Uchaguzi 2020 Samia Suluhu Hassan: Askari wa Serikali ya CCM akipiga mtu risasi 3 akamkosa atawajibika

Uchaguzi 2020 Samia Suluhu Hassan: Askari wa Serikali ya CCM akipiga mtu risasi 3 akamkosa atawajibika

Ulitaka waanze kumuhoji na kampeni hizi si atalalamika! Halafu usitumie tuli mi sihusiki wewe acha kuwa na akili mgando..
Matukio mengine yanahitaji muda.. tunajadili hatima ukifata process hutaelewa kamwe.
Kumbe na wewe huwa unatetea unyama ???
 
Maza umeongea upuuzi wa kiwango cha juu sana.kwa kipindi chote hicho umekaa kimya leo umewashwa na nini sasa?achana na mipasho isiyokuwa na ulazima ili uendelee kuheshimiwa.
 
Hebu tujiulize yaliyofuata baada ya shambulizi lile
Kwa akili yako, mission ya kuuwa inayotolewa na kiongozi mkuu wa nchi, Kama mbavyotaka kutuaminisha, anatumwa police officer[emoji23]? Mnapenda kuchukulia vitu easy sana.Risasi 38, kukiwa hakuna ulinzi wowote, gari umesimama commando ashindwe kukuuwa [emoji23][emoji23][emoji23], huyo alikuwa ana winda ndege labda.

NB Ingekuwa Ni agizo kutoka juu, Kama mnavyodai, na kwa mazingira ya tukio, Hali ingekuwa tofauti kidogo.Wachunguzane tu hukohuko ndani ya Chama Chao.
 
Ndugu haya ni maandiko hayajalishi cheo au umaarufu wa mtu kwa Mungu hvyo vyote havina nafasi.Na uzuri uislamu haurembeshi wala kufichaficha ikiwa Mtume amekosolewa nan mwenye cheo kumshinda yeye ktk uislamu?ktk hii dini hakuna kumtukuza mtu isipokuwa Mungu pekee,tafakar chukua hatua
Nayaheshimu Sana maandiko, Ila nusingeweza kukaa kimya na kuvumilia, hata baada ya wewe kuniita sherwani🤔!
Ninachokiona hapa Ni kwamba, unajaribu kutusi watu huku ukijificha kwenye mrengo wa maandiko matakatifu, kitu ambacho sio kizuri kabisa🙏
 
Nan kakwambia shule kila mmoja inamtoa ujinga?wengne wamezidi kuwa mazumbukuku
Kwa iyo Chadema wapange kumuua, Serikali wagome kuchunguza, Magufuli atoe maagizo kwa ndugai kukataa kulipia Matibabu na mwisho CCTV camera kwenye eneo la tukio zitolewe na bunge la ndugai wamvue ubunge Lissu!!


Labda tuseme hujaenda shule, haya mambo yote yataingia akilini mwaki kweli???!
 
Kwa hiyo mama anataka kusema nini?
Yaani kwa mfano Lissu angepigwa lisasi tatu tu na kufariki hapo ndio tungehitimisha kuwa hao waliompiga Lissu ni askari wa serikali ya CCM!
Hiyo ni akili ya uwendawazimu.

Hivi huyo mama anajua kuwa waliomuua Rais Abeid Karume kule Zanzibar walikuwa ni askari wa serikali ya CCM na walimimina zaidi ya risasi kumi mwilini mwake?

Hivi huyo mama anajua kuwa waliomuua aliyekuwa mkuu wa idara ya usalama wa taifa, Imrani Kombe kule Kilimanjaro walikuwa ni askari wa serikali ya CCM na walimimina zaidi ya risasi tatu mwilini mwake?

Mama anapaswa kutuambia kwa nini mpaka leo hii wahusika wa tukio lile la kutaka kumuua Lissu hawajatafutwa, kutajwa, kukamatwa na kushtakiwa na serikali?

Kama mama Samia anawajua wahusika wa tukio lile la shambulizi dhidi ya Lissu basi awataje, na kama hawajui (ama anaogopa kuwataja) ni vyema akakaa kimya, kuliko kuchokonoa mzinga wa nyuki.

Ni bora hata mama Samia angetuambia basi kwa uchache ni akina nani walimlisha sumu Mzee Mangula akiwa ndani ya ofisi kuu za CCM kiasi cha kuponea chupu chupu kupoteza maisha.

Mwisho napenda kumwambia mama Samia anapaswa kufahamu tu, kikulacho kiko nguoni mwako, asitukane mamba kabla ya kuvuka mto, kilichompata Lissu huenda kitakuja au kingeweza kumpata mtu mwingine yoyote katika Tanzania hii ya sasa.

Yote kwa yote, mama Samia anapaswa kujua Karma ipo, na ipo siku itajibu mapigo. Namkumbusha tu Dr. Omar Ali Juma alifariki ghafla kwa mshtuko wa moyo (Cardiac arrest) mwaka 2001 akiwa makamu wa rais wa Mkapa, ambapo miaka 19 baadaye Mkapa naye alifariki ghafla kwa mshtuko wa moyo (Cardiac arrest). Wote hao wanahusishwa na vifo vya wazanzibar kwenye maandamano ya mwaka 2001.
Dr omary alilishwa Sumu baada ya taarifa kuvuja kuwa anajiaandaa kuvunja muungano awe Rais wa Zanzibar huru isiyo koloni la Tanganyika hata mkapa zipo tetesi kuwa nae kifo chake kina utata kutokana na yeye kuwa alikuwa amekasirika akataka kuanika ukweli juu ya mikataba ya madini
 
Hebu tujiulize yaliyofuata baada ya shambulizi lile
Hiyo bado haitoshi kumattack Magufuli moja kwa moja.Tambua kwamba Tz tuna mihimili mitatu, binge Ni mihimili unaojitegemea, kwa mujibu wa katiba.
 
Huu ndio ukweli hakuna askari mwenye mafunzo apige risasi kumi na sita akose hahahah chadema ndio walumpiga risasi lissu kisa Urais! Lissu amepigwa na watu wa chadema
Alafu watu wa Chadema ndo walizuia pia Lissu kulipiwa matibabu na serikali????

Watu wa Chadema ndo walizuia Lissu kuchangiwa damu?????

Watu wa Chadema ndo walizuia watu kuvaa tshirt za pray for Lissu na kumfanyia maombi viwanja vya sinza pale?????

Watu wa Chadema ndo walienda mbali zaidi hadi kumvua Lissu Ubunge?????

Watu wa Chadema ndo hadi leo hawajamuhoji yeyote yule juu ya tulio laLissu kupigwa risasi????

Watu wa Chadema ndio walioenda eneo la tukio na kutoa CCTV camera zote????

CCM kweli damu ya Lissu inawatesa sana!!! Hadi mnatia huruma!!
 
Lissu itakuwa alipigwa risasi na Wadeni wake au alikua anachukua wake za watu, ndiyo hayo matatizo kajisababishia!!
Ni kweli alipigwa na wadeni na wale alikwachukulia wake zao. Walimfuatilia muda mrefu hadi aliwatolea taarifa polisi, wakamfuata hadi Dodoma, wakaondoa ulinzi area C, wakammiminia risasi, wakang'oa CCTV camera, wakazuia asichangiwe damu, wakazuia albadri zisisomwe, wakazuia malipo yake ya matibabu, wakazuia polisi wasifanye uchunguzi wowote, wakazuia mzuia Ndungai asijua mbuge wake yuko wapi. Huyo mke Ni mke wa aina gani? First Lady? Hapana! Huyu mama anajihesimu. Makamu wa Rais? Hapana! Huyu Ni muadilifu! Ni nani Sasa huyo?
Kama Ni mdeni, Lisu anafanya biashara gani? Ni wakili, Ndiyo Ni wakili. Inamaana ameshindwa kutekeleza jukumu la uwakili, Kuna mteja kashindwa kesi Sasa ameamua kufanya haya yote kushirikiana na kamanda anyepanga walinzi, akamtuma house boy wa Kalemani anyofoe camera, akamshawishi spika amvue Lisu ubunge? Huyo mteja anakesi gani? Ya madai au jinai? Tumuachie Mungu, yeye anajua kwanini alimponya, kwanini ameteuliwa kuwa Mgombea urais, yeye anajua kwanini watu wanavutiwa na ujio wake na kumiminika kwa wingi katika mikutano yake, Mungu anajua kwanini dunia imemulika macho yao kwa uchaguzi huu, Mungu anajua kwanini kaka wa Taifa wa Lupaso ametangulia mbele ya haki, Mungu anajua kilakitu kuhusu uchaguzi huu, tumpe muda.
 
Haya co maneno yangu kama unayataka yapo ktk suratinnaasi, ukiona binaadamu yoyote anashabikia lile jaribio la mauaji kwa namna yoyote ile ujue huyo hana tofauti na shetani
Nayaheshimu Sana maandiko, Ila nusingeweza kukaa kimya na kuvumilia, hata baada ya wewe kuniita sherwani[emoji848]!
Ninachokiona hapa Ni kwamba, unajaribu kutusi watu huku ukijificha kwenye mrengo wa maandiko matakatifu, kitu ambacho sio kizuri kabisa[emoji120]
 
Kumbe na wewe huwa unatetea unyama ???
Kuwa muelewa sisemi natetea lissu kupigwa risasi ila naona Kuna utofauti serikali kuhusika moja kwa moja kwenye tukio lake.. ukiangalia anaehusishwa zaidi ni rais Tena ambae anawatu wenye weledi mpana wanaoweza kufanya tukio timilifu zaidi ya kile kilichowaunganisha!.. tukio la lissu ni tata Sana na ndio maana hata serikali hawataki kukurupuka hovyo maana linaweza tumika kisiasa!.. tanua ubongo wewe usikariri..
 


=======
Mama Samia Suluhu Hassani ambaye ni mgombea mwenza wa kiti cha urais kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM) amesema kuwa anawaomba wafanye kampeni kwa amani wakipita wawasikilize wala wasigombane nao.

Amesema kuwa wapo wagombea watakwenda kuwaambia kuwa walivunjwa miguu na mwingine alimsikia akisema kuwa alipigwa risasi 16.

''Watakuja kuwaambieni wameunjwa miguu lakini waulizeni ilikuwaje wakavunjwa miguu, wengine jana nilisikia mmoja anasema amemimiwa risasi 16 nataka niwaambie huyo sio askari wetu wa serikali ya chama cha Mapinduzi, askari wetu akipiga mtu tatu akamkosa atawajibika sikwambii askari aliefundishwa akapiga 16 huyo mtu atoke mzima".
Tusaidie kuwaambia maana watufanya Sisi mapoyoyo
 
kuna dhambi nyingi lakini mbaya moja wapo ni kumdhania mtu.

sisi kama binadamu wa kutumia akili tunaamini serikali ama system ina mbinu nyingi sana za kutumia, kumzima mtu, kuliko hiyo yenye kelele na misuko suko mingi, na hata kama itabidi kuitumia si kwa watu ambao hata harufu zao zitasikika.
mara bashite wa watu masikini, leo heri na nyauringo wanatajwa, keshokutwa atatajwa mtu wa kukodi kutokea israel nk. yote ilimradi kubahatisha tu.

lakini jambo la msingi linabaki pale pale, lissu alishambuliwa na watu gani, kwa lengo gani??? ni hao hao ambao yuko nao sasa hapa nchini kisha wanampa na ulinzi au wengine!!!
Tundu alishambuliwa na hao aliowatuhumu na sasa analindwa na mungu pamoja na malaika
 


=======
Mama Samia Suluhu Hassani ambaye ni mgombea mwenza wa kiti cha urais kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM) amesema kuwa anawaomba wafanye kampeni kwa amani wakipita wawasikilize wala wasigombane nao.

Amesema kuwa wapo wagombea watakwenda kuwaambia kuwa walivunjwa miguu na mwingine alimsikia akisema kuwa alipigwa risasi 16.

''Watakuja kuwaambieni wameunjwa miguu lakini waulizeni ilikuwaje wakavunjwa miguu, wengine jana nilisikia mmoja anasema amemimiwa risasi 16 nataka niwaambie huyo sio askari wetu wa serikali ya chama cha Mapinduzi, askari wetu akipiga mtu tatu akamkosa atawajibika sikwambii askari aliefundishwa akapiga 16 huyo mtu atoke mzima".
Usisahau kama kuna Mungu
 
Kuwa muelewa sisemi natetea lissu kupigwa risasi ila naona Kuna utofauti serikali kuhusika moja kwa moja kwenye tukio lake.. ukiangalia anaehusishwa zaidi ni rais Tena ambae anawatu wenye weledi mpana wanaoweza kufanya tukio timilifu zaidi ya kile kilichowaunganisha!.. tukio la lissu ni tata Sana na ndio maana hata serikali hawataki kukurupuka hovyo maana linaweza tumika kisiasa!.. tanua ubongo wewe usikariri..
Mlitaka afe kwa risasi zenu kwa sababu Mungu ni mkuu kamponya kuwaonyesha Mungu ni mkubwa kuliko madaraka yenu.

Nyoyo zenu zimejaa Sonona kwa Mungu kuwaumbua na huo unyama wenu, miili yenu mizima lakini nyoyo zenu zimekufa kwa kujitwisha Uungu wa kutoa uhai wa wenzenu.

Mnachopaswa kutambua Mungu ni mwema sana.
 
Back
Top Bottom