Kwanza hakuna mahala Lissu alisema matibabu yatakuwa bure hata kwa unemployed au mtu yeyote.

Pili Rwanda hapo jirani zetu wanamfumo huo wa UHI, Je wanalipa euro 300 kwa kila raia?.

Jambo lamsingi lakuelewa nikuwa kila mwananchi atalipa kulingana nakipato chake lkn matibabu yatakuwa sawa kwa wote.

Jambo lingine lakawaida tu ambalo halihitaji hata certificate kulitambua, nikuwa kila nchi hulipa gharam kulingana nahali ya uchumi wanchi husika.
 
Wajinga wengi hawaelewi hili kuwa uchumi wa belgium euro 275 niela ndogo sana.
 
Wewe naona ni muelewa. Lakini Kama kawaida ya makada wa CCM huwa Mnajitahidi kujitoa ufahamu.
Lisu alikuwa anaelezea utaratibu wa bima kwa Ubeligiji, we unachukulia kuwa life standard za huko Ni sawa na za huku na hivo hata gharama za matibabu unazifananisha? Yaaani haspitali yenu ya koromije iwe s itawa na alikokuwa Lisu? Hakika mnastahili kunyofolewa madarakani
 
Hapa bima NHF ni 650,000 sawa na hiyo ya ubelgiji kwa maana hiyo maneno mengi ni burudani za kapeni tu
Maneno mengi utekelezaji 0 ili mradi mtaji wa kura umepatikana
 
Acha kuleta propaganda za kitoto.
 
Mtu.alipigwa risasi bila sababu yyte
Kisha yupo msukule anamwita kubaraka wa mabeberu...
 
Namshauri Tundu Lissu katika kampeni zake kuwa, mbali na kuahidi kuboresha masilahi ya wafanyakazi, ni vizuri pia akaweka wazi athari za kiuchumi kwa Taifa na kwa mtu mmoja mmoja ili umma kuelewa kuwa jambo hili lina madharaja si kwa watumishi tu, bali kwa Taifa zima.

Mfano,Lissu afafanue ni namna gani nyongeza ya mishahara ya mfanyakazi wa umma inaweza kumgusa mama lishe, fundi ujenzi, fundi seremala, fundi cherehani, mvuvi wa samaki, muuza bucha, dereva wa boda boda, n.k

Lissu aeleze ni namna gani mzunguko wa fedha unaweza kuboreshwa kupitia nyongeza ya mishahara ya watumishi wa umma na hivyo kunufaishi hata wasio watumishi.

Lissu aeleze ni kwa namna gani nyongeza ya mishahara ya watumishi wa umma inaweza kutoka fedha Benki kuu na kuziingiza katika mzunguko kupitia Benki za kibiashara ambako watumishi wana akaunti za Benki.

Awaeleze watanzania ni namna gani nyongeza ya mishahara anaongoza kiwango cha watumishi wa umma kukopesheka na nina gani mkopo anaouchukua mtumishi unaweza kumnufaisha fundi ujenzi, n.k.

Lissu aeleze umma wa watanzania ni kwa namna gani serikali yenyewe itafaidika na nyongeza hii kupitia PAYE na kodi nyingine zitazoongezeka kupitia ongezeko hilo kama vile mapato ya serikali kutokana na ongezeko la Mikopo katika mabenki, n.k

Kwa kueleza umuhimu huu kwa wananchi na athari zake, Lissu atafanya kila mtanzania aone ni namna gani agenda hii ya nyongeza ya mishahara inagusa karibu kila mtu wakiwemo hata wasio wa watumishi na Taifa kwa ujumla.

Huu ndio ushauri wangu kwa Lissu na CHADEMA kwa ujumla.
 
watu wameshamchoka hakuna anachowaeleza kuhusu shida za wananchi anachofanya ni matangazo ya jinsi alivyopigwa risasi sasa nani anataka kusikia hayo?kila siku?
 
Pia elezeni idadi kamili ya wafanyakazi wa #UMMA na pia mueleze ni asilimia ngapi ya idadi ya watanzania
 
Lissu atakama hakusema utatibiwa bure directly implicitly nonetheless ame imply ivyo kwa mfumo anaotaka kuiga, vinginevyo angetolea mfano huo mfumo wa Rwanda.

Halafu Rwanda health budget yao inachangiwa na serikali at 12% of their GDP, development partners na insurance unayoiongelea ambayo na yenyewe ni kama upatu.

Kwanza huduma za afya zimejikita at basic primary care intervention huduma za zahanati kwa sana hakuna ata X-rays. Ikitokea umeumwa serious unahitaji referal ya kwenda kutibiwa hospitali za rufaa kilichopo kwenye kopo la kijiji ndio kinatumika kukulipia.

Nina uhakika ukipekuwa sana utakuta ni kwa ajili ya walalahoi hoi tu hila wanyarwanda wenye hela zao wanaotaka quality medical intervention at all times wanalipia kama kawa private hospitals.

Unaposema universal credit kama anavyodai Lissu it means you receive medical care at point of entry yaani kilichopo mbele yako ndio icho unaingia uitaji referral na kuhudumiwa bila ya kuulizwa nani analipia wakimalizana na wewe bill anapelekewa muhusika.
 
Waambie Mods wakusaidie kuhariri heading yako, nitakuja kuchangia baadaye.
 

..nyinyi mnapinga tu kwasababu aliyetoa wazo hili ni TL.

..mko tayari wananchi wapate shida, kuliko kuchukua wazo zuri kama hili.

..kwa maoni yangu hii ndio the best idea to come up in this election.

..tunachotakiwa ni kulibeba wazo hili na kuliboresha kwa manufaa ya waTz wote.

..pale kwenye mapungufu tupaboresha, tuacheni na haya mambo ya kumtukana na kumdhalilisha TL.

..Mzee Kikwete alisema "hoja au wazo halipigwi rungu."
 
Swala sio kumpinga Lissu insurance ya Rwanda ni $2 mpaka $8 kwa hela hiyo uwezi kupata huduma tofauti na Tanzania. Kwanza huduma zenyewe wanazopata Tanzania NGO za afya zinatoa bure tatizo labda useme sio kila mtu ana access nazo.

Kwa ivyo mtu anaeitaji kuwa realistic ni Lissu kwanza nchi aliyotoka on average a family household inachangia kama €800 kwa mwaka na mwajiri anachangia €1600 per employee na employment rate ni 95% you get the idea why it’s possible.

Sasa uwezi kuja na wazo la kuponda hatua za serikali na kupendekeza tuige health system ambayo aiwezekani, wewe unadhani kwa nini universal health service inapigwa vita marekani?
 

..Universal Health Care ni wazo zuri.

..tunachopaswa kusisitiza ni huduma bora za viwango ktk hiyo UHC anayopendekeza TL.
 
Kwa kuwa Lissu anasema kwamba kama ataingia madarakani basi ataunda serikali yenye mfumo nafuu tofauti na sasa, basi hili la bima kwa kila mwananchi linawezekana hata kama halitokuwa sawa na Ubelgiji.

Mfumo wa bima ya afya ni wa lazima kwa baadhi ya nchi za ulaya kutokana na gharama kubwa za matibabu. Kule nchini Uholanzi kama huna bima ya afya na wewe ni mkazi wa pale basi unaweza kushtakiwa, kwa sababu huwezi ukalipia gharama za matibabu jinsi zilivyo kubwa na pengine unaweza kupata ugonjwa unao ambukiza na usipotibiwa kwa kuwa huna bima unaweza kuhatarisha maisha ya wengine, kwa sheria zao mtoto anapozaliwa adi kufikia miaka 21 serikali ndio inamlipia matibabu lakini kwa sharti la kwamba mmoja kati ya wazazi yuko na bima ya afya, bila hivyo hawezi kutibiwa.

Kwa yeye kulipa EU 275 sina uhakika nalo sana, kwa sababu sijui ni mfumo gani uliotumika katika bima yake.
Lakini tukirudi nyuma kidogo Ubelgiji imesaidiwa sana na muungano wa nchi za ulaya, kabla ya hapo pesa yake ilikuwa inatofautiana na pesa ya Kenya kwa shilingi 7 tu ya Kenya. Na mpaka sasa gharama za maisha kwa Ubelgiji bado ziko chini kidogo ukilinganisha na baadhi ya nchi nyingine za ulaya, hata kimatibabu Ubelgiji gharama zao bado ziko chini kidogo.

Nchini Uingereza hawana mfumo wa bima kwa kila mtu, siku za nyuma mtu yeyote akiingia pale alikuwa akitibiwa hata kama ana tatizo kubwa, lakini nasikia kwa sasa hivi wameondoa mfumo huo na kuweka utaratibu kwa raia wao na wakazi wenye kibali cha kuishi nchini mwao.

Hivyo mfumo wa bima ya afya, ama utaratibu wa matibabu kwa kila nchi duniani ni jambo zuri na lenye unafuu kwa watu kutokana na gharama za matibabu.
Kwa TZ naamini kwamba inawezekana lakini kunahitajika mabadiliko ya mfumo mzima wa maisha (kipato) cha mwananchi.
 
Tuendelee namfumo uliopo Tz au tuboreshe?.
 
sasa mabombadia ya nn hii nchi tajiri tunaweza kuweka bima kitu kidogo kama miaka mi 5 mabombadia 11 tushindwe bima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…