Uchaguzi 2020 Ahadi na Sera za Tundu Lissu katika Uchaguzi Mkuu 2020
Lisu hata kwa mtutu hawezi kuwa rais wa tz full stop.
Mitutu tena?? Mitutu ni ya wasiojulikana.

Hata kwa mtutu?? Mlisema hivyo hivyo Lissu hatarudi akarudi, mkajiapiza hadi kufa eti hawezi kupitishwa na NEC zikapangwa njama wakishirikiana na mahakama zikafeli.

Hivi kwanini mnakuwa wagumu kuelewa Nguvu ya Lissu?? Its devine power ndani yake.
 
Nyota njema huonelana asubuhi. Bab yenu kafanya mkutano mmoja tu yuko hoi. Leo lala siku ya tano na siku zinakatika kama barafu kwenye moto. Vijana makamanda wanachanja mbuga tu.
Buddy leo tuu magu na mama samia wanafanya jumla ya mikutano tisa... Magu akimalizia singida na mama samia kilosa just a single day wote watakuwa wamewafikia watu wangapi.

Lissu leo unakuwa mkutano watano kwa siku tano ndugu tazama nachokuambia kwa big picture sio narrow spectrum of understanding.
You have a work to do fanyeni kampeni kwa speed kuwafikia watu wengi ndugu hamuonekani kama u really need this.

Huku social media mnadanganyana tu.
 
Kwenye mikutano yako

A) Anza kuwakumbusha wananchi ulaghai wa CCM kwa jinsi ilivyotoa ahadi za uwongo kwa wananchi kwenye ILANI YAO ILIYOPITA NA MIKUTANO YAO YA KAMPENI na hivyo basi wananchi wawakatae kwa sababu hata wanayoahidi sasa hawatatekeleza

1) Wakumbushe wananchi jnsi CCM ilivyoahidi katiba mpya kwenye ilani ya mwaka 2015 lakini Rais Magufuli akakataa baada ya kuapishwa akadai eti hakuinadi kwenye kampeni wakati imo kwenye ilani yao-Waulize wananchi kama wanaweza kuendelea kuwaamini watoa ahadi za uwongo

2)Wakumbushe wananchi ahadi ya CCM iliyoko kwenye ilani yao ya 2015 kuwa watatoa milioni 50 kila kijiji—Mpaka sasa hawajatoa hata thumni, Waulize wananchi wana sababu gani za kuendelea kuamini watu waongo

3)Wakumbushe wananchi namna Magufuli alivyoahidi kugawa laptop kwa kila mwalimu ili imsaidie kuboresha ufudishaji—Waulize wananchi ziko wapi hizo laptop na pia waulize wananchi kwa vipi waendelee kuamini watu wasioishi neno lao?

4) Wakumbushe wananchi namna ilani ya uchaguzi ua CCM ya mwaka 2015 inavyozugumzia kuendelezwa kwa sera ya kilimo kwanza lakini Magufuli alipoingia tu miongoni mwa vitu alivyoanza navyo ni kuifutilia mbali sera hiyo licha ya kuwa ni mpango upo katika ilani yao ya mwaka huo

5. Wakumbushe wananchi jinsi Ilani ya CCM ya mwaka 2015 ilivyosema kuwa watoto watakaopata ujauzito serikali haitowafukuza shule—Wakumbushe jinsi Magufuli alivyoingia madarakani alivyokana ilani yake mwenyewe kwa kusema kuwa hao mabinti wakipata mimba atawafukuza shule za serikali kwa sababu hasomeshi wazazi.

B) Anza kuwaambia wananchi Ulaghai wa CCM ya sasa na hivyo Wasiiamini tena kuipa kura

1. Bashiru aliuambia umma kuwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu hawatotumia wasanii—Uongo mtupu, leo CCM wamegeuka waandaaji wakubwa wa disco za hadhara, juzi dodoma kulikuwa na wasanii zaidi ya 100. Kwa sababu CCM hawana sera za maana za kushawishi wananchi, wanasafiria nyota za wasanii

2)Wakumbushe wananchi kauli ya Magufuli mwanzoni mwa mwaka huu kuwa uchaguzi utakuwa huru na haki—Lakini mpaka hivi sasa tangu njama za kuengua wapinzani na kuvuruga uchaguzi ili CCM ipate ushindi wa mezani inaonyesha namna kauli kutoka kwa viongozi wa CCM jinsi zisivyo za kweli.

3)Wakumbushe wananchi jinsi CCM ilivyojifanya kupiga mkwara kuwa haitopitisha watoa rushwa kwenye kugombea, lakini pamoja na hayo wameishia kuteua wagombea wengine waliokamatwa kwa rushwa waziwazi na badala ya TAKUKURU iliyo chini ya serikali kufanya kazi yake, nayo imeacha kutimiza wajibu wake kwa kuwafumbia macho—Waulize wananchi wana sababu gani ya kumuamini Magufuli wakati ameshindwa kusimamia kauli ya chama chake ya awali kuhusu watoa rushwa?. Pia waulize wananchi, iweje wachague chama kuunda serikali, chama ambacho wagombea wake wamepatikana kwa rushwa, Je chama hicho kitaweza kupambana na rushwa na ufisadi wakati hawahawa wanaotegemea kupigana vita hiyo wamepatikana kwa rushwa?

C ) Kila kituo cha kampeni utakachokwenda anza kupre-empt na kuneutralize Talk points za CCM
1. Tafuta rebuttal nzuri sana ya Ishu ya SGR hii usipinge ujenzi wake, pinga namna inavyojengwa, tafuta data za mikopo ya ujenzi wa reli hii na itaavyowatia umasikini watoto wetu kwa sababu ya deni la Taifa kupaa sana. Waonyeshe wananchi kuwa unaunga mkono ujenzi wa SGR ila kwa mpango mbadala (chukua ule mpango wa ACT wazalendo wa kujenga SGR kupitia PPP), na pia mataaluma ya reli tunaagiza nje, tunapeleka mabilioni ya dola nje badala ya kuboresha kwanza Liganga na mchuchuma ili chuma chetu cha ndani ndo kijenge mataaluma hayo, ili pesa hiyo ndefu na ajira zibaki ndani badala ya kuwapelekea wajapan dola hizo na ajira kwao

2. Kuhusu Stieglers, Usiupinge mradi bali pia kosoa namna ya ujenzi wa mradi huo, tafuta data unajengwaje, wananchi wananufaikaje, je kuna technology transfer au tunaishia kuwa wabeba zege na mafundi mchundo tu?. Waambie wananchi kuwa ukiacha Stieglers wewe utajenga Vinu vingine vya umeme kwa kutumia gesi ya Mtwara, umeme utakaokuwa mwingi kuliko utakaozalishwa na Bwawa la Stieglers. Stieglers itazalisha around Megawatts 2000 na ushehe, wewe plan yako ionyeshe utaleta umeme wa gesi mkubwa mara tatu ya huo

3. Kuhusu ndege, hiyo endelea kuponda, piga spana kwelikweli, ni mradi feki

4. Kuhusu kujenga uwanja wa ndege Chato, yaani hii usiiache kila mahali, piga spana, piga nyundo, siliba kwelikweli

5. Kuhusu Elimu bure, waambie wananchi juu ya uwepo wa waraka wa siri wa wakuu wa shule kuendelea kuwachangisha wazazi baadhi ya michango, waambie kuhusu michango ya baadhi ya mikoa wazazi kuambiwa kila mtoto anayeanza kidato cha kwanza aende na dawati lake mwenyewe!. Waambie hii Elimu ni elimu gani wakati mwanafunzi anaambiwa aende na dawati lake. Waambie wananchi kuwa wewe utakuja na mpango mzuri zaidi wa elimu bure tena siyo bure tu bali iliyobora na ikikupendeza mheshimiwa rais mtarajiwa ifanye iwe bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha sita!. Mpango wako wa Elimu uwe ELIMU BURE NA BORA KWA WOTE! (haya ni maoni yangu binafsi yakikupendeza yachukue)

D). Kwenye kutafuta kura kutoka kwa makundi maalum ya kijamii

1. Kwa waislamu, tumia kauli indirectly kuwa "Sitoteua watu kwa wingi kuliko wangine kwa sababu ni wa imani yangu bali nitateua kwa vigezo na vigezo ninavyovitska vipo kwa watu wa imani zote—Hapa utakuwa umemchapa Jiwe konzi moja nzito mno na Waislamu watakuelewa sana maana teuzi za Jiwe zinanuka udini mno na waislamu linawachukiza sana hilo

2) Endelea kuwasemea Masheikh waislamu, Jana umefanya kazi nzuri sana Arusha kwa kuwasemea Masheikh 70 wa arusha walioko ndani.
Pia endelea kuwasemea Masheikh wa Zanzibar (Usitumie neno Masheikh wa uamsho, hilo neno ni divisive, Tumia tu neno Viongozi wa dini ya kiislamu walioko jela), Wakumbushe waislamu kuwa Magufuli ameshasamehe wafungwa wa kila aina wakiwemo waliofungwa kwa ubakaji lakini anaona tabu kuwaachia Masheikh—Waambie wananchi kuwa ukichaguliwa kuwa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania utawaweka huru hao masheikh.
(Ukitaka kuwakong'a nyoyo waislamu zaidi, waambie utawalipa fidia hao masheikh kwa kuonewa, kupotezewa muda, kuathiriwa kisaikolojia na kuzitia umasikini familia zao kutokana na vichwa vya familia kuwekwa ndani miaka 6 bila kosa lolote—Kaka ukipiga hii, utapata kura za waislamu haijapata kutokea)

3) Kundi la wanawake, wakumbushe wananchi jinsi Magufuli alivyoteua wanawake wachache mno katika serikali yake kulingsnisha na Kikwete, hii itasaidia kuneutralize soft power ya uwepo wa makamu wa rais mwanamke katika tiketi yake.
Umefanya kazi nzuri kumsiliba Maguful kwa kauli zake tata juu ya wanawake, kauli ile ya jogoo usiiache, endelea kupiga spana, kauli ile ya kupiga mashangazi endelea kupiga nyundo kwelikweli.

Endelea kuwakumbusha wanawake kuwa mwaka 2015 Magufuli aliwaahidi kuwatua ndoo kichwani, yaani akimaanisha kuwaletea maji. Lakini badala ya kuwaletea maji kwa kasi ya kutosha yeye anachukua pesa ananunulia ndege na kujenga uwanja wa ndege Chato

E. Endelea kuwakumbusha wananchi juu ya Ufisadi

Ishu ya Trilion 1.5 zisizo na maelezo yenye mashiko bado ipo kwenye kumbukumbu za wananchi, japo waliunda kamati ya kuwasafisha, lakini maelezo yao hayana mashiko, Endelea kuwakumbusha wananchi juu ya utata wa Trilion 1. 5
Usisahau kuwakumbusha wananchi Jinsi CAG Assad alivyotimuliwa kwa kusimamia taaluma yake ya uhasibu na pia jinsi manunuzi ya ndege yasivyokaguliwa kutokana na Jiwe kuweka ishu za ndege chini ya ofisi ya rais ambayo haikaguliwi na CAG

F. Usisahau ishu ya Maji na Kilimo
Maji bado ni tatizo kubwa, hili umepwaya kidogo, hujaligusia kabisa katika hotuba zako
Pia Kilimo hujakizungumza in details, tafuta mpango mkakati wa kuuza sera zako za kilimo kwa wananchi, waambie wwnanchi serikali yako itakavyowatafutia soko la mazao yao kupitia balozi zilizo nje. Badala ya mabalozi kukaa huko nje na kuuza sura, waanze sasa diplomasia ya kiuchumi ikiwemo kuwatafutia wakulima wetu masoko ya mazao yao ya kilimo.

G. Usiache hata kidogo kuwakumbusha wananchi magumu ya kiuchumi waliyopitia, uwe unawauliza kwenye kia mkutano wako, Je wako tayari kuendelea na mifuko iliyokauka kwa miaka mingine mitano?. Waulize wananchi je bado wanataka kuendelea na vyuma kukaza?. Waulize wananchi kuwa wako tayari kuendelea kukamuliwa na trafiki buku tano tano ili zikang'arishe viatu vya Trafiki? —Waambie wananchi kuwa kama hawataki hayo basi wampige chini Magufuli wakuchague wewe ukarekebishe mambo.

H. Lissu baba, wakumbushe wananchi juu ya adha za faini ya tochi za Trafiki —Waambie wananchi kuwa hutogeuza tochi chanzo cha mapato, bali utaongeza hata speed limit kwenye barabara kuwa 80 hadi 100 kulingana na mahali husika, badala ya 50 hata sehemu zilizowazi kabisa.

Aisee kaka Lissu, Ukiendelea kumwaga sera zako ulizoanza kumwaga kisha ukaongezea na hizi CCM watatafutana!

Piga Spana kaka
Duhh umetukumbusha mengi kweli. Mimi ni mmojawapo ambae sijaona alichofanya Magufuli kama raisi, nimeona kama waziri wa ujenzi. Nitawashangaa wananchi wanaoamini utendaji wake. Ninatabiri yafuatayo 1. Raisi aliyeko madarakani anaweza kupata kura nyingi sana kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi 2. wapinzani wanaweza kupata kura nyingi sana kutoka kwa wapiga kura, lakini kwa sababu wapinzani wako wengi watazigawana na hivyo kila mmoja kupata kura chache. Kwa mwenendo huu wa Upinzani hamuwezi kamwe kuitoa ccm madarakani jiongezeni tafuteni mbinu mbadala
 
Buddy leo tuu magu na mama samia wanafanya jumla ya mikutano tisa... Magu akimalizia singida na mama samia kilosa just a single day wote watakuwa wamewafikia watu wangapi...
Hahaha eti social media hata mikutano huioni? Mtaendelea kubisha hivyo hivyo sisi tunachana mbuga tu. Hao wazee waende huko na uzee wao. Inabdi wajigawe hivyi hivyo kwenda na kasi ya Lissu hawawezi
 
Anahubiri uhuru yeye mwenyewe yuko huru alipo.

Ahahubiri kutaka haki iwepo, wakati tuna mahakama ambao ni mhimili wa kutoa haki upo imara kabisa
Sera za kuongeza mdege tano. Yaani hapo kajitahidi kubadili upepo wa kampeni.😀😀
 
Mitutu tena?? Mitutu ni ya wasiojulikana.

Hata kwa mtutu?? Mlisema hivyo hivyo Lissu hatarudi akarudi, mkajiapiza hadi kufa eti hawezi kupitishwa na NEC zikapangwa njama wakishirikiana na mahakama zikafeli.

Hivi kwanini mnakuwa wagumu kuelewa Nguvu ya Lissu?? Its devine power ndani yake.
Nguvu ipi buddy... Hili ni kosa mnalifanyaga sana kuamini mshashinda wakati ni mwanzo wa mbio... Uzeni sera kwa watanzania wawaelewe
Mark words ndugu lema hashind arusha mjini na Lisu atapata kura less ya magufuli na trust me wala hawataibiwa kura zao...
 
Kwa sera hizi za Lissu na zile sera za kununa ndege tano za


Magufuli basi nashauri Magufuli atafute kazi nyingine ya kufanya.View attachment 1555267
Muheshimiwa yupo Vizuri; ILA naomba ufafanuzi wa Agenda #1 kuwa atafanyaje ili kuongeza ajira kwa vijana ili ajitofautishe na viongozi wengine wanaotamka tu bila uhalisia...
 
Nguvu ipi buddy... Hili ni kosa mnalifanyaga sana kuamini mshashinda wakati ni mwanzo wa mbio... Uzeni sera kwa watanzania wawaelewe
Mark words ndugu lema hashind arusha mjini na Lisu atapata kura less ya magufuli na trust me wala hawataibiwa kura zao...
Baba sera zinauzika na matunda tunayaona. Uwe unataka au hutaki huo ndio ukweli.
 
Lissu ni failure, hana mikakati, hadi kampeni zinakuja kuisha atakuwa amepita nusu tu ya majimbo Tz bara, hata nyumbani kwao Singida Magu atamshinda vibaya sana. Hakuna mkoa hata mmoja ambao Lissu anaweza mshinda Magu.
 
Shida ni uwasilishaji wake na kejeli dharau na matusi. Atapata kura za wapenda fujo tuu, wapenda maendeleo wanamchagua Magufuli.
 
Lissu ni failure, hana mikakati, hadi kampeni zinakuja kuisha atakuwa amepita nusu tu ya majimbo Tz bara, hata nyumbani kwao Singida Magu atamshinda vibaya sana. Hakuna mkoa hata mmoja ambao Lissu anaweza mshinda Magu.
Sasa kama.atakuwa amepita Nusu ta Majimbo si ndio vizuri ili nyinyi chichiem mshinde??
Kazi kweli kweli
 
Labda marekani ya chato!!!

Magufuli kaajiri marubani wawili tu kwa kipindi cha miaka sita. Hizo ndizo ajira tunazoambiwa na ccm.

Ajira za marubani wawili na "air hostages" sita!
Ameshindwa kuajieri hata wafanya kazi milioni moja kwa miaka mitano. Huyu jamaa hata apewe miaka 30 atakuwa anatupotezea muda tu.
 
Shida ni uwasilishaji wake na kejeli dharau na matusi. Atapata kura za wapenda fujo tuu, wapenda maendeleo wanamchagua Magufuli.
Kuna mtu mpumbavu kama Jiwe? Kwa jinsi anavyowasilisha matamshi yake?
 
Ata hili bima kwa watanzania wote nalenyewe ni kusadikika HALIWEZEKANI!!!
Hayo yote yanawezekana mkuu! Ni suala la utashi tu wa serikali! Kama tujenga madaraja hadi baharini, tukajenga mengine hewani, Kwanini suala Bima ya afya kwa kila mtu lishindikane? Mbona Nyerere hakuchimba madini na wala hakuwa na soko pana la watalii, hakuwa taasisi rasmi za kukusanya mapato kama ilivyo sasa TRA, Lakini alitoa elimu bure mpaka University na wengine wakasomeshwa hadi nje ya nchi! Alitoa huduma za afya bure!

Alilipa walimu mishahara na posho za kufundishia, yaani kila mtumishi kwa kada yake alikuwa na mshahara na posho ya kiofisi na refreshment nyingine kibao! Wanafunzi wa shule za boarding walipewa hadi usafiri wa kupelekwa makwao nyakati za likizo! Je sisi na utitiri wa makusanyo toka vitegauchumi vyote hivi vilivyotuzunguka tumerogwa na nani hata tushindwe kutekeleza hayo? Kinachofanywa sasa ni misslocation of funds!

Tunawekeza kwenye vitu visivyo na faida! Mfano kugharamia watu wanaotukana na kunyanyasa wapinzani, kuandaa matamasha na makongamano ya wasanii wakati shule hazina madawati!

Hivi serikali ingefanya kutembea na hawa wasanii mikoa yote kuhamasisha uchangiaji wa madawati na huduma kwa miaka hii yote mitano sasa hivi matatizo hayo si yangekuwa historia! CCM acheni kuwa ving'ang'anizi wa madaraka, Pisheni watu wenye maono na mitazamo mipya watuvushe tulipokwama!
 
Sasa kama.atakuwa amepita Nusu ta Majimbo si ndio vizuri ili nyinyi chichiem mshinde??
Kazi kweli kweli

Kwani CCM kushinda ni swali ? Huu ni uchaguzi wa kutafuta Magu atashinda kwa % ngapi , ni banda la 90% au 80 au akishuka sana 75%.
 
Back
Top Bottom