Wanajeshi kwa waliohusika na tukio hili wawajibishwe
Najua hawapendi nzi.....
Najua hawawezi shoot yeye sio muhalifu.
Ni bora usababishe jam, ila sio uingie Ndani kwao.
Japo inaonekana Huyu Dogo ( nahisi ni kijana mdogo) alikuwa na makosa.....
Na ana kiburi chake binafsi cha hadi ya familia aliyotoka.
Uko sahihi.
Kwasababu anasema taa zimemruhusu, sasa zilimruhusu yeye mwenyewe??

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Pole yake sana...

Hawana mamlaka hayo wanatakiwa wakukabidhishe kwa traffic alafu wao waendelee na mambo yao, hawapaswi kupoteza muda na raia mambo yao ni chap chap...
 
Hii Tabia ya kuonea raia kisa tu ofisa wa usalama wa Taifa kakwaruzana na waendesha magari barabarani inatoka wapi?
Hii inaonyesha kuwa tuna Usalama wa Taifa incompentent, wasiojua kazi zao, ambao wanatumia nafasi zao kuonea watu.

Ni wapi katika majukumu ya usalama wa Taifa, Usalama wa Taifa unafanya kazi za Trafiki barabarani?

Leo hii ofisi na premise za usalama wa Taifa zinaenda kutumika kama parking ya kukamatia raia eti kisa raia kakwaruzana na ofisa mmoja huko barabarani ni ushamba wa hali ya juu na ni kuipaka Idara matope.

Tunataka Idara ya Usalama wa Taifa TISS imchukulie hatua za kinidhamu huyo ofisa anayeonekana kuleta kiburi kwa kutumia kazi yake kuonea watu.

Kibaya zaidi anaamrisha raia anyang'anywe simu yake bila search warrant au bila kufuata sheria za kipolisi, huu kama siyo ujambazi ni nini.

Huu utovu wa nidhamu ukomeshwe mara moja, hatutaki usalama wa Taifa unaoendeshwa kihuni.

View attachment 2182358
.
 
Hii ncho kila mtu anatakiwa awe na mtu fulani ndio mambo yaende tofauti na hapo utateseka sana
 
Kwa nini unasema hakukuwa na haja ya kumpeleka hapo?

Mimi Naona wamefanya sawa tu!
Fikiria, kamtoa kwenye mataa (kwa kumfanya kijana amfuate nyuma) hadi hapo kwao, lengo ni nini..?? Probably "hujanijua Mimi ni nani, ngoja nikuonyeshe". Unaweza fikiria kidogo ni umbali gani kutoka walipoanza kutofautiana hadi hapo kwao, kwann hakumzuia huko...?? Acheni ulimbukeni, kila mmoja akiwa hivyo hatutafika
 
Uko sahihi.
Kwasababu anasema taa zimemruhusu, sasa zilimruhusu yeye mwenyewe??

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app

Umesikia kachomekewa pia?

Je magari hata yamegusana?

Je alisimamishwa hata kuongea tu ila kuingiza gari getini?

Ukitaka undani wa yote fika knyama hao ndugu wote kwenye kadhia hii yumkini maelezo tayari wameandikishwa.

Je yote haya yalikuwa lazima?

Na aliwe mtu kichwa tu hapa.
 
Fikiria, kamtoa kwenye mataa (kwa kumfanya kijana amfuate nyuma) hadi hapo kwao, lengo ni nini..?? Probably "hujanijua Mimi ni nani, ngoja nikuonyeshe". Unaweza fikiria kidogo ni umbali gani kutoka walipoanza kutofautiana hadi hapo kwao, kwann hakumzuia huko...?? Acheni ulimbukeni, kila mmoja akiwa hivyo hatutafika
.
 
k
Hivi trafiki tuu ndio wakikusimamisha barabarani unalazimika kutii!?

Sent from my SM-G5500 using JamiiForums mobile app
Kwani sheria inasemaje?
Wewe siyo askari wa barabarani unisimamishe pasipo jambo la maana,nisimame ili nikuelimishe nini?
Kama hapo makosa ni ya huyo anayesimamisha,nisimame ili nini kitokee?
Badilisha akili yako.
 
Kwanza una uhakika gani huyo mtu kaonewa?

Pili clip inaanza kuonesha akilalamika na kuamriwa kupaki gari yake, haioneshi chanzo cha iyo tafrani ni nini? Una uhakika gani kuwa huyo afisa ndo mwenye kosa?

Tatu tangu lini kuambiwa upaki gari kukawa kuonewa?

Nne kupiga picha kwenye eneo ambalo hairuhusiwi kupiga picha Au kuchukua video ni kosa!
Point !
 
Wajeda hawajafanya poa ila na yeye jamaa ana chembechembe za uzembe ndani yake.

Kuna watu wanapenda sana haki ilhali hapa kwwtu huwa haipo, wewe umeona jamaa kakuchomekea kakukosa, jamaa kaja simama mbele yako yote hiyo anakutafuta tu. Unaacha kutafita upenyo usepe we unakaa kumsubiri hadi ashuke mbishane na ushajua atakuletea matatizo ikiwemo kukupotezea muda.

Kuepusha zogo ni kusepa tu, ushajua hawa watu akili zao ni ndogo nenda nao ivoivo uepukane na upotezewaji wa muda bila sababu za msingi, mashahidi wenyewe waoga kichizi hata kushuka hawashuki.

Zingatia umri na uzoefu wa dogo kimaisha ...
 
Hao ni chombo cha ulinzi na Usalama! Wana mandate zote kama kikosi cha ulinzi na usalama

Kaka polisi anavyosimama hao nao wanasimama barabarani na kutoa maelekezo wakiwa kwenye shughuli zao?

Mbona huulizi wakiwa kwenye kuongoza msafara inakuwaje wanatoa amri uwapishe na wewe unatii?
Hayo mambo yanafanyika nchi zenye raia wengi wasiojielewa na wenye maisha ya bora liende, hewala hewala.
Kwenye nchi ambazo utawala wa sheria unafanya kazi sawa sawa polisi wa barabarani tu ndio wanahusika kutoa muongozo wa matumizi ya barabara wakati wa hali ya kawaida ya amani kwenye nchi.
 
Back
Top Bottom