Maswali yangu kwa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) kuhusu Tamko la Mkataba wa Bandari

Maswali yangu kwa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) kuhusu Tamko la Mkataba wa Bandari

Wapi imesemwa waarabu wanakuja kujenga misikiti?
Serikali ya Tanzania hajawahi kuwa na mkataba wowote mzuri. Kama wanakuja kutujengea Misikiti then ni sawa. Otherwise, hakuna kingine wanaweza kutusaidia hawa Waarabu.
 
Serikali ya Tanzania hajawahi kuwa na mkataba wowote mzuri. Kama wanakuja kutujengea Misikiti then ni sawa. Otherwise, hakuna kingine wanaweza kutusaidia hawa Waarabu.
Wapi kwenye mkataba imesemwa watu wanakuja kutengeneza msikiti? Hivi nyie watu mna akili kweli? Au ni milobot mliyoshikiwa akili?
 
Majibu:

1. Siyo kweli wananchi walitaka tuendelee na chama kimoja bali ni wana CCM na hasa UVCCM ndiyo walitaka chama kimoja kwa kujikomba kwao kwa Nyerere lakini akawatolea nje.

2. Muhimili wa mahakama haujatoa uamuzi wake kwa madai hauna mamlaka ya kuingilia maamuzi ya bunge lakini ulibainisha wazi kuwa mkataba una kasoro nyingi. Kwa kuzingatia kasoro hizo maaskofu wamesema hawaungi mkono mkataba huu.

3. BAKWATA hawajasema cho chote hivyo usiwawekee maneno kinywani.

..SHURA YA MAIMAMU walitoa tamko zuri na liko very balanced na hakuna kilichoharibika.

..TEC kwenye hiyo statement yao wameeleza kwamba wamekutana na watu wa serikali ktk ngazi mbalimbali.

..Mimi nadhani Watanzania tunapaswa kujiongeza ili tuweze kusikiliza maoni ya Mashekhe, au Maaskofu, bila kushinikizwa na IMANI zetu.
 
Mkataba wa bandari ni mkataba wa kurudisha utawala wa sultan sio wa kuleta maendeleo

Alichofanya samia ni kusaidia waarabu kuja kutawala TANGANYIKA
Hisia zako zinakudanganya. Lakini ni hisia zinazotokana na imani yako kidini hivyo zina mizizi mizito na sio rahisi kwako kuachana nazo.
 
Wewe unaenda jwa Wakristi wenzako ambao huu mkataba wanautazama kwa jicho la udini
Mkuu hili swala mnalazimisha kuliunganisha na dini, hakuna muislam aliyeenda shule atakubaliana na mkataba usiojulikana mwisho wake miaka mingapi. Kingine sababu ya watu kuunganisha hili swala na udini ni kwasababu waislam wana ubaguzi wa asili, Wana tabia ya kutetea chochote hata uozo na upumbavu Ili mradi kafanya muislam mwenzie na wanajua waarabu walivyo wabaguzi kwahiyo wakichukua bandari asilimia kubwa ya watakaopewa ajira bandarini watakuwa waislam, mifano hai ipo kwa Azam, Mo, Ramadhan Dau akiwa NSSF n.k, mifano kibao. Mkristo hamuiti Jina lolote baya muislam officially zaidi ya utani. Lakini muislam hadi kwenye vitabu vya dini anamuita mkristo KAFIRI, ni tusi kubwa sana. Ndo chanzo cha waislam kukumbwa na migogoro isiyoisha ukiwemo UGHAIDI (TERRORISM), Sikutaka kuingiza maswala ya dini umenilazimisha. Kama ulichelewa kuanza darasa la kwanza kwasababu ya kujifunza kiarabu niliyoelezea hapa yote hutayaelewa, sababu kabla hujaanza kujua elimu inayotumika duniani ulimezeshwa na kukaririshwa vitu visivyohitajika sana kwenye ulimwengu wa kiteknolojia,kibailojia na kisayansi.
 
Maaskofu wa Tec wanapinga mkataba au wamapinga vipengele vya mkataba?
 
Bottom line hatutaki Bandari zetu zigawiwe kwa foreigners mkilazimisha msije kurukana huko mbele kwani ni lazima mtalipa, Watanzania wengi hawataki hivyo ni kama mlivyosikiliza na kumwachia W.Slaa pia na hili msikikize sauti ya wengi ni sauti ya Mungu …
Hawataki kwa sababu ya uelewa mdogo wa nini kinachokwenda kufanyika, hawataki kwa sababu ya kudanganywa na wapigaji wa bandarini na wao wakaingia kichwa kichwa kwenye siasa za kibaguzi.

DPW wapo katika bandari za maana za dunia hii, UK, USA, China kote huko wapo, eti Tanzania wasiwepo kwa sababu waarabu inaaminika wanataka kurudisha sera za utumwa mwaka 2023!!.

Hatupo informed wabongo na hatujui kwamba hatujui lolote.
 
1. Wanadai Serikali iachane na Mkataba wa Bandari kwa sababu wananchi wamegawanyika kuhusu mkataba huo!
Swali langu kwao, Ni jambo lipi nchi hii limewai kukubaliwa na asilimia 100 ya wananchi wote? Kwenye Mfumo wa vyama vingi, Mbona asilimia kubwa ya Wananchi walikataa mfumo huo ila Serikali wakauunga mkono! Je kwa nini hawakutoa tamko kipindi icho kutaka nchi iendelee kuwa ya Chama kimoja? Kwa tamko lao walilosema maamuzi ya wananchi yaheshimiwe basi wanaungana mkono Serikali I reverse maamuzi yake ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi na turudi kwenye mfumo wa Chama kimoja?

2. Kwenye tamko lao wanadai Mihimili ya dola iheshimiwe. Swali langu kwao! Juzi Mahakama Kuu wametoa maamuzi ya kutupilia mbali maombi ya watu walioshtaki mkataba wa Bandari.

Sasa kwa nini wanataka mihimili ya dola iheshimiwe na wao hawataki kuheshimu maamuzi ya Mahakama? Kama Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 hasa ibara ya 107A inasema Mahakama ndio Mhimili wa mwisho katika kutoa haki sasa kwa nini hawaheshimu maamuzi ya Mahakama alafu wanatoa tamko kusema Mihimili ya dola iheshimiwe?

3. Wao wanavyotoa tamko kutaka Serikali iachane na mkataba wa bandari kesho BAKWATA wakitoa tamko Serikali iendelee na mkataba wa Bandari wanataka Serikali imsikilize nani? Kesho kutwa mabudha wakitoa tamko pia wanataka Serikali imsikilize nani kati yao?

Kwa hali hii sasa naamini kwa nini mapadre wa kanisa katoliki walishtakiwa kwa kuhamasisha mauaji ya kimbari Rwanda!

Mods! Naomba sana msiunganishe huu uzi!!

Hili la bandari halihusiani kabisa na mauaji ya kimbari. Historia inaonyesha wana siasa wanachosema hawamaanishi. Wengi ni waongo na wanatanguliza mbele maslahi yao.
Nionavyo mimi, hata kama huu mkataba utapita, haitachukua muda utakataliwa
 
1. Wanadai Serikali iachane na Mkataba wa Bandari kwa sababu wananchi wamegawanyika kuhusu mkataba huo!
Swali langu kwao, Ni jambo lipi nchi hii limewai kukubaliwa na asilimia 100 ya wananchi wote? Kwenye Mfumo wa vyama vingi, Mbona asilimia kubwa ya Wananchi walikataa mfumo huo ila Serikali wakauunga mkono! Je kwa nini hawakutoa tamko kipindi icho kutaka nchi iendelee kuwa ya Chama kimoja? Kwa tamko lao walilosema maamuzi ya wananchi yaheshimiwe basi wanaungana mkono Serikali I reverse maamuzi yake ya kuruhusu mfumo wa vyama vingi na turudi kwenye mfumo wa Chama kimoja?

2. Kwenye tamko lao wanadai Mihimili ya dola iheshimiwe. Swali langu kwao! Juzi Mahakama Kuu wametoa maamuzi ya kutupilia mbali maombi ya watu walioshtaki mkataba wa Bandari.

Sasa kwa nini wanataka mihimili ya dola iheshimiwe na wao hawataki kuheshimu maamuzi ya Mahakama? Kama Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 hasa ibara ya 107A inasema Mahakama ndio Mhimili wa mwisho katika kutoa haki sasa kwa nini hawaheshimu maamuzi ya Mahakama alafu wanatoa tamko kusema Mihimili ya dola iheshimiwe?

3. Wao wanavyotoa tamko kutaka Serikali iachane na mkataba wa bandari kesho BAKWATA wakitoa tamko Serikali iendelee na mkataba wa Bandari wanataka Serikali imsikilize nani? Kesho kutwa mabudha wakitoa tamko pia wanataka Serikali imsikilize nani kati yao?

Mods! Naomba sana msiunganishe huu uzi!!
Umekurupuka maswali yote hayana mashiko ukweli unabaki hapohapo wananchi wengi hawakubaliani na suala la ubinafsishaji wa bandari kwa sababu ya mkataba mbovu hilo liko wazi habari za takwimu msituulize Ila kama nyie mnazo za kwenu wa wengi kukubali zilete hapa na wakati huohuo mtueleze kwa nini mnahangaika kubadili sheria ili kufunika maovu yaliyopo katika huo mkataba kwa nini serikali inahangaika unataka kufanya utapeli gani kwenye rasilimali za Taifa?

Maamuzi ya mahakama hatujayakubali na ndio mana tutakata rufaa ngoja Mwabukusi na team yake wapumue kwanza baada ya kuwa huru leo tunarudi vitani
 
Bunge limesharidhia serikali inaendelea na mchakato. Ila mpo huru kutoa maoni yenu hamjakatazwa hii ni awamu ya 6 ya mama samia.
Ndo hapo wanadai mihimili ya dola iheshimiwe.

Bunge lilitoa maamuzi, Mahakama imetoa maamuzi wao hawataki kuheshimu alafu wanasema eti Mihimili iheshimiwe. They don't practise what they preach sasa sijui wana preach nini
 
Back
Top Bottom