Iam not a single mother(yet).
Ila hata ikitokea nimekua hakuna mtu atasema neno la kunishusha thamani sbb ya usingo maza nikaliamini.
Wapo watu wameoa singo maza na wanaishi kwa amani kuliko waliooa waliotupa watoto chooni
Unajua ni swala la maamuzi. Wengi wa mabinti kabla ya kuzaa wanakuwa hawajafanya maandalizi ya kuwa mke wa mtu then straight uwe mama?!
Yaani unataka kuwa askari jeshi ila unakwepa mafunzo ya mgambo ebo.
Kosa ambalo kama jamii tunakosea kwanza ni kutowaandaa watoto wa kike kuwa wake.
Mwanaume haandaliwi kuwa Mume hata siku moja, kuwa mume bora ni matokeo ya kupata mwanamke anayejua kushikamana katika ujenzi wa familia na nyumba yaani mwanamke anayejua kubalance majukumu yake, ajue saa ipi awe mke na saa ipi awe mama, na saa ipi awe mwanamke.
Sasa hawa viumbe wa kisasa wao wanachojua ni kuwa supa woman, mwanamke wa shoka, mama shupavu, hizi sio sifa za mwanamke anayeweza kuishi na mwanaume kama Mke.
Kama mtabisha mbishe tu ila huu ndio ukweli. Jamii imeacha kutengeneza wake inatengeneza wanawake wapambanaji ambao wanaume hawahitaji wanaishia kuwazalisha ila ndani ya nyumba hawawezi kuishi pamoja hata kidogo sababu hawakuandaliwa.
Haiwezekani miaka ya nyuma kuna wanaume wanakuta mwanamke ameshazalishwa watoto hata watatu ila ule utii na adabu ya mke mwanaume anachukua anaweka ndani na anaoa na kujenga blended family bora kabisa.
Ila miaka hii mwanamke ukute ana mtoto wake aisee ni tatizo. Ambaye umepata nae mtoto utavumilia sababu alibeba damu yako ndio analea ila ikiwa ni mtoto ambaye si wako aaah mwanaume lazima uteme mzigo maana tensions zinazokuja na mwanamke ambaye hajui majukumu ya mke unaweza jikuta unatoa kichapo ili kutengeneza discipline.