Nchi yetu inaendeshwa kwa utawala wa sheria na serikali yetu ni ya kidemokrasia inayotokana na watu wenyewe kwa mujibu wa Katiba yetu.
Nchi Ina mihimili 3 ya serikali, bunge (wananchi) na mahakama. Kati ya mihimili hii 3 wananchi bila kujali umri, jinsia na dini zao wanawakilishwa na wabunge wao wa majimbo katika kufanya maamuzi kuhusu wao.
Baraza la Maaskofu limesika likitoa matamko na maazimio kuhusu uwwkezaji kwenye bandari, Huku likisema wananchi wengi hawaupendi mkataba wa ubinafsishaji wa bandari. Hao wananchi ni akina nani, wako wangapi na wamekutana wapi kuwauliza maoni Yao? Nchi Haina dini, tukutane kwenye kampeni za uchaguzi na kisanduku chakula kama Kuna mwenye njia/sera mbala ya namna ya kuindesha nchi badala ya kikundi Cha watu kutaka kuwasemea wananchi wote nchini kitapeli.
Jambo lolote na hoja yoyote haiwi na nia njema kama ikichanga maneno kama Tanganyika, Zanzibar, watanganyika, wazanzibar, waisilamu, wakristo, wazayuni, Wazungu, au Waarabu. Maneno haya ni hatari sana kusikika majumbani, mtaani, kazini na kwenye taasisi mbalimbali. Ukiyasikia yaepuke na yazimwe kwa gharama yoyote ile ili yasiote, kumea na kuzaa mbegu.
Tutailinda Katiba