Shaka apiga ‘stop’ agizo la kuzuia bodaboda, bajaji kuingia katikati ya Mji wa Dar
Huu ni ule ule upumbavu wa kusema rais anapotoshwa na washauri wake utadhani rais ni zuzu asiye na akili. Rais ndiye anajichonganisha mwenyewe. Nchi yetu system ya uongozi imepitwa na wakati. Haiwezekani rais ndiye awe think tank wa kila kinachotokea kwenye nchi. Akiambiwa inahitajika system overhaul anajitoa akili na kusema eti apewe muda aujenge uchumi wakati kujenga uchumi bila kwanza kuweka misingi mizuri ya uongozi ni kitu kisichowezekana.
Rais hajasema watu wanyaing'nywe bidhaa zao,
Hajasema wapelekwe Porini,
Hajasema wanyanyaswe ,

Hivyo Chama kiko sahihi,
 
Mtoto wa maskini?!

Huyo wa mtoto wa maskini ni yupi... mmiliki wa ajaji/bbodaboda, dereva au anayepanda bajaji/bbodaboda?

Kama anayepanda... HAPANA!

Labda kama ule uchumi wa kati waliotuambia The World Bank, ndo upo hapo Daslam!!
Africa ni Bara Masikini,
Wewe ni mwana wa Africa
Hata wewe ni masikini,
 
Boda boda hawezi kukaa sehemu pasipo na muingiliano wa Watu.
Kupangwa upya kwa wafanya biashara automatically kutafanya Boda Boda nao kujipanga upya hata kama wasipopangwa.
 
Makala kwao mambo safi anaamini watz wote ni mambo safi.Ongezeko la
Machinga na bodaboda chanzo ni ccm kuuwa kilimo
 
CCM imepata viongozi imara sana,
Leo nimeona nguvu ya chama dhidi ya dola,

Hongera sana Shaka, endelea kutupigania ndg zako,
Hahahahah......Upumbavu mwingine Wa baadhi ya wanaJF bana! Utadhani kabla Shaka hajaja na press yake hakukaa na uongozi wa mkoa wa DSM kuteta haya mambo na kupata cha kuongea leo mbele ya waandishi wa habari. Alichokiongea Shaka leo Makala anataarifa nacho na SSH anataarifa nacho. It's a collective decision.
Hata issue ya machinga walilijadili sana pembeni hatimaye ikakubalika Amos Makala aje nalo front ndo maana Shaka kimyaaaaaa. Wachana na blackmailing press!
 
Hivi kwanini ccm wanaona raha sana wanapotamka umaskini!!!? Umaskini wameutengeneza wao kama chama tawala na sasa wanautumia kama mtaji wa kisiasa,,,,basi tu sema wtz wengi ni mbuzi,,wanyonge kama alivyowabatiza Magufuli nao wakashangilia utadhani unyonge ni sifa njema
 
Katibu wa Halmashauri kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Ndugu. SHAKA HAMDU SHAKA leo Oktoba 31 atazungumza na waandishi wa vyombo vya Habari kuanzia saa 6 mchana ofisi Ndogo za CCM - LUMUMBA Dar es salaam.

=====

CCM yapiga ‘stop’ agizo la kuzuia bodaboda, bajaji kuingia mjini

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeagiza marufuku ya waendesha bodaboda na bajaji kutofika au kufanya shughuli zao katikati jiji la Dar isitishwe mara moja kwa kuwa si muafaka lakini pia imetolewa kwa kukurupuka.

Kauli hiyo ya CCM imekuja siku moja baada ya Kamishana Msaidizi wa Polisi, Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Abdi Issango kunukuliwa akipiga marufuku bodaboda na bajaji wote kuingia mjini na wale walioko mjini watoke isipokuwa bajaji za walemavu. Marufuku hiyo ilikuwa ianze kutekelezwa rasmi tarehe 1 Novemba mwaka huu.

Aidha, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo tarehe 31 Oktoba, 2021, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka amesema marufuku hiyo ilitolewa bila kuzingatia taratibu za msingi zinazopaswa kufanya uamuzi unaogusa masilahi ya wananchi.

Amesema jambo hilo limeleta taharuki na CCM imepokea kwa mshangao mkubwa kwani ni jambo ambalo halikuwa na matayarisho mithili ya watu kukurupuka katika kutoa maamuzi hayo.

“CCM kimepokea na kufuatilia malalamiko ya wananchi mbalimbali ikiwamo, machinga, waendesha bodaboda, sanjari na malalamiko hayo, CCM kinaungana na Rais Samia katika dhamira yake ya kuona nchi yetu inapangwa vizuri na kuwa kivutio kwa kuwapanga vema machinga na wafanyabiashara wengine.

“Tuliona sasa Rais amewajali na kuwathamini kwa kutoa maelekezo kwamba watoa huduma hizo wapangwe katika maeneo rafiki,” amesema.

Amesema Chama kimeagiza Mamlaka za kiserikali mkoa wa Dar es Salaam zinazohusisha viongozi na watendaji, vyombo vya dola na mamlaka zingine zenye majukumu ya kusimamia usafiri na usafirishaji maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam chini ya mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na wadau wengine katika sekta hiyo, zikutane kwa haraka iwezekanavyo.

“Lengo ni kuangalia iwapo kuna changamoto zozote zilizojitokeza ili zijadiliwe na kupata ufumbuzi wa muda mfupi, wa kati na mrefu ama ufumbuzi wa kudumu ili kutoathiri na kubughudhi ustawi wa shughuli za makundi ya watu wanaohusika.

“Chama kinasisitiza kwa kuzingatia umuhimu wa suala hili, kitafuatilia na kuhakikisha

utekelezaji huu unafanyika kwa mafanikio makubwa,” amesema.

Pia soma:

Thread 'Kuanzia Novemba Mosi Bajaji na Bodaboda marufuku kuingia Mjini' Kuanzia Novemba Mosi Bajaji na Bodaboda marufuku kuingia Mjini
CCM CHAMA,

Hongera sana Shaka H Shaka
 
Katibu wa Halmashauri kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi Ndugu. SHAKA HAMDU SHAKA leo Oktoba 31 atazungumza na waandishi wa vyombo vya Habari kuanzia saa 6 mchana ofisi Ndogo za CCM - LUMUMBA Dar es salaam.

=====

CCM yapiga ‘stop’ agizo la kuzuia bodaboda, bajaji kuingia mjini

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeagiza marufuku ya waendesha bodaboda na bajaji kutofika au kufanya shughuli zao katikati jiji la Dar isitishwe mara moja kwa kuwa si muafaka lakini pia imetolewa kwa kukurupuka.

Kauli hiyo ya CCM imekuja siku moja baada ya Kamishana Msaidizi wa Polisi, Mkuu wa Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Abdi Issango kunukuliwa akipiga marufuku bodaboda na bajaji wote kuingia mjini na wale walioko mjini watoke isipokuwa bajaji za walemavu. Marufuku hiyo ilikuwa ianze kutekelezwa rasmi tarehe 1 Novemba mwaka huu.

Aidha, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo tarehe 31 Oktoba, 2021, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka amesema marufuku hiyo ilitolewa bila kuzingatia taratibu za msingi zinazopaswa kufanya uamuzi unaogusa masilahi ya wananchi.

Amesema jambo hilo limeleta taharuki na CCM imepokea kwa mshangao mkubwa kwani ni jambo ambalo halikuwa na matayarisho mithili ya watu kukurupuka katika kutoa maamuzi hayo.

“CCM kimepokea na kufuatilia malalamiko ya wananchi mbalimbali ikiwamo, machinga, waendesha bodaboda, sanjari na malalamiko hayo, CCM kinaungana na Rais Samia katika dhamira yake ya kuona nchi yetu inapangwa vizuri na kuwa kivutio kwa kuwapanga vema machinga na wafanyabiashara wengine.

“Tuliona sasa Rais amewajali na kuwathamini kwa kutoa maelekezo kwamba watoa huduma hizo wapangwe katika maeneo rafiki,” amesema.

Amesema Chama kimeagiza Mamlaka za kiserikali mkoa wa Dar es Salaam zinazohusisha viongozi na watendaji, vyombo vya dola na mamlaka zingine zenye majukumu ya kusimamia usafiri na usafirishaji maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam chini ya mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na wadau wengine katika sekta hiyo, zikutane kwa haraka iwezekanavyo.

“Lengo ni kuangalia iwapo kuna changamoto zozote zilizojitokeza ili zijadiliwe na kupata ufumbuzi wa muda mfupi, wa kati na mrefu ama ufumbuzi wa kudumu ili kutoathiri na kubughudhi ustawi wa shughuli za makundi ya watu wanaohusika.

“Chama kinasisitiza kwa kuzingatia umuhimu wa suala hili, kitafuatilia na kuhakikisha

utekelezaji huu unafanyika kwa mafanikio makubwa,” amesema.

Pia soma:

Thread 'Kuanzia Novemba Mosi Bajaji na Bodaboda marufuku kuingia Mjini' Kuanzia Novemba Mosi Bajaji na Bodaboda marufuku kuingia Mjini
Ccm inahujumiwa
 
NUKUU: KATIBU WA NEC ITIKADI NA UENEZI CCM TAIFA SHAKA HAMDU SHAKA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO TAREHE 31/10/2021

"Chama Cha Mapinduzi ndicho kimepewa dhamana ya kuongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hivyo ndicho chenye mkataba na wananchi nini kifanyike
Eneo kubwa na la msingi tulioahidi watanzania ni namna ya kusimamia haki na usawa na fursa za maendeleo zinatolewa wakati wote na kuhakikisha upatikanaji wa Ajira kwa Vijana"

Rais Samia alitoa malekezo kwa viongozi kuwapanga upya wamachinga,Rais Samia alisisitiza upangaji huo uambatane na wafanyabishara hao kupewa maeneo rafiki ya kufanyia biahara hizo"

"Chama Cha Mapinduzi tunawapongeza wafanyabiashara wadogo almaarufu machinga kwa mapokeo yao mazuri ya maelekezo ya kuhamia kwenye maeneo rasmi waliyotengewa kufanyia kazi"

Chama cha mapinduzi inatoa kauli ifuatayo 1 marufuku ya waendesha bodaboda au bajaji sio muafaka bali ingetumia taratibu shirikishi kwa wananchi na viongozi wao hivyo CCM inasitisha mara moja jambo hilo"

"Chama Cha Mapinduzu kinaonya kuhusu utaratibu ulioanza kuibuka kwa mtu au mamlaka kuanza kutoa kauli au maagizo yasiyokihaki hali ambayo inaibua sintofahamu kwa wananchi wetu"

"Mhe Rais Samia Suluhu Hassan alitoa malekezo kwa viongozi kuwapanga upya wamachinga,Rais Samia alisistiza upangaji huo uambatane na wafanyabishara hao kupewa maeneo rafiki yakufanyia biahara zao"

"Kitendo cha kuwahamisha wafanyabiashara wadogo bila kuwawekea mazingira rafiki na mazuri. watakaofanyia biashara zao ni marufuku na haikubaliki
Chama Cha mapinduzi tunazielekeza kamati za siasa za Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuwa maelekezo ya Mhe. Rais kwenye mikoa yao yanatekelezwa kwa malengo tarajiwa ikitokea haziendi vema kweye jambo hili na hazioneshi mafanikio kama ilivyo malengo ya Mhe.Rais Samia basi zitawajibika"

#KaziInaendele

IMG-20211031-WA0000.jpg


IMG-20211031-WA0001.jpg


IMG-20211031-WA0002.jpg


IMG-20211031-WA0003.jpg


IMG-20211031-WA0004.jpg
 
Akikamatwa mwenye pikipiki kwa kuingia mujini, Shaka hataenda field kuzuia ukamataji.

Tufikie sehemu taaluma (badala ya emotions) ziamue mambo yetu! Ni tabia hii ya maamuzi yanefanya Dar kuwa mji mkubwa usiopangwa ktk afrika mashariki na kati. Makazi yasiyopangwa!!
 
Back
Top Bottom