Rais Samia: Hatukutoa fursa ya Mikutano ya hadhara watu wakavunje sheria, wasimame kutukana, kukashifu na kuchambua dini za wengine

CCM ni mabingwa wa kuhamisha gia angali.Wanakwepa mijadala inaohusu wanakimbilia kudai wametukanwa🤔
Sasa kuongelea DP World imekuwa matusi especially kwa dini Fulani.
 
Mkialikwa, njooni, msipotokea TWASONGA MBELE!
N.b, mabwana zenu E.U,wamefika mkutanoni na wanaona kazi nzuri inayofanywa na serekali ya awamu ya sita (6).
Hakuna awamu ya 6 ...hiyi ni awamu ya ajali ...baada ya kifo cha jiwe
 
Hatukuwapa watu ridhaa ya kuongoza ili wauze raslimali za nchi watakavyo na kwa faida zao!
 
Huyu mama ana matatizo tusiyoyajua, ni mkutano gani wa kisiasa ambao dini yake imechambuliwa?
 
Mkuu siku nyingine usichanganye hotuba ya Rais na hawa wapambe wake akina Jenister , Lipumba na Zitto , tunashindwa kuchambua .

Tuchambue Jenister , Lipumba , Zitto au Rais .
 
Samia apimwe akili, ameruhusu mikutano ili asifiwe au akosolewe?
 
huyo lisu wako alitandikwa risasi na magufuli hao mabalozi wako walichukua hatua gani?
 
Leo tumejua kuchambwa mpaka tukachambika maana hakuna rangi tumeacha kuona..
Tumechaaambwa Kipwani
Tumechaaambwa Kingazija
Tumechaaambwa Kikwere
Tumechambwa Kizimkazi mpaka Mchambawima, Paje mpaka Makunduchi

Lilikosekana dera , kigoma na tarumbeta.. Ila kwa vichambo tuu tumevipokea na bakshish[emoji23]..m!!!!

Kumbe kwenye hii kaya kuna mijitu na vijitu....! Sina hakika Kama kuna kuna watu maana sikusikia wakitajwa popote...

Kilikuwa kikao cha vichambo[emoji23][emoji1544][emoji1550][emoji1550][emoji1550]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Your browser is not able to display this video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…