Uchaguzi 2020 Ahadi na Sera za Tundu Lissu katika Uchaguzi Mkuu 2020
Yupo vizuri. Yule wa upande mwingine ni mweupe sana kichwani na ni mnafiki sana na pia ana roho mbaya kama nyoka
 
Kwa comments hizi, na

Kwa kinachoendelea kwenye siasa, na hisia za watu inaonyesha Taifa lina maumivu na majeraha makubwa ambayo yanapaswa kutibiwa, kuponywa, na kupewa tumaini.

Mungu tupe mtu atakaesimama kwa zamu yake kutengeneza mahala palipomoka.

Taifa linamhitaji mtu wa namna hii
 
Shikamoo Slaa 2010
Chadema hii ya Lisu ni bure kabisa
20200814_164215.jpg
20200814_164053.jpg
20200814_164156.jpg
20200814_164132.jpg
 
Kwa kweli tangu juzi kawe, jana segerea na Leo Arusha Tundu Lissu ameanza kutema sera kali kweli
Zinahusu maisha ya mwananchi mmojammoja na Taifa kiujumla
Uzuri wa sera zake kuna zile ambazo ziko specific kwa mji husika na kuna zile ambazo zinahusu nchi nzima

1. Lissu kazungumzia ugumu wa maisha ya mfanyakazi na jinsi atakavyoyaboresha kwa kulipa malimbikizo yote wanayodai na kuwalipa nyongeza zao za mishahara za kisheria(annual increments)

2. Amezungumzia uonevu wanaofanyiwa wafanyabiashara wetu na kwamba ataundoa

3. Amezungumzia kuhusu elimu bora na siyo bora elimu, amezungumzia kuhusu elimu ya ujuzi wa kazi siyo ya kukariri

4. Amezungumzia kuhusu viwanda na kuvutia mitaji ili kutoa ajira kwa vijana wetu

5. Amzezungumzia kuhusu diplomasia yetu iliyoshuka na jinsi atakavyorudisha mahusiano bora ya kimataifa

6. Amezungumzia bima ya afya kwelikweli siyo hii ambayo wazee wetu wakishastaafu wanaambiwa waongeze hela ili waweze kuwekwa kwenye bima ya magonjwa nyemelezi ya wazee

7. Amezungumzia kuhusu kuirejesha Arusha kuwa kitovu cha utalii

8. Amezungumzia kuhusu katiba mpya, ameonyesha ubovu wa katiba ya sasa ambayo imelinyima hata bunge uwezo wa kuanzisha hoja ya namna ya kutumia pesa za nchi isipokuwa tu kama hoja hiyo imeanzishwa na serikali.

9.Amezungumza kuhusu haki za watu, ametetea masheikh walio jela kinyume cha sheria, kwa mfano amesema Arusha peke yake kuna Masheikh 70 wako jela achilia mbali wale masheikh wa uamsho.

10. Amezungumzia kuvunjia wananchi nyumba kikatili etc

11. Kszungumzia mzigo mzito wa makato ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu na amesema atashusha makato hayo kwa mwezi kutoka 15% hadi 3% ya mshahara kwa mwezi

12. Amezungumzia kuhusu adha za vitambulisho vya kimagumashi vya wamachinga amesema ataondoa mzingo wa shilingi 20000 ya kitambulisho cha wamachinga pesa iliyoanzishwa na Bashite na Magufuli

13. Amesema ataanzisha sheria ya haki ya mlipa kodi "Bill of taxpayers rights" ili waweze kulindwa kisheria badala ya utaratibu wa sasa ambao wafanyabiashara wanaonewa sana na TRA na hawana pa kukimbilia, kila wanapokimbilia wameshafungwa minyororo

14. Amezungumzia kuhusu uhuru wa habari, kuwa ataondoa sheria kandamizi zilizotungwa na Magufuli kumlinda yeye badala ya kusaidia taaluma kukua

15. Amesema ataomesha matumizi ya hovyo ya pesa za serikali, siyo rais akiamka asubuhi anajenga uwanja wa ndege kijijini kwake ambapo ndege inatua mara mbili kwa mwaka siku anayoenda kula Christmass na pasaka

16. Lissu anazungumzia kuhusu UHURU, HAKI, MAENDELEO

Kwa kweli Lissu unatisha baba endelea kupiga spana mwana wa Tanzania
1).Pia asisahau kurudisha maduka ya Jeshi duty free shops
2) Kuna kitu wanasiasa hukisahau na Ni muhimu kwa uchumi na ustawi wa watu Ni
SUSTAINABLE URBAN AND RULAL PLANNIG" au upangaji wa miji na vijiji ili kuondoa makazi holela,

hatuwezi kuwa na population ya 60+ mil. Bila kupanga makazi na shughuli za kiuchumi

Mheshimi raisi Lissu likumbuke hili liwe kwenye vipaumbele vyako
 
Watanzania mwaka 2015 waliyahitaji mabadiliko, lkn hawakumuhitaji kiongozi muimla, walimchagua Lowassa bali kwa uhuni wa kimfumo akaletwa Pombe. Wameshaleweshwa kwa pombe haramu ya yule ambaye hawakumchagua.

Watanzania kwa mara nyingine tena hawataki kuleweshwa kwa itikadi chafu yenye kuwatia unajisi. Hawataki tena kuletewa madarakani mtu wasiyemtaka, bali wanamtaka kiongozi wa nchi awe kipenzi chao.
 
Watanzania mwaka 2015 waliyahitaji mabadiliko, lkn hawakumuhitaji kiongozi muimla, walimchagua Lowassa bali kwa uhuni wa kimfumo akaletwa Pombe. Wameshaleweshwa kwa pombe haramu ya yule ambaye hawakumchagua.

Watanzania kwa mara nyingine tena hawataki kuleweshwa kwa itikadi chafu yenye kuwatia unajisi. Hawataki tena kuletewa madarakani mtu wasiyemtaka, bali wanamtaka kiongozi wa nchi awe kipenzi chao.
Naomba nikiri. Nilimpa kura JPM 2015 na kumfanyia sana kampeni humu jukwaani but he has disappointed me big time!!
Kwa jinsi ninavyoiona Tanzania ikizidi kudidimia kiuchumi, kiutawala hasa kwenye misingi ya utawala bora na haki, kimaendeleo hasa katika kubadirisha maisha ya watanzania kuwa mazuri na ya kupendeza sioni namna naweza mchagua Magufuli mwaka huu!! No way!!
 
Mods wa JF siyo kila thread ni ya kumerge, mnapoteza latest hot issues eti kwa sababu content zinashabihiana na mada ya wiki iliyopita, mnasababisha watu waliosoma mada wiki jana wasione umuhimu wa kusoma ya leo.
Kwenye siasa 24 hours ni nyingi sana kubadili upepo. Acheni kumergemerge threads mnapoteza moto, na mzuka, na kufuatilia habari

Sasa habari ya J'mosi utaimerge vipi na habari ya Jumatatu wakati mambo mengi yeshatokea hapo katikati? –Mnaboa na mnazingua kichizi sometimes.
 
Kwa kweli tangu juzi kawe, jana segerea na Leo Arusha Tundu Lissu ameanza kutema sera kali kweli. Zinahusu maisha ya mwananchi mmojammoja na Taifa kiujumla. Uzuri wa sera zake kuna zile ambazo ziko specific kwa mji husika na kuna zile ambazo zinahusu nchi nzima....
Jamaa ana akili mpaka basi
 
Eti sumu haionjwi kwa kidole!! Mwaka huu ni heri kuionja "sumu" mpya kwa kiganja. Hata kama hatafanya chochote, walau tutaanza sehemu flani
 
Ni nani alipigwa risasi 16 kisha akapona?nitajie hata mmoja tofauti na Lissu.Kupona kwake ni mpango wa Mungu ili Tanzania ikombolewe katika nyanja zote.

Lissu ameandaliwa na Mungu kuwa rais wa Tz.Mungu mbariki Lissu,Mungu wabariki watanzania wote wampe Lissu kura za ndiyo Oktoba 2020.

Wauaji,Wachawi,Wavunjifu wa amani,Wapiga risasi watu,Watekaji,Waweka mapingamizi feki,Wanaojifanya wazalendo wakati si wazalendo washindwe kwa jina lako.
 
Back
Top Bottom