Rais hajashauriwa na wenye elimu tu, kwa mkataba kama ule hata wasio na elimu waliona wazi kuwa tunapeleka nchi shimoni. tungekuuliza wewe sana ambaye unaumia kwanini vipengele vinavyowapendelea waarabu vimeondolewa. imeisha hiyo.
Km unaamini asie na elmu anaweza kumshauri Rais basi ndio ujue umuhimu wa kuacha pombe za moshi.
Utadhurika kabla ya siku zako.
Acha gongo dogo
 
Simba keshokutwa kama DP World Dar.
Meli 400 za DP World kuja moja kwa moja bandari ya Dar.
zikija tutashukuru, hata mimi magari nitakuwa naagiza uarabuni sasa kwa bei ndogo kabisa na yanafika kwa uwepesi kwasababu wao ndio wanaendesha. ila sio kwa mkataba ule mliokuwa mnataka kututumbukiza shimoni., na tusingestuka ninyi mlishakubali kuuza nchi. nje ya mkataba ule, yaani sasaivi, hata wangewapa DSM port yote mi sina shida.
 
Km unaamini asie na elmu anaweza kumshauri Rais basi ndio ujue umuhimu wa kuacha pombe za moshi.
Utadhurika kabla ya siku zako.
Acha gongo dogo
wananchi hadi darasa la saba wamepiga kelele, na Rais amesema amezingatia maoni ya kila mtu aliyesema. hao kina mdude hawana hata elimu ya chuo, ila wana akili kuliko wewe. though najua kwa hakika hata wewe mimi nimekuzidi elimu. ila sina majivuno ya elimu kama wewe.
 
Kuna mambo mawili serikali ya samia inachanganya kulazimisha mkataba mbaya kati ya tanzania na dubai kuhusu bandari. Ule mkataba na dubai wa kibeberu kuhusu wao kupewa hati miliki miradi ya kujenga na kuendesha bandari zetu zote umekataliwa na wananchi. Kwanza mkataba ulikua kinyume na sheria ndio maana wakataka kubadili sheria jambo halikufanyika. Sasa kupewa DPWorld kuendesha bandari hatuna uhakika ni chini ya huo mkata au ni kwa msingi wa kandarasi iliyotangazwa na bandari. Ingefaa jambo hili liwekwe wazi na kama hakuna mahusiano masharti ya DP kupewa kuendesha bandari ya dar es Salaam yawekwe wazi kwa wananchi kuona.
Sababu ya hawa wahuni kulazimisha uwekezaji wa DP world hazina wala uzito ila kuonesha uzembe mtupu na kutowajibika kwa viongozi. Wanatoa mfano wa ufanisi wa mombasa bandari shindani na dar es Salaam ila jambo hawasemi mombasa haina uwekezaji wa nje bali inaendeshwa na shirika la bandari la kenya KPA.
 
Bado kuna vitu havipo wazi wanawekeza vitu vya thamani Gani ??
Na wakodisha Kwa $ ngapi Kwa Mwaka kwa hiyo miaka 30 tunategemea kupata Kiasi Gani , na hiyo kupitia utendaji wao WA miaka 5 tusiporidhika , tukavunja mkataba nini madhara kwetu na pia kwao Kwa kushindwa kushindwa kutekeleza masharti ya mkataba.
Huu mkataba naufananisha na Ile hadithi ya naomba niweke shingo Tu kitandani mwishowe ni kusukumizwa kabisa.
 
Safi sana.

Asante Yesu nchi yetu sasa imejifunza kuweka siasa za uzandiki pembeni na kuanza kufanya mambo ya msingi kwa maendeleo ya kweli

Kazi iendelee
Nakubaliana na raisi SSH kuwa wananchi wamekuwa na mchango mkubwa kwa kufikia makubaliano. Isingekuwa hivyo, tusingepata mkataba huo. Kwa hiyo washukuriwe wote walioshiriki kukosoa MOU ambayo iliandikwa na kutiwa sahihi kiovyo kabisa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…