Hello Wakuu
Nilikuwa na mahusiano na single maza mmoja tangu mwaka jana mwanzoni, huyu mwanamke nilikutana ane fb ye yupo Tabora.
Katika kuwasiliana na kuzoeana sana nikagundua ni single mama na mumewe alishafariki kwa ajali akamwachia mtoto wa kiume yup darasa la nne,
Ni mwanamke mpambanaji,anajielewa ana malengo mazuri tu na Maisha
Niliendelea nae nikawa mfariji wake kipindi cha msiba wa aliekuwa mzazi mwenzie, yeye yupo Tb mi nipo mkoa mwingine ,
Siku zikasogea hatimae tukakutana mkoani kwangu tukafanikiwa kufahamiana zaidi na kila mmoja kuweka hisia zake wazi kwa mwenzie
Kiukweli alikwepa sana kunipa utamu na kweli akafanikiwa,sikuwa na nia ya kumla na kukimbia ila ye ndo alikuwa anawaza ivyo
Nikaona okey sio mbaya akaniomba nimuoe! Sikumkatalia
Ila kadri nikilichakata lile suala naona litakwama tu sehemu, sio kwasababu kaninyima penzi lahasha wanawake ninao wengi tu ninawachakata,
ila yule single maza nilitokea kumwelewa tu na kumpenda kwa hali yake,
nilivyochakata ilo suala nikaona kikwazo kitakuwa kwa ndugu zangu tu, kila nikivuta picha dingi hatonielewa wala Mama acha hao Dada zangu wazaramo wale naona watanichana live
nikampa wazo tuzae then ndo mtoto atupe kiingilio cha kwenda kumtambulisha home, wazo halikumuingia hata,
Nikaona tofauti na hapo nitampoteteza muda,
nilikuwa nawasiliana nae kama dozi tunafurahi na kucheka kila siku, nikakata mawasiliano gafla bila sababu
kwa muda wa wiki tatu mfululizo ni kimya tu akipiga ntamwambia badae na iyo badae ndo kseho kutwa
Ikabidi anitafute analia nimwambie ukweli mi nikamchana live u uhusiano nimefeli mimi,
kama sikumuoa single maza huyu basi sioi tena singo maza
Atalia atakuwa sawa kuliko kumpotezea muda