Mwigulu Nchemba: Tumefuta baadhi ya tozo, nyingine tumepunguza kwa asilimia 10-50


Akizungumza leo bungeni, Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba amesema uongezwaji wa wigo wa kukusanya mapato kupitia tozo uliibua malalamiko kwenye jamii, hivyo Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi iliagiza upitiwaji upya wa tozo hizi na kuzingatia maoni ya wananchi.

Marekebisho yafuatayo yamefikiwa-
  • Kufuta tozo ya kuhamisha fedha kutoka benki kwenda mitandao ya simu kwa pande zote.​
  • Kufuta tozo ya kuhamisha fedha ndani ya benki moja na kutoka benki moja kwenda benki nyingine.​
  • Kutowahusisha wafanya biashara wadogo (merchants) kama ilivyokuwa kweye kanuni ya sasa.​
  • Kusamehe tozo ya miamala kwenye utoaji wa fedha taslimu kupitia wakala wa benki yaani ATM kwenye miamala yenye thamani ya chini ya tsh 30,000/=​
  • Kupunguza gharama ya miamala kwa asilimia 10-50 kutokana na makundi ya miamala​

Marekebisho haya yataanza kufanya kazi Octoba 1, 2022. Aidha Serikali itafuta utaratibu wa kodi ya zuio ya pango inayotaka kukusanywa na mpangaji, hivyo kwa sasa itapaswa kulipwa na mmiliki wa nyumba na siyo mpangaji.

Kwa kuwa pesa hizi zitaipunguzia mapato serikali, Waziri ameelekeza Serikali ianze kubana matumizi yake mfano kwenye vikao, mafunzo ya semina, warsha, safai za ndani na nje, misafara, kukagua miradi n.k

Wataalamu wa wizara ya fedha na mipango ndiyo wamefanya mapitio haya wakiwa ofisini kwa kuwa ni sehemu ya majukumu yao. Taarifa za kuwa kuna tume iliundwa kutoka nje ya wizara ni uzushi.

Hili la kodi ya pango kulipa mwenye nyumba kama ni kweli limebadilishwa basi sisi tuliokuwa tunapinga hili wametusikiliza

Na nawapongeza kwa hilo lakini pia bado sijajua vizuri zile tozo zingine za kutoa pesa pale kwa dirisha nazo zipo au mimi ndio sijaelewa.
 
KAZI nzuri ya CCM. Imesikia kilio hiki. Tozo sio tatizo lakini shida Ilikuwa ni kiwango Cha tozo.

Hakuna nchi duniani inaweza kuhudumia watu wake bila kulipa Kodi na tozo zinazostahili. Hata kama ni chadema(japo waameishiwa hoja) wakibahatika kupata serikali labda kuanzia miaka ya 2150 watatoza tozo.

Nimpongeze sana bwana nchemba Kwa kusikia kilio hiki na maelekezo ya CCM.
KIBARAKA WEYE!
 
Kwenye Kodi ya nyumba kwamba atalipa mwenye nyumba badala ya mpangaji is a game of minds!

Hii ni sawa na mganga wa kutibu ambaye anaweza kuhamisha jipu toka kwapa ya kushoto na kupeleka kwapa ya kushoto na kutamba kwapa ya kushoto iko salama.

Kodi ya nyumba itapanda, mpangaji hajapona jipu kwenye mwili wake, limhamia sehemu nyingine ya mwili!
 
Huyu jamaa ni janga kwa Taifa. Ni vile tu Nchi yetu ni ya One Man Show!

Tungekuwa na utawala bora na wa wazi, alitakiwa alazimishwe kujiuzulu. Maana hana uwezo wa kuongoza hii Wizara kwa ufanisi.
Acha tu.

"Kusamehe tozo ya miamala kwenye utoaji wa fedha taslimu kupitia wakala wa benki yaani ATM kwenye miamala yenye thamani ya chini ya tsh 30,000/="


Wanavyo sema kusamehe kama vile tumefanya kosa kuhifadhi hela kwenye banks.
 


Akizungumza leo bungeni, Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba amesema uongezwaji wa wigo wa kukusanya mapato kupitia tozo uliibua malalamiko kwenye jamii, hivyo Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi iliagiza upitiwaji upya wa tozo hizi na kuzingatia maoni ya wananchi.

Marekebisho yafuatayo yamefikiwa-
  • Kufuta tozo ya kuhamisha fedha kutoka benki kwenda mitandao ya simu kwa pande zote.​
  • Kufuta tozo ya kuhamisha fedha ndani ya benki moja na kutoka benki moja kwenda benki nyingine.​
  • Kutowahusisha wafanya biashara wadogo (merchants) kama ilivyokuwa kweye kanuni ya sasa.​
  • Kusamehe tozo ya miamala kwenye utoaji wa fedha taslimu kupitia wakala wa benki yaani ATM kwenye miamala yenye thamani ya chini ya tsh 30,000/=​
  • Kupunguza gharama ya miamala kwa asilimia 10-50 kutokana na makundi ya miamala​

Marekebisho haya yataanza kufanya kazi Octoba 1, 2022. Aidha Serikali itafuta utaratibu wa kodi ya zuio ya pango inayotaka kukusanywa na mpangaji, hivyo kwa sasa itapaswa kulipwa na mmiliki wa nyumba na siyo mpangaji.

Kwa kuwa pesa hizi zitaipunguzia mapato serikali, Waziri ameelekeza Serikali ianze kubana matumizi yake mfano kwenye vikao, mafunzo ya semina, warsha, safai za ndani na nje, misafara, kukagua miradi n.k

Wataalamu wa wizara ya fedha na mipango ndiyo wamefanya mapitio haya wakiwa ofisini kwa kuwa ni sehemu ya majukumu yao. Taarifa za kuwa kuna tume iliundwa kutoka nje ya wizara ni uzushi.

Iyo no nne namna GANI pale , mfano mwanafunzi,au mfanyakazi ambae Sasa anatoa pesa atalazimika kuwa anatoa elfu thelathin ili akwepe Makato , Hawa watu wa Mipango wanajielewa kweli ?

Mabenki yanalipa kodi pitia miamala mbalimbali inayofanywa na watanzania, tozo za benk zinatakiwa kuondoka zote, Mambo kama haya ya ajabu ndo maana mnazalilishwa nje HUKO,

Waziri jiuzuru ijulikane MOJA ,
 
Nani aliwashauri kuziweka hizo tozo na viwango vyake mara ya kwanza kabla ya kusikia kilio hiki?
Ukiombwa utoe risiti za malipo ya Kodi huwezi kutoa. Halafu kutwa kucha unashinda humu na malalamiko ya serikali haijuhudumii. Wenzako wakatwe Kodi wewe unakuza masaburi tu.
 
Waenda na biti mmeanza panya nyie. Si mlikuwa mnatetea Tozo mnasema ni lazima zilipwe na mkaisifu serekali na kuainisha sijui zinajenga vituo vya afya vingapi sijui. Hebu oneni aibu saa zingine kuwa mabendera fata upepo
Unajua wangapi wanalipa Kodi kati ya wanaostahili kulipa?. Je njia rahisi ni ipi ya kuwafanya walipe pia?
 
Acha tu.

"Kusamehe tozo ya miamala kwenye utoaji wa fedha taslimu kupitia wakala wa benki yaani ATM kwenye miamala yenye thamani ya chini ya tsh 30,000/="


Wanavyo sema kusamehe kama vile tumefanya kosa kuhifadhi hela kwenye banks.
Yaani hapa tumepigwa changa laacho. Kiufupi bado tozo zipo kwenye hiyo miamala ya kibenki! Sasa elfu 30 ndiyo hela gani hiyo katika dunia ya sasa!!
 
Halafu baada ya kuongea hayo atatarajia kusifiwa...

Tengeneza tatizo, rekebisha tatizo, then pata ujiko...
 
Back
Top Bottom