BABA Dillish
JF-Expert Member
- Jan 20, 2016
- 2,362
- 3,252
Mwanazuoni halisi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni uwekezaji mkubwa wenye kulenga uboreshaji wa utoaji huduma bandarini.Kwa hiyo wewe unamwona 'Kalamu' kuwa hana akili kichwani?
Usinifanye nikudharau sana kwa ujinga wa namna hii.
Sasa mnaokoteza visababu mbalimbali ili mradi mtimize lengo la kuvuruga nchi?
Eti "vita ya kiuchumi"?
Halafu unione mimi kuwa "msaliti wa nchi", na wala hujui chochote kunihusu mimi, na ninapambania maslahi ya nani huyo anaye nilipa hivyo vipande?
Hivi unaelewa kinachoendelea hapa, au unajiandikia tu mradi uandike?
Huoni hao wasaliti wanaojificha wakati wakituingiza kwenye mikataba mibovu, halafu wewe hapa unageuka na kulaumu wasiohusika kabisa?
Wewe unalipwa na nani.
Tueleze uzuri wa masharti ya hayo makubaliano. Hapo utakuwa umemaliza kazi ya uzalendo wako.
Mkataba gani hauna muda kwamba unaanza lini na kuisha lini
Tundu Lissu akiongea na waandishi wa habari amesema haya...
Kwenye mamlaka ya moja kwa moja waliyonayo kama Wazanzibar kwenye huu MKATABA kwa makusudi kabisa hawajajumuisha bandari ya kwao Zanzibar ilhali ni jambo la MUUNGANO.
Hawa WAZANZIBAR wameuza mali yetu Watanganyika kwa MKATABA wa milele. Namaanisha hadi bahari itapokauka!"
Mimi ninao huo MKATABA lakini sijaona wapi pameandikwa tutapata hizo hela zinazosemwa na wapambe waliohongwa."
Ni wazi wao kuanzia Samia, Mbarawa na Katibu mkuu wa wizara husika ni WAZANZIBAR na kwa makusudi wameuza mali ya Tanganyika kwa sababu haiwahusu!"
Wengi wenu mnafikiri ni bandari pekee imeuzwa na hao WAZANZIBAR mnajidanganya! Kwa mjibu wa MKATABA hiyo reli ya Magufuli na mabarabara ni ya waarabu hadi maeneo yote maalum ya kibiashara yanakuwa yao."
Bandari kavu kwa mfano ile ya Isaka na zingine zote zinakuwa za waarabu wameuziwa na Samia ambaye ni Mzanzibar."
DPW wamehonga karibia kila awaye na ushawishi. Waandishi zaidi ya 40 walipelekwa kula raha na miongoni mwao yupo mmoja amenieleza kwa siku tatu alizokaa kule alirejea na hongo ya mililioni 6!"
Kama kweli huo mkataba una manufaa na faida kwanini hao WAZANZIBAR ( Samia na Mbarawa ) wameziacha bandari zao?!"
HATUPO TAYARI RASILIMALI ZETU WATANGANYIKA ZIUZWE HOVYO NA WAZANZIBAR - HATUPO TAYARI NASEMA!"
Hili suala halitaisha leo wala kesho na lazima Samia atambue. Huu MKATABA haufai na mbovu kuliko ubovu wenyewe!"
Lissu.
Na umejiunga hapa JF juzi tu, kwa maksudi maalum; kwa jina la bandia!Suala la bandari ni vita ya kiuchumi na mkuu Kalamu kaamua kuisaliti nchi yake kwa vipande thelathini vya fedha kama Yuda.
Lakini mwisho wa usaliti unakaribia. Tutaibuka washindi katika vita hii iliyojaa maadui tunaokula nao chakula meza moja.
Ni nani asiyeyajua haya uliyotaja hapa juu, na bado huelewi swali unaloulizwa, na kwa kuwa upo hapa kupotosha, unakimbilia kueleza mambo yanayofahamika na yeyote.Ni uwekezaji mkubwa wenye kulenga uboreshaji wa utoaji huduma bandarini.
Ingizo la teknolojia linakwenda kuongeza tija zaidi ya mara mbili ya hii ya sasa.
Rasilimali muda katika dunia ya sasa ni nyeti sana, na kwa kuimarika huduma kwa maana ya wingi wa meli zitakafanyiwa kazi na bandari inamaanisha utabakia muda mwingi wa kushughulika na masuala mengine. Msemo wa time is money unakwenda kutimizwa kwa vitendo.
Pesa nyingi inayopatikana ikiwa ni faida ya mradi inakwenda kugusa sekta nyingi ambazo kwa muda huu zinashindwa kukwamuliwa na zinaonekana zimelala.
Ningependa sana kuamini ulichoandika hapa, lakini huna ushahidi wowote unaosimamia maneno yako haya.Mbona hakuna points hapa kasema nini? Sbb naona kelele tupu..
Bunge lilishapendekeza kipengele cha muda wa Mkataba urekebishwe, pia ni bandari ya Dar tu gati 8 hadi 11 tu na si bandari yote ya Dar au bandari zote za Tanzania kuwa DPW watachukua, Tundu Lissu aache kupotosha.
NAKAZIAShikilia hapohapo TL, napenda sana ugomvi.
Uzuri au ubaya wa makubaliano unatafsirika kwa vitendo baada ya mkataba kuanza kutekelezwa. Vifungu vya kisheria hukosa maana kama havitekelezeki.Ni nani asiyeyajua haya uliyotaja hapa juu, na bado huelewi swali unaloulizwa, na kwa kuwa upo hapa kupotosha, unakimbilia kueleza mambo yanayofahamika na yeyote.
Tueleze uzuri wa makubaliano uliomo kwenye Mkataba. Hlo ndilo swali. Achana na haya tunayoyataka sisi sote.
Hopeless ni nyinyi msioitakia TZ mema mkiwa mmetumwa na nchi jirani ili muihujumu nchi yenu wenyewe.Na umejiunga hapa JF juzi tu, kwa maksudi maalum; kwa jina la bandia!
Leo hii wewe ndiyo unajitangaza 'mzalendo', kumbe uwepo wako humu jukwaani ni kwa kazi maalum uliyopangiwa kuifanya!
Hopeless Kabisa.
Prof Tibaijuka ni CDM?Baada ya kiki ya kuzurura Mikoani kubuma Sasa chadema wanatembea na kiki ya Bandari
Chama Cha matukio 😁😁
Mawazo hafifu sana haya.Ni uwekezaji mkubwa wenye kulenga uboreshaji wa utoaji huduma bandarini.
Ingizo la teknolojia linakwenda kuongeza tija zaidi ya mara mbili ya hii ya sasa.
Rasilimali muda katika dunia ya sasa ni nyeti sana, na kwa kuimarika huduma kwa maana ya wingi wa meli zitakafanyiwa kazi na bandari inamaanisha utabakia muda mwingi wa kushughulika na masuala mengine. Msemo wa time is money unakwenda kutimizwa kwa vitendo.
Pesa nyingi inayopatikana ikiwa ni faida ya mradi inakwenda kugusa sekta nyingi ambazo kwa muda huu zinashindwa kukwamuliwa na zinaonekana zimelala.
IGA ikisema Bandari zote Tanganyika ziwe chini ya himaya ya Kampuni ya nchi husika, na kama matatizo yakitokea mbele ya safari kwenye utekelezaji huna njia ya kuondokana na masharti hayo; hili nalo unaliona ni jambo linalosubiri utekelezaji wa mikataba mbalimbali?Uzuri au ubaya wa makubaliano unatafsirika kwa vitendo baada ya mkataba kuanza kutekelezwa. Vifungu vya kisheria hukosa maana kama havitekelezeki.
ishu ya bandari ccm waangalie sana inaweza kuwang'oaTatizo ni katiba yetu mbovu, inampa absolute power rais ambaye siyo raia wa Tanganyika kufanya lolote altakalo bila hofu ya kuhojiwa wala kushitakiwa na chombo ama mtu yeyote.
Kwa kauli hizi za Tundu Lisu nayaona maridhiano yakitumbukia kwenye tundu la choo
Hana uwezo wa kutoa ufafanuzi. Badala yake ndio atavuruga kabisa. Ndiyo maana kamwachia Mbarawa.Prof Tibaijuka ni CDM?
Kardinari Pengo ni CDM?
Mimi ni CDM?
Nashauri SA100 atoke aitishe PRESS atoe ufafanuzi.
Jambo hili halileti AFYA Kwa utangamano wa Nchi yetu hata kdg.
Huu ni upumbavu unaokusumbua mpuuzi wewe.Hopeless ni nyinyi msioitakia TZ mema mkiwa mmetumwa na nchi jirani ili muihujumu nchi yenu wenyewe.
Wapi huko ndugu Kalamu?Hana uwezo wa kutoa ufafanuzi. Badala yake ndio atavuruga kabisa. Ndiyo maana kamwachia Mbarawa.
Lakini nikubaliane nawe, kwenye jambo lenye hisia nyingi kama hili, ilitakiwa ajitokeze aeleze ukweli wenyewe uliopo nyuma ya jambo hili.
Hata lilivyoshughulikiwa tokea mwanzo, kunatia mashaka sana.
Rais mzima kaenda kuwekwa ndani na kufundwa jinsi ya kuendesha maswala ya nchi yake?
Karibu wiki nzima alipotea, kumbe kafichwa mahala kwa siri kubwa akiamua mambo ya nchi yake na viongozi wa nchi nyingine.
Huko huko kwa wajomba zake.Wapi huko ndugu Kalamu?