Utiaji saini Mkataba wa Tanzania na DP World: Mkataba utakuwa wa miaka 30 na utendaji kazi wake utapimwa kila baada ya miaka 5 na sio miaka 100
Haya mambo kwako mama ni mazito ni sawa na kumpiga chuma jiwe. TEC hawawezi kuudhuria kama vile vifungu walivyovikataa havijafanyiwa marekebisho, hiyo ni sawa na kujipaka kinyesi. Hapo vipengere vimesharekebishwa na wameviona jinsi vilivyorekebishwa na ndio maana wamehudhuria. TEC noma.
Tunashukuru kwa TEC kuunga mkono serikali .Mama samia anaupiga mwingi 2025- 2030 twende na Samia.
 
Matatizo ya umeme itakuwa historia
Tutauza umeme nje
 
Mimi namsikiliza mkurugenzi wa TPA na tunaamini anachokisema ni kweli kuwa wamesikiliza maoni ya watu ..sasa ni miaka 30 sio mia au milele…lakini bado tutakuwa na shauku ya kuona hayo marekebisho!

Kwenye hili TEC,Chadema,Slaa,Mdude na Mwambukusi wanastahili kupongezwa sana
Huo mkataba wa miaka 100 na milele haujawahi kusainiwa usipotoshwe na porojo za wapinzani
 
Mmh! Hata kwenye gesi ya Mtwara tuliambiwa sasa Mtwara itakuwa kama NewYork na umeme utakuwa bure kama mwanga wa jua.

Wakati kiwanda cha Dangote kinajengwa, tuliambiwa bei ya sementi itapungua na kuwa sh elfu 5.

Lakini Sasa yako wapi??
 
Nimefuatilia hafla ya utiaji saini kati ya Serikali yetu na DP World, Nimegundua kuwa Mwarabu wa DP World ni kibaraka wa MABEBERU wazungu.

Kuna beberu anamwelekeza mwarabu Mahali pa kusaini Kisha naye anasaini.

Ukimtizama, ni mtu mwenye wasiwasi na haraka sana.

Na mbaya kuliko yote, hataki na amekwepa picha ya pamoja.

Kumbe vita ya mataifa makubwa ndo inatuhenyesha Nchi za kiafrika.

Naanza kuona connection kati ya Royal tour na DP world.

Magu: Vita ya kiuchumi ni ngumu sana.

Tutakukumbuka Magufuli.

R. I. P.
 
Mikataba inayosainiwa leo ni baina ya Nchi mwenyeji, mkataba wa ukodishaji na uendeshaji wa gati namba 4-7 lakini pia kutakuwa na sehemu ambayo gati 0-3 zitaendeshwa kwa ushirikiano wa pamoja kati ya TPA na kampuni ya DP World kwa shughuli za kibiashara na shughuli za kiserikali.

Mikataba hii haihusishi eneo lote la bandari wala bandari zingine za Tanzania. Upande wa gati namba 8-11, mchakato wa kumpata mwendeshaji mwingine umeshaanza kufanyika na akipatikana mwekezaji mwingine mwenye sifa atakabidhiwa na sio DP World.
Hongereni sana Sauti ya Watanzania, Special thanks to Mwabukusi, Mdude, Dr Peter Slaa and much thanks to TEC na watanzania woote.

Uwekezaji tunauhitaji kuboresha huduma na tija ya bandari.

Kama majibu haya yangetoka tangu mwanzo kulikuwa hakuna ugomvi.
Kila la Kheri Rais Dr Samia na Watanzania tunaunga mkono.

Ila isije kuwa ni changa la macho mwanaharamu apite.
 

Attachments

  • CA973065-5532-4991-AE34-766224E8DE35.jpeg
    CA973065-5532-4991-AE34-766224E8DE35.jpeg
    42.4 KB · Views: 4
Back
Top Bottom