Tusuburi vikao na waraka wa siri vitembee kwenye masinagogi, mahekalu na misikiti
 
Hoja 8 muhimu za TEC

14. Ibara zifuatazo za Mkataba huu zina matatizo yatakayosababisha nchi kutofikia uhuru wa kiuchumi (economic independence):

14.1. Ibara ya 2 (1): inayohusu lengo la Mkataba huu ambalo ni kuweka utaratibu unaoibana Tanzania kisheria katika kuendeleza, kuboresha na kuendesha bandari zote za bahari na maziwa, maeneo maalum ya uwekezaji, maeneo ya usafirishaji wa mizigo, na maeneo mengine ya kiuchumi.

14.2. Ibaraya 4: inayohusu wigo wa Mahusiano na Utekelezaji unaoitaka Serikali ya Tanzania kuwajibika kuijulisha Dubai kila fursa ya uwekezaji inapojitokeza.Hiiinakinzana na baadhi ya sheria za nchi yetu, kwa mfanosheria ya ushindani na ile ya manunuzi.

14.3. Ibaraya 5: ambapo DPWorldimepewa haki ya kuendeleza, kusimamia na kuendesha miradi pekee yake, wakati Tanzania inabaki na wajibu wa kumwezesha kufurahia haki hiyo.

14.4. Ibaraya 6:inayoitaka Tanzania kuwajibika kuipatia DP World vibali na vivutio vya kutekeleza miradi yake kama Serikali. Hii inapingana na baadhi ya sheria za kiutaratibu.

14.5. Ibaraya 7: inayoitaka Serikali kuwajibika kutoa mamlaka yanayotakiwa na mwekezaji bila ucheleweshaji.

14.6. Ibaraya 8: Haki ya kutumia ardhi ambapo Mkataba unasababisha uvunjifu wa sheria za ardhi na sheria zinazohusu masuala ya ardhi.

14.7. Ibaraya 10: Usiri wa Mkataba ambapo Mkataba unazuia mamlaka nyingine kama TAKUKURU /BUNGE kufuatilia mikataba.

14.8. Ibara za 23 na 24: zenye ugumu wa kujitoa kwenye Mkataba
 
Roma Locuta, Causa Finita Est.
 
Santeee (in Anna Makinda voice)
 
Ni nchi ya kuchekeana tu, watu hawana utaalamu wowote wa sheria halafu wanatishia nyau serikali.

Pili lipo wazi Dr.Slaa hawezi siasa wala hana huo ushawishi, kitu pekee anachoweza ni kukimbilia kanisani na kutafuta mmoja wa kushawishi wengine kuja na matamko ya kipuuzi kama hayo.

Tatu watu wa mungu Tanzania huwa wanakaa chonjo ni waoga, ila wanapoona kiongozi wa nchi ni dhaifu ndio wanaleta fujo.

Nne hapo hakuna good intentions ni raisi wa nchi katishiwa hadharani; na asipo jibu mapigo mbele giza.

Siasa za Tanzania watu wa mitandaoni wanaweza soma mchezo na ku-analyse future trends kuliko huko serikalini. Labda wale wanaosema werevu wa Tanzania wapo nje ya ulingo wa siasa wana hoja.
 
Wakatoliki ndo hawataki mkataba na Dpworld kisa ni waarabu waislam...
Hakuna cha kasoro za mkataba zirekebishwe wala Mahakama imesema mkataba hauna shida...

Wako very very clear....
Only watu wajinga ndo watajifanya hawajaelewa
 
Muulize Kabila kitu Maaskofu wa Katolik walinfanyia kule Congo, au Muulize Mugabe alivyo kuwa anapelekwa mputa na hao katolik, usiche na hao watu
Hata kwny Mauaji ya Kimbari walishiriki mstari wa mbele kukusanya watutsi kwny Makanisa kama vile wanawaokoa lakini wakishajaa wanawaita Wahutu waje wawanalize, halafu cha kushangaza hao Watutsi waliowakusanya na kuwateketeza makanisani walikuwa Wakristo wenzao
 
expand...
Hakuna hoja hapa.

Sasa mimi kukujulisha wewe fursa zilizopo kuna shida gani? Kama kipengele kingeandikwa nitawajibika kukupq fursa hapo ndo kuna shida. Kumjulisha mtu fursa zilizopo shida iko wapi? Na sheria ipi imevunjwa hapo? Sheria ya manunuzi haiongelei kama mtu akijulishwa fursa zilizopo basi taratibu za manunuzi zimevunjwa!

Hiyo 2(1) inaweka utaratibu unaoibana vipi serikali? Maana hakuna kitu kinachoibana Serikali kwenye icho kipengele

Ibara ya 6 haipingani na Sheria yeyote! Wangeitaja iyo sheria wangekuwa na hoja


Ibara ya 7 ina shida gani? Maana hivyo ndo dunia inavyoenda. Wanataka wawekezaji wacheleweshewe vibali? Hawa jamaa hamnazo kabisaaa!! Na nahisi pia wanachangia sana kuhamasisha ukiritimba kwenye serikali yetu.


Haki ya Kutumia ardhi ina shida gani?? Kama wangepewa exclusive right of ownership( haki ya umiliki) hapo at least wangekuwa na hoja! Sasa haki ya kutumia inashida gani? Hawa jamaa sio wazima kwa kweli
 
Na huyo Kitima si wa huko huko Ngara.
 
Tatizo mnajibu hoja bila hata ya kusoma na kuelewa kilichoandikwa.

Kwanza ufute maneno yako kuwa eti wananchi wote wanawakilishwa na wabunge. Hoja yako ingekuwa sahihi kama hao wanaoitwa wabunge kama kweli wangekuwa walichaguliwa na wananchi. Hawa wanaoitwa wabunge, ni majizi ya kura, na wengine hawakuchaguliwa wala hata kuwa na kura hata moja ya mtu yeyote, tena miongoni mwao akiwemo Waziri Mkuu. Kiuhalisia wananchi hawana mwakilishi yeyote.

Jambo la pili unatakiwa kufahamu kuwa, hata kama tungekuwa na bunge, bado kuna taasisi mbalimbali ambazo kupitia kwazo, watu wa makundi mbalimbali wanawakilishwa. Taasisi hizo ni pamoja na taasisi za kidini, taasisi za kiweledi (kama vile vyama vya madaktari, wahasibu, wanasheria, wahandisi, wakulima), vyama vya makundi maalum, vyama vya wafanyakazi, n.k. Hizi taasisi zote ni taasisi ambazo zipo karibu zaidi na wanachama wao kuliko hata mbunge. Ndiyo maana taasisi hizi, zina uwezo wa kushauri, kutetea, kuonya, kukosoa na hata kupinga, japo hawana mamlaka ya kufanya maamuzi ambayo serikali inalazimika kutimiza.

Tumeona, wakati wa utawala wa Mwinyi, kupitia BAKWATA, waislam waliitaka Serikali iwaruhusu wanafunzi wasichana kuvaa mashuleni mavazi yanayoendana na imani yao. Baadaye Serikali ikaridhia. Kama kungekuwa na wajinga, wanaofikiria kwa namna kama yako, wangesema kuwa BAKWATA haina mamlaka ya kufanya maamuzi na kisha kupeleka matakwa ya waislam Serikalini.

TEC wamesema wazi kuwa wana mfumo wao wa kupata maoni ya waumini wao toka ngazi ya kaya mpaka Taifa, na kwa utafiti wao, wananchi walio wengi hawataki huo mkataba wa hovyo uliosainiwa na Serikali na kisha kupitishwa na bunge haramu. Nasema ni bunge haramu kwa sababu ni zao la uovu.

UTAMBUE
Wananchi wote, mmoja mmoja au kwa kupitia taasisi zao wana haki ya kukosoa, kupinga, kukataa, kushauri au hata kulaani au kupongeza maamuzi ya Serikali. Ambaye halijui hili, ni dhahiri itakuwa ni kwa sababu ya ujinga wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…