Papa Francis: Mapenzi ya Jinsia Moja siyo Kosa, siyo Uhalifu, lakini ni Dhambi
They are known to be conservatives, makanisa mengine hata ndoa wanawafungisha but sio RC.
Kwa upande wa dini ushoga ni dhambi.
Japo akienda kanisani ama sehemu ingine hatofukuzwa ushoga wake.
Dhambi kubwa tukiamza kuuana ikiwa uchoko wao hauletwi kilazima kwangu.
au siyo,unahalalisha tu!!..na nani aliyesema mashoga wauane!?...kwa hiyo sodoma na Gomorrah mungu aliwaonea!?
 
Wapi aliposema haki za mashoga? Amezungumzia kuwa ni dhambi, ila sio uhalifu, na ni kweli kabisa. Wewe ukifumaniwa na mke wa mtu leo, hakuna sheria inayokupa adhabu, lakini ni dhambi.

Tatizo umeingia kwenye mtego wa kufiiri unatetea Ukatoliki. Acha hizo nukuu za BBC, nimesikiliza mahojiano yote. Hata hizo nukuu za BBC anasemaje juu ya Maaskofu wanaopinga hizo haki? Hakuna Kanisa haifanyi kuhitaji yeye kusema wapokelewe! Kwani Kanisa linawakataa? How?

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
HAkuna popote pale ambapo Kanisa liliwahi kubariki Mahusiano ya watu wa jinsia moja. Siku zote Kanisa limekua likisema kwamba halibariki mahasiano ya watu wa junsia moja, wala haliungi mkono watu wa jinsia moja wanaoishi kama wenza ku adopt watoto sababu that home won't be a great home kwa watoto hao na hakutakua na funzi jema juu ya maana halisi ndoa na ndiyo mwanzo wa kubomoka kwa mafundisho ya kanisa.
Pamoja na ukosoaji huo wote, siku zote kanisa limesema lina wajibu kwa watu hao ni si sawa kwa Kanisa na jamii kuwatenga.

Kama Kanisa litawatenga, je ni nini maana ya Kanisa? Na faida ya Kanisa ni nini?

Hata Yesu alisema "hakuja kuwaita watu wema bali wenye dhambi ili wapata kutubu". Sasa kanisa likiwatenga wakatubie wapi? Lipo kwa ajili ya nani?
Jamii inapoharibikiwa inahitaji utulivu na tafakari ili kupata busara ya kuzuia uharibufu huo na si kuruhusu mihemuko kwani ndiyo uharibifu utazidi mara kumi zaidi.
 
Ukisema ushoga si uhalifu chanzo chake si sheria zilizopitishwa kuwa si uhalifu? Anaposema kanisa liwapokee kwani Kanisa lini limewakataa? Kanisa lifanye nini kipya?
Kwanza ujue kanisa linaundwa kuanzia ngazi ya familia hadi jamii yote kwa ujumla. Sasa kama wewe tu unaonesha kuwa hauko tayari kuwapokea, ni nani ulitaka awapokee kwa niaba yako? Katika watoto wako mmoja wao akiwa shoga, ukimtenga unataka na kanisa limtenge? Yesu mwenyewe alichangamana na wenye dhambi hadi wayahudi wakawa wanasema kwa nini anachangamana nao, kama mnavyosema ninyi humu

Luka 15: 1-10
1 Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. 2 Mafarisayo na waandishi wakanung'unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao. 3 Akawaambia mfano huu, akisema,

4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? 5 Naye akiisha kumwona, humweka mabegani pake akifurahi. 6 Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea.

7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu. 8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione? 9 Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea. 10 Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.
 
Luka 15: 1-10
1 Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. 2 Mafarisayo na waandishi wakanung'unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao. 3 Akawaambia mfano huu, akisema,

4 Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda nyikani, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone?

5 Naye akiisha kumwona, humweka mabegani pake akifurahi.

6 Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea.

7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.

8 Au kuna mwanamke gani mwenye shilingi kumi, akipotewa na moja, asiyewasha taa na kufagia nyumba, na kutafuta kwa bidii hata aione?

9 Na akiisha kuiona, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimeipata tena shilingi ile iliyonipotea.

10 Nawaambia, Vivyo hivyo kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye.
 
Kwa muktadha huu saa iwe rasmi kitu kinachoitwa uchumba sugu katika kanisa kifutwe, na watuhumiwa wa uchumba sugu kama wawaitavyo wapokelewe katika kanisa.

Ifike sasa kanisa kitambue ndoa ya mke zaidi ya mmoja, hiini kwa definition ya papa kuhusu dhambi na uhalifu.
 
Mwenye kiherehere ni wewe unayeuliza maswali ya kijinga...kuanzia Sasa patakua na vilainishi kanisani
Tafuta pesa uache masikitiko.

Papa kasema ukweli. Hataki mbambamba na UNAFIQ.

Kwanza si ajabu wewe ndo lifiraji likuu.
 
HAkuna popote pale ambapo Kanisa liliwahi kubariki Mahusiano ya watu wa jinsia moja. Siku zote Kanisa limekua likisema kwamba halibariki mahasiano ya watu wa junsia moja, wala haliungi mkono watu wa jinsia moja wanaoishi kama wenza ku adopt watoto sababu that home won't be a great home kwa watoto hao na hakutakua na funzi jema juu ya maana halisi ndoa na ndiyo mwanzo wa kubomoka kwa mafundisho ya kanisa.
Pamoja na ukosoaji huo wote, siku zote kanisa limesema lina wajibu kwa watu hao ni si sawa kwa Kanisa na jamii kuwatenga.

Kama Kanisa litawatenga, je ni nini maana ya Kanisa? Na faida ya Kanisa ni nini?

Hata Yesu alisema "hakuja kuwaita watu wema bali wenye dhambi ili wapata kutubu". Sasa kanisa likiwatenga wakatubie wapi? Lipo kwa ajili ya nani?
Jamii inapoharibikiwa inahitaji utulivu na tafakari ili kupata busara ya kuzuia uharibufu huo na si kuruhusu mihemuko kwani ndiyo uharibifu utazidi mara kumi zaidi.
Ni kweli Kanisa halibariki na halitokuja kubariki sababu hakuna mwenye mamlaka hiyo. Ila hizi confusion ndio zinazochanyanga hata waamini na kufikiri Kanisa linalegeza mafundisho yake.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Kwa muktadha huu saa iwe rasmi kitu kinachoitwa uchumba sugu katika kanisa kifutwe, na watuhumiwa wa uchumba sugu kama wawaitavyo wapokelewe katika kanisa.

Ifike sasa kanisa kitambue ndoa ya mke zaidi ya mmoja, hiini kwa definition ya papa kuhusu dhambi na uhalifu.
Zote hizo ni dhambi, na hakuna mtu mwenye 'uchumba sugu' aliyetengwa, otherwise haujaelewa maana ya kutengwa. Ukitengwa na Kanisa, siku ya kurudi ni lazima ukiri upya imani mbele ya kanisa. Pengine labda unachanganya kati ya kuzuiwa sakramenti na kutengwa. Wenye vizuizi vya sakramenti hawajatengwa, na kila siku huwa tunao jumuiyani na makanisani ili waelewe umuhimu wa kuishi katika ndoa takatifu
 
Back
Top Bottom