Tundu Lissu: Rais Samia na Mbarawa wameiuza Tanganyika yetu kwa Waarabu
Hivi kwa nini hutaki kuelewa.

Maana ya kuwepo kwa IGA ni nini?

Kuna sababu zipi zinazolazimisha kupoteza muda wa wabunge, na hata kuwahonga pesa na wengine kutishiwa kabisa wasithubutu kupinga hiyo IGA?

Hivi akili unaziweka wapi wewe unapoandika haya unayoweka humu kutetea ujinga?

Na kwa bahati mbaya kabisa, unazo akili za kutambua na Kuuita huo "MKATABA MAMA", lakini bado huoni umuhimu wake?

Tunaiita Katba ya nchi" kuwa ni sheria MAMA", sheria zote zinachimbuka tokana na Katiba hiyo, sasa wewe leo hii, wewe unaona unaweza kutunga sheria amabazo zitakinzana na Sheria Mama"?

Nimejadili na wewe vya kutosha, na inanilazimu niseme yafuatayo kukuhusu wewe, kama wewe:

Ninakuona kuwa ni mtu mwenye busara ya kutosha, asiyechafukwa na akili kwa haraka na kupoteza fahamu (kwa sababu nimekuchokoza maksudi mapema sana, lakini ulibakia kuwa na fahamu zako).

Bila shaka wewe ni mfanya kazi, aliye karibu sana na hili swala la Bandari. Mmepewa majukumu ya utetezi wa jambo bovu kabisa kwa nchi yetu.

Swala la 'uzalendo' uliloliongelea mapema sana, ninakuona kwamba pengine binafsi, wewe halikugusi kwa karibu sana, kutokana na majukumu uliyo nayo na kuyatekeleza, au unufaikaji binafsi unaoupata kutokana na mkataba kama huu.

Ninakuomba sana, wewe kama mTanzania, uweke mbele zaidi maslahi ya nchi yako na maskini wa nchi hii.
Kazi za bandari hazina 'rocket' sayansi yoyote. Hao DP World hawakuzaliwa wakijua kila kitu, na kwamba hata hiyo teknologia wanayotumia sasa siyo wao pekee wenye uwezo nayo. Hata kama inatulazimu kuwaweka hapo watufanyie kazi kwa ubora, ni jukumu letu, kwamba kazi hizo tutazimudu wenyewe katika muda maalum, isiwe zaidi ya miaka 20 tena kama tulivyofanya na TICTS.

Kama taifa, ni lazima tuwe na mpango wa kujitegemea kufanya mambo mengi yanayotuhusu wenyewe. Tusijiweke waziwazi namna hii tunavyofanya sasa kuwa wategemezi kwa watu wengine milele..

Hayo ni baadhi ya maoni yangu tu kwa kifupi kwako, bila kujali maslahi unayoyapigania sasa hivi katika jambo hili linaloendelea.
Una hoja murua kabisa na yenye mashiko: kujimudu au kujitegemea wenyewe katika kujijengea uwezo wa kuendesha, kusimamia na kudhibiti rasilimali zetu wenyewe.
 
Ukitaka twende huko, ninapaweza sana.
Kwa hiyo sasa ninakwambia kwamba huna kitu kichawni. Wewe ni wakala tu unayetumwa kuja hapa kutafuta wapumbavu wenzako. Nilitaka tumalizane hapa, sasa nimeamua nikomae nawe hadi tutakapofikia.
Nashauri achana naye tu. Asiyetaka kukuelewa mwachie aendelee na uelewa wake. Usipoteze muda na akili yako kufundisha asiyefundishika kwako.
 
Wanasheria wa serikali wanazunguka huko kuipa jamii uelewa wa nini kinachotaka kufanyika. Ni kazi ya kizalendo itakayokuja kueleweka umuhimu wake siku moja.
Huu mstari huu, umenifikirisha kidogo, na kupata picha linavyochezwa.

Ninakuomba jaribu sana "kufikiri kidogo nje ya boksi". Sasa hivi naona kama umejitwisha boksi zito sana. Nimekwishaligusia hili hapo juu. Ni juu yako kunielewa au la!.
 
Hapo kaongea kwa hisia bila facts
Wewe jamaa vipi tena? Kaongea Kwa hisia!!!??

"Kuongea kwa hisia" maana yake ni kuongea kwa kudhani au bila kuwa na uhakika..

Lakini Je, ndivyo ilivyo kweli Kwa Tundu Lissu jana?

Jibu ni HAPANA kubwa!!

Kwa sasa yeye na hata wewe unahitaji ushahidi wa fact gani tena wakati alikuwa na facts zote mkononi mwake ambao ni mkataba (makubaliano ya maandishi) yaliyosainiwa na waziri wake Prof. Mbarawa (Mzanzibari) kwa yeye mwenyewe Rais Samia Suluhu Hassan (Mzanzibari pia) kumpa kumpa "full authority" kuuza mali zetu watanganyika ?

Please, try to think twice and carefully about this..

Rais Samia Suluhu Hassan kwa hili, katukosea sana Watanganyika...!!
 
Hayo maandishi ya habari yaliyopewa hongo yanajisikiaje nchi yao inauzwa kwa waarabu? Njaa zingine ni za kuedekeza
 
Sasa kama hao wazanzibar wameamua kwa makusudi kuuza mali za tanganyika mnajuaje kama wanalipa kisasi kwa tanganyika kung'ang'ania visiwa vyao? Hii ishu itatikisa muungano kwa style ambayo haikutegemewa. Watanganyika wamechachamaa hawataki bandari yao iuzwe kwa mwarabu bila mkataba wa kueleweka
 
Moyo wa mtu ni kiza kinene

Ukimuona samia anavyotabasamu akiwa na watanganyika utadhani anawajali

Kumbe ana nia ovu ya kuuza nchi kwa waarabu

Siku zote ukiona mtu anajifanya mwema sana kwako shituka

Nilipoona samia anakaa karibu na wapinzani nilijua huyu ana nia ovu ya kuingamiza Tanganyika

Ni wazi mungu atamuondoa kwenye kiti kikuu
Huwezi kuwadhulumu watanganyika milion 59 ukaasalimika
Samia utaondoka na waarabu wataondoka
waarabu wataondokaje kama tayari wamesaini mkataba usio na ukomo kumiliki bandari?
 
Kuna mambo ya kujiuliza.., kwa nn Mwarabu tu. Maana nasikia yuko pia TANESCO, POSTA, TPDC daaah kazi ipo.
nani alileta sera ya uwekezaji? Matokeo yake ndiyo hayo. Eti uwekezaji, mara ubia! Haya sasa ngoma ndiyo imenoga. Bado wachina nao watataka sehemu za kuwekeza kwa hoja ya kuleta ufanisi. Wanasiasa wenyewe ndio hawa, watawekezwa na wao
 
Hapa Ccm Wanapita Wanasonya Tu Na Kutema Mate Mbali Huku Wanapatwa Kiungulia Maeneo Ya Kifuani
ccm inavulia mambo ya ajabu sana, sio kama haiwahusu ila ni nani atamfunga paka kengele? Itabidi wakubaliane tu na serikali yao inavyoamua kufanya wanapitisha wote huku wanaona si vema. Ni unafiki tu huko mbeleni wataanza kusema ubaya wake
 
Mwarabu Ametapakaa Ghafla Tanzania Nzima
tuseme ukweli tu, huu ni ukoloni kutawaliwa kiuchumi, kiutamaduni tayari imebaki kisiasa, soon wakikamata uchumi wa nchi wanaibukia siasani na huenda tayari wana vibaraka wao wanaofanikisha malengo yao
 
Hao waandishi wa habari waliopata milioni sita kutetea mauzo ya sehemu ya nchi yao ni hasara na laana kubwa kwao na vizazi vyao vijavyo.
njaa mbaya sana, esau akauza urithi wake ili tu atulize njaa yake. Umasikini nao ni mbaya, nchi itajaa wawekezaji na wabia wa aina hii wengi tu. Kuna wengine wako kwenye migodi, wengine kwenye wanyama, wengine watataka ardhi walime mazao yao, kama zamani ukoloni wa zama mpya unaibuka, kuja kuwatoa wakoloni waliosaini mikataba ya milele ni shughuli pevu kwa vizazi vyetu
 
Bahati nzuri waandishi wa habari wanaotumika ni walewale tu, tangu mgogoro wa Loliondo mpaka leo, jambo lolote linalopingwa wanatengeneza agenda kubwa na kufanya promo....hizi media houses za Bongo uozo mtupu
hizi media zina njaa kali sana, hazioni hasara kufanya promo mikataba ya ajabu na wawekezaji
 
Hii DP world itasimamia bandari za Tz nzima mpaka za Zanzibar ( maana ni sehemu ya Tz) au Tanganyika tu kama Lissu anavyodai ? Kwani mamlaka ya bandari si hiyo hiyo moja ?.....

Lissu awe makini asipoteze muelekeo wa mjadala na akanasa kwenye mtego wa wajanja, ajikite na makubaliano ya hiyo MOU tu, hayo ya Tanganyika na Zanzibar ni spinning za watu wenye malengo yao.

Kalamu Nguruvi3 JokaKuu Pascal Mayalla
Mkuu naona yupo makini, na anasema anao huo Mkataba huo. Lisu ni Mwana Sheria Msomi anaelewa na ana uhakika na kile anasema.
 
Kwako mwanasiasa Tundu Lissu!

Ukiwa kama mwanasiasa na mwanasheria mzoefu hebu punguza kulialia kwenye media na kuja na hoja dhaifu za kuwagawa Watanzania katika mapande mawili ya U-tanganyika na U-zanzibar linapokuja suala la maslahi mapana ya Taifa.

Umesema kuwa mkataba unao na ukiwa kama mwanasheria hebu tumia fursa hii kurekodi walau video mtandaoni ambazo zitaelezea hivyo vipengele vya mkataba wa DP world ambavyo unaona havina maslahi kwa Taifa la Tanzania.

Hoja ya kuwa nchi imeuzwa kwa waarabu haisaidii mbona husemi nchi yetu imeuzwa kwa wazungu pindi wanapochangia sehemu kubwa ya bajeti yetu kila mwaka.?

Punguza kulialia ,njoo na suluhisho nini kirekebishwe ili kuhakikisha huu mkataba unakuwa na usawa !

Asante.
 
Back
Top Bottom