Tundu Lissu: Rais Samia na Mbarawa wameiuza Tanganyika yetu kwa Waarabu
Wapumbavu ni nyinyi mnaoeleweshwa halafu hamuelewi chochote. Kujiunga humu miaka mingi iliyopita sio wingi wa akili au busara.

Tundu Lissu ni CHADEMA, walioamua kuikomoa bandari ya Tanzania kwa siasa nyepesi za ujira mdogo unaokwisha kesho tu.
Dah!

Hizi ndio 'talking points' mulizopewa hivi karibuni mkapige propaganda?
Mbona ni pointi mfilisi kabisa.
Hizi labda mzilenge kwa watu wasiokuwa na upeo kabisa wa haya maswala ya mahusiano.

Samia alipokubaliana na Uhuru, halafu baadae na Ruto kupeleka bpmba la gesi kuwanufaisha hao majirani ambao sasa ndio wanaotupiga vita, hata kabla ya huyu Samia kufikiria kuwanufaisha waTanzania na hiyo gesi yao, bila shaka wewe ulikuwa hujazaliwa, au siyo?

Hizi propaganda zilizochoka sana za "vita vya kiuchumi" tafuta wajinga wa kuwapelekea ujinga huo.

Jirani huyo huyo, unaruhusu aingie na malori yake hadi shambani kwa mkulima wako, na kuzoa mazao yote, akihatarisha usalama wa nchi yako; hukuona vita hiyo ya kiuchumi, hadi alipokuja Mwarabu na tende na kashata ndiyo ukaona vita?

Tafuta wajinga wengine wa kuwauzia upuuzi huo unaoutembeza sasa hivi. Usiulete kwa Kalamu.
 
Unarudia makosa yale yale ya wengi wetu kudhani kwamba mkataba uliosainiwa bungeni ndio huo unaokwenda kutumika katika michakato ya kibiashara.
Hivi kwa nini hutaki kuelewa.

Maana ya kuwepo kwa IGA ni nini?

Kuna sababu zipi zinazolazimisha kupoteza muda wa wabunge, na hata kuwahonga pesa na wengine kutishiwa kabisa wasithubutu kupinga hiyo IGA?

Hivi akili unaziweka wapi wewe unapoandika haya unayoweka humu kutetea ujinga?

Na kwa bahati mbaya kabisa, unazo akili za kutambua na Kuuita huo "MKATABA MAMA", lakini bado huoni umuhimu wake?

Tunaiita Katba ya nchi" kuwa ni sheria MAMA", sheria zote zinachimbuka tokana na Katiba hiyo, sasa wewe leo hii, wewe unaona unaweza kutunga sheria amabazo zitakinzana na Sheria Mama"?

Nimejadili na wewe vya kutosha, na inanilazimu niseme yafuatayo kukuhusu wewe, kama wewe:

Ninakuona kuwa ni mtu mwenye busara ya kutosha, asiyechafukwa na akili kwa haraka na kupoteza fahamu (kwa sababu nimekuchokoza maksudi mapema sana, lakini ulibakia kuwa na fahamu zako).

Bila shaka wewe ni mfanya kazi, aliye karibu sana na hili swala la Bandari. Mmepewa majukumu ya utetezi wa jambo bovu kabisa kwa nchi yetu.

Swala la 'uzalendo' uliloliongelea mapema sana, ninakuona kwamba pengine binafsi, wewe halikugusi kwa karibu sana, kutokana na majukumu uliyo nayo na kuyatekeleza, au unufaikaji binafsi unaoupata kutokana na mkataba kama huu.

Ninakuomba sana, wewe kama mTanzania, uweke mbele zaidi maslahi ya nchi yako na maskini wa nchi hii.
Kazi za bandari hazina 'rocket' sayansi yoyote. Hao DP World hawakuzaliwa wakijua kila kitu, na kwamba hata hiyo teknologia wanayotumia sasa siyo wao pekee wenye uwezo nayo. Hata kama inatulazimu kuwaweka hapo watufanyie kazi kwa ubora, ni jukumu letu, kwamba kazi hizo tutazimudu wenyewe katika muda maalum, isiwe zaidi ya miaka 20 tena kama tulivyofanya na TICTS.

Kama taifa, ni lazima tuwe na mpango wa kujitegemea kufanya mambo mengi yanayotuhusu wenyewe. Tusijiweke waziwazi namna hii tunavyofanya sasa kuwa wategemezi kwa watu wengine milele..

Hayo ni baadhi ya maoni yangu tu kwa kifupi kwako, bila kujali maslahi unayoyapigania sasa hivi katika jambo hili linaloendelea.
 
Dah!

Hizi ndio 'talking points' mulizopewa hivi karibuni mkapige propaganda?
Mbona ni pointi mfilisi kabisa...

Talking Points mlizopewa nyinyi ndio huu ujinga unaouandika humu JF?. Hii ni biashara kubwa inayopigwa vita kutoka kila upande.

Kama ilivyopigwa vita reli ya SGR ilipoanza kujengwa, kama yalivyopigwa vita manunuzi ya ndege za ATCL.

Wanasheria wa serikali wanazunguka huko kuipa jamii uelewa wa nini kinachotaka kufanyika. Ni kazi ya kizalendo itakayokuja kueleweka umuhimu wake siku moja.
 
Nimewasikiliza sana watu kama Wassira, Prof Kitila, Tulia, Zungu na wengine wengi wanao zungumza kutetea uhalifu huu dhidi ya Bandari zetu na ujuha wa kama ule wa Mangungo dhidi Carl Peters na nikawakumbuka vijana machachari walio fanya mageuzi makubwa kwenye nchi zao.
Vijana hao walijua wakubwa wameshika mpini na ukishindana nao unaumia basi wakafanya nao yao na kunyoosha nchi zao.
Hao sio wengine ni;
Thomas Sankara,
Jerry Rawlings,
Yacub Gowon,
Obasanjo nk.
Kwa wale wazamani kidogo watakumbuka hao vijana nchi zao ziliharibiwa na ufisadi, ubishi na uchoyo wa viongozi ukiambatana na kutokujali wengine wanasemaje kama ilivyo sasa kwa nchi hii inayokabidhiwa kwa waarabu.
Jee tunao wenye mawazo kama ya kina Rawlings?
Mimi sijui.
 
Hivi kwa nini hutaki kuelewa.

Maana ya kuwepo kwa IGA ni nini...
IGA ni mkataba MAMA wa jumla. Ipo mikataba ya kibiashara itakayoingiwa kati ya DP World na wafanyabiashara mbalimbali wazalendo hiyo ndio yenye ukomo.

Na kumbuka kuwa hiyo mikataba mipya itawezesha kuanzishwa kwa makampuni yatakayosajiliwa humu nchini kwa sheria zetu.

Ujinga ni wewe kushindwa kuelewa ukidhani kuwa hiyo IGA ndio itakayotumika katika biashara nzima ya uwekezaji wa hao waarabu.
 
Hao ni golden era, look how jamii zetu zimetetereka kimaadili miaka ya sasa.
Mapinduzi ya namna hiyo yanahitaji support sana, tatizo umoja hatuna na kila mtu kishakuwa mwoga
 
Kwanza Nawasalimu kwa Jina la Kristu....
Hongereni sana kwa mjadala wa hekima ya Kina juu ya Mkataba wa Bandari yetu na DP WORLD.
Lkn hili la Bandari litumike kuwatoa usingizini maaskafu wetu wa Kikristu. Tunajua Ukristu na Unafiki ni mwiko lkn jiulizeni. Pamoja na Madhaifu yoooote ya Kiungozi yaliyopo mmewasikia Masheikhe wanavyo comment kuhusu Uongozi wa Nchi? Je Kuhusu Mkataba wa DP World? Je, Kuhusu haiba ya Mhe.Rais?
Mmesikia Maoni ya Sheikh Ponda kuhusu DP WORLD? Maaskofu mna kazi ya kufanya dhidi ya Waumini wenu wanaposhika Madaraka hasa URAIS.
Tumeona jinsi Viongozi wenzenu wanavyomlinda mfuasi wao kwa nguvu zote na kwa njia zote?
Maaskofu nyie tukirudi kwenu mlitumika sana kushambulia Kiongozi wa Nchi mfuasi wenu RIP JPM mkisoma takwimu za CORONA, Mkisoma Takwimu za Unyanysaji, mkisoma Idadi ya Uonevu wake. Bagonza, Mwamakula nk waligeuka kuwa mwiba kwa Mtawala Mfuasi wa Madhehebu yenu. Leo Mungu amejibu maombi yenu yule Mtawala mliyekesha mkiitisha Press Conference za Ubaya wake hayupo. Kawaletea mliyetaka na leo mnaendekeza Vilio vingine.
Bwana Awe Nanyi Viongozi wangu mnapaswa kukaa kimia tu maana mlipewa Upande wenu lkn mkageuka timu pinzani.
SALA YANGU IMEFIKA MWISHO..mimi Mkiristo nikiwa Kiongozi Askofu wangu anageuka Mpinzani wangu kwenye Madhabahu ya Bwana! Mjitafakari na Mtwambie Kiongozi wa BAKWATA hata mmoja tu anayekosoa Kiongozi wetu na Mikataba yake!
 
Talking Points mlizopewa nyinyi ndio huu ujinga unaouandika humu JF?. Hii ni biashara kubwa inayopigwa vita kutoka kila upande.

Kama ilivyopigwa vita reli ya SGR ilipoanza kujengwa, kama yalivyopigwa vita manunuzi ya ndege za ATCL.

Wanasheria wa serikali wanazunguka huko kuipa jamii uelewa wa nini kinachotaka kufanyika. Ni kazi ya kizalendo itakayokuja kueleweka umuhimu wake siku moja.
Mkuu, 'Steven Joel Ntamusana', pamoja na kwamba umekwishanisoma hayo ya mwanzo niliyoandika hapo, ninakuomba ukanisome tena katika yale niliyoongezea baada ya wewe kunisoma kwa hico kipande kifupi.

Niseme tena hapa. Hiyo "vita ya kiuchumi" mnayoitangaza sasa, ni 'afterthought', kati ya mbinu mbovu kabisa za kupoteza watu wasiokuwa na uelewa mzuri wa mambo.
Usijaribu kuniuzia upuuzi huo mimi.
 
Mkuu, 'Steven Joel Ntamusana', pamoja na kwamba umekwishanisoma hayo ya mwanzo niliyoandika hapo, ninakuomba ukanisome tena katika yale niliyoongezea baada ya wewe kunisoma kwa hico kipande kifupi.

Niseme tena hapa. Hiyo "vita ya kiuchumi" mnayoitangaza sasa, ni 'afterthought', kati ya mbinu mbovu kabisa za kupoteza watu wasiokuwa na uelewa mzuri wa mambo.
Usijaribu kuniuzia upuuzi huo mimi.
Kujiona wewe mpuuzi ni hisia zako binafsi, hakuna mtu wa kuziingilia.

Uelewa wangu na wako juu ya mkataba wa DP World ni vitu tofauti kabisa.
 
IGA ni mkataba MAMA wa jumla. Ipo mikataba ya kibiashara itakayoingiwa kati ya DP World na wafanyabiashara mbalimbali wazalendo hiyo ndio yenye ukomo.

Na kumbuka kuwa hiyo mikataba mipya itawezesha kuanzishwa kwa makampuni yatakayosajiliwa humu nchini kwa sheria zetu.

Ujinga ni wewe kushindwa kuelewa ukidhani kuwa hiyo IGA ndio itakayotumika katika biashara nzima ya uwekezaji wa hao waarabu.
Unarudiarudia jambo ambalo halina ugumu kuelewa; ina maana una tatizo na 'thought process' yako.

Soma tena nilivyokufahamisha muunganiko kati ya huo unaouita "Mkataba Mama" na hiyo mikataba mingine itakayofuata.

Kama unaanza na Mkataba Mama mbovu, utategemea vipi utoke na mikataba mizuri huko baadae?
 
Kujiona wewe mpuuzi ni hisia zako binafsi, hakuna mtu wa kuziingilia.

Uelewa wangu na wako juu ya mkataba wa DP World ni vitu tofauti kabisa.
Ukitaka twende huko, ninapaweza sana.
Kwa hiyo sasa ninakwambia kwamba huna kitu kichawni. Wewe ni wakala tu unayetumwa kuja hapa kutafuta wapumbavu wenzako. Nilitaka tumalizane hapa, sasa nimeamua nikomae nawe hadi tutakapofikia.
 
Unarudiarudia jambo ambalo halina ugumu kuelewa; ina maana una tatizo na 'thought process' yako.

Soma tena nilivyokufahamisha muunganiko kati ya huo unaouita "Mkataba Mama" na hiyo mikataba mingine itakayofuata.

Kama unaanza na Mkataba Mama mbovu, utategemea vipi utoke na mikataba mizuri huko baadae?
Hauna ubovu wowote huo mkataba Mama. Kaka hii mikataba inaandikwa sio ndani ya siku moja, inajumuisha wataalam wa Dubai na Tanzania.

Tupunguze huu ujuaji wetu wa JF, waliosaini huu mkataba ni madaktari wa sheria wenye uzoefu mkubwa wa kusaini na kufanya majadiliano ya kina juu ya haya masuala.
 
Mmh! Watanzania unawafahamu vizuri mkuu? Hii ishu inaongelewa kwenye mitandao tu lkn mitaani watu wako bize na Yanga na Simba.

Tena hata mitandaoni huku, unaweza kukuta ni mtu mmoja mwenye ID 4 hapa JF halafu huyo huyo anaandika na Instagram, Twitter, Facebook, n k

Kuna haja ya dunia kufanya tafiti upya ili kujua aina ya binadamu wanaopatikana Tanzania
Sio kweli, nipo WhatsApp magroup ya shule, kila siku ubishani ni huo wa bandari.

Mtaani pia mjadala ni huu
 
Sasa kama masheikh hawayajui kiundani mambo ya bandari unataka waongee nini..? Si wataanza kuvurunda bora wakae kimya
 
Lissu anatamka hadharani katika IGA hakuna sehemu aliyoona imeandikwa wanawekeza kiasi gani na wanategemea kurudisha kwa muda gani.

Kwa kifupi hiyo ndio ‘consideration’ kwenye mkataba; kama hayo maelezo hayapo hiyo ni agreement tu; lakini sio mkataba.

Uwezi kwenda mahakamani kama amna consideration kwenye maandishi ya unayoita mkataba.

Serious majirani zetu wakenya, waganda, wanyarwanda watakuwa wanatudharau sana; hao watu mnaowategemea wanauwezo mdogo mno wakudadavua mambo ya mikataba ya biashara.
 
Back
Top Bottom