Ligogoma
JF-Expert Member
- Aug 27, 2010
- 3,503
- 6,415
Kasahau bodi ya mikopo
Soma point no. 11
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kasahau bodi ya mikopo
Sijaona la maana hapo, anaongea mambo yasiyo na uhalisiaKwa kweli tangu juzi kawe, jana segerea na Leo Arusha Tundu Lissu ameanza kutema sera kali kweli
Zinahusu maisha ya mwananchi mmojammoja na Taifa kiujumla
Uzuri wa sera zake kuna zile ambazo ziko specific kwa mji husika na kuna zile ambazo zinahusu nchi nzima
1. Lissu kazungumzia ugumu wa maisha ya mfanyakazi na jinsi atakavyoyaboresha kwa kulipa malimbikizo yote wanayodai na kuwalipa nyongeza zao za mishahara za kisheria(annual increments)
2. Amezungumzia uonevu wanaofanyiwa wafanyabiashara wetu na kwamba ataundoa
3. Amezungumzia kuhusu elimu bora na siyo bora elimu, amezungumzia kuhusu elimu ya ujuzi wa kazi siyo ya kukariri
4. Amezungumzia kuhusu viwanda na kuvutia mitaji ili kutoa ajira kwa vijana wetu
5. Amzezungumzia kuhusu diplomasia yetu iliyoshuka na jinsi atakavyorudisha mahusiano bora ya kimataifa
6. Amezungumzia bima ya afya kwelikweli siyo hii ambayo wazee wetu wakishastaafu wanaambiwa waongeze hela ili waweze kuwekwa kwenye bima ya magonjwa nyemelezi ya wazee
7. Amezungumzia kuhusu kuirejesha Arusha kuwa kitovu cha utalii
8. Amezungumzia kuhusu katiba mpya, ameonyesha ubovu wa katiba ya sasa ambayo imelinyima hata bunge uwezo wa kuanzisha hoja ya namna ya kutumia pesa za nchi isipokuwa tu kama hoja hiyo imeanzishwa na serikali.
9.Amezungumza kuhusu haki za watu, ametetea masheikh walio jela kinyume cha sheria, kwa mfano amesema Arusha peke yake kuna Masheikh 70 wako jela achilia mbali wale masheikh wa uamsho.
10. Amezungumzia kuvunjia wananchi nyumba kikatili etc
11. Kszungumzia mzigo mzito wa makato ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu na amesema atashusha makato hayo kwa mwezi kutoka 15% hadi 3% ya mshahara kwa mwezi
12. Amezungumzia kuhusu adha za vitambulisho vya kimagumashi vya wamachinga amesema ataondoa mzingo wa shilingi 20000 ya kitambulisho cha wamachinga pesa iliyoanzishwa na Bashite na Magufuli
13. Amesema ataanzisha sheria ya haki ya mlipa kodi "Bill of taxpayers rights" ili waweze kulindwa kisheria badala ya utaratibu wa sasa ambao wafanyabiashara wanaonewa sana na TRA na hawana pa kukimbilia, kila wanapokimbilia wameshafungwa minyororo
14. Amezungumzia kuhusu uhuru wa habari, kuwa ataondoa sheria kandamizi zilizotungwa na Magufuli kumlinda yeye badala ya kusaidia taaluma kukua
15. Amesema ataomesha matumizi ya hovyo ya pesa za serikali, siyo rais akiamka asubuhi anajenga uwanja wa ndege kijijini kwake ambapo ndege inatua mara mbili kwa mwaka siku anayoenda kula Christmass na pasaka
16. Lissu anazungumzia kuhusu UHURU, HAKI, MAENDELEO
Kwa kweli Lissu unatisha baba endelea kupiga spana mwana wa Tanzania
Ila hizo hoja zote ni nzito sana!! Na tukisema ukweli awamu ya 5,zote imezipuuzia kabisa, kama wananchi wangekuwa wanasikiliza sera na kuzifanyia kazi haki ya mungu, mapeeema sana!! Ila kwa kuwa ndio wale wale.... Ila hakuna mtanzania hata mmoja ambaye haguswi na hoja hizo hapo juu!!! Hizo hoja ni kama maji, isipokugusa hii, inayofuata lazima tu ikuguse!!!Magufuli anatosha, hizi zingine mbwembwe tu
Hiyo nayo treni au ni makumbusho ya Taifa, watoto waone mkoloni alivojenga reli ya kuhamisha raslimali zetu. Labda wifanye kambi ya CCM ya kuandaa mapingamizi ya uchaguzi.Hawa watu wa Arusha hawana shukrani, wamesahau kama Profesa Magufuli ameifufua ile reli ya mkoloni iliyokuwa imekufa.
Na juzi kati mshakunaku polepole alikuja kumsifia master wake.
Mzee Pombe anatosha vipi hatujapandishiwa mishahara kwa miaka mitano na mnatukata 15% ya mshahara kulipa mkopo wa Chuo??Magufuli anatosha, hizi zingine mbwembwe tu
Punguza jaziba mkuuAnatosha kwa mamako labda!
Ndumba imepenya kunakoooMshalogewa chato nyie..
Mataga mmeanza kuhara damu 🤣Mara kwhiooo tumeibiwaaaaa!
Meko ni rais pekee unayeweza kumtega na mahindi kama kuku wa kienyeji!!Kwa miaka yote mitano Magufuli hakuwahi kukutana na kisiki cha mpingo kama hiki , tuone kama atakula tena mahindi barabarani
Mataga mmenywea kama kuku wenye mdondo 🤣Kwa kuwa hashidi inabaki kuwa kelele tu
Dah ile clip nilicheka sana, yaani utadhani jamaa aliyetokea interior huko asiyejua hata ustaarabu wa mjini, Meko kama sio kulindwa anaweza kuvua viatu akiiona lami.Bora hata angekuwaa anayala kistaarabu,anatafuna huku anaongea,mama unataka kupanuliwa wapi mama,huko mbelee...dah
Reli alijenga mkoloni na bado akatimuliwa, ije kuwa huyu Pombe!!Hawa watu wa Arusha hawana shukrani, wamesahau kama Profesa Magufuli ameifufua ile reli ya mkoloni iliyokuwa imekufa.
Na juzi kati mshakunaku polepole alikuja kumsifia master wake.
Mdahalo na Lisu ataweza?Meko ni rais pekee unayeweza kumtega na mahindi kama kuku wa kienyeji!!
Sera siyo lazima zitekelezwe za aliyeshinda tu. 2015 alishinda JPM wa CCM, lakini sera nyingi za CDM zimebebwa na CCM. Moja tu katika nyingi ni ya Elimu bure, japo utekelezaji wake ni jambo linalohitaji mjadala mwingine.Kwa kuwa hashidi inabaki kuwa kelele tu