Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC): Hatuungi mkono Mkataba wa Bandari. Sauti ya Watu ni sauti ya Mungu
Au unataka tena nianze kukuita Shetwani ndio ujibu swali?
Je, walipatiwa hizo fedha za escrow wahusika?
Ulitaka maana ya neno escrow umepewa. Sasa unataka kuambiwa sakata zima hapa?

Sasa kukusaidia ndo nakuelekeza go to post 23 na fuata maelekezo. Utapata sakata lote la escrow maana JF ni kisima
 
Baada ya kupewa jibu umehamisha goli tena?

Nataka kukuthibitishia tu mimi sio hao wajjnga unaodhani ni wajinga. Ni vile tu hatutumii actual id zetu humu. Mimi ni kipanga kweli. Ukoo wenu wote mnaweza msinifikie
Wewe utakuwa kibanga na si kipanga.
 
Mungu yupi huyo? baba, Mama, Mwana au Roho?

Mmechelewa jamvini, karamu imeshaliwa.

Hivi mnangoja mkataba wa kibiashara uanikwe kama IGA?

Hakuna biashara ya Kimataifa duniani ikaendeshwa hivyo.
Mungu wa kweli. Jina lake anaitwa JEHOVA.
Wa kwenu anitwa nani? au hana jina?
 

Utatu Mtakatifu: Kiri ya Imani ya Kanisa: Baba, Mwana na Roho Mt.​

Mama Kanisa anakiri na kufundisha katika Mungu mmoja aliye katika Nafsi tatu, yaani Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu. Kanisa linatufundisha kwamba mgawayiko huu wa Nafsi hujidhihirisha katika kazi zao: Mungu Baba Mwenyezi ndiye muumbaji, Mungu Mwana ni mkombozi na Mungu Roho Mtakatifu ni mfariji.
Yohana 17:3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

Hivi huwa hamuelewi mnachokisoma au ndiyo macho mnayo llakini hayaoni?
 
Ulitaka maana ya neno escrow umepewa. Sasa unataka kuambiwa sakata zima hapa?

Sasa kukusaidia ndo nakuelekeza go to post 23 na fuata maelekezo. Utapata sakata lote la escrow maana JF ni kisima
Jibu swali. Je, wahusika walipata pesa zao?
A. Ndio
B. Hapana
C. Sijui
 
Yaani hela za Rugemalila zilifuata taratibu zote za kifedha;

1. Electrinic transfer toka akount moja kwenda nyingine kwa kiasi kikubwa cha fedha.

2. Hela ya Rugemalila, ilikatwa kodi ya serikali. Hapa usisahau serikali huwa haichukui kodi toka kwenye fedha haramu

3. Hela ya Rugemalila, maamuzi ya nani ampe na asimpe yalikuwa ni yake binafsi. Ni kama hela yako hakuna mtu anayekupangia nani wa kumpa au nani wa kumnyima.

SASA WEWE NIAMBIE, ZILE ZA KWENYE MASANDARUSI ZILIKUWA ZA NANI?

HUONI KUWA ZA KWENYE MASANDARUSI HAZIKUFUATA TARATIBU ZA KIFEDHA?

KIASI KIKUBWA VILE CHA FEDHA, UNACHUKUAJE KAMA CASH TOKA BANK?
Matapeli ni matapeli tu !
 
Sijasomaa ilaa Kusema Mbona swissport wanaendesha Uwanja wa Dar kujustify waarabu wapewe bandari ni Unaziii...!!
 
Mjumbe wa kamati ya kitongoji anajiita mwanasheria! Kibaka huyo.
Nakwambiaje. Mimi ni mwanasheria nguli na hapa nimekuja China kuonana na wateja wangu ambao ni Kampuni ya wachina iliyowekeza Tanzania hapo.

Kama nalipiwa hadi Ticket ya ndege kuja huku jua tu mimi sio mwenzako.


Vumilia tu! Wengine tumebarikiwa zaidi!!
 
Yohana 17:3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

Hivi huwa hamuelewi mnachokisoma au ndiyo macho mnayo llakini hayaoni?
Biblia haisomwi kama Msahafu bibi.
Soma sura yote.

22 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. 23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.
 
WACHA TUSEME, TANZANIA NI YETU SOTE SIO MALI YA WAKRISTO

Hivi karibuni kumezuka mjadala mkali kuhusu Serikali kuingia kwenye makubaliano ya kuendesha bandari za Tanzania na kampuni ya DP World.

Mjadala huu ulianza na sura ya kisiasa wakati Mwenyekiti wa Chadema Bwana Freeman Mbowe alipotoa shutuma kali kuwa bandari za Tanganyika zinauzwa na Wazanzibari yaani Waziri wa Ujenzi, Mhe Makame Mbarawa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan.

Lakini ghafla mjadala ukahama kwenye Siasa na ukatawaliwa na hisia kali za kidini.

Sote tumeshuhudia namna viongozi wa dini ya Kikristo hasa wakatoliki wakiongozwa na Kadinali Pengo walivyokuwa wakilipigia kelele suala la Bandari.

Hoja zinazotawala mjadala huu ni mbili.

Hoja ya kwanza ni kwamba mkataba ule umesainiwa na Waziri Mzanzibari na Rais Mzanzibari na kwamba Wanzanzibari hawa wawili wanauza mali za Tanganyika. Hoja yao ya pili inadai kuwa mkataba hauna ukomo wa muda, yaani ni mkataba wa milele.

Hii hoja hii ya pili inashabikiwa sana na viongozi wa Kanisa.

Jambo la kushangaza ni kuwa mpaka sasa hakuna hata msemaji mmoja, awe mwanasiasa au kiongozi wa Kanisa aliyetoa hoja za kiuchumi na utendaji za kupinga makubaliano hayo.

Badala yake, viongozi wengine kama vile mama Anna Tibaijuka anadiriki kusema uwongo kuhusu sababu za DP World kukataliwa kuendesha Bandari za Marekani.

Mama Tibaijuka anajua vyema lakini hakutaka kusema kuwa sababu ya kukataliwa kuongoza Bandari za New York na New Jersey ni Uwarabu wao na wala si utendaji wao.

Ni kweli Bunge la Marekani lilikataa DP World wasipewe Bandari hizo lakini walisema wazi kuwa Marekani haiwezi kuwapa Waarabu kuendesha Bandari zao kwa sababu za kiusalama.

Hakuna asiejua msimamo wa Marekani kuhusu Waarabu na Waislamu.

Kwa makusudi kabisa, mama huyu anapotosha watu kwa kufananisha suala la bandari za Marekani na bandari za Dar es Salaam.

Kwenye suala la Dar es Salaam, DP World haikutaka kununua TPA.

Inachopendeza ni kuendesha na si kununua Bandari ya Dar es Salaam.

Suala hili la kuendesha si geni Tanzania.

Kampuni ya TICTS imeendesha Bandari ya Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 20.

Kampuni ya “Swissport” inaendesha Kiwanja cha Ndege cha Dar es Salaam kwa muda mrefu.

Mbona hizi kelele hatukuzisikia?

Wakati wa utawala wa Donald Trump Marekani ilifika hatua ya kupiga marufuku baadhi ya Mataifa ya Arabuni kwa maana Waislamu kuingia Marekani.

Kwa hiyo mama Tibaijuka hakutaka kuwa mkweli kuhusu suala hili.

Ametumia kivuli chake cha kuwa mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa kwa wakati ule kuwaaminisha Watanzania kuwa yeye anafahamu zaidi kuhusu ubaya wa DP World.

Mama Tibaijuka amekosa uadilifu (moral authority) wa kuweza kukemea kile alichokiita mkataba mbovu kwa sababu wakati kampuni ya TICTS iliyokuwa inaendesha Bandari ya DSM kwa utendaji wa ovyo huyu mama alikaa kimya hata pale ambapo TICTS walipopewa nyongeza ya mkataba wa miaka 15 bila kufuata sheria za manunuzi.

Lakini jambo la pili, nani asiyejua kuwa mama Anna Tibaijuka alikiri hadharani kuwa alipokea shs 1.6 bilioni ya fedha za rushwa za ESCROW?

Huyu mama ambaye alisema kwa majigambo kuwa shs 1.6 bilioni ni pesa ya mboga ana uchungu gani wa kuwatetea Watanzania masikini?

Bado tunarejea kusema tena kwa kinywa kipana, mpaka sasa hakuna mtu hata mmoja aliyesema kwa kuonesha ushahidi kuwa DP World hawana uwezo kifedha au utendaji wao ni mbovu. Hakuna aliyesema kuwa hizo fedha ambazo tunaahidiwa ni ahadi hewa kwa sababu DP World hawana uwezo wa kuvutia mizigo kupitia Bandari ya Dar es Salaam.

Kwa kuwa mjadala umetawaliwa na CHUKI za kidini na wasemaji wakubwa wamekuwa viongozi wa Kanisa.

Tukumbuke kuwa ni Wakristo hao hao ambao mmoja kati ya viongozi wao waliosema kuwa Rais Samia anafanana na muuza vitumbua!

Makanisa hawakukemea kauli hii ya kumkosea adabu Rais.

Kwa kuwa mjadala wa bandari una chuki za udini, naomba tujikumbushe nafasi ya Makanisa katika nchi hii.

TUKUMBUKE MWAKA 1992
Mwaka 1992, Serikali iliingia Mkataba na Makanisa kupitia Taasisi zao za TEC na CCT.

Chini ya Makubaliano yale, hospitali za Makanisa zitatumika kwa wananchi wote pale ambapo serikali haina hospitali.

Kwa kufanya hivyo, Serikali itakuwa na wajibu wa kuyapa Makanisa fedha za kuendesha hospitali hizo ingawa umiliki wa hospitali utabaki kuwa wa makanisa.

Ifahamike kuwa fedha hizo zinatokana na kodI za Watanzania wote:

Waislamu, Wakristo, Mabaniani, Magoha, Makadiani, na hata wale wasio na dini.

Nini athari za Mkataba huu?

Mkataba huu wa kibaguzi una athari nyingi.

Kwanza:

Serikali inatumia kodi za wananchi kuyapa makanisa kuendesha shughuli zake za kuimarisha Ukristo.

Tunasema hivyo kwa sababu utaratibu unaotumika ni kuwa serikali inatoa fedha kwa makanisa ambayo wao ndio wanapanga matumizi ya fedha zile na sio Serikali.

Pili, kwenye Jamii, makanisa yanaonekana ndio yanatoa huduma za Jamii na hivyo kujenga saikolojia kwa wananchi kuwa Ukristo ndio unajali wananchi.

Athari ya tatu ni kuwa makanisa yananyonya wananchi kwa sababu pamoja ya kuwa hospitali zile zinapata fedha kutoka serikalini, bado wananchi wanalipia huduma.

Nne, Mkataba hauna ukomo, yaani ni wa milele.

(Wakristo wataendelea kupewa hayo mabilioni na Waislamu watanyimwa milele).

Kwa tafsiri nyingine ni kuwa Serikali imejivua kwenye wajibu wa kutoa huduma za Jamii na kuchagua Makanisa kuwa ndio wakala wake.

Tunapenda kuwakumbusha Watanzania kuwa wakati Mkataba huo unasainiwa aliyesaini Mkataba ni Bwana Edward Lowassa aliyekuwa Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu.

Huyu ni Mkristo.

Kwa utaratibu wa Serikali, Lowassa alikuwa Waziri wa Nchi, hivyo basi Waziri mwenye dhamana ni yule mwenye ofisi yake kwa maana ni Waziri Mkuu.

Wakati unatiwa saini Mkataba, huo Waziri Mkuu alikuwa John Samwel Malecela ambaye ni Mkristo.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ndie aliyeishauri Serikali isaini Mkataba ule ambao kwanza hauna ukomo (mkataba wa maisha) na pili unatumia kodi za wananchi kuimarisha Ukristo alikuwa Damian Lubuva ambaye ni Mkristo.

Kwa upande wa Kanisa mwanasheria wao alikuwa Prof Balozi Costa Mahalu, Mkristo.

Kwa maana hiyo, upande wa Serikali, Mkataba ule umeasisiwa na kusimamimwa na Wakristo watupu. Waziri wa Nchi Mkristo, Waziri Mkuu Mkristo, Mwanasheria Mkuu Mkristo.

Ni Wakristo! Wakristo! Wakristo!

Kama kwenye hoja ya makubaliano ya Bandari ni Wazanzibari wawili (ambao ni Waislamu) wamesaini makubaliano ya kuiuza Tanganyika, Mbona Waislamu hawakulalamika pale Wakristo 3 wazito Serikalini walipobuni mbinu za kutumia kodi za wananchi kuimarisha dini yao Ukristo Tanzania?

Kama hoja ni ukomo wa mkataba, mbona Mkataba huu wa Serikali na Makanisa hauna ukomo?

Ni mkataba wa milele na ndio maana mpaka leo (miaka 30 sasa) bado unaendelea kutumika.

Bado Serikali inaendelea kutekeleza mkataba wa kibaguzi ambapo inatumia kodi za wananchi wote kuimarisha shughuli za Kanisa.

USHAHIDI

Tarehe 23 Januari 2019, Rais Magufuli alikutana na viongozi wa dini zote IKULU.

Kwenye Mkutano ule Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Tanga Bwana Maimo Mndolwa alilalamika kwa Rais Magufuli kuwa Serikali inavunja mkataba kwa kujenga hospitali kwenye maeneo ambayo Kanisa imeachiwa kuwa na hosptali ambazo zinapewa fedha na Serikali.

Amelalamika hivyo kwa sababu Mkataba wa Makanisa na Serikali hauna ukomo.

Kila penye hospitali ya Kanisa, Serikali haikutakiwa kujenga hospitali yake.

Badala yake, Serikali inatakiwa kuendelea kutoa fedha za kodi kuwapa Makanisa ili ziendeshe hospitali zao na kuimarisha Ukristo kwa kutumia jasho la Watanzania.

Katika kusisitiza madai yake, Askofu Mkuu alitoa ushahidi wa hospitali zilizojengwa na Serikali katika Wilaya ya Ifakara, Ngara na Muheza ambazo kwa mujibu wa Mkataba wa 1993, Serikali haikutakiwa kujenga hospitali hizo za Wilaya.

Kitendo cha Serikali kujenga hospitali hizo kinatafsiriwa na Kanisa kuwa Serikali imevunja Mkataba kwa sababu sasa inatoa huduma hiyo muhumu kwa wananchi.

Askofu Mkuu alifafanua kua matatizo haya yapo kwenye ngazi ya Wilaya kwa sababu kwenye ngazi za juu, hakuna tatizo kwa kuwa kuna Msimamizi anaesimamia Mkataba huo.

Hapa Askofu Mkuu alikuwa ana maana kuwa hospitali za KCMC ya Moshi, Bugando ya Mwanza na CCBRT ya Dar es Salaam ambazo zote ni mali ya Kanisa bado zinaendelea kupata fedha za kodi huku zikiendelea kuwalipisha wananchi kwa huduma wanazopewa kwenye hospitali hizo.

Rais Samia Suluhu Hassan alifanya Mkutano na Baraza la Maaskofu la Kanisa Katoliki Tanzania uliofanyika Kurasini tarehe 25 Juni 2021.

Katika risala yao, Baraza la Maaskofu limeilaumu Serikali kwa kujenga hospitali zake kinyume cha Mkataba wa 1992, na Makanisa.

Kwenye risala hiyo, Baraza la Maaskofu limeshangaa kuona Serikali inajenga hospitali kwenye Wilaya ambazo Makanisa tayari yana hospitali zao.

Wamehoji kwa nini kuwepo na ushindani wa kutoa huduma hizo?

Kwa maana nyepesi, kwa nini Makanisa yasiachiwe kuendesha hospitali maisha (milele) na kuendelea kupewa ruzuku zinazotokana na kodi za wananchi?

Risala hiyo ni ya chombo cha juu kabisa katika Kanisa Katoliki ambao leo viongozi hao hao wanaohoji na kulalamika kuhusu makubaliano ya Serikali na DP World kuwa hayana ukomo!

Kanisa hilo hilo ambalo linapiga kelele kuhusu mkataba wa Serikali na DP World, ndilo ambalo kiongozi wake Askofu Method Kilaini alipewa shs. 80.9 milioni, Askofu Eusebius Nzigirwa alipewa shs. 40.4 milioni na Mchungaji Alphonce Twimanye Simon alipewa shs 40.4 milioni fedha za Rushwa zilizotokana na kashfa ya akaunti ya Tegeta ESCROW.

Hadi leo Kanisa halijatangaza hadharani hatua za kinidhamu iliyowachukulia viongozi hao.

Ukimya huu tuutafsiri vipi?

Kwa ukimya huu, Kanisa linapata wapi “moral authority” ya kupinga mkataba wa DP World.

Watanzania hawajasahau wakati wa utawala wa Magufuli wameshuhudia mauwaji kule Kibiti na Rufiji ambayo ni Wilaya zenye Waislamu wengi.

Watanzania bado wanakumbuka viroba vyenye miili ya watu vilivyokuwa vinaokotwa Coco Beach kila uchao.

Kanisa lilikuwa wapi wakati Magufuli anatoa roho za watu wasio na hatia?

Masheikh wangapi wamepotea ambao mpaka leo hawajulikani walipo wakati wa utawala wa Magufuli?

Hao waliobahatika wametoka jela wakiwa vilema kama alivyo Sheikh Abdallah Maginga Wambura ambaye kakatwa mguu kutokana na vipigo vya Polisi?

Yuko wapi mwanasiasa Ben Saanane ambaye “kosa” lake ni kuandika kuwa PhD ya Magufuli ni feki?

Yuko wapi mwandishi Azory Gwanda ambaye “kosa” lake lilikuwa kuandika ukweli kuhusu mauwaji ya Kibiti?

Wakati wa utawala wa Magufuli, Mbunge wa Kilwa Kusini Mhe Selemani Bungara maarfu “Bwege” aliwahi kusema Bungeni kuwa raia wake walichukuliwa na askari msikitini na wamepotea mpaka leo hawajulikani walipo.

Kanisa halikuyaona haya?
Kama Kanisa ilifumbia macho udhalimu na ukatili huu, leo wanapata wapi mdomo wa kukemea hicho wanachokiita mkataba usio na maslahi kwa wananchi?

Ni wananchi gani hao ambao leo Kanisa linajifanya kuwatetea?

Sasa Watanzania wanakumbuka kuwa pamoja na ukatili wote wa Magufuli, ni viongozi hao hao wa Kanisa waliokuwa wakimkaribisha kila Jumapili kwenye Makanisa yao na kumpa nafasi ya kuzungumza.

Leo Kanisa linataka kuwadanganya Watanzania kuwa lina maslahi na wananchi?

Kuna kitu kikubwa zaidi ya uhai?
Wakati watu wanatolewa roho zao na Magufuli Kanisa lilikuwa wapi?

KWANINI WAKRISTO WANAPINGA MKATABA WA BANDARI

Mpaka sasa si Makanisa wala wanasiasa ambao wametoa hoja ya kiuchumi.

Tofauti na Wamarekani ambao walisema hadharani kuwa hawawezi kuwapa Waarabu kuendesha Bandari zao, hapa Tanzania sababu haswa ya kupinga Mkataba haisemwi hadharani.

Vinatafutwa visingizio tu. Ukweli ni kuwa Mkataba wa Bandari unapingwa na kuwepo kwa fikra potofu za Kanisa kuwa:

Iwapo DP World watapewa zabuni ya kuendesha Bandari, uwepo wao Tanzania utawanufaisha Waislam kwa namna moja au nyingine.

Kuna wanaohofia kuwa iwapo Bandari itafanikiwa, na endapo itatokea fursa ya miradi mingine mikubwa ya kiuchumi, Dubai watakuwa na nafasi nzuri ya kupewa miradi hiyo. Kwa hiyo kuwepo kwao kutaimarisha Uislamu.

Ikiwa DP World watapata tenda ya Bandari, nchi itapata mafanikio makubwa ya kiuchumi ambayo kwa fikra zao potofu yatakuwa yameletwa na Rais Mwislamu. Kwa maana hiyo, Waislamu wanaweza kuongoza nchi kwa ufanisi.

Tayari kuna watu wanaosema kuwa Samia awe Rais wa mwisho Mwislamu Tanzania

Kuna wanaosema Bandari ikipata mafanikio itaonekana kuwa kumbe wanawake wanaweza kuongoza nchi vizuri
Kuna wasemao kuwa Bandari ikifanikiwa itaonekana Wanzanzibari nao wana uwezo sawa na wa Bara katika kuliongoza taifa letu.

Hoja zote hizo ni za kipuuzi.
Mafanikio yakiletwa na Rais Mwislamu au mwanamke au Mzanzibari wataonufaika ni wananchi wote.

Fedha za Bandari zitawanufaisha WOTE kwani anaepanga matumizi ya fedha ni Bunge letu ambalo lina Wabunge Waislamu, Wakristo na wasiokuwa na dini.

MWISHO
Nchi hii Waislamu wamekuwa wakidai kuwa Tanzania ni NCHI YETU SOTE, Waislamu wamekuwa wakidai kuwa idadi yao ni kubwa

Waislamu wanajigamba kuwa wamesoma lakini hawapewi fursa sawa

Kinachoshangaza ni kuwa tokea Mjadala wa Bandari uanze na hata mijadala mingine inayohusu UDINI huwasikii Waislamu kusema lolote.

Wao ni kimyaaaaaaaaaa.

Mjadala wa Bandari umetawaliwa na viongozi wa dini ya Kikristo, Wasomi Wakristo, Taasisi za Kikristo na hata wanasheria waliofungua kesi Mahakamani ni Wakristo.

Kwenye mjadala wa Bandari kuna mafunzo kwa Waislamu.

Sote tujiulize maswali yafuatayo:

Hao Wasomi Waislamu wanaolalamika hawapati fursa leo wako wapi?

Mbona hawapazi sauti zao?

Au Usomi wao ni wa makaratasi na kutafuta ajira tu?

Hiyo haki wanayoidai inaenda na WAJIBU.

Lazima watimize wajibu wao kwa kutumia taaluma na vipawa vyao kupaza sauti zao.

ZIKOWAPI TAASISI ZA KIISLAMU

Au zinasubiri mwezi wa Ramadhani kuomba msamaha wa kodi za tende?

WAKO WAPI MABARAZA YA ULAMAA

Au wanasubiri mwezi wa Ramadhani kualikwa futari IKULU?

WAKO WAPI VIJANA WA KIISLAMU

Hivi kweli nchi hii hakuna hata Waislamu wa kawaida kwenye magenge na vijiwe wakajibu hoja za Wakristo?

Bwana Mtume SAW Anatufundisha tunapoona uovu tuuondoe kwa mikono yetu. Kama hatuwezi basi tukemee.

Na kama hatuwezi kukumea basi angalau tuchukie ingawa kuchukia ni imani dhaifu.

Leo Waislamu kwa mamilioni yetu tunashindwa hata KUSEMA?

Tumeamua kuwa na imani dhaifu na kuwaacha waseme Wakristo peke yao?

MWENYEZIMUNGU ASHUHUDIE TUMEFIKISHA
Hapa umetetea mkataba wa DP World au umetetea uislamu? Nani anawadanganya waisilamu au wakristo kuwa kizazi hiki kinaamini sana kwenye hizi dini zenu? Kwa sasa dini ya kweli ni pesa, hizo dini zenu ziko kimazoea zaidi, ndio maana kizazi hiki hakifuati sana mafundisho ya dini, bali kinaamini kwenye digital.

Ni hivi, mkataba wa bandari haufai, hao TEC wamesema waziwazi kuwa mkataba huo haufai, kama unaona kwa kusema hivyo wanauoinga uislamu huo ni mtazamo wako.
 
Nakwambiaje. Mimi ni mwanasheria nguli na hapa nimekuja China kuonana na wateja wangu ambao ni Kampuni ya wachina iliyowekeza Tanzania hapo.

Kama nalipiwa hadi Ticket ya ndege kuja huku jua tu mimi sio mwenzako.


Vumilia tu! Wengine tumebarikiwa zaidi!!
Umelipiwa tiketi ya tatumzuka.Iangalie vizuri.
 
Matapeli ni matapeli tu !
Chambua hoja kwa hoja... !! Kila mtu anajua kuwa matapeli ni matapeli tu, je! Rugemalira kwa hoja nilizokuwekea, bado unamuweka kwenye kundi la matapeli? Kama jibu ni ndiyo, weka hoja za kuhalalisha jibu lako. Binafsi nimekuwekea hoja za jibu langu, kwamba yeye siyo tapeli..!! Nje ya hapo ni blah blah za kulishwa maneno tu na kuacha kutumia akili yako vizuri
 
Back
Top Bottom