Tundu Lissu kulihutubia taifa Desemba 31, Watanzania tuwe tayari kumsikiliza

Tundu Lissu kulihutubia taifa Desemba 31, Watanzania tuwe tayari kumsikiliza

Tunasubiri hotuba kwa hamu kubwa. Hapa katikakati kumekuwa na hotuba za kurushiana maneno na unafiki mwingi.

Ngoja tukisikilize chuma cha reli kutoka Ubeligiji.
 
Offcourse Kwa social media hata mirinda na fanta ndipo zinapokutana na nyie vijana mliopotea

National address ina protocols zake

Na huwezi kuzijua if you dwell on insta, Facebook, wosapu, etc.

Endeleeni kunywa mirinda

Wala hatuhitaji kujua hizo protocals za taifa maana hata hao viongozi tunawadharau sana, kwani wako madarakani kwa wizi wa kura. Hatuna muda wa kusikiliza uongozi najisi. Nyie wazee ndio mna muda wa kusikiliza majizi ya kura kwenye usingizi mliolazwa juu ya kitanda kiitwacho amani.
 
Kwa akili yako unafikiri kwa nini nchi haikuchukuliwa mwaka 2010, 2015 na 2020?

Haya “matumaini” hewa yanapaswa kutupwa kule then lifanyike linalopaswa kufanyika. NEC hii na Katiba ya sasa haiwezi kumkabidhi Nchi mtu mwingine zaidi ya mgombea wa CCM. Kwa sasa hata Kibajaji au Msukuma akisimamishwa, atatangazwa mshindi
ninajua hakuna mazingira fair kisiasa bt mapambano dhidi ya katiba mpaya yanaleta tumaini kwa wapenda haki kuelekea 2025.
 
Huko shule mlienda kusomea ujinga au?,hayo maisha bora yanakujaje bila kuwa na katiba imara[emoji706][emoji706][emoji706].....,watanzania bado tuna safari ndefu
Mbowe, Msigwa, Heche, Lema na Mnyika wote wamekuwa na maisha bora tena chini ya katiba hii hii ya mwaka 1977.

Sasa wewe wanakwambia ili upate maisha bora mpaka kuwe na katiba mpya?
 
Mbowe, Msigwa, Heche, Lema na Mnyika wote wamekuwa na maisha bora tena chini ya katiba hii hii ya mwaka 1977.

Sasa wewe wanakwambia ili upate maisha bora mpaka kuwe na katiba mpya?

Zinduka wewe ZOMBIE umeshawekwa BOND.

Kwa taarifa yako hata chini vya wakoloni, kuna watanzania walikuwa na maisha bora, lakini bado tulidai uhuru bila kujali kuwa kuna watanzania wana maisha bora ndani ya huo ukoloni. Pls stop childsh arguments.
 
Hivi huyu bwana anatoa wapi moral authority ya kusema analihutubia taifa? Taifa gani linalohutubiwa na huyu bwana,ubeligiji, Tanzania au Kenya maana kwa Mara ya mwisho alikuja akaishia Kenya?

Hivi taifa linaweza hutubiwa na yeyote? Hata Mimi mwalimu niliyeko huku mpigamiti - Liwale naweza toa alert kuwa Leo watu wawe makini kunisikiliza kwani nitahutubia taifa!?

Serikali iwe makini na huyu mtu,hafai kabisa,anapenda kujipa mamlaka ambayo si ya kwakwe.

By the way Mr Robert Amsterdam hajambo huko ubeligiji?
Kwani hapa si unaongea na taifa?Mamlaka unatoa wapi?Tofauti nyenu ni kwamba yeye katoa taaruifa ila wewe unaropoka tu wkati wowote ila nyie wote ni wananchi
 
Mafundi wa TCRA tunawaweka standby kuanzia sasa hadi trh 2 jan 2022.

Wakae jirani na waya.
 
Jembe, Mungu akubarikia. Njoo nyumbani tumekumiss sana, na unahitajika kuliko wakati wowote ule.

atakuja 2025 kwenye uchaguzi mkuu.
Ukiisha atasema anawindwa atakimbia tena..kama mechi za ndondo cup tu...

2020 aliomba ahakikishiwe usalama ili arudi, bila shaka alihakikishiwa akarudi akagombea unyerere then usalama haukuwa guaranteed, akakimbia kulinda uhai wake...
 
Tarehe 31 Disemba,2021 saa kumi na mbili jioni Mheshimiwa Tundu Lissu Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa kulihutubia Taifa- kufunga mwaka 2021 kuzungumzia mipango na mikakati ya kuingia mwaka 2022.
View attachment 2062266
Duh....kuhutubia taifa?! Yeye Lissu skiwa Kama Nani? Ni Rais tu ndiye anayeweza kuhutubia taifa....ni Rais wa JMT ndiye anayeweza kuhutubia taifa...
 
Sema

Tundu Lissu kuhutubia Chadema na sio Taifa.
Yeye ni kiongozi wa chama chenu cha siasa.

Tuna vyama zaidi ya 20 vya siasa nchini na vyote vina wenyeviti na Makamu wenyeviti kama Lisu.

Mbona hatuwasikii wakifanya hizi mbwembwe za kifipa.

Masuala yenu ya chama yanabaki kuwa ya kwenu na wanachama wenu kitaifa.

Sio kutuletea upigaji hapa kujifanya anaongea na taifa wakati atawahutubia nyinyi kama nyinyi.

Mnajitahidi sana kumtengenezea mazingira ya kuendelea kukubalika huko Ubelgiji.kwamba Labda Lissu ana mamilioni nyuma yake, wakati uhalisia ni kwamba sivyo kabisa.

Lakini hata hao wazungu wanajua na kuona kinachoendelea hapa nchini kwa ufasaha kabisa.
 
Jipeni moyo na tutasubiri mtuketee ushahidi wa idadi ya wafuatiliaji wa hiyo hotuba.

Juzi kwenye lile mliita kongamano mbona hamkutupatia muendelezo?

Na yenyewe ilikuwa hivi hivi?

Tumechoka nae yuko huko kwa maria sarungi kila siku anabwabwaja, mbona hatuoni wafuatiliaji?
 
Mgombea Urais huyu alitutangazia kifo cha Rais wetu mpendwa tena mpaka ugonjwa uliomuua ilihali dola ilikuwa bado haijaamua kutuambia....

Wasiojua protocal, anapokufa Rais wa nchi huwezi tu kutangaza hovyohovyo harakaharaka maana kifo ni kitu cha ghafla na kwa wakati huo lazima dola ijipange kwanza kwa kuweka mambo sawa...Rais ni kiongozi wa dola, anapokufa lazima watu waitane kwanza waweke mambo sawa na kuset utaratibu na kuinform inner circle yote juu ya mipango na utaratibu...

Mgombea Urais huyu akatutangazia Kifo cha Mlinzi wa Rais Marehemu JPM na ugonjwa wake uliomuua tena kwenye media kubwa kabisa duniani BBC, ilihali huyu mlinzi alikuwa hai na mzima wa Afya kabisa..

Tunaweza kumuamini mtu kama huyu, eti tumpigie kura na kumpa dola...?
Wanachofanya ni kumtafutia au kumtengenezea mazingira ya kuendelea kuonekana na wazungu huko ubelgiji kwamba ana umuhimu kwao.
Wanamjengea Popularity isiyokuwepo.

Chadema ufanyaji siasa wenu ndio hupelekea muhisiwe vibaya saa ingine.
 
Hapo Hotuba yake nzima itakuhusu:

  • Mbowe
  • Katiba mpya
  • Tume huru ya uchaguzi
  • Kuhusu yeye mwenyewe

Wakati mahitaji ya Wananchi ni:

  • Gharama za maisha
  • Ajira
  • Umeme
  • Maji
  • Usalama.

Hawa watu ndio maana hakuna mwenye akili timamu huwa anawatilia maanani kabisa.
Ndugu
Ungekuwa kweli waamini hivyo unavyosema, usingekuwa unaendelea kuloloma na kulolosa. Ungeshajinyamazia.
Tumia uhuru na haki yako kumsikiliza umtakae hutakua unatenda kosa lolote wala kumkosea HESHIMA mtu yeyote. AMEN
 
Back
Top Bottom