Kwani wananchi ni Chadema,na kipi kinachowafanya muamini nyie ndo mko sawa na wala sio yeye,ila namsifu dogo yaani hajataka hata kuwajibu yaani kuiweka level yake juu zaidi ya mgombea mmoja wa uraisi yule kichaa wa ubelgiji
Kwani sasa kashindwa,kwa kipimo gani kilichoonyesha kashindwa,nyie ndo mmejionyesha msivyo na akili
 
Ninazo sababu nzuri, sasa unazihitaji za nini wakati umeshaniita mfuata mkumbo?

Wewe umefanya kwa sababu zipi mkuu, ili tukuondoe pia kwenye group la wafata mkumbo, maana umeshasema si mwanasiasa na si mwanaharakati.
 
Ni kwelu
 
Lissu ni mwanaharakati au ni kiongozi wa Chadema?Ukijibu hili swali utajielewa kama wewe ni Nyumbu au binadamu wa kawaida
 
Unapo simama na upande usio wa haki una poteza yote kutoka kwa wapenda haki na ustawi wa taifa.
𝚄𝚙𝚊𝚗𝚍𝚎 𝚞𝚜𝚒𝚘 𝚗𝚊 𝚑𝚊𝚔𝚒 𝚔𝚠𝚊 𝚖𝚊𝚘𝚗𝚘 𝚢𝚊𝚔𝚘 𝚋𝚘𝚝𝚑𝚎𝚛..! 𝚠𝚊𝚙𝚘 𝚠𝚊𝚗𝚊𝚘𝚗𝚊 𝚔𝚞𝚠𝚊 𝙸𝚜𝚛𝚊𝚎𝚕 𝚗𝚒 𝚑𝚊𝚔𝚒 𝚢𝚊𝚘 𝚔𝚞𝚛𝚞𝚜𝚑𝚊 𝚖𝚊𝚔𝚘𝚖𝚋𝚘𝚛𝚊 𝙶𝚊𝚣𝚊 𝚔𝚞𝚠𝚊𝚞𝚊 𝚆𝚊𝚙𝚎𝚕𝚎𝚜𝚑𝚒𝚗𝚊 𝚕𝚊𝚔𝚒𝚗𝚒 𝚠𝚊𝚙𝚘 𝚠𝚊𝚗𝚊𝚘𝚗𝚊 𝚆𝚊𝚙𝚊𝚕𝚎𝚜𝚝𝚒𝚗𝚊 𝚠𝚊𝚗𝚊 𝚑𝚊𝚔𝚒 𝚔𝚞𝚕𝚒𝚙𝚒𝚐𝚊𝚗𝚒𝚊 𝚃𝚊𝚒𝚏𝚊 𝚕𝚊𝚘.
 
Unapokuwa

1. Mfanya biashara

2. Msanii

3. Mtumishi wa Mungu (sheikh, mchungaji no)

Unayehudumia watu wa vyama, dini, itikadi na mitazamo tofauti.

Epuka kujifungamanisha upande mmoja, toa huduma kwa usawa bakia katikati...

Ukijifungamanisha na upande mmoja nakuwazodoa wa pande zingine basi kubali matokeo. Watakapo kusurubu usitafute mchawi.
 
Naona unachanganya biashara na haki. Yule ni mfanyabiashara, na mfanyabiashara yeyote anafata masirahi. Weka hii akilini
Ashakula biashara yake, bila shaka ilimlipa sana.

Sasa ni nini tena anataka?

Kama anataka biashara nyingine atayapata Chato makaburini

Si ana miguu aende
 
Ninazo sababu nzuri, sasa unazihitaji za nini wakati umeshaniita mfuata mkumbo?
Punguza jazba mkuu,

Tusaidie izo sababu ili tunufaike na kuelimika pamoja.
 
Haikuwa busara kwa mond kipigania ccm kwenye uchaguzi wakati akijua watz ni wanachama wa vyama mbali mbali!!!Hata ivyo atamfuata mwendazake kimziki halafu badae kiroho na nafsi!!
 
Lissu ni mwanaharakati au ni kiongozi wa Chadema?Ukijibu hili swali utajielewa kama wewe ni Nyumbu au binadamu wa kawaida

Kwanza upo nje ya mada by 180 degrees hebu jitafakali uone hilo la Lisu na huu uzi.
 
Bila kumtaja Ney wa mitego na Roma utakuwa unajidanga akili yako tu
 
Mkuu unataka kusema Abood Mabasi yake hayana wateja, Mwana FA mziki wake hausikilizwi pia gwajima kanisa lake sasa ivi halina waumini.

Au nataka kutuambia kuwa wanaccm wasi support mziki wa professor J kwa sababu ni wa upande wa pili
 
Hawa watu wanatuchanganya mkuu, Wako bungeni miaka kibao leo wanataka mapishi yaliyowashinda wao wakati wako jikoni wamtwishe Diamond.

Yani Diamond leo ndo kawa sababu ya chama fulani kutofanikiwa katika mambo fulani.
Niliingia kwenye website ya change.org nikaangalia petition inayotaka diamond asiwemo kwenye kinyang'anyiro na nikaangalia petition inayotaka diamond abaki kwenye kinyang'anyiro.

Zote zimetoa sababu kwanini zinaamini petition yao inastahili kupigiwa kura. Hata wewe kama una hamu ya kujua kilichopelekea petition kuanzishwa ingia change.org juu kulia kuna mistari 3 inaangalia chini. Bonyeza hiyo mistari utaona option ya search.

Kubali search na andika 'bet diamond' itakuja petition utasoma sababu za walioanzisha petition na utaacha kubishana na watu humu.

Kutoka hapo mimi nasema kwamba ilikua ngumu sana kwa diamond na wasanii wengine kujiweka mbali na makonda na ccm kwa ujumla. Na wala haina haja ya kuelezea kila mtu anajua maisha yalivyokua.

Roma alisema vyema, alisema 'Siogopi kufa ila nawaachaje wanaobaki?' ile crackdown ilikua ni ama ikuguse au uwe karibu na serikali ili isikuguse. Wanafananisha na swala la kile kitengo cha SARZ cha Nigeria, kuna tofauti kubwa kati ya kutaka askari waache ukatili na kutaka rais aache ukatili.

Watu wana chuki zinaishi kwa miaka katika hii petition ndiyo wamepata pa kupumzikia. Jana nacheki ilikua signed na watu 7K leo jioni imepostiwa screenshot ni 12K and counting. Ya kutaka asitolewe jana niliona ina saini 100 leo 1K and counting.

Mashabiki badala ya kuonyesha mnavyomkubali kwa kwenda kusaini petition ili asiondolewe mpo bize kuanzisha nyuzi za lawama.
 
Narudia,
Nina sababu tofauti kabisa na wanzosema wengi lakini nieleze kwa nini nikueleze wakati kila post yako unanipachika jina la kejeli?

Umeanza kuniita mfuata mkumbo sasa unaniita mwenye jazba sijui utakanijibu hii utaniitaje.


Punguza jazba mkuu,

Tusaidie izo sababu ili tunufaike na kuelimika pamoja.
 
Hawa watu siku wakishika usukani tutegemee visasi tu
Kwahali iliyopo ni bora hao na visasi vyao kutawala maana watadeal ns wabaya wao kuliko ninyi mnaowaua waliowashinda katika chaguzi wasiohatia ili mtawale kwa dhulma.
 
Hahahahaha
Kama wao walishindwa kubadili mapishi wakiwa kule jikoni na walikuwa wengi, Diamond ndo ataweza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…