Uchaguzi 2020 Yaliyojiri upigaji kura za maoni za wagombea wa Ubunge na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia CCM - Julai 20-21, 2020
20 Julai 2020
Tunduma, Songwe
Tanzania

SILINDE KAWAPIGIA MAGOTI CCM KASEMA HAYA KWA WAJUMBE WA CCM JIMBO LA TUNDUMA ,NITUMENI NIKAWATUMIKIE



Source : MbeyaYetuOnlineTV
 
BADO MAKONDA NI MSHINDI

Na, Robert Heriel

Makonda anayohaja ya kuwashukuru sana watu wa kigamboni. Kwa kweli matokeo aliyoyapata kwake ni kama ushindi kutokana na kuwa, mpinzani wake alikuwa anatetea ubingwa.
Tofauti ya kura 68 ni ndogo sana.

Ukiangalia matokeo katika maeneo mengine utaona watu wakiachwa kwa mamia ya kura, wengine wakiadhibiwa kwa kushindwa kufikisha kura kumi tuu.

Makonda bado ni mshindi, na unapaswa umshukuru Mungu na watu wa kigamboni kwa kura ulizopata.

Naamini utaibuka kidedea huko mbeleni. Kila la kheri.



Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Uchambuzi wako siyo sahihi hata kidogo. Unachotakiwa kufahamu ni kuwa Makonda ni alikuwa RC wa mkoa ambao Jimbo la Kigamboni limo. Yeye ni tofauti na wakuu wa mikoa wenzie wa mikoa mingine ambao walikuwa wakuu wa mikoa kwenye mikoa mingine, wakaenda kugombea mikoa mingine.

Makonda kushindwa kupata kura nyingi ndani ya mkoa aliokuwa akiuongoza kunaleta taswira kuwa wananchi wa Dar hawamtaki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sijapenda kabisa kwa CCM kumrudisha tena Ndungulile sisi Wanakigambon hatumkubali kabisa huyu mtu hakuna alicho Fanya hatuna soko hatuna barabara nzur yani CCM mmpeteza jimbo tunampa mpinzani mnakera sana.
Umetumwa na Konda??? 😃😃😃😃😃
 
Sasa kama kamati kuu inaweza kubadili matokeo hizo kura za maoni umuhimu wake ni nini kama sio kupoteza tu muda.Mambo mengine hayaingii akilini.
Mnaosema hivi mnajisahau nn kama haya matokeo ya mwanzo ni geresha maana kamat kuu inaweza kumchagua hata wa pili kugombea usije shangaa jamaa asirudi kupika kwenye meli ya wagiriki akateuliwa yeye wa pili kugombea ubunge
 
Mpoki anaendelea na uigizaji usikute hapo alikua location anatengeneza film hilo halina ubishi, tukimgeukia makonda sijui ataendelea na fani gani?
 
Busara itumike Jimbo la Vunjo, Kimei arudi

Aporudi akienda upinzani atamchanachana mpinzani wake vibaya sana
Hakuna cha busara wala nini, Demokrasia ndio iamue, na Demokrasia ya wanaCCM wa Vunjo ndio imeamua kumpiga chini Dr. Kimei. Na bila wasiwasi wowote Dr.Kimei hawezi kuhamia upinzani. Kwanini? Kimei sio mwanasiasa, mpole na muoga sana. Siasa za Upinzani haziwezi. Chini ya Magufuli, akihamia upinzani ataishia kufilisiwa, kushtakiwa au kuozea jela.

Kabla ya CCM kumbeba Dr.Kimei, lazima wajiulize, Dr.Kimei ameifanyia nini CCM Vunjo?
Kwa siasa za Vunjo, Kimei bado ni mwanasiasa mchanga sana. Kama anautaka sana ubunge, kwa sasa atulie huku akijipanga kwa 2025, huko huenda akawa na nafasi nzuri zaidi.
 
Uchambuzi wako siyo sahihi hata kidogo. Unachotakiwa kufahamu ni kuwa Makonda ni alikuwa RC wa mkoa ambao Jimbo la Kigamboni limo. Yeye ni tofauti na wakuu wa mikoa wenzie wa mikoa mingine ambao walikuwa wakuu wa mikoa kwenye mikoa mingine, wakaenda kugombea mikoa mingine.

Makonda kushindwa kupata kura nyingi ndani ya mkoa aliokuwa akiuongoza kunaleta taswira kuwa wananchi wa Dar hawamtaki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ngoja nimuulize Pompeo
 
Uchambuzi wako siyo sahihi hata kidogo. Unachotakiwa kufahamu ni kuwa Makonda ni alikuwa RC wa mkoa ambao Jimbo la Kigamboni limo. Yeye ni tofauti na wakuu wa mikoa wenzie wa mikoa mingine ambao walikuwa wakuu wa mikoa kwenye mikoa mingine, wakaenda kugombea mikoa mingine.

Makonda kushindwa kupata kura nyingi ndani ya mkoa aliokuwa akiuongoza kunaleta taswira kuwa wananchi wa Dar hawamtaki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Uchambuzi mzuri, mleta thread ni muimba mapambio wa Lumumba.
 
Sasa kama kamati kuu inaweza kubadili matokeo hizo kura za maoni umuhimu wake ni nini kama sio kupoteza tu muda.Mambo mengine hayaingii akilini.
Hiyo ndio CCM ilivyo.
Wakubwa wakitaka watakubeba na wakikukataa watakukata.
Waulize wanaCCM wa Zanzibar, nini kimewakuta juzi Dodoma wakati wa kupitisha mgombea wao wa urais wa Zanzibar. Sasa hivi wanalazimishwa kumpigia kampeni kwa hali na mali hata kama wazanzibar wengi hawamtaki.
 
Watoto wa kiume wa Mwalimu Julius Nyerere, Baba wa Taifa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Makongoro na Madaraka, wamekataliwa kwa kura nyumbani kwao Butiama, Mara.

Watoto hao wa Mwalimu Nyerere, walikuwa wakiomba ridhaa ya kupitishwa, kugombea ubunge na wajumbe wa mkutano mkuu wa Jimbo la Bunda, kupitia chama cha CCM.

Katika mkutano huo ulifanyika leo, matokeo yanaonyesha kwamba vijana hao wa Mwalimu, wamebwangwa vibaya.

Hadi naandika hapa, matokeo yameonyesha kuwa Makongoro na Madaraka wote wameshindwa kuingia hata 10 bora.

Sasa wanasubiri kudra za Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kama atakuwa na njia ya kurejea jina la mmoja wao au wote, kati ya matatu ili kupata mmoja atakayepeperjsha benders ya chama hicho tawala kwa nafasi ya ubunge wa jimbo hilo.

Matokeo yanasomeka: Jumanne Sagini (kura 84), Frank Mahemba (80), Joseph Nyamboha (46), Manyerere Jackton (22), Makongoro Nyerere (3), Madaraka Nyerere (2).

Wagombea walikuwa 59, wapiga kura 555.

Akitangaza matokeo haya, msimamizi wa uchaguzi huo, Msafiri Mtemi amesema zoezi la kupiga kura lilifanyika kwa uwazi mkubwa na kuwataka wagombea wote kuheshimu matokeo.

Msimamizi huyo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, amesema uamuzi wa nani atakuwa mgombea utatangazwa na chama chao baada ya kufanyika kwa mchakato mwingine katika mgazi za wilaya, mkoa na hatimaye halmashauri kuu.

Makongoro ambaye amewahi kuwa mbunge wa Arusha kupitia chama cha NCCR - Mageuzi na baadaye kuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, wakati Madaraka ndiyo ameingia mara ya kwanza kujaribu bahati yake.
 
Back
Top Bottom