● Mfumo wa kodi zetu utajengwa juu ya Uhuru wa watu wetu, haki za watu wetu na Maendeleo ya watu wetu, kwahiyo mfumo huu utafumuliwa na kujengwa upya ili uwe rafiki kwa walipa kodi.

● Tutapandisha mishahara ya wafanyakazi kila mwaka na kuwalipa mapunjo (arrears) wafanyakazi wote ambao hawakupandishwa mshahara kwa Miaka mitano ya serikali ya hapa kazi tuu.

● Watanzania wote walionufaika na mkopo ya Elimu ya Juu,watarejesha 3%
tu ya deni lao kama mkataba wao na bodi ya mikopo unavyojieleza na siyo 15% kama wanavyokatwa sasa.

● Tutaimarisha sekta ya ujenzi ya ndani na makampuni ujenzi kwa kuzipatia tenda mbali mbali za ujenzi wa miundombinu ya serikali na umma.

● Tutatengeneza mfumo ambao utamwezesha kila mtanzania kuwa na Bima ya afya.Hivyo kuwa na uhakika wa matibabu wakati wowote

● Serikali yetu itabadili falsafa nzima ya elimu, Elimu yetu iwe wezeshi katika kutatua matatizo ya watu wetu, watu wetu waajirike na elimu itakayowafanya wawe na uwezo wa kushindani katika soko la Ajira na na kufundisha vijana stadi za maisha, ili wawese kujiajiri kwa urahisi wakiwezeshwa, siyo Elimu ya Pass mitihani tuliyonayo leo.

● Katiba mpya, tutaunda katiba mpya kuzingatia maoni ya wananchi kupitia tume ya Warioba

●ustawi wa sekta binafsi iwe injini wa uchumi wa nchi.

Hivi ni baadhi ya vipaumbele vya Tundu Lissu Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema.
 
Na pia kuweka rehani kwa wazungu mali asili za nchi.
 
Ooh Ok
 
Sio Kipaumbele Chetu. Walioweka Rehan Mali Ya Nchi Ni wale walio sighn Makubaliano Tofaut na Barrick
Mgombea wenu si amesema atatumia rasilimali zetu kama collateral kupata mikopo toka nje ? Si ndio rehani hiyo au ?
 
Wakati huu tunaweka collateral gani kupata mikopo toka nje?
Mgombea wenu si amesema atatumia rasilimali zetu kama collateral kupata mikopo toka nje ? Si ndio rehani hiyo au ?
 
Dog whistle threads....ukiona mpaka comment ya tano,kumi,mnaongea wenyewe wenye fikra moja,you're in for a rude awakening.fanyeni kampeni no time to rest.
 
Watanzania gani au wale wa Belgium?
oktoba 28 tukamchague Mgombea wa CCM Dkt Magufuli aliyeweza kuunganisha Watanzania wote pamoja.
Hakika tuna kila sababu ya kumchagua tena MAGUFULI
 
Lisu anabomoa nchi ...pia ni rais wa mitandaoni especially jf😀😀
 
NDUGU HII NCHI TAYARI ILISHAUNGANISHWA KITAMBO SANA NA HAYATI BABA WA TAIFA, HUYO LISU NDIO MDUDU GANI?
 
Dog whistle threads....ukiona mpaka comment ya tano,kumi,mnaongea wenyewe wenye fikra moja,you're in for a rude awakening.fanyeni kampeni no time to rest.
Ukiona hivyo wazalendo maslahi wametoka nduki,kiasi Cha kuooteza miguu yao katika mbio.
 
Mapunguani yalikua yanasema CHADEMA ni chama cha wachaga.
Sasa sjui lisu nae mchaga.
Jpm hafai ni mkabila na mdini sana. Bora tuchague kinyeo kuliko hili jiwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…