Wengi wanaopiga kelele kuhusu bandari ni wapitisha mizigo kimagendo bandarini

Wengi wanaopiga kelele kuhusu bandari ni wapitisha mizigo kimagendo bandarini

Mkuu wa tz wengi hawana msimamo wao kila kitu wakiambiwa na mwanasiasa wanakieka kichwani na kuanza kubwabwaja..
Kampuni kibao tunaendesha wenyewe zinafanya utumbo tuh
.1.ttcl
2.atcl
3.Tanesco
4 bandari nk
Zote izo tuko nazo wenyewe na kila cku zinapata hati chafu na ufisadi ulikithir.afu bdo jitu linajidai kwan hatuezi jiendesha wenyewe 🥸
Nadhani changamoto ni elimu ya ujasiriamali wengi wanao simamia hizo kampunin wamesoma kuhusu biashara na siyo kufanya biashara yaani entrepreneurship skills
 
Kwa hio wataka kusema tpa haina makosa ila tra ndio inafanya wizi
mleta mada anashinswa kutofautisha majukumu ya TRA na TPA mulize yeye sijasema chochote kuhusu TRA kufanya wizi bandari hii ni mada Mpya unataka kuleta.

Pale bandari hakuna wizi ni uzushi tu wakalazimisha bandari iuzwe nakama wizi upo basi hawa DP uwezo wakuzua hao wezina hawana
 
Nadhani changamoto ni elimu ya ujasiriamali wengi wanao simamia hizo kampunin wamesoma kuhusu biashara na siyo kufanya biashara yaani entrepreneurship skills

Inshort serikali na biashara kwa tz ni ngumu..hata kandarasi zinazojenga ma shule na vitu vya umma je?mara ngapi tumeona chumba kimoja cha darasa kimejengwa kwa million 200 na zile hostel hata mwaka hazina zikapata ufa tukaambiwa ni expansion joint [emoji1787][emoji1787][emoji1787]yaan mifano mingi tunayo jinsi tunavoboronga
 
Mi sio mnufaika ila wasiwasi wangu ni kwamba tunaingia mkataba usiokuwa na time frame

Kingine kama wasimamizi wakubwa wa huu mkataba kwa maana ya Rais na Waziri mwenye dhamana wote ni wakazi wa upande wa pili, imekuaje waingize bandari za Bara katika ubinafsishaji na upande ule haujaingia ilihali bandari ni suala la Muungano?

Ikiwa kuna faida na hawatuuzi kwenye gunia basi nashauri upande ule nao ujumuishwe, lakini pia muda wa mkataba ujulikane lini unaanza lini unaisha.
 
mleta mada anashinswa kutofautisha majukumu ya TRA na TPA mulize yeye sijasema chochote kuhusu TRA kufanya wizi bandari hii ni mada Mpya unataka kuleta.

Okey ila hao dp world wakiendesha hio bandari mapato c yanaongezeka mara mbili yatunavo pata tena kwa ufanisi mkubwa hapo shida ikowapi
 
Baada ya kufanya utafiti mdogo imebainika kuwa wengi wa wapiga kelele kuhusu bandari ni wale walio zoea kupitisha mizigo kimagendo yaani kupitisha mizigo kwa kukwepa kulipa malipo halali.

Lakini wengine ni lile kundi ambalo lina danganya nyaraka mfano mtu kaingiza kontena 100 akidai kwamba ndani zina mtumba lakini kati ya hizo kontena 100 kuna kontena 20 au 40 ndani zina magari ya kifahari mtakumbuka makontena yaliyo kamatwa ndani yakiwa na range rover mpya wakati yalisadikika ni mitumba ya furniture.

Kundi lingine ni wale wanufaika wa rushwa na wizi hapo bandarini katika uendeshaji na usimamizi na ndio maana kama mnakumbuka hata wakati wa zama za magufuli kulikuwa na kesi ya mita za kusoma mafuta kuhujumiwa kila mara

Lakini pia kuna taasisi za kidini ambazo pia kupitia msamaha wa kodi zilikuwa zina pitisha bidhaa binafsi kwa mgogo wa taasisi wakati huo kilichomo ndani ya kontena sicho kunacho paswa kuwepo

Hao ndio wengi wanapiga sana kelele maana wanaziona kabisa dalili ya mirija yao kuziba

Wanzania ni wezi na wabinafsi hatuna uwezo wa kusimamia miradi ya serikali huo ndio ukweli

NASHANGAA KWANINI TRENI YA MWENDO KASI DAR -MORO BADO HAIJAANZA KUFANYA KAZI HADI SASA = JIBU hujuma za wenye mabasi ya abiria kwa kushiriliana na TRC

#NASHANGAA KWANINI MAPENDEKEZO YA NAULI YA TRENI YA MWENDO KASI NAULI ZILIKUWA GHALI MARA MBILI YA MABASI =JIBU Hujuma za wenye mabasi ya abiria kwa kushirikiana na TRC

Kwa style hii bora tuwape wawekezaji nalubariki hilo 100%
Sasa wamepatikana.
Tena wengine walikuwa wamegeuza Bandari ndio shamba la bibi..

Serikali kamatia hapo hapo.
 
hoja yako nzima ni upuuzi , napitisha kontena zaidi ya 200 dar kila wiki za wateja , kwanza suala la mapato ni la TRA sio port , pili kuna teknolojia mpya za kuzuia udanganyifu ila serikali ndio inajivuta , kenya , port of mombasa siku hizi deal yyte huwezi piga kuna scanners hatari , mbona TPA na TRA wasiweke ??? Kwa hiyo jibu la matatizo yetu ni mwarabu ???? twaelekea neo colonialism kwa mwendo huu
 
Mi sio mnufaika ila wasiwasi wangu ni kwamba tunaingia mkataba usiokuwa na time frame

Kingine kama wasimamizi wakubwa wa huu mkataba kwa maana ya Rais na Waziri mwenye dhamana wote ni wakazi wa upande wa pili, imekuaje waingize bandari za Bara katika ubinafsishaji na upande ule haujaingia ilihali bandari ni suala la Muungano?

Ikiwa kuna faida na hawatuuzi kwenye gunia basi nashauri upande ule nao ujumuishwe, lakini pia muda wa mkataba ujulikane lini unaanza lini unaisha.

Hakuna kitu icho kwenye mkataba kausome vizur...afu kingine hio bandari inatunufaisha sisi wa bara na itachangia mapato makubwa zaid kwenye budget ya serikali huoni hayo ww unaona chuki tuh mkuu
 
Dunia inashift kuelekea kwenye Artificial intelligence kwa kasi sana,twende kazi DP World.
 
Okey ila hao dp world wakiendesha hio bandari mapato c yanaongezeka mara mbili yatunavo pata tena kwa ufanisi mkubwa hapo shida ikowapi
Sio kweli kwasabu DP sio watoza ushuru wa forodha hapo bandari hadi mapato yaongezeke malambili hizo pesa watazitoa nfuko mwao?
 
hoja yako nzima ni upuuzi , napitisha kontena zaidi ya 200 dar kila wiki za wateja , kwanza suala la mapato ni la TRA sio port , pili kuna teknolojia mpya za kuzuia udanganyifu ila serikali ndio inajivuta , kenya , port of mombasa siku hizi deal yyte huwezi piga kuna scanners hatari , mbona TPA na TRA wasiweke ??? Kwa hiyo jibu la matatizo yetu ni mwarabu ???? twaelekea neo colonialism kwa mwendo huu

Nyie ndio mnapitisha kimagendo mnaona uendeahaji mpya ukija utawabana [emoji1787][emoji1787][emoji1787]hakuna ujanja janja tena ..
 
Sio kweli kwasabu DP sio watoza ushuru wa forodha hapo bandari hadi mapato yaongezeke malambili hizo pesa watazitoa nfuko mwao?

Umeona xx wewe waongea kwa hisia ila kwenye mkataba suala la mapato liko na tumekubaliana..xx kama wataka tuongee mambo ambayo ayapo kwenye mkataba sawa
 
Nyie ndio mnapitisha kimagendo mnaona uendeahaji mpya ukija utawabana [emoji1787][emoji1787][emoji1787]hakuna ujanja janja tena ..
pale TPA hamna janja yyte , pili mizigo hulipwa in advance before shipping na wateja , wanao kuja pale kulipa physically ni wachache na wengi huwa ni importers binafsi wa magari , nina zaidi ya mwaka na nusu sijatua pale physically , invoices zinatembea tu kwa network yao , makarani walipo pale these days hata siwajui , sasa naibaje , unajua kwa mwezi komntena kama 1000 napiga hela kiasi kipi ndio nikimbilie mashilingi shillingi ya laana kisa wizi ??? mawakala wa waarabu mna poteza nchi nyie , dili zinapigwa agencies zote mpaka usalama , mbona makaa mjini ipo , inapitaje mikoa yote hiyo kama sio rushwa ??? kwa hyo tubinafsishe pia police ??? acha fikra za kimaskini
 
Na ndio hapo hapo ambapo watanzania mnafeli kujifanya mnahitaji takwimu za kisomi na kuachana na ku deal na tatizo

Utatuzi na ubainifu wa matatizo ni vitu viilivyo kuwepo kabla hata ya hizo porojo za methods na methodology unazo taka ? Ina maana matatizo yalikuwa hayatatuliwi? Acha kujifanya msomi wakati umekalili.
Hapa ndipo unaanguka Mkuu wangu, nani kasema 1. Mimi msomi? 2. Nani kasema hapo awali methodology hazikutumika katika kubaini chanzo cha tatizo ama kupata utatuzi wa Tatizo?

Vipi tuendelee?
===
Lengo la badiko langu ulilonukuu, ni kuepusha hisia za mtu kutumika kudanganya kwa kisingizio cha taratibu za utafiti ambazo hajaziweka wazi!
 
Umeona xx wewe waongea kwa hisia ila kwenye mkataba suala la mapato liko na tumekubaliana..xx kama wataka tuongee mambo ambayo ayapo kwenye mkataba sawa
Dp kama wanafanya operations pale bandarini TPA wameshindwa nini kwanini tuwaondoe TPA kwanini tusiwawezeshe TPA waongeze mapato kama ni kuongeza meli na mizigo kuwa mingi kwanini hawa DP?

unakaka kunubia kwamba hawa DP watakuwa wanazipigia simu meli zije kushusha hapa Dar hata kama mizigo inaenda Bara lingine ili tuongeze mapato?
 
pale TPA hamna janja yyte , pili mizigo hulipwa in advance before shipping na wateja , wanao kuja pale kulipa physically ni wachache na wengi huwa ni importers binafsi wa magari , nina zaidi ya mwaka na nusu sijatua pale physically , invoices zinatembea tu kwa network yao , makarani walipo pale these days hata siwajui , sasa naibaje , unajua kwa mwezi komntena kama 1000 napiga hela kiasi kipi ndio nikimbilie mashilingi shillingi ya laana kisa wizi ??? mawakala wa waarabu mna poteza nchi nyie , dili zinapigwa agencies zote mpaka usalama , mbona makaa mjini ipo , inapitaje mikoa yote hiyo kama sio rushwa ??? kwa hyo tubinafsishe pia police ??? acha fikra za kimaskini

We ndio una fikra za kimasikini tena za kifukaraaa kabisa ..hao matajiri wakubwa kwann wanaingia ubia kwenye makampuni na watu wengine?
Wizi wa bandari hauwezi kuisha kama mwenyekiti wa bodi ya bandari alikiri juu ya wizi uliokuepo baada ya ripoti ya cag kutoka.
We utasema nn kuisafisha
 
Back
Top Bottom