Mwigulu: Tumesikia malalamiko ya Watanzania kuhusu tozo za miamala na Rais ametoa maelekezo ya kuzitazama upya
Hili suala lilizungumzwa kwenye kikao cha baraza la mawaziri, na yeye Samia akiwa kama Mwenyekiti wa baraza.. Waliyajadili, wakakubaliana na ndo maana likapelekwa bungeni kama muswaada...
Hata mi nashangaa, eti Kuna watu wanasema baadhi ya mawaziri wanataka kimwingiza Chaka mama kwani yeye hakuipitia budget yake?

Huyu mama anajua kila kitu na hayo makato alikubaliana nayo ndiyo wakaipeleka budget bungeni.
 
Na si ajabu kama zitafanyiwa marekebisho kidogo, wale UVCCM, waliokuwa wamepongeza tozo hizo, watajitokeza tena kumpongeza Rais!!kuwa ni msikivu!!hii mijitu huwa hata siielewi, ina simamia wapi?bali ni kufuata upepo tu!!tatizo wameshatuona wananchi mabwege tu, yaani tatizo wanalitengeneza wao, huko wanalileta kwetu kwa makusudi , tukilalamika wanasema ngoja tukaliangalie upya, wanakuja na ufumbuzi watu tunaanza kushukuru tena, na kuwaona wanatupenda!!
Cc jingalao,huyu jamaa Huwa simuelewagi Mana analipenda Sana CCM kuliko Wananchi wake
 
Kwahiyo unatarajia Rais awe anasoma miswada inayotoka bungeni?! Like serious?! Na pia unatarajia Rais awe anasoma mikataba?! Hivi una habari mikataba inakuwa na lugha za kisheria huku rais anaweza kutoka kwenye taaluma yoyote ile including Sayansi Kimu? Rais asome mikataba wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Timu yake wanafanya kazi gani? Rais asome miswada inayotoka bungeni wakati wasaidizi wake kama Chief Secretary anafanya kazi ipi?...
Lazima usome chochote ambacho kinahusu kuweka sahihi
 
Mkumbo upi na vitu viko wazi tu,wewe ni mjinga mmoja unayejua kuandika tu.Hao unaowatetea wangefanya tu utafiti wa watu hata mia tu wangeona reaction ya wananchi ikoje.Huwezi kutunga sheria ya kipumbavu kama hiyo halafu utegemee wananchi wareact positive!..
Sijui labda wananchi wa huko unapokaa wewe.Stupid.
Really?

Unamaanisha utumie opinions za watu mia kudefine za 60 million?
Well that's what I call bullshit right there.

Sababu hao watu mia Itategemea na viwango vyao vya uchumi which means there's a higher chance of getting something worse then the current circumstance we're facing.

And how could you tell that what we're facing right now isn't about cheap popularity and it's not a part of the research regarding the complexity and that this is the reaction and research you're babbling about so to figure out which is which?

Well as I said Africans ni wavivu wa kufikiri na wewe ni mfano hai that your mind is full of applesauce.
 
Yaani hawa wanasiasa wanatuchezea sana. Suala ni simpo. Tupunguze sana kutumia simu za mkononi. Nadhani turudishe simu za line za ttcl. Kwani kule kuna tozo? Wakishituka tutatafuta mbadala. Ila na sisi tunazitumia sana hizo simu za mkononi. Kwani tusipozitumia itakuwaje? Mbona zamani hazikuwepo na maisha yaliendelea!!!! Tujifunze kutozitumia sana. Yaani tupungue matumizi.
Kweli kabisa tubane matumizi
 
Mwigulu na zungu wamehongwa na mabenk kupitisha tozo hizi za kijinga.
Hayo mabenk ukiritimba wao tu ndo umechangia kampuni za simu kuteka soko,waongeze ubunifu nao waache kufanya hujuma kama hizi.
Huduma za benk ni gharama za chini kuliko za simu tangu awali tofauti ni kwamba simu hadi uchochoroni unapata huduma benk kupata huduma kama wakala,atm,ni hadi uzitafute kwa torch.
Mabenk kuweni wabunifu acheni kuhonga wanasiasa kuumiza wananchi.
Duniani nzima Hakuna tozo haramu kama hizi only in tz.
 
Mwigulu na zungu wamehongwa na mabenk kupitisha tozo hizi za kijinga.
Hayo mabenk ukiritimba wao tu ndo umechangia kampuni za simu kuteka soko,waongeze ubunifu nao waache kufanya hujuma kama hizi.
Huduma za benk ni gharama za chini kuliko za simu tangu awali tofauti ni kwamba simu hadi uchochoroni unapata huduma benk kupata huduma kama wakala,atm,ni hadi uzitafute kwa torch.
Mabenk kuweni wabunifu acheni kuhonga wanasiasa kuumiza wananchi.
Duniani nzima Hakuna tozo haramu kama hizi only in tz.
 
Mwigulu jiuzulu...Mnashindwa kumsaidia mama....Wananchi wamechukia na wanalalamika sana.
 
Huyu waziri hatakiwi kuwepo hapo kama waziri, he must resign.

Yeye amelileta hili tatizo, na ameongea sana kututaka wananchi tuzoee shida na machungu ya tozo.

Hatakiwi kuwepo hapo ili alitatue tatizo alilolileta. Kichwa chake hakina uwezo huo.

Awaachie wengine watakaokuwa huru kufikiri bila mipaka kuleta suluhisho
 
Fedha mtaaani hakuna halafu wananchi tunabebeshwa mizigo ya miamala. Mwigulu alimshauri vibaya Rais Samia kuhusu tozo ya miamala ya simu. Juzi nkatuma 30,000/= tozo 11,00/=, jana nkatuma tena tozo 11,00/=, leo nimetuma 105,000/= tozo 2530/=!. Ni nn hiki Mwigulu Nchemba?. Hii ni dhuluma na wizi mtupu. Nafuu ungeshauri kuwa kila muamala mwananchi atozwe mia 500/= kuliko dhuluma hii ambayo sijawahi kuisikia tangu Hayati J.K. Nyerere.

Achia dhamana Mwigulu haufai kabisa!. Kwa hili, kwa hili, kwa hili hautoshi kuendelea kuitwa waziri wa fedha. Eti unasema unawahurumia watanzania!. Kama unawahurumia uza ule msafara wako wa magari ya kifahari uwasaidie watanzania vinginevyo acha unafiki!. Unaibua tatizo halafu unakuja na ngonjera kuwa waziri Mkuu ameishaitisha kikao!. Hivi watanzania maskini wanasaidiwa kwa kubebeshwa mizigo ya miamala ya simu Mwigulu?. Eti unawahurumia watanzania!. Kama unawahurumia mbona hausemi unapunguza burungutu la msahahara wako mnono ili uwasaidie watanzania unaowahurumia?. Wewe unaamini utakuja kuupata urais kwa propaganda zako za Maji taka!.
 
Ukweli ni kuwa hela tulizo nazo wananchi lazima zote zizunguke na kurudi kwenye mfuko mkuu wa serikali halafu mzunguko uanze tena. Tatizo ni mbinu zinazotumiwa kuurejesha mzunguko unakinzana na uhalisia wa mzunguko unavyotaka
 
Mwigulu nadhani anashindwa kuwaelewa watz ,sisi waTZ tunamaindi vitu vidogo sana ,tuko tayari kutembea kilomita moja kwenda kununua unga kilo 2 uliopunguzwa Tsh 100 na kuacha duka lililo mita 20 kutoka mlangoni mwake.
Kama Sina kazi inayoweza kuniingizia hiyo shilingi 200 kwanini nisitembee kuufuata huo unga wa bei punguzo
 
Mhe. Rais naye ameguswa na jambo hili, amesikia maoni ya Watanzania wote, ameshatoa maelekezo kwamba tuyafanyie kazi haya malalamiko ambayo wananchi wanayatoa." - Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba.

"Nitoe rai kwa wananchi kuwa Serikali imesikia malalamiko ya wananchi na tayari tumeendelea kuyafanyia kazi, Waziri Mkuu ameshaitisha kikao kesho kuendelea kupitia masuala haya haya."

"Kwa sababu hii ni sheria ya Bunge, na tayari imeshapitishwa na inatakiwa kutekelezwa, lakini kuna maeneo ambayo yanaangukia kwenye kanuni ambazo zinaangukia Wizara ya Fedha na Wizara ya Teknolojia ya Mawasiliano."

Hawajasikia kilio wala nini, bali nguvu ya umma imewakalia vibaya. Walichokifanya ni kwenda kuwaharibia biashara hayo makampuni ya simu.
 
Back
Top Bottom