Uchaguzi 2020 Yaliyojiri upigaji kura za maoni za wagombea wa Ubunge na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia CCM - Julai 20-21, 2020
HABARI: Cosato Chumi ameshinda kura za maoni kuwania ubunge Mafinga Mjini kwa tiketi ya CCM baada ya kupata kura 135 kati ya 293-MCL
Jul 20 4:14pm
HABARI: Abbas Tarimba ameshinda kura ya maoni CCM kuwania Ubunge wa Kinondoni baada ya kupata kura 171 akifuatiwa na Idd Azan aliyepata kura 77. kura zilizopigwa zilikuwa 403-MCL
Jul 20 5:30pm
HABARI: Enock Koola ameshinda kura ya maoni CCM kuwania Ubunge wa Vunjo baada ya kupata kura 187 akifuatiwa na Charles Kimei aliyepata kura 178. kura zilizopigwa zilikuwa 567-MCL
Jul 20 5:40pm
HABARI: Mussa Azan Zungu ameshinda kura ya maoni CCM kuwania Ubunge wa Ilala baada ya kupata kura 148 akifuatiwa na Sophia Mjema aliyepata kura 103. kura zilizopigwa zilikuwa 278-MCL
Jul 20 5:46pm
HABARI: AbdulAziz Abood ameshinda kura ya maoni CCM kuwania Ubunge wa Morogoro Mjini baada ya kupata kura 524 akifuatiwa na Merkiory Manset aliyepata kura 17. kura zilizopigwa zilikuwa 638-MCL
Jul 20 5:51pm
HABARI: Japhet Hasunga ameshinda kura ya maoni CCM kuwania Ubunge wa Viwawa baada ya kupata kura 552 akifuatiwa na Erick Minga aliyepata kura 129-MCL
Jul 20 5:56pm
HABARI: Dotto Biteko ameshinda kura ya maoni CCM kuwania Ubunge wa Bukombe baada ya kupata kura 555 kati ya 569-MCL
Jul 20 5:59pm
HABARI: Dk Godwin Molel ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Siha kwa kupata kura 148, akifuatiwa na Agrey Mwanry aliyepata kura 147-MCL
Jul 20 6:03pm
HABARI: Prof Joyce Ndalichako ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Kasulu Mjini kwa kupata kura 405, akifuatiwa na Daniel Nsanzugwanko aliyepata kura 80 kati ya 501-MCL
Jul 20 6:09pm
HABARI: Ibrahim Shayo ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Moshi Mjini kwa kupata kura 140, akifuatiwa na Priscus Tarimo aliyepata kura 137, kura zilizopigwa zilikuwa 370-MCL
Jul 20 6:15pm
HABARI: Ahmed Shabiby ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Gairo kwa kupata kura 532, akifuatiwa na Joel Mmasa aliyepata kura 8, kura zilizopigwa zilikuwa 590-MCL
Jul 20 6:30pm
HABARI: Naibu Spika Dk Tulia Ackson ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Mbeya Mjini kwa kupata kura 843, akifuatiwa na Hamande Mabula aliyepata kura 16, kura zilizopigwa zilikuwa 885-MCL
Jul 20 6:38pm
HABARI: Anne Kilango Malecela ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Same Mashariki kwa kupata kura 258, akifuatiwa na Florence Masunga aliyepata kura 51-MCL
Jul 20 6:44pm
HABARI: Livingstone Lusinde ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Mtera kwa kupata kura 571, akifuatiwa na Dk Michael Msendekwa aliyepata kura 122-MCL
Jul 20 7:06pm
HABARI: Abas Mtemvu ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Temeke kwa kupata kura 203, akifuatiwa na Doroth Kilave aliyepata kura 182, kura zilizopigwa zilikuwa 583-MCL
Jul 20 7:11pm
HABARI: Dk Charles Tizeba na Erick Shigongo wametoshana nguvu katika kura za maoni za CCM kuwania Ubunge wa Buchosa baada ya kupata kura 354 kila mmoja kati ya kura 751 zilizopigwa-MCL
Jul 20 7:22pm
HABARI: Prof Kitila Mkumbo ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Ubungo kwa kupata kura 172, akifuatiwa na Mwantumu Mgonja aliyepata kura 73, kura zilizopigwa zilikuwa 375-MCL
Jul 20 7:27pm
HABARI: Dk Faustine Ndugulile ameshinda kura za maoni CCM kuwania Ubunge wa Kigamboni kwa kupata kura 190, akifuatiwa na Paul Makonda aliyepata kura 122-MCL
Jul 20 7:32pm
HABARI: Adolf Mkenda ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Rombo kwa kupata kura 285, akifuatiwa na Anthony Mseke aliyepata kura 87 -MCL
Jul 20 8:28pm
HABARI: George Simbachawene ameshinda katika kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Kibakwe kwa kupata kura 667, akifuatiwa na Kwame Mwaga aliyepata kura 151 kati ya kura 894 zilizopigwa -MCL
Jul 20 8:33pm
HABARI: Peter Serukamba ameshinda kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Kigoma Kaskazini kwa kupata kura 261, akifuatiwa na Assa Makaniki aliyepata 81 na aliyepata kura Seleman Mvunge 51-MCL
29 min
HABARI: Charles Sungura ameshinda kura za maoni ndani ya CCM kuwania Ubunge wa Handeni Vijijini kwa kupata kura 168, akifuatiwa na Mboni Mhita aliyepata kura 136 na Ramadhan Diliwa akipata kura 135-MCL
24 min
HABARI: Jimbo la Mwanga kura za maoni CCM, Profesa Jumanne Maghembe ambaye amekuwa mbunge kwa vipindi vinne ameshika nafasi ya pili akipata kura 130 huku wakili Joseph Tadayo aliyeongoza akipata kura 176 na Shabibu Mruma amepata kura 56-MCL
18 min
HABARI: Jimbo la Kigoma Kusini kura za maoni CCM, Hasna Mwilima ameshinda kwa kupata kura 273 akifuatiwa na Nashon Bidyanguze mwenye kura 118, January Kizito kura 118 huku David Kafulila akipata kura 64-MCL
WANAOPITISHWA
I AZZAN
C.KIMEI
COSATO
M.ZUNGU
A.ABOOOOD
PROF NDALICHAKO
D.KILAVE
HASNA.MJL
J.TADAYO
M.MHITA
A.MAKANIKI
G.SIMBA CHAWENE(BABALAO)
E.SHIGONGO
 
Katika kura zilizonivitia ni hizi za Tunduma.
Silinde amehama kutoka Upinzani na hapo hapo akahama jimbo.
Ukitazama matokeo ya kura za maoni utaona ni kwa kiasi gani ameweza kujenga ushawishi ndani ya CCM katika muda mfupi.
Hapa ndio unaelewa ile hofu ya MNeC kutoka Tunduma.
All in All CCM inayo hazina ya taarifa ya mchakato ulivyoenda nchi nzima...yaani nani kashinda kwa kuchaguliwa bila kuhonga,nani kahonga na wakati gani alihonga.
Nani anakubalika na wananchi kwa ujumla nani ana uwezo wa kukinadi chama ndani ya jimbo,nje ya jimbo na kimataifa n.k

Kwa hiyo tushushe pumzi mchakato unaendelea.
 
Haya matokeo ya kihuni mnaleta hapa mengi sio ya ukweli, kisha yakitoka matokeo rasmi tunakuta ni mambo tofauti. Hiyo figure yako haiendani na matokeo.
Inashangaza sana Chadema badala mfikirie hali yenu mbaya ya kisiasa mnawaza matokeo ya Ccm.
 
Kumbuka kama Makonda hajui kujenga hoja, hajazoea kuulizwa maswali na huwa na majibu mafupi na ya kebehi/kiburi. Kama angeenda Ubungo angeshindana na Prof Mkumbo ambaye anajua kujieleza na kujenga Hoja. Kawe Wagombea ni wengi. Kibamba ni jimbo jipya na CCM haina nguvu.
Lakini lipo tatizo la wateuliwa kudhani hawawajibiki kwenye chama, hayo ndio matokeo yake, una shindwaje kuwashawishi voters 300? Kingine Ni uroho wa madaraka na dharau, kwani angeenda ukonga kibamba ubunge kawe angeshindwa nn? Na hata angeshindwa huko tungejua alienda kukipambania chama kulikoni kwenda kubanana na ndugulile, kwanza mumemtimua uwaziri bado mnamfuatafuata
 
Hawa wapuuzi flani walihama wakapewa nafasi CCM saivi wamewanyoosha, Shukwani ziwaendee CCM na mwenyekiti wao. Mwenyekiti kashamaliza teuzi za UDAS, URC, UDC, U-RAS, U-DED waliopoteza watajutia nafasi walizopoteza.

  • Mtulia
  • Katambi
  • Kafulila
  • Nassari
  • Silinde
  • Lijualikali

Wateule walioacha teuzi nao wamegaragazwa
  • Makonda

Wasanii waliojiforogoa kwamba wanaipenda CCM nao CHALIIIII

Wanaharakati CHALIIII!!

Vigogo CHALIII!
  • Kimei
  • Mwakyembe
 
Lakini lipo tatizo la wateuliwa kudhani hawawajibiki kwenye chama, hayo ndio matokeo yake, una shindwaje kuwashawishi voters 300? Kingine Ni uroho wa madaraka na dharau, kwani angeenda ukonga kibamba ubunge kawe angeshindwa nn? Na hata angeshindwa huko tungejua alienda kukipambania chama kulikoni kwenda kubanana na ndugulile, kwanza mumemtimua uwaziri bado mnamfuatafuata
Angekuja Kibamba asubuhi mapema angechukua jimbo.
 
Katika kura zilizonivitia ni hizi za Tunduma.
Silinde amehama kutoka Upinzani na hapo hapo akahama jimbo.
Ukitazama matokeo ya kura za maoni utaona ni kwa kiasi gani ameweza kujenga ushawishi ndani ya CCM katika muda mfupi.
Hapa ndio unaelewa ile hofu ya MNeC kutoka Tunduma.
All in All CCM inayo hazina ya taarifa ya mchakato ulivyoenda nchi nzima...yaani nani kashinda kwa kuchaguliwa bila kuhonga,nani kahonga na wakati gani alihonga.
Nani anakubalika na wananchi kwa ujumla nani ana uwezo wa kukinadi chama ndani ya jimbo,nje ya jimbo na kimataifa n.k

Kwa hiyo tushushe pumzi mchakato unaendelea.


Sisi huku Bashite wetu kachezea kichapo.
 
Na yule Serukamba nae jina lake ni Abdulkareem, au?! Hivi nyie watu mbona mnapenda sana kuendekeza udini? Tena Serukamba alikuwa Mbunge pale wakati CHADEMA ina nguvu kweli kweli Kigoma. Licha ya propaganda za CCM kwamba CHADEMA ni Chama cha Wakristo lakini Kaboor akaigeuza Kigoma kuwa ngome ya CHADEMA!!

Sasa hayo mambo ya kuangalia majina mnayatoa wapi?
Kama mkristo na kama mtanzania naunga mkono hoja.. Sio kila kitu ni dini au kabila..
 
Kigoma Mijini waislam ni wengi kwa maana hiyo wao ndiyo waamuzi wa nani awe mbunge.

Ni Kama Zanzibar. Pale Mkristo akigombea hawezi kushinda.

Kwa hiyo usitoe povu sana wakati mwenzako kasema ukweli
We jamaa unaelekea mdini sana! Kwahiyo Joyce kenda Kasulu kwa sababu anajua kwavile yeye ni Mkristo, na Kasulu wengi ni Wakristo, basi watamchagua kwa sababu ni Mkristo mwenzao sio?
 
Kumbuka kama Makonda hajui kujenga hoja, hajazoea kuulizwa maswali na huwa na majibu mafupi na ya kebehi/kiburi. Kama angeenda Ubungo angeshindana na Prof Mkumbo ambaye anajua kujieleza na kujenga Hoja. Kawe Wagombea ni wengi. Kibamba ni jimbo jipya na CCM haina nguvu.
Unachosema Ni sahihi kibamba ccm haina nguvu hivyo aliogopa kupetwa na John mnyika, kawe hata Kama angepita angekumbana na kisiki halima mdee, kimsingi makonda ni mwoga sana
 
Katika kura zilizonivitia ni hizi za Tunduma.
Silinde amehama kutoka Upinzani na hapo hapo akahama jimbo.
Ukitazama matokeo ya kura za maoni utaona ni kwa kiasi gani ameweza kujenga ushawishi ndani ya CCM katika muda mfupi.
Hapa ndio unaelewa ile hofu ya MNeC kutoka Tunduma.
All in All CCM inayo hazina ya taarifa ya mchakato ulivyoenda nchi nzima...yaani nani kashinda kwa kuchaguliwa bila kuhonga,nani kahonga na wakati gani alihonga.
Nani anakubalika na wananchi kwa ujumla nani ana uwezo wa kukinadi chama ndani ya jimbo,nje ya jimbo na kimataifa n.k

Kwa hiyo tushushe pumzi mchakato unaendelea.
Weka matokeo ya kura kudhihirisha hoja yako. Bila kuonyesha matokeo hatuna cha ku comment.
 
Back
Top Bottom