Kumbe tayali kachaguliwa kuwa mbuge !!! Uchaguzi Ni October 2020Yani Jangili, jambazi Suleiman Nchambi mmelipitisha tena liwatumikie miaka 5 ijayo!!!!
Inauma Sana kwa kweli.
Nmeambiwa jamaa kagawa mkwanja kwa kila Mjumbe laki moja ,hapo si mnawauza mnaowawakilisha.
Mbunge wa Kishapu, Suleiman Nchambi (CCM) mbaroni kwa kukutwa na Silaha 16 na risasi 536
Mbunge wa Kishapu(CCM), Suleiman Nchambi aliyekutwa na silaha 16 aburuzwa mahakamani, asomewa mashitaka 12
Duh!, kwanini lakini!? damn!Chenge hana mpinzani keshawaroga wanyantuzu ni mbunge wao forever
Kasoro nyingine ni kuwa nimeona kwa mfano Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ambaye anawajua wajumbe wote wa mkutano wa kumchagua mbunge nae anaamua kuchukua fomu ili agombee ubunge, kwa mtu kama huyu utakuta tayari kawasuka hao wajumbe wasiozidi 500 na ni rahisi kwake kupita kwa kuwa katika miaka mitano ya uenyekiti amekuwa karibu na wajumbe wote,huu si utaratibu mzuri,ungewekwa utaratibu kuwa anayetaka kutia nia akiwa kama ni mbunge ,au waziri ,au mwenyekiti wa CCM kwenye jimbo basi anatakiwa ama atoe notisi kabla ya miaka 3 au 5 kuwa ama achague kuendelea na vyeo alivyonavyo au aachie akisubiri kuja kugombea ubunge katika msimu mwingine wa uchaguzi.Watia nia masikini na ambao hawana nyadhifa serikalini inakuwa vigumu kuweza kupata nafasi ya kuteuliwa kwa huu mfumo, sasa nafasi zitakuwa ni za wenye nyadhifa serikalini na kwenye chama,huu si mfumo rafiki kwa mlala hoi.
Hivi Musiba alitia nia kule Mwibara?Hawa wapuuzi flani walihama wakapewa nafasi CCM saivi wamewanyoosha, Shukwani ziwaendee CCM na mwenyekiti wao. Mwenyekiti kashamaliza teuzi za UDAS, URC, UDC, U-RAS, U-DED waliopoteza watajutia nafasi walizopoteza.
- Mtulia
- Katambi
- Kafulila
- Nassari
- Silinde
- Lijualikali
Wateule walioacha teuzi nao wamegaragazwa
- Makonda
Wasanii waliojiforogoa kwamba wanaipenda CCM nao CHALIIIII
Wanaharakati CHALIIII!!
Vigogo CHALIII!
- Kimei
- Mwakyembe
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Mwakyembe haamini [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kuna kitu hujaeleweka pia, unasema "hii kazi ya kuchagua wagombea wasingeachiwa wajumbe peke yao" lakini hujasema wateuliwe na nani. Na kama hutaki wajumbe ndio wateue, unataka mtu mmoja ndiye ateue? maana kama kuna kamati unafikiri ndiyo ingefanya kazi hiyo then ujue kamati hiyo nayo itakuwa na wajumbe na wajumbe hao ndio watakapofanya uteuzi!Kwa kasi aliyonayo Mh. Rais na kwa sababu nchi inataka kuelekea uchumi mkubwa wa kati yaani higher middle economy country, hii kazi ya kuchagua wagombea wasingeachiwa wajumbe peke yao maana wao wanaweza fanya kwa maslaahi yao au kwa ushabiki ni bora hawa wagombea ubunge wangeteuliwa tu kwa maslahi ya taifa.
Nimesikia mahali Silinde ameshindwa, hebu tuwekee matokeo hapa tumalize utata.
Yule aliyepata hujuma ya ujangili wa wanyama pori.
hayo waulize wapiga kuraCCM siyo chama rafiki kwa wanyonge. Pamoja na muamko mkubwa uliooneshwa wanyonge ktk uchaguzi huu kuchukuwa fomu za kugombea ubunge, lkn hakuna hata mmoja ambaye ni mnyonge atapata nafasi ya kupitishwa.
Kwanini? Kura za maoni wengi wao wamepata sufuri kabisaa! Ndiyo kisema hata majina yao hayawezi kupelekwa kwa " "mzee wa mood" (a.k.a inategemea nimeamkaje).
Wenye nazo tu ndiyo wamejizolea kura nyingi karibu kila Jimbo.
Shauri zenu......!!!!
Acha kulalamika, October utakuwa na wagombea wengine wengi maana huu wa ccm ni mchakato wa kupata mpeperusha bendera wao, na chadema nao watakuwa na wa kwao, viyo hivyo kwa cuf, act nk. Kama utaona katika wote hao hakuna anayefaa, basi nalo litakuwa ni neno!Na hii ndio sababu iliyochangia watu wengi wakachukia ccm naamini ccm mpya itakuwa na sura mpya nyingi zenye kiu na uwezo wa kulipeleka taifa mbele sioni sababu ya mtu aliyekuwa mbunge kwa vipindi kadhaa na hakufanya lolote kurudi tena bungeni.
Taifa lina vijana wengi wazalendo ambao wangeweza kuwa viongozi wazuri lakini hata pesa ya kuchukua form walikosa naimani sana JPM hatotuangusha.