Uchaguzi 2020 Ahadi na Sera za Tundu Lissu katika Uchaguzi Mkuu 2020
Hahaha nasikia hata Polepole na Bashiru wana mpango wa kumpigia kura Lisu wamechoka kutishwa kufukuzwa na Magufuli.
 
Mimi si mwandishi muzuri! Napenda kuwajulisha ukweli mchungu usiozungumzwa popote kwa woga wa kupoteza au kupotea kuwa kati ya 100% ya wana CCM salio jinsi kisha na watakaopiga kura, 90% watampigia Lissu wa yupinzani, sababu chache ni hizi:

Moja, Magufuli aliua njia zao za kujipatia rizki! Wengi wakajenga visasi na wakakosa pa kuyasemea haya sasa watakua sema kwa vitendo

Pili, Suala la ununuzi wa Wapinzani kisha kuwapa madaraka huku wenyeji wakitolewa kauli za kishenzi ni uthibitisho mzuri mwingine, munamkumbuka Shonza? Unajua alitoka wapi?

Tatu, Kuwachagua watu wenye vinasaba naye vya kiukoo au kiukabila! Huku wengi kuwaacha wakiwa wanakufa njaa.

Nne, Kuwaweka watu anaowataka yeye kuwa Wagombea ubunge na kuwaacha ware waliochaguliwa kihalali na Wajumbe.

Tano, Dharau zinazooneshwa waziwazi na top layer leadership kwamba wao wanatosha kukiongoza chama chetu.

Unaweza kuyaongeza kadiri umavyokumbuka
By the way wana ccm ,act,cuf,chadema na wengineo ni watz na ni ndugu taifa moja.Ugumu wa maisha,taabu na mateso ni kwa wote.
 
Ukiniambia hawa wanaCCM damu wafuatao watakwenda kupigia kura Magufuli kwa moyo mkunjufu, utakuwa wewe mwenyewe unaonekana kioja:
1. Nape Nappy
2. Kamba Makamba wote wawili
3. Kinaina

Weka na wengine wenye 'principles' na sio wanazi wa kizembe kama akina Warioba, Butiku na watu wa aina yao wengi tu

Watakaolazimika kumpigia kura Magufuli, ni hao wanaofaidika moja kwa moja na uteuzi wanaoupata kama akina Popole, Bushiu, Bashite...n.k.

Huu mchezo wa huyu mtu umekwisha haraka sana kuliko nilivyotegemea itakuwa. Kazi iliyobaki sasa ni kuhakikisha kura hazivurugwi.
Bila kusahau wasira,ngereja,Lowasa na maige
 
Mimi si mwandishi muzuri! Napenda kuwajulisha ukweli mchungu usiozungumzwa popote kwa woga wa kupoteza au kupotea kuwa kati ya 100% ya wana CCM salio jinsi kisha na watakaopiga kura, 90% watampigia Lissu wa yupinzani, sababu chache ni hizi:

Moja, Magufuli aliua njia zao za kujipatia rizki! Wengi wakajenga visasi na wakakosa pa kuyasemea haya sasa watakua sema kwa vitendo

Pili, Suala la ununuzi wa Wapinzani kisha kuwapa madaraka huku wenyeji wakitolewa kauli za kishenzi ni uthibitisho mzuri mwingine, munamkumbuka Shonza? Unajua alitoka wapi?

Tatu, Kuwachagua watu wenye vinasaba naye vya kiukoo au kiukabila! Huku wengi kuwaacha wakiwa wanakufa njaa.

Nne, Kuwaweka watu anaowataka yeye kuwa Wagombea ubunge na kuwaacha ware waliochaguliwa kihalali na Wajumbe.

Tano, Dharau zinazooneshwa waziwazi na top layer leadership kwamba wao wanatosha kukiongoza chama chetu.

Unaweza kuyaongeza kadiri umavyokumbuka
Haswaaa 😊😊😊 miongoni mwao Ni hawa
Shift, naona umeamua kuja na porojo za vijiweni. Watanzania tunachagua mtu ambaye ataleta maendeleao ya vitu, maendeleo ya vitu yanatumiwa na watu. Ili uweze kuendelea lazima wachache waumie. Wacha tuumie ili wajukuu zetu waje kula mema ya nchi hii. 5 MINGINE KWA JPM. CCM OYEEEEEEEEE
Tulia wewe😊😊😊😊😊 wenzako wankucheka unaharisha pekeako tu🤣🤣🤣
 

Attachments

  • VID_48221104_221141_428.mp4
    3.2 MB
Mimi si mwandishi muzuri! Napenda kuwajulisha ukweli mchungu usiozungumzwa popote kwa woga wa kupoteza au kupotea kuwa kati ya 100% ya wana CCM salio jinsi kisha na watakaopiga kura, 90% watampigia Lissu wa yupinzani, sababu chache ni hizi:

Moja, Magufuli aliua njia zao za kujipatia rizki! Wengi wakajenga visasi na wakakosa pa kuyasemea haya sasa watakua sema kwa vitendo

Pili, Suala la ununuzi wa Wapinzani kisha kuwapa madaraka huku wenyeji wakitolewa kauli za kishenzi ni uthibitisho mzuri mwingine, munamkumbuka Shonza? Unajua alitoka wapi?

Tatu, Kuwachagua watu wenye vinasaba naye vya kiukoo au kiukabila! Huku wengi kuwaacha wakiwa wanakufa njaa.

Nne, Kuwaweka watu anaowataka yeye kuwa Wagombea ubunge na kuwaacha ware waliochaguliwa kihalali na Wajumbe.

Tano, Dharau zinazooneshwa waziwazi na top layer leadership kwamba wao wanatosha kukiongoza chama chetu.

Unaweza kuyaongeza kadiri umavyokumbuka
Mimi pia ni mccm. Kura yangu siipeleki lumumba katu.
 
Haiingia akilini tuna Bandari ila wafanya biashara wanachukua nguo Uganda nchi inayo tegemea bandari ya Mombasa na Dar es salaam.

Burundi hawana bandari ila magari kwao ni cheap sana kuliko Tanzania.

Hii inapaswa kuongelewa pia make tuna kodi za kukomoana sana
 
Mhe. Lissu salaam, pole na majukumu na mizungunguko yako ya kunadi sera zinazotugusa sie tulio wanyonge haswa. Binafsi nimekuwa nikikufutilia kwa karibu kampeni zako popote kwa njia ya mtandao na agharabu niliwahi kuhudhuria kwenye uzinduzi wa kampeni moja mkoa wa nyanda za juu kusini, hakika Mungu akulinde.

Kuna mambo mengi yakuleta matumaini umekuwa ukiyaeleza vizuri namna utakavyo yashughulkia kwa kweli inatia moyo. Lakini kuna jambo moja bado hujaliweka wazi sana namna utakavyo shughulika nalo na hili unalijua lina kundi kubwa la watu na unalijua vizuri.

Binafsi pia ningependa uliongee kila pahala unapokwenda kunadi sera (nitalieza). Kwakifupi niorodheshe mambo unayoyaeleza vizuri na hayana shaka ili uliongeze na hilo liwe miongoni mwa haya(msomaji waweza ongeza ambayo nimesahau) .

1. Kila mtanzania kumpatia bima ya afya
2.Kuongeza mishahara kwa watumishi(mujibu wa sheria)
3. Kulipa malimbikizo kwa watumishi.
4. Kurudisha fao la kujitoa
5. Kupunguza makato bodi ya mikopo mpaka 3% ya awali
6. Kutoa mikopo kwa waombaji/ wanafunzi wote elimu ya juu.
7. Kulipa fidia kwa wahanga waliobomolewa nyumba zao kupisha ujenzi wa barabara na kuwafariji wahanga wa tetemeko Kagera.
8. Kuondoa kitambulisho cha ujasiliamali kwa machinga na wengineo
9. Kuwapatia watanzania katiba mpya(ya Jaji Warioba).
10. Kurudisha ardhi iliyopokwa kwa wananchi.
11. Kuwatoa magerezani Mashehe wa uamsho(na wanaharakati waliobambikiwa kesi).
12. Kuunda tume ya maridhiano kwa viongozi waliojihusisha kunyanyasa raia bila makosa ukiwemo wewe, kuuweka bayana wa mambo hayo na sababu ya kufanyika kwake na kisha kusamehana.
13. Kuondoa vikwazo kwa wakulima (kundoa kodi za magetini, kuwa na soko huru na upatikanaji rahisi wa pembejeo za kilimo pamoja na bei zake).
14. Kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara(kuondoa kodi mpaka kufika 10%, kuifumua upya TRA, nk).
15. Kuweka mazingira safi ya Uwekezaji ili kukuza uchumi na kuongeza ajira.
16. Kurekebisha mfumo wa elimu ili uweze kumpa maarifa mwanafunzi na sio kuongeza ufaulu tu bila kuwa na maarifa. (Kuaandaa wasomi watakaoajirika popote duniani na kuwa katika soko la ushindani).
17. Kuzipa nafasi sekta binafsi kuratibu shughuli zao kwa uhuru na kuifanya serikali kuwa msimamizi na kuzipa mazingira safi ya shughuli zao.
18. Kuwa na serikali za majimbo na viongozi wake kupatikana kwa kuchaguliwa ama kuondolewa na wananchi(kurudisha nguvu na mamlaka kwa wananchi).
19. Kulinda na kutetea haki, utu, na uhuru wa kila raia.
20. Kujenga uhusiano mzuri na mataifa mengine(Diplomacy Restoration)ambayo pengine yamezorota hivi karibuni.
21. Kuondoa laana ya rasilimali(wananchi kutobugudhiwa/kubezwa kwa rasilimali zinazopatikana maeneo waliopo/yanaowazunguka). Raia kuwa wanufaika kwa rasilimali zinazopatikana mahala walipo.
22. Kurudisha uhuru wa vyombo vya habari (kuondoa sheria kandamizi za utoa aupokeaji wa habari)
23. Kuondoa kinga ya viongozi na kupunguza mamlaka ya Rais. (Kuweza kushtakiwa akifanya makosa). nk nk

Kwa uchache hayo ndiyo nayasikia mara nyingi na yanatugusa mojakwamoja. Sasa hitaji langu nitajikita kwenye namba 16 kwa sababu kwa namna moja ama nyingine vijana na wazazi wameathiriwa vibaya mno na hili.

MFUMO WA ELIMU na AJIRA kwa VIJANA
------------------------------------------------------
Mh. T. A. Lissu kama unavyojua mfumo wa elimu umekuwa ukituandaa vijana kuwa tegemezi(dependents) yaani soma, faulu, na uandaliwe ajira. Mfumo huu hautupi uwezo wa maarifa na kisha kupambana na mazingira bali uajiriwe baada ya kuhitimu. Hiki ndicho kinachogharimu wasomi wengi na kufifisha matumaini kwa wazazi wanaosomesha vijana wao. Nimeridhika na namna unavyotaka sekta binafsi zipunguze tatizo la ajira lakini ujue kuna kundi lililomaliza vyuo toka 2015-2020 almost 6years halina ajira rasmi na liliandaliwa na mfumo huo tegemezi wa elimu.

Hivyo basi ningependa katika kampeni zako ungeliongelea katika kila mkutano wa kampeni ipi mipango mikakati ya dharura ya kushughulika na kundi hili kabla ya kuanza na mfumo mpya wa elimu. Kumbuka hawa vijana ni kundi kubwa wao na wazazi/walezi wao wanataka kujua hatma yao na namna utawafanya wawe kwenye ajira rasmi.

Serikali ya sasa nikama haina mipango yoyote juu ya hili na ndio maana kumekuwa na ukosefu mkubwa wa ajira kwa miaka hii mitano. Hawa ni vijana waliosomeshwa na wazazi maskini kwa kuuza mazao yao, mali zao, mashamba, mifugo ili tuu wapate elimu.

Katika kundi hili ni wachache wanaopatiwa ajira rasmi agharabu kwa wale wenye ndugu walio na nafasi kubwa serkalini ila the rest wapo mitaani. Kwa heshima yako naomba utoe mwongozo kwa vijana, wazazi au walezi kila mkutano wako wa kampeni maana ni tatizo la nchi nzima.
Asante na kila la kheri katika mapambano yako. (Nashuku katika kampeni zako jana 27/09/2020 Musoma umeanza kuliongelea kiundani, ningependa liwe ni endelevu kwa kila mkutano wako).
Naomba kuwasilisha.
 
Suala la ulinzi wakura ni wajibu na jukumu la kila mpenda Haki na Taifa letu la Tanzania.Tusimwachie Mh.Lissu na CHADEMA peke yao.
Tumefurahishwa sana uungwaji mkono mkubwa wa Lissu kila kona ya nchi. Kwa kweli Lissu ameshashinda kikubwa ni kudhibiti wizi wa kura tu.
 
Chadema wa jf kwenye kujifariji mpovizuri.
tukutane October 28 ndo mtajua watanzania hawana utani kwenye sanduku la kura.
Nanukuu mwasilishaji wa huu uzi kipandee...

"Hoja ya magufuri imebaki kuwa ni watu wajiajiri wakati yeye mtoto wake Jesca amemwajiri wizara ya mambo ya nje, mwingine amempa RAS iringa .hao walishindwa kujiajiri hadi awaajiri. Watoto wa wanyonge ndio wanaohimizwa kujiajiri"

Mama angu mzazi alinambia usimpigie kura Magufuli 2020

Anaenda mbali kanambia ametunza kweny kabati degree 3 za watoto wake

Leo hii mtoto wa Raisi binti mdogo wa Raisi anapewa kazi wizara ya Mambo ya nje....

Ukiwa mtoto wa Raisi Ni mfano Hai KWA vijana kuhusu kujiajiri....maana
hawezi kulalamika mtaji
hao ndio walikuwa watu wa kutengeneza fursa KWA vijana wengine wajiajiri

Mtu mwenye akili timamu ataelewa na anaelewa uchungu

Tena WAZAZI walio somesha watoto wao na Still... wapo wapo nyumbani uta waambia nini?
Wamekosa hata Kazi ya upolisi au magereza au JW
Wamepelekwa huko Jkt kupotezewa muda wao wa MIAKA miwili

Hao walimu wa BAED wangepelekwa primary school wakafundishe ELIMU yetu ingepanda thamani.

KINACHO FANYIKA MNYONGE WA NCHI HII ANAZIDI ZOHOFISHWA AWE MNYONGE ZAID NA ZAID
 
atilie mkazo kuhusu FAO la kujitoa.... kazi nyingi sector binafsi ni kazi ya mikataba.. mkataba unapoishi tunatamani tuchukue pesa zetu tukajiajili wao wanazikatilia ni kuendelea kutufanya wanachi kuwa masikini ili hali wanapiga pambio la vijana kujiajili. maneno na vitendo haviendani.
 
Lissu atakuwa rais wa Twitter na Facebook sio Tanzania ambayo mwasisi wake ni hayati Julius Nyerere.

Hawezi kumkejeli mwasisi wa taifa halafu unataka uliongoze taifa hilo hilo.
 
Nampenda lissu kwa kutetea haki. Tunapaswa kuwa na Rais mpenda haki.Mtanzania yeyote ana haki zake ziheshimiwe.
Mkuu mwogope mwanasiasa anapokuwa jukwaani.
Wote wakiwa hapo huwa na sifa moja...waongo!
28/10 kafanye yako kwa kufariji nafsi yako na urudi kupambani kuihudumia familia yako. Usimtegemea mwanasiasa kwa maneno yake matamu jukwaani.
 
Lissu ni kama vile ameshashinda uchaguzi huu kwa hoja zake 7 ambazo zimepata nguvu na kuaminiwa na jamii. Na hii inajidhihirisha maeñeo mbalimbali ambayo amepita kufanya kampeni.

Lissu ni kama vile mhubiri wa injili, kila eneo analopita shetani anapoteza nguvu na neno linabaki mioyoni mwa watu. Maeneo ambayo bado hajapita ndio yamebaki kuzungumzia habari za CCM, lakini yatakapofikiwa na habari njema ya injili ya wokovu na ubatizo wa maji mengi na wao wataachana na CCM.

Hoja 7 ambazo Lissu zimemwongezea nguvu toka kwa makundi mbalimbali ambazo CCM wamekosa majibu yake

1. Vitambulisho vya wajasiliamali;

Ni hoja ambayo imepokelwa vizuri na watamzania, kila kona.CCm wameshindwa kujibu hadi sasa, wamebaki tu kudema dema kwenye majibu yao kwamba magufuri anawapenda wamachinga, Mara vitambulisho sio lazima ,wakati wamevitungia na sheria tayari. Lissu shikilia hapo hapo kwa mpaka waeleze ni lini wamachinga walioomba wauziwe vitambulisho visivyo na picha wala jina

2. Maslahi ya watumishi, nyongeza ya mshahara.

Hoja ambayo haijajibiwa hadi Leo, na ccm wamekosa majibu wakaeleweka kwa wananchi. . Nyongeza ya mshahara ni takwa la kisheria na sio takwa la mtu . Alisikika Mara moja akisema hajapandisha mshahara ila edhibiti mfumuko wa bei, na akapata majibu yake toka kwa Lissu kwamba bei ya sukari ya 2015 na Leo 2020 ipo sawa, ? "Wananchi hapana" Lissu " anatuambia nini. Baba shikilia hapo hapo wameshalegea na hawana majibu

3. Suala la pension na kiinua mgongo kwa wastaafu

Watu wengi walikuwa gizani na suala lakini baada ya kulitolea maelezo sasa nalo limepata hamasa miongoni kwa watanzania kwamba kuanzia mwakani wastaafu hawatapata pension zao zote baadala yake watapata nusu. Hilo limeonekana kuwa chuki kwa makundi hayo na CCM wameshindwa kutolea majibu ya kueleweka . Lissu shikilia hapo hapo wamesha nyooka tayari

4. Ujenzi wa uwanja wa ndege Chato na hifadhi ya wanyama

Hoja hapa sio ujenzi ,hoja inayoonekana hapa ni namna mradi unavyotekelezwa kwa ufisadi mkubwa wa kupeana tenda na Ndugu yake Mayanga . Mpaka Leo hoja hiyo Magufuli na CCM yake wameshindwa kuitolea majibu, kwa nini aingilie mchakato wa tender na kuagiza apewe ndugu yake na watu sasa huku wanasema ni kama mtu ameamua kupitishia di kwa ndugu yake. Amenipigia pasi kwa mbele ,na suala la hifadhi pia ndio hawana majibu kabisa .Baba Lissu shikilia hapo hapo wamesha nyong'onyea tayari

5. Suala la ununuzi wa ndege

Hii hoja ilianza kwa kasi mwanzoni kunadiwa na ccm lakini baada ya Lissu kuanza kushughurika Nayo wameshakimbia. Lissu amezungumzia masuala ya Faida na mchakato wa ununuzi wa midege hiyo imegubikwa na ufisadi mkubwa na kwamba anayejua ni Magufuri na mjomba wake Dotto James. CCM mpaka Leo wamepoteana na ajenda ya ndege sio ajenda yao tena kwenye kampeni zao.Lissu wabananishe hapo hapo kwenye kona washindwe pa kutokea.

6: Ukosefu wa Ajira kwa makundi mbalimbali

Eneo hili limepata uungwaji mkono mkubwa toka kwa makundi mbali mbali ya vijana. Tangu 2015 ajira zimetolewa kwa walimu wa sayansi na kada za afya. Kada nyingine hazijaguswa kabisa . Hoja yake hapa magufuri imebaki kuwa ni watu wajiajiri wakati yeye mtoto wake Jesca amemwajiri wizara ya mambo ya nje, mwingine amempa RAS iringa .hao walishindwa kujiajiri hadi awaajiri. Watoto wa wanyonge ndio wanaohimizwa kujiajiri. Hapo napo Lissu shikilia hapo hapo pana tija na kundi kubwa la wahanga

7: Waathirika wa vyeti feki
Hii ni hoja ambayo imepata kusemwa na Lissu, kwamba hao walio wa ajiri ni wao ccm na kinachozungumzwa hapa ni watu kufukuzwa kama mbwa bila kupewa mafao yao, ambayo wamechangia kwa miaka mingi halijulikani lilipo enda. Hao ni watanzania wenzetu na sio wakenya wala wamalawi, wamelitumikia na kutufundishia watoto wetu kwa miaka mingi hadi wengine wamekuwa maprofesa. Michango yao ipo wapi kama hawajapewa, Magufuri na ccm yao iliyojaa roho ya kuumiza watu waseme wamepeleka michango yao ya pension waliyokuwa wanachangia kwenye mifuko ya hifadhi

Nashauri Lissu sasa kwa kuwa kwenye miji yote na vijijini amefanikiwa kuiteka sasa ajikite katika kuwaaminisha watanzania ni namna gani walinde kula zao. CCM wamebaki na mbinu moja tu ya kuwategemea wakurugenzi na NEC, ili wawavushe hapo walipo kwenye tope kwenda nchi kavu. Katika hotuba zake sasa ajikite kuwahimiza wananchi kulinda kura zao, hii ngoma imeshaisha . Wakurugenzi na hawa watendaji kata ambao wamepewa maelekezo marafuku kuwatangaza wapinzani kwenye maeneo yao ndio imekuwa mwiba na Wapinzani wasipo jipanga vizuri mwishoni wataumizwa na hao watu.

Ushauri wangu Lissu sasa ajikite katika kulinda kura. Watendaji wa kata si wa kuchekewa na kuendelea kuachwa kwani kwanza ni watu wa chini mno, lakini ni watu ambao wameshapokea vitisho, hivyo inabidi kazi ya ziada ifanyike. Umati kwa umati Huo Huo wanaojaa kwenye mikutano yao wahimizwe pia wawepo hivyohivyo kwenye kulinda kulinda kura zao kwenye vituo vya kata na ofisi za wakurugenzi. Kwa umati ule wa mwanza wakifanikiwa kukaa kwenye kata na ofisi za wakurugenzi kazi itakuwa imeisha.

Kama una hoja nyingine ambayo unaona bado Lissu bado hajaizungumzia ambayo inaweza kuteka mioyo ya watu iweke hapa ,lakini pia unaweza kupendekeza mbinu sahihi ya kulinda kura

Chaaaaao, tuonane 28 oktoba
Pia, Utamaduni mpya uliasisiwa na CCM MPYA nchini, yaani utekaji wa watu na ubambikaji wa kesi zisizo na dhamana kwa wananchi wasio na hatia
 
Lissu ni kama vile ameshashinda uchaguzi huu kwa hoja zake 7 ambazo zimepata nguvu na kuaminiwa na jamii. Na hii inajidhihirisha maeñeo mbalimbali ambayo amepita kufanya kampeni.

Lissu ni kama vile mhubiri wa injili, kila eneo analopita shetani anapoteza nguvu na neno linabaki mioyoni mwa watu. Maeneo ambayo bado hajapita ndio yamebaki kuzungumzia habari za CCM, lakini yatakapofikiwa na habari njema ya injili ya wokovu na ubatizo wa maji mengi na wao wataachana na CCM.

Hoja 7 ambazo Lissu zimemwongezea nguvu toka kwa makundi mbalimbali ambazo CCM wamekosa majibu yake

1. Vitambulisho vya wajasiliamali;

Ni hoja ambayo imepokelwa vizuri na watamzania, kila kona.CCm wameshindwa kujibu hadi sasa, wamebaki tu kudema dema kwenye majibu yao kwamba magufuri anawapenda wamachinga, Mara vitambulisho sio lazima ,wakati wamevitungia na sheria tayari. Lissu shikilia hapo hapo kwa mpaka waeleze ni lini wamachinga walioomba wauziwe vitambulisho visivyo na picha wala jina

2. Maslahi ya watumishi, nyongeza ya mshahara.

Hoja ambayo haijajibiwa hadi Leo, na ccm wamekosa majibu wakaeleweka kwa wananchi. . Nyongeza ya mshahara ni takwa la kisheria na sio takwa la mtu . Alisikika Mara moja akisema hajapandisha mshahara ila edhibiti mfumuko wa bei, na akapata majibu yake toka kwa Lissu kwamba bei ya sukari ya 2015 na Leo 2020 ipo sawa, ? "Wananchi hapana" Lissu " anatuambia nini. Baba shikilia hapo hapo wameshalegea na hawana majibu

3. Suala la pension na kiinua mgongo kwa wastaafu

Watu wengi walikuwa gizani na suala lakini baada ya kulitolea maelezo sasa nalo limepata hamasa miongoni kwa watanzania kwamba kuanzia mwakani wastaafu hawatapata pension zao zote baadala yake watapata nusu. Hilo limeonekana kuwa chuki kwa makundi hayo na CCM wameshindwa kutolea majibu ya kueleweka . Lissu shikilia hapo hapo wamesha nyooka tayari

4. Ujenzi wa uwanja wa ndege Chato na hifadhi ya wanyama

Hoja hapa sio ujenzi ,hoja inayoonekana hapa ni namna mradi unavyotekelezwa kwa ufisadi mkubwa wa kupeana tenda na Ndugu yake Mayanga . Mpaka Leo hoja hiyo Magufuli na CCM yake wameshindwa kuitolea majibu, kwa nini aingilie mchakato wa tender na kuagiza apewe ndugu yake na watu sasa huku wanasema ni kama mtu ameamua kupitishia di kwa ndugu yake. Amenipigia pasi kwa mbele ,na suala la hifadhi pia ndio hawana majibu kabisa .Baba Lissu shikilia hapo hapo wamesha nyong'onyea tayari

5. Suala la ununuzi wa ndege

Hii hoja ilianza kwa kasi mwanzoni kunadiwa na ccm lakini baada ya Lissu kuanza kushughurika Nayo wameshakimbia. Lissu amezungumzia masuala ya Faida na mchakato wa ununuzi wa midege hiyo imegubikwa na ufisadi mkubwa na kwamba anayejua ni Magufuri na mjomba wake Dotto James. CCM mpaka Leo wamepoteana na ajenda ya ndege sio ajenda yao tena kwenye kampeni zao.Lissu wabananishe hapo hapo kwenye kona washindwe pa kutokea.

6: Ukosefu wa Ajira kwa makundi mbalimbali

Eneo hili limepata uungwaji mkono mkubwa toka kwa makundi mbali mbali ya vijana. Tangu 2015 ajira zimetolewa kwa walimu wa sayansi na kada za afya. Kada nyingine hazijaguswa kabisa . Hoja yake hapa magufuri imebaki kuwa ni watu wajiajiri wakati yeye mtoto wake Jesca amemwajiri wizara ya mambo ya nje, mwingine amempa RAS iringa .hao walishindwa kujiajiri hadi awaajiri. Watoto wa wanyonge ndio wanaohimizwa kujiajiri. Hapo napo Lissu shikilia hapo hapo pana tija na kundi kubwa la wahanga

7: Waathirika wa vyeti feki
Hii ni hoja ambayo imepata kusemwa na Lissu, kwamba hao walio wa ajiri ni wao ccm na kinachozungumzwa hapa ni watu kufukuzwa kama mbwa bila kupewa mafao yao, ambayo wamechangia kwa miaka mingi halijulikani lilipo enda. Hao ni watanzania wenzetu na sio wakenya wala wamalawi, wamelitumikia na kutufundishia watoto wetu kwa miaka mingi hadi wengine wamekuwa maprofesa. Michango yao ipo wapi kama hawajapewa, Magufuri na ccm yao iliyojaa roho ya kuumiza watu waseme wamepeleka michango yao ya pension waliyokuwa wanachangia kwenye mifuko ya hifadhi

Nashauri Lissu sasa kwa kuwa kwenye miji yote na vijijini amefanikiwa kuiteka sasa ajikite katika kuwaaminisha watanzania ni namna gani walinde kula zao. CCM wamebaki na mbinu moja tu ya kuwategemea wakurugenzi na NEC, ili wawavushe hapo walipo kwenye tope kwenda nchi kavu. Katika hotuba zake sasa ajikite kuwahimiza wananchi kulinda kura zao, hii ngoma imeshaisha . Wakurugenzi na hawa watendaji kata ambao wamepewa maelekezo marafuku kuwatangaza wapinzani kwenye maeneo yao ndio imekuwa mwiba na Wapinzani wasipo jipanga vizuri mwishoni wataumizwa na hao watu.

Ushauri wangu Lissu sasa ajikite katika kulinda kura. Watendaji wa kata si wa kuchekewa na kuendelea kuachwa kwani kwanza ni watu wa chini mno, lakini ni watu ambao wameshapokea vitisho, hivyo inabidi kazi ya ziada ifanyike. Umati kwa umati Huo Huo wanaojaa kwenye mikutano yao wahimizwe pia wawepo hivyohivyo kwenye kulinda kulinda kura zao kwenye vituo vya kata na ofisi za wakurugenzi. Kwa umati ule wa mwanza wakifanikiwa kukaa kwenye kata na ofisi za wakurugenzi kazi itakuwa imeisha.

Kama una hoja nyingine ambayo unaona bado Lissu bado hajaizungumzia ambayo inaweza kuteka mioyo ya watu iweke hapa ,lakini pia unaweza kupendekeza mbinu sahihi ya kulinda kura

Chaaaaao, tuonane 28 oktoba
HOJA HIZO ZINAWAGUSA WATANZANIA WENGI WANAONYANYASWA NA WERIKALI ONEVU
 
Back
Top Bottom