na wengine hata kutoka CCM lakini wanaweka siasa kando!
Trust me, majority wangejua kabisa kwamba "the building is too big for me!" lakini kwavile bunge limeshuka hadhi, kila mmoja anaamini "kama mambo yenyewe ndo yale, hata mimi naweza!"