Papa Francis: Mapenzi ya Jinsia Moja siyo Kosa, siyo Uhalifu, lakini ni Dhambi
Read between the lines, Anyway,

- Ni kweli sote ni wa Muumba

-Ni kweli kwa nchi zilizohalalisha ushoga, inakuwa si uhalifu.

Ila je, amesema sio dhambi?
Binafsi naona kuna mambo ya kuwa straight na mambo ya kulainisha lainisha. Mkuu wa kanisa akiuzungumzia ushoga auadress kama jambo ambalo kweli ni chukizo mbele za MUNGU.
 
Hello Wadau.

Papa Francis wa RC ya Vatican ameupiga Mwingi Kwa Kuunga mkono ushoga,na kusema Mashoga sio wahaliifu, na kwamba ni Wana wa Mungu pia.🙄🙄

Haijaeleweka mara Moja ikiwa huu ndio Msimamo wa Kanisa Katoliki au ni maoni ya binafsi ya Papa Francis.

Commets ziwe fupi fupi tafadhari.
Soma hii hapa chini itakusaidia kuelewa, na bahati nzuri ililetwa humu humu JF

 
Papa Francis amekosoa sheria zinazoharamisha mapenzi ya jinsia moja kuwa "sio haki", akisema Mungu anawapenda watoto wake wote jinsi walivyo na kuwataka maaskofu wa Kikatoliki wanaounga mkono sheria hizo kuwakaribisha watu wa LGBTQ kanisani.
"Kuwa mpenzi wa jinsia moja si kosa," Francis alisema wakati wa mahojiano Jumanne na The Associated Press.
Francis alikiri kwamba maaskofu wa Kikatoliki katika baadhi ya sehemu za dunia wanaunga mkono sheria zinazoharamisha mapenzi ya jinsia moja au kubagua jamii ya LGBTQ, na yeye mwenyewe alitaja suala hilo kwa maneno ya "dhambi".
Lakini alihusisha mitazamo hiyo na asili ya kitamaduni na kusema maaskofu hasa wanahitaji kupitia mchakato wa mabadiliko ili kutambua utu wa kila mtu.
"Maaskofu hawa wanapaswa kuwa na mchakato wa uongofu," alisema, akiongeza kwamba wanapaswa kutumia "huruma, upole, kama Mungu ana kwa kila mmoja wetu".
Baadhi ya nchi 67 au mamlaka duniani kote zinaharamisha shughuli za ngono za watu wa jinsia moja zilizokubaliwa, 11 kati ya hizo zinaweza au kutoa hukumu ya kifo, kulingana na Human Dignity Trust, ambayo inafanya kazi kukomesha sheria hizo. Wataalamu wanasema kwamba hata pale ambapo sheria hazitekelezwi, zinachangia unyanyasaji, unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya watu wa LGBTQ.
Akitangaza sheria kama hizo "sio za haki", Francis alisema Kanisa Katoliki linaweza na linapaswa kufanya kazi ili kukomesha. "Lazima ifanye hivi. Ni lazima ifanye hivi,” alisema.
Francis alinukuu Katekisimu ya Kanisa Katoliki kwa kusema wapenzi wa jinsia moja lazima wapokewe na kuheshimiwa, na hawapaswi kutengwa au kubaguliwa.

BBCswahili.com

================
Hapa ndipo ninapomkubali saaana Kamanda PUTIN
Taarifa hii ina upotoshaji wa makusudi, ipuuzwe
 
Huwa sichangii topics ambazo watu hutumia hisia zaidi kuliko akili Ila nitajibu kwa huu upotoshaji unaofanywa na hii thread

Papa hajasema ushoga sio dhambi na hana mamlaka hiyo ya kuihalalisha dhambi maana ukisema anayo bhasi utaamini papa yupo juu ya mamlaka ya Mungu, kitu ambacho si kweli

Ila kitu alichomaanisha
"Kila uhalifu ni dhambi Ila si kila dhambi ni uhalifu"

Ndio maana hata wewe upo huru kuisaliti ndoa yako utakavyo pasipo dini kusema upigwe mawe kwa sababu si uhalifu

Kingine Mungu aliiteketeza sodoma na Gomorah kwa sababu ya homosexuality lakini gharika ya Mungu iliteketeza kila mtu. hata Yona alitumwa kuwahubiria watu wa ninawi kuwa hasira ya Mungu ipo juu yao na mji ungeteketezwa
Hivyo, utaona kuwa HASIRA YA MUNGU IPO KATIKA KILA UHARIBIFU NA UCHAFU TUNAOUFANYA

Na kama haitoshi, biblia ikaainisha wazi kuwa ni dhambi gani isiyosameheka

M A R K O 3:28-29 “Amin, nawaambia, Dhambi zote watasamehewa wanadamu, na kufuru zao watakazokufuru zote; bali mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hana msamaha hata milele; ila atakuwa ana dhambi ya milele”.


Hivyo, wewe mzinzi, mlevi, msengenyaji, mwizi na kila aina ya dhambi, HASIRA YA MUNGU IPO JUU YETU SOTE lakini Mungu kwa rehema zake, wote ni wake na tunastahili msamaha wake tukijinyenyekeza na kufanya toba

Hivyo,kwa kauli hii, papa hajakosea [emoji1431][emoji1431]
Nimekupenda bure
 
Hivi hili Kanisa nalo Lina waumini ??. jamaa ni anaruhusu Waumini wake kufirana , yaan Anasahau kwamba Sodoma na Gomorra zilichomwa moto Kwa sbabau ya mapenzi ya Jinsia Moja!!!

Saa 1 iliyopita
Papa Francis amekosoa sheria zinazoharamisha mapenzi ya jinsia moja kuwa "sio haki", akisema Mungu anawapenda watoto wake wote jinsi walivyo na kuwataka maaskofu wa Kikatoliki wanaounga mkono sheria hizo kuwakaribisha watu wa LGBTQ kanisani.

"Kuwa mpenzi wa jinsia moja si kosa," Francis alisema wakati wa mahojiano Jumanne na The Associated Press.

Francis alikiri kwamba maaskofu wa Kikatoliki katika baadhi ya sehemu za dunia wanaunga mkono sheria zinazoharamisha mapenzi ya jinsia moja au kubagua jamii ya LGBTQ, na yeye mwenyewe alitaja suala hilo kwa maneno ya "dhambi".

Lakini alihusisha mitazamo hiyo na asili ya kitamaduni na kusema maaskofu hasa wanahitaji kupitia mchakato wa mabadiliko ili kutambua utu wa kila mtu.

"Maaskofu hawa wanapaswa kuwa na mchakato wa uongofu," alisema, akiongeza kwamba wanapaswa kutumia "huruma, upole, kama Mungu ana kwa kila mmoja wetu".

Baadhi ya nchi 67 au mamlaka duniani kote zinaharamisha shughuli za ngono za watu wa jinsia moja zilizokubaliwa, 11 kati ya hizo zinaweza au kutoa hukumu ya kifo, kulingana na Human Dignity Trust, ambayo inafanya kazi kukomesha sheria hizo. Wataalamu wanasema kwamba hata pale ambapo sheria hazitekelezwi, zinachangia unyanyasaji, unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya watu wa LGBTQ.

Nchini Marekani, zaidi ya majimbo kumi na mbili bado yana sheria za kupinga mapenzi ya jinsia moja kwenye vitabu, licha ya uamuzi wa Mahakama ya Juu wa 2003 kutangaza kuwa ni kinyume cha katiba.


Umoja wa Mataifa mara kwa mara umekuwa ukitoa wito wa kukomeshwa kwa sheria zinazoharamisha mapenzi ya jinsia moja , ukisema zinakiuka haki za faragha na uhuru wa kutobaguliwa na ni ukiukaji wa majukumu ya nchi chini ya sheria za kimataifa kulinda haki za binadamu za watu wote, bila kujali mwelekeo wao wa kijinsia au utambulisho wa kijinsia.

Akitangaza sheria kama hizo "sio za haki", Francis alisema Kanisa Katoliki linaweza na linapaswa kufanya kazi ili kukomesha. "Lazima ifanye hivi. Ni lazima ifanye hivi,” alisema.

Francis alinukuu Katekisimu ya Kanisa Katoliki kwa kusema wapenzi wa jinsia moja lazima wapokewe na kuheshimiwa, na hawapaswi kutengwa au kubaguliwa.

"Sisi sote ni watoto wa Mungu, na Mungu anatupenda jinsi tulivyo na kwa nguvu ambayo kila mmoja wetu anapigania utu wetu," Francis alisema, akizungumza na AP katika hoteli ya Vatican anakoishi.

Sheria hizo ni za kawaida barani Afrika na Mashariki ya Kati na ni za wakati wa ukoloni wa Waingereza au zimeongozwa na sheria za Kiislamu.

Baadhi ya Maaskofu wa Kikatoliki wameziunga mkono kwa nguvu kwamba zinaendana na mafundisho ya Vatikani ambayo yanachukulia vitendo vya mapenzi ya jinsia moja kuwa "vina machafuko ya asili", huku wengine wakitaka zibatilishwe kama ukiukwaji wa utu msingi wa binadamu.



Mnamo mwaka wa 2019, Francis alitarajiwa kutoa tamko la kupinga kuharamishwa kwa mapenzi ya jinsia moja wakati wa mkutano na vikundi vya haki za binadamu ambavyo vilifanya utafiti juu ya athari za sheria kama hizo na kile kinachoitwa "matibabu ya ubadilishaji".

Hatimaye, papa hakukutana na makundi, ambayo badala yake yalikutana na mtu Nambari 2 Vatikani, ambaye alithibitisha tena "hadhi ya kila mtu na dhidi ya kila aina ya vurugu".

Siku ya Jumanne, Francis alisema kuna haja ya kuwa na tofauti kati ya uhalifu na dhambi kuhusiana na mapenzi ya jinsia moja.

"mapenzi ya jinsia moja si kosa," alisema. "Sio uhalifu. Ndio, lakini ni dhambi. Sawa, lakini kwanza tutofautishe kati ya dhambi na uhalifu.”

"Pia ni dhambi kukosa hisani," aliongeza.

Mafundisho ya Kikatoliki yanashikilia kwamba ingawa wapenzi wa jinsia moja lazima waheshimiwe, vitendo vyao "vina machafuko ya asili". Francis hajabadilisha mafundisho hayo, lakini amefanya kufikia jumuiya ya LGBTQ kuwa alama mahususi ya upapa wake.

Kuanzia na tamko lake maarufu la 2013: "Mimi ni nani kuhukumu?" alipoulizwa kuhusu kasisi aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wa jinsia moja , Francis ameendelea kuhudumu mara kwa mara na hadharani kwa jumuiya ya wapenzi wa jinsia moja na waliobadili jinsia .

Akiwa askofu mkuu wa Buenos Aires, alipendelea kutoa ulinzi wa kisheria kwa wapenzi wa jinsia moja kama njia mbadala ya kuidhinisha ndoa zao, jambo ambalo mafundisho ya Kikatoliki yanakataza.

Licha ya mawasiliano hayo, Francis alikosolewa na jumuiya ya Wakatoliki wa LGBTQ kwa amri ya 2021 kutoka ofisi ya mafundisho ya Vatikani kwamba kanisa haliwezi kubariki muungano wa watu wa jinsia moja "kwa sababu Mungu hawezi kubariki dhambi".

Vatikani mwaka wa 2008 ilikataa kutia saini tamko la Umoja wa Mataifa lililotaka kukomeshwa kwa mapenzi ya jinsia moja, ikilalamika kuwa maandishi hayo yalikwenda nje ya upeo wa awali na pia yalijumuisha lugha kuhusu "mwelekeo wa kijinsia" na "utambulisho wa kijinsia" .

Katika taarifa yake wakati huo, Vatikani ilizitaka nchi kuepuka "ubaguzi usio wa haki" dhidi ya wapenzi wa jinsia moja na kukomesha adhabu dhidi yao.
 
Tuanze na hii. Hapa Bongo mlishawahi kusikia mtu amepelekwa mahakamani kwa kosa la kuwa shoga?
Yap kipindi cha yule bwana wa Chato James Delicious alikanyaga kisutu na vimatako vyake
 
Niliwahi kusema swala hili wana jf baadhi wakanibishia haya sasa yakowapi maneno yangu ndio haya leo bbc wanayasema
FB_IMG_16728100172396636.jpg
 
Maaneno kama haya ya papa ni maumivu sana. Kwahyo kuoa wanawake wawili kwa mkatolik ni uhalifu/dhambi
 
Binafsi naona kuna mambo ya kuwa straight na mambo ya kulainisha lainisha. Mkuu wa kanisa akiuzungumzia ushoga auadress kama jambo ambalo kweli ni chukizo mbele za MUNGU.

Kiongozi wa Dini ana kazi ya kuzungumzia kila dhambi kama chukizo mbele za Mungu maana kila dhambi inaleta uharibiifu hivyo, Papa sio kiongozi wa kuendana na matakwa yetu sisi kuliko uhalisia wa kimaandiko na sheria ambazo anazisimamia

Japo kama kweli kasema, hii topic ni sensitive sana haswa kwa kipindi hiki ambazo tabia hizi zinakithiri na kupigwa vita hasa katika nchi ambazo kidini na kitamaduni zinauchukulia ushoga kama dhambi kubwa kuliko uuaji

Hivyo, lazma awe makini sana kama wale waliopita ambao hawakulizungumzia hili suala kiundani kabisaa kuogopa hizi backlash..

Ubaya kwa tunapokwenda, there is no way taasisi kubwa kama kanisa katholiki itaepuka kuliongelea japo kwa msimamo wa kibiblia there is no way wataitofautisha na dhambi nyinginezo kwa sababu hakuna kifungu imetofautishwa. Ngoja tuone
 
Back
Top Bottom