Uchaguzi 2020 Ahadi na Sera za Tundu Lissu katika Uchaguzi Mkuu 2020
Amani iwe nanyi wadau!

kama nilivyosema hapo juu mwaka 2015 sikumpigia kura Lowassa kwa sababu kadhaa ikiwemo kuwa sikuamini kama yeye ndo mtu sahihi anayebeba maono ya Tanzania. Nilimuona kama opportunist aliyekosa nafasi CCM basi akaenda chadema ili atimize ndoto zake. Miaka 5 sasa nimejilidhisha kuwa Lowasa niliyegoma kumpa kura 2015 yupo vilevile kama nilivyomuona mwaka ule. Sasa amerudi CCM na anakula meza moja na CCM.

Mwaka huu 2020 nimejilidhisha vya kutosha, na bila shaka yeyote nasema rasmi nitampa kura yangu Tundu Lissu na nitawaelimisha watanzania wengine wampe kura zao Tundu Lissu. Sababu zangu za kumpa kura Tundu Lissu mwaka huu ni hizi

1. Tanzania inahitaji Katiba Mpya haraka iwekezanavyo. Na sioni Magufuli kama anaweza kutupa iyo katiba mpya ambayo ni ya wananchi.

Kwenye hili Ni kweli kuwa katika miaka 5 ya serikali ya Awamu ya Tano ndo kipindi ambacho nimeona umuhimu wa katiba mpya. Katiba inayopunguza nguvu za Raisi na kuweka Uhuru wa Mahakama, Bunge na vyombo vingine .
Mambo nikiyoyaona kwenye Awamu hii hasa bunge kutunga sheria za hovyo, Mahakama kushindwa kusimamia wajibu wake wa kulinda haki za wananchi huku watu wakionewa mchana kweupe na taasisi mbalimbali vikiwemo vyombo vya Habari kinyanyaswa vibaya sana ni dhahili kuwa Ni sasa na si vinginevyo, Tanzania tunaitaji katiba Mpya. Na kwa sababu Magufuli hawezi kutupa katiba mpya ya wananchi basi lazima nimchague Tundu Lissu.

2. Mfumo wa Tanzania wa Elimu kuhitaji mabadiriko ya haraka ili kulinusuru Taifa.

Wandugu, tuseme tu ukweli , Elimu ya Tanzania ni ya hovyo kupindukia. Ni elimu inayohimiza mtu kuwa na uwezo wa kukariri huku akiwa hawezi kudeliver kwenye kazi. Ni elimu iliyopitwa na wakati ambayo haimuandai mtu kuweza kushindana kwenye soko la ajira sio ndani ya nchi Bali hata nje ya nchi. Nimeshihudia hata kwenye makampuni yetu makubwa ya ndani yanayofanya vizuri, wakuu wa haya makampuni hata kama amesoma tanzania basi huwa wengi wamesoma vyuo ya nje au shule la nje. Huu ni uthibitisho tosha kuwa elimu yetu iko sehemu mbaya sana.

Ni mara Chacha sana kukuta Mtanzania Ameshika nafasi kubwa nchi za wenzetu( na hao wachache huwa wanechanganya elimu ya nje ya Tanzania pia) lakini ni mara nyingi watu wa nje unawakuta kwenye nafasi kubwa katika makampuni ya ndani yanayofanya vizuri.
Kwa sababu hii nakubaliana na Lissu kuwa mfumo wetu wa elimu lazima ubadilishwe, hivyo nitamchagua Lissu mwaka huu!!

3. CCM imetengeneza madaraja makubwa katika raia na kuwafanya wengi wa watanzania kuona kama umaskini ni haki yao.

Katika suala la uchumi, napenda kukiri kuwa CCM haijafanya kazi kubwa katika kuwatengeneza watanzania kiuchumi. Na kuwa fanya watanzania kuwa aggresive kwenye kutengeneza maisha bora kwa ajili yao na vizazi vyao.

Kati ya nchi nilizotembea ni Tanzania tu ambayo nimeona watu wanaridhika kukaa mazingira ya hovyo na hawana namna ya kufanya. Mtu anaridhika kukaa kwenye eneo chafu ambalo halihapimwa na anaona hiyo ndo stahili yake. Leo hii Kuna maneno Kama wakishua, ushuani, uswahilini kwa sababu CCM imetengeneza madaraja na mbaya zaidi kuwafanya wananchi kuridhika na madaraja hayo na kuwa proud kuwa kwenye mfumo huo wa madaraja ya kiuchumi. Watu hadi wamefungwa akili na kufanywa mtu ndoto yake kubwa iwe kununua gari!! Tumekuwa na nchi hadi wahubiri wanahuburi watu kununua magari ndo ionekane kama maendeleo makubwa mtu anaweza kufanya huku akiwa anakaa kwenye eneo chafu ambalo halijapimwa wala kupangiliwa vizuri!!

4. Chadema na Lissu kuja na Sera ya kukuza uchumi kwa kutegemea sekta Binafsi.
Napenda kusema wazi katika tafiti nikizofanya maeneo mbalimbali , sijaona nchi wala taifa lililopiga hatua kubwa kimaendeleo bila sekta binafsi kuchukua sehemu kubwa kwenye uchumi. Na hili ndo lilifanya hata China, nchi tunaowaiga kila siku kupiga hatua kubwa kimaendeleo.

Hapa Tanzania serikali ya Awamu ya Tano tunaona inarudisha nyuma sana sekta binafsi, sasaivi Tunaona kandarasi za ujenzi wakipewa majeshi, shughuli za kufanywa na sekta binafsi zikifanywa na serikali Mf biashara ya kuuza mafuta.
Hili Ni bomu ambalo hatujui ukubwa wake utakuwaje. Duniani pore, sekta binafsi ndo walipa kodi wakubwa, ndo waajiri wakubwa. Hakuna namna vijana wetu wote wataajiliwa serikalini kwa sababu kamwe serikali haijawai na haitowai kuwa na huo uwezo. Hivyo kwa sababu Chadema wamekuja na Sera ya kuendesha Uchumi wa nchi kwa kutegemea sekta binafsi, hivyo nasema wazi, kura yangu mwaka huu nampa Tundu Lissu.

5. Haki ya Mlipa Kodi!!
Baada ya magufuli kuingia madarakani na TRA kuanza kuwabana wafanyabiashara, niliwai kutana na mfanyabiashara ambayo aliniambia, vyovyote vile Tanzania itakuwa nchi ya wachuuzi na sio wafanyabiashara.

Na huu ndo ukweli niliouona. Ndani ya miaka 5 biashara nyingi zimefungwa kutokana na ubabe na uonevu wa Tra. Wengi wameona bora watumie wamachinga na kuwapa bidhaa wakapange barabarani. Hili limefanya taifa kama taifa kukosa kodi kwa kiwango kikubwa. Hii ni kwa sababu mchuuzi halipi kodi. Ila mfanyabiashara Mwenye TIN no na sehemu rasmi ya kufanyia biashara ni lazima atalipa kodi.

Kwenye hili Lissu amesema atakuja na haki ya mlipakodi. Kusema kweli kwa hili lazima nimchague Lissu!!!

Napenda kumaliza kwa kusema, Lissu amenishawishi, na nitampa kura yangu na kumuombea awe raisi wa Tanzania 2020- 2025
Kufanya kosa sii kosa Ila kurudia kosa.Watu wanabaini kichaka Cha uzalendo was kinafiki kwa Kasi ya 6G
 
Mbona sasa kama unajichanganya mwenyewe? Aliyemleta Lowasa chadema ni huyo huyo Tundu Lisu ambaye wewe leo hii unaona anafaa kuliko Lowasa, isitoshe Lowasa alileta kura zaidi ya milioni 6 chadema record haijawahi kufikiwa na Upinzani Tanzania pamoja na Wabunge wengi na madiwani, Lowasa aliisimamisha Dar, Tundu Lisu &Co. wameshindwa na hawatakiwi Dar, hata leo hii bado chadema inatembelea na kujivunia mchango wa Lowasa, ...

Kazi mnayo. Buku 7 zitapatikana kweli kwa mtaji huu?
 
Mbona sasa kama unajichanganya mwenyewe? Aliyemleta Lowasa chadema ni huyo huyo Tundu Lisu ambaye wewe leo hii unaona anafaa kuliko Lowasa, isitoshe Lowasa alileta kura zaidi ya milioni 6 chadema record haijawahi kufikiwa na Upinzani Tanzania pamoja na Wabunge wengi na madiwani, Lowasa aliisimamisha Dar, Tundu Lisu &Co. wameshindwa na hawatakiwi Dar, hata leo hii bado chadema inatembelea na kujivunia mchango wa Lowasa, ...
Ulikuepo? Na aliyeleta Ndege za maonyesho ni nani?
 
Mbona sasa kama unajichanganya mwenyewe? Aliyemleta Lowasa chadema ni huyo huyo Tundu Lisu ambaye wewe leo hii unaona anafaa kuliko Lowasa, isitoshe Lowasa alileta kura zaidi ya milioni 6 chadema record haijawahi kufikiwa na Upinzani Tanzania pamoja na Wabunge wengi na madiwani, Lowasa aliisimamisha Dar, Tundu Lisu &Co. wameshindwa na hawatakiwi Dar, hata leo hii bado chadema inatembelea na kujivunia mchango wa Lowasa, ...
Dar haijafanya uamuzi wa kuwapiga chini Chadema. Nina picha kubwa sana ya Dar . Naona kama Dar ndo sehemu ambayo Lissu ataongoza kwa kura!!! Time will tell.
 
Amani iwe nanyi wadau!

kama nilivyosema hapo juu mwaka 2015 sikumpigia kura Lowassa kwa sababu kadhaa ikiwemo kuwa sikuamini kama yeye ndo mtu sahihi anayebeba maono ya Tanzania. Nilimuona kama opportunist aliyekosa nafasi CCM basi akaenda chadema ili atimize ndoto zake. Miaka 5 sasa nimejilidhisha kuwa Lowasa niliyegoma kumpa kura 2015 yupo vilevile kama nilivyomuona mwaka ule. Sasa amerudi CCM na anakula meza moja na CCM.

Mwaka huu 2020 nimejilidhisha vya kutosha, na bila shaka yeyote nasema rasmi nitampa kura yangu Tundu Lissu na nitawaelimisha watanzania wengine wampe kura zao Tundu Lissu. Sababu zangu za kumpa kura Tundu Lissu mwaka huu ni hizi

1. Tanzania inahitaji Katiba Mpya haraka iwekezanavyo. Na sioni Magufuli kama anaweza kutupa iyo katiba mpya ambayo ni ya wananchi.

Kwenye hili Ni kweli kuwa katika miaka 5 ya serikali ya Awamu ya Tano ndo kipindi ambacho nimeona umuhimu wa katiba mpya. Katiba inayopunguza nguvu za Raisi na kuweka Uhuru wa Mahakama, Bunge na vyombo vingine .
Mambo nikiyoyaona kwenye Awamu hii hasa bunge kutunga sheria za hovyo, Mahakama kushindwa kusimamia wajibu wake wa kulinda haki za wananchi huku watu wakionewa mchana kweupe na taasisi mbalimbali vikiwemo vyombo vya Habari kinyanyaswa vibaya sana ni dhahili kuwa Ni sasa na si vinginevyo, Tanzania tunaitaji katiba Mpya. Na kwa sababu Magufuli hawezi kutupa katiba mpya ya wananchi basi lazima nimchague Tundu Lissu.

2. Mfumo wa Tanzania wa Elimu kuhitaji mabadiriko ya haraka ili kulinusuru Taifa.

Wandugu, tuseme tu ukweli , Elimu ya Tanzania ni ya hovyo kupindukia. Ni elimu inayohimiza mtu kuwa na uwezo wa kukariri huku akiwa hawezi kudeliver kwenye kazi. Ni elimu iliyopitwa na wakati ambayo haimuandai mtu kuweza kushindana kwenye soko la ajira sio ndani ya nchi Bali hata nje ya nchi. Nimeshihudia hata kwenye makampuni yetu makubwa ya ndani yanayofanya vizuri, wakuu wa haya makampuni hata kama amesoma tanzania basi huwa wengi wamesoma vyuo ya nje au shule la nje. Huu ni uthibitisho tosha kuwa elimu yetu iko sehemu mbaya sana.

Ni mara Chacha sana kukuta Mtanzania Ameshika nafasi kubwa nchi za wenzetu( na hao wachache huwa wanechanganya elimu ya nje ya Tanzania pia) lakini ni mara nyingi watu wa nje unawakuta kwenye nafasi kubwa katika makampuni ya ndani yanayofanya vizuri.
Kwa sababu hii nakubaliana na Lissu kuwa mfumo wetu wa elimu lazima ubadilishwe, hivyo nitamchagua Lissu mwaka huu!!

3. CCM imetengeneza madaraja makubwa katika raia na kuwafanya wengi wa watanzania kuona kama umaskini ni haki yao.

Katika suala la uchumi, napenda kukiri kuwa CCM haijafanya kazi kubwa katika kuwatengeneza watanzania kiuchumi. Na kuwa fanya watanzania kuwa aggresive kwenye kutengeneza maisha bora kwa ajili yao na vizazi vyao.

Kati ya nchi nilizotembea ni Tanzania tu ambayo nimeona watu wanaridhika kukaa mazingira ya hovyo na hawana namna ya kufanya. Mtu anaridhika kukaa kwenye eneo chafu ambalo halihapimwa na anaona hiyo ndo stahili yake. Leo hii Kuna maneno Kama wakishua, ushuani, uswahilini kwa sababu CCM imetengeneza madaraja na mbaya zaidi kuwafanya wananchi kuridhika na madaraja hayo na kuwa proud kuwa kwenye mfumo huo wa madaraja ya kiuchumi. Watu hadi wamefungwa akili na kufanywa mtu ndoto yake kubwa iwe kununua gari!! Tumekuwa na nchi hadi wahubiri wanahuburi watu kununua magari ndo ionekane kama maendeleo makubwa mtu anaweza kufanya huku akiwa anakaa kwenye eneo chafu ambalo halijapimwa wala kupangiliwa vizuri!!

4. Chadema na Lissu kuja na Sera ya kukuza uchumi kwa kutegemea sekta Binafsi.
Napenda kusema wazi katika tafiti nikizofanya maeneo mbalimbali , sijaona nchi wala taifa lililopiga hatua kubwa kimaendeleo bila sekta binafsi kuchukua sehemu kubwa kwenye uchumi. Na hili ndo lilifanya hata China, nchi tunaowaiga kila siku kupiga hatua kubwa kimaendeleo.

Hapa Tanzania serikali ya Awamu ya Tano tunaona inarudisha nyuma sana sekta binafsi, sasaivi Tunaona kandarasi za ujenzi wakipewa majeshi, shughuli za kufanywa na sekta binafsi zikifanywa na serikali Mf biashara ya kuuza mafuta.
Hili Ni bomu ambalo hatujui ukubwa wake utakuwaje. Duniani pore, sekta binafsi ndo walipa kodi wakubwa, ndo waajiri wakubwa. Hakuna namna vijana wetu wote wataajiliwa serikalini kwa sababu kamwe serikali haijawai na haitowai kuwa na huo uwezo. Hivyo kwa sababu Chadema wamekuja na Sera ya kuendesha Uchumi wa nchi kwa kutegemea sekta binafsi, hivyo nasema wazi, kura yangu mwaka huu nampa Tundu Lissu.

5. Haki ya Mlipa Kodi!!
Baada ya magufuli kuingia madarakani na TRA kuanza kuwabana wafanyabiashara, niliwai kutana na mfanyabiashara ambayo aliniambia, vyovyote vile Tanzania itakuwa nchi ya wachuuzi na sio wafanyabiashara.

Na huu ndo ukweli niliouona. Ndani ya miaka 5 biashara nyingi zimefungwa kutokana na ubabe na uonevu wa Tra. Wengi wameona bora watumie wamachinga na kuwapa bidhaa wakapange barabarani. Hili limefanya taifa kama taifa kukosa kodi kwa kiwango kikubwa. Hii ni kwa sababu mchuuzi halipi kodi. Ila mfanyabiashara Mwenye TIN no na sehemu rasmi ya kufanyia biashara ni lazima atalipa kodi.

Kwenye hili Lissu amesema atakuja na haki ya mlipakodi. Kusema kweli kwa hili lazima nimchague Lissu!!!

Napenda kumaliza kwa kusema, Lissu amenishawishi, na nitampa kura yangu na kumuombea awe raisi wa Tanzania 2020- 2025
Kama ni mtu sahihi na mwenye maono sahihi kabisa, mwenye kuhitajika kutokana na wakati kuwaongoza Watanzania kwa sasa, basi mtu huyo si mwingine bali ni Tundu Lissu. CCM, chama ajuza kimepitwa na wakati, na kikapumzike kwa amani.
 
Mbona sasa kama unajichanganya mwenyewe? Aliyemleta Lowasa chadema ni huyo huyo Tundu Lisu ambaye wewe leo hii unaona anafaa kuliko Lowasa, isitoshe Lowasa alileta kura zaidi ya milioni 6 chadema record haijawahi kufikiwa na Upinzani Tanzania pamoja na Wabunge wengi na madiwani, Lowasa aliisimamisha Dar, Tundu Lisu &Co. wameshindwa na hawatakiwi Dar, hata leo hii bado chadema inatembelea na kujivunia mchango wa Lowasa, ...
Usiishi jana ..hiyo 2015 Lissu wakati wake ulikuwa bado
 
Kwa kweli tangu juzi kawe, jana segerea na Leo Arusha Tundu Lissu ameanza kutema sera kali kweli
Zinahusu maisha ya mwananchi mmojammoja na Taifa kiujumla
Uzuri wa sera zake kuna zile ambazo ziko specific kwa mji husika na kuna zile ambazo zinahusu nchi nzima

1. Lissu kazungumzia ugumu wa maisha ya mfanyakazi na jinsi atakavyoyaboresha kwa kulipa malimbikizo yote wanayodai na kuwalipa nyongeza zao za mishahara za kisheria(annual increments)

2. Amezungumzia uonevu wanaofanyiwa wafanyabiashara wetu na kwamba ataundoa

3. Amezungumzia kuhusu elimu bora na siyo bora elimu, amezungumzia kuhusu elimu ya ujuzi wa kazi siyo ya kukariri

4. Amezungumzia kuhusu viwanda na kuvutia mitaji ili kutoa ajira kwa vijana wetu

5. Amzezungumzia kuhusu diplomasia yetu iliyoshuka na jinsi atakavyorudisha mahusiano bora ya kimataifa

6. Amezungumzia bima ya afya kwelikweli siyo hii ambayo wazee wetu wakishastaafu wanaambiwa waongeze hela ili waweze kuwekwa kwenye bima ya magonjwa nyemelezi ya wazee

7. Amezungumzia kuhusu kuirejesha Arusha kuwa kitovu cha utalii

8. Amezungumzia kuhusu katiba mpya, ameonyesha ubovu wa katiba ya sasa ambayo imelinyima hata bunge uwezo wa kuanzisha hoja ya namna ya kutumia pesa za nchi isipokuwa tu kama hoja hiyo imeanzishwa na serikali.

9.Amezungumza kuhusu haki za watu, ametetea masheikh walio jela kinyume cha sheria, kwa mfano amesema Arusha peke yake kuna Masheikh 70 wako jela achilia mbali wale masheikh wa uamsho.

10. Amezungumzia kuvunjia wananchi nyumba kikatili etc

11. Kszungumzia mzigo mzito wa makato ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu na amesema atashusha makato hayo kwa mwezi kutoka 15% hadi 3% ya mshahara kwa mwezi

12. Amezungumzia kuhusu adha za vitambulisho vya kimagumashi vya wamachinga amesema ataondoa mzingo wa shilingi 20000 ya kitambulisho cha wamachinga pesa iliyoanzishwa na Bashite na Magufuli

13. Amesema ataanzisha sheria ya haki ya mlipa kodi "Bill of taxpayers rights" ili waweze kulindwa kisheria badala ya utaratibu wa sasa ambao wafanyabiashara wanaonewa sana na TRA na hawana pa kukimbilia, kila wanapokimbilia wameshafungwa minyororo

14. Amezungumzia kuhusu uhuru wa habari, kuwa ataondoa sheria kandamizi zilizotungwa na Magufuli kumlinda yeye badala ya kusaidia taaluma kukua

15. Amesema ataomesha matumizi ya hovyo ya pesa za serikali, siyo rais akiamka asubuhi anajenga uwanja wa ndege kijijini kwake ambapo ndege inatua mara mbili kwa mwaka siku anayoenda kula Christmass na pasaka

16. Lissu anazungumzia kuhusu UHURU, HAKI, MAENDELEO

Kwa kweli Lissu unatisha baba endelea kupiga spana mwana wa Tanzania
 
Kwa kweli tangu juzi kawe, jana segerea na Leo Arusha Tundu Lissu ameanza kutema sera kali kweli
Zinahusu maisha ya mwananchi mmojammoja na Taifa kiujumla
Uzuri wa sera zake kuna zile ambazo ziko specific kwa mji husika na kuna zile ambazo zinahusu nchi nzima

1. Lissu kazungumzia ugumu wa maisha ya mfanyakazi
2. Amezungumzia uonevu wanaofanyiwa wafanyabiashara wetu
3. Amezungumzia kuhusu elimu bora na siyo bora elimu, amezungumzia kuhusu elimu ya ujuzi wa kazi siyo ya kukariri
4. Amezungumzia kuhusu viwanda na kuvutia mitaji ili kutoa ajira kwa vijana wetu
5. Amzezungumzia kuhusu diplomasia yetu iliyoshuka na jinsi atakavyorudisha mahusiano bora ya kimataifa
6. Amezungumzia bima ya afya kwelikweli siyo hii ambayo wazee wetu wakishastaafu wanaambiwa waongeze hela ili waweze kuwekwa kwenye bima ya magonjwa nyemelezi ya wazee
7. Amezungumzia kuhusu kuirejesha Arusha kuwa kitovu cha utalii
8. Amezungumzia kuhusu katiba mpya, ameonyesha ubovu wa katiba ya sasa ambayo imelinyima hata bunge uwezo wa kuanzisha hoja ya namna ya kutumia pesa za nchi isipokuwa tu kama hoja hiyo imeanzishwa na serikali
9.Amezungumza kuhusu haki za watu, ametetea masheikh walio jela kinyume cha sheria, kwa mfano amesema Arusha peke yake kuna Masheikh 70 wako jela achilia mbali wale masheikh wa uamsho
10. Amezungumzia kuvunjia wananchi nyumba kikatili etc

Kwa kweli Lissu unatisha baba endelea kupiga spana mwana wa Tanzania
Dah kanigusa sana.

Hayo mambo yote ndio tunataka.
 
Kwa kweli tangu juzi kawe, jana segerea na Leo Arusha Tundu Lissu ameanza kutema sera kali kweli
Zinahusu maisha ya mwananchi mmojammoja na Taifa kiujumla
Uzuri wa sera zake kuna zile ambazo ziko specific kwa mji husika na kuna zile ambazo zinahusu nchi nzima

1. Lissu kazungumzia ugumu wa maisha ya mfanyakazi
2. Amezungumzia uonevu wanaofanyiwa wafanyabiashara wetu
3. Amezungumzia kuhusu elimu bora na siyo bora elimu, amezungumzia kuhusu elimu ya ujuzi wa kazi siyo ya kukariri
4. Amezungumzia kuhusu viwanda na kuvutia mitaji ili kutoa ajira kwa vijana wetu
5. Amzezungumzia kuhusu diplomasia yetu iliyoshuka na jinsi atakavyorudisha mahusiano bora ya kimataifa
6. Amezungumzia bima ya afya kwelikweli siyo hii ambayo wazee wetu wakishastaafu wanaambiwa waongeze hela ili waweze kuwekwa kwenye bima ya magonjwa nyemelezi ya wazee
7. Amezungumzia kuhusu kuirejesha Arusha kuwa kitovu cha utalii
8. Amezungumzia kuhusu katiba mpya, ameonyesha ubovu wa katiba ya sasa ambayo imelinyima hata bunge uwezo wa kuanzisha hoja ya namna ya kutumia pesa za nchi isipokuwa tu kama hoja hiyo imeanzishwa na serikali
9.Amezungumza kuhusu haki za watu, ametetea masheikh walio jela kinyume cha sheria, kwa mfano amesema Arusha peke yake kuna Masheikh 70 wako jela achilia mbali wale masheikh wa uamsho
10. Amezungumzia kuvunjia wananchi nyumba kikatili etc

Kwa kweli Lissu unatisha baba endelea kupiga spana mwana wa Tanzania
Missile of the Nation tutafutie clip tafadhali!
 
2015 nilimchagua JPM, 2020 nitamchagua tena JPM , ikiwezekana hata 2015 nitafanya hivyo .
 
Back
Top Bottom