Ndugai ni Spika asiye na sifa za kuwa spika
Sauti ya MUZIKI au RADIO tunaisikia kupitia SPIKA skuizi kuna zile wanaita Subwoofer afu kuna tule tudogo wanaita tweeter

Kumbuka ADUI mkubwa wa SPIKA ya RADIO ni MAJI na MASIKA ndio hii sijui kama itaisha salama bila SPIKA kulowana na SPIKA ikilowa tu inakufa haisikiki tena
Aisee 🤔🤔
 
kwanini ndugai anampaka mama yetu kipenzi matope ya makusudi?

Hivi ni kweli ndugai hajui katiba yetu inasema nini kwa wabunge wasio na chama?

Lengo la ndugai kwa mama yetu ni nini?

Ndugai haoni ni muda wa mama kuzungumza mambo makubwa ya kujenga nchi kuliko kupoteza muda kwa vitu vidogovidogo kama hivi vya kushindania katiba inasema nini kwa wabunge wasio na chama?

Kwanini kama taifa tunalotaka maendeleo

Tunashindana vitu viko wazi namna hii?

Hivi hatuoni kama tunalichafua taifa bila sababu yoyote ya msingi?

Mama ongea neno moja kuhusu hili kwenye vikao vya sirini
 
Kutokana na Mgogoro ambao umemhusu Mbunge wa kibamba Mhe John Mnyika nimebaini Pasipo na shaka kuwa Job Ndugai ambae ni Spika, hana uwezo kabisa wa kuongoza chambo kikuu cha maamuzi kama Bunge.

Japo kuwa ni Spika Tayari lakini tunatakiwa kujua kuna watu ni Marais lakini hawana sifa za kuvaa uhusika hivyo hivyo Ndugai hafai kuwa Spika na Wala tusitegemee jipya lolote kutoka kwenye Bunge analoliongoza yeye na msaidizi wake Tulia Ackison.

Nimesema hivyo hana sifa yoyote ambayo imetokana na Nadhalia za uongozi ususani skill model of Leadership.

Na hizi ndio sifa za Job Ndugai ambazo zinamfanya kukosa sifa za kuwa Spika japo ni Spika na kwa maana hiyo Bunge la sasa ni Dhaifu sana.

1)-Anajaziba, kutokana na hii sifa siku zote hawezi kutoka maamuzi sahihi sifa hii inaonekana pale alipompiga Mgombea mwezake wa ndani ya chama chake.

2)-Ni Mtu wa kujipendeza, na hii inafanyika ili atete kiti chake cha uspika ndio maana anatumia nguvu nyingi kuwaonea wapinzani ili amfurahishe Rais ambae ndio Mwenyekiti wa chama.

3)-Nimkurupukaji, kutokana na sifa hii inamfanya afanye maamuzi na atoe kauli za kitoto ambazo zinalifanya Bunge kuwa dhaifu sababu linaogozwa na watu dhaifu.

Mfano aliposema Lusinde wewe ni kiboko yao mpaka wote wameondoka hii nikauli ya kitoto haikupaswa kusemwa na mtu kama Spika.

4)- ni kigeu geu, sio mtu wa kuamini au kupanga nae mambo makubwa na hii inasababishwa na yeye kuwa mtu wa kujipendekeza.

5)-Anaongozwa na Mhemko, Hana Busara wala Hekima kwa Suala la Mnyika hajatumia Busara wala Hekima Mropokaji.

Kutokana na madhaifu yake yote hayo mzee Chenge ameonyesha uwezo mkubwa kuliko yeye pamoja na msaidizi wake Tulia Ackison.

Kutokana na wabunge kuonewa katika kipindi chake na Serikali au na yeye Mwenyewe pamoja na Msaidizi wake wamefanya ubunge kutokueshimaka kabisa na watu.

Nilikuwa sijawahi kusikia Kwamba Mbunge anaweza kuwekwa ndani mwezi 4 na hajaua ni kipindi cha Ndugai kwa maana hiyo pale amekaa kuziba nafasi isiwe wazi na sio kuliongoza Bunge kupitisha maamuzi sahihi kwa maslahi ya nchi yetu kama lilivyokuwa Bunge la 2005- 2010 kila mtu alitamani kuwa Mbunge.

Ni Mhere Mwita.
Mama analijua hilo sakata Ila amechagua kukaa kimya ingali mengine mengi anayakemea waziwazi, hapo ndipo napimuangalia Ndugai kama mtu anayejua kabisa kwamba anatekeleza maelekezo ya boss wake.
 
Kubabaika huku si kwa kawaida na nahisi kuna jambo kubwa ambalo hatulijui.
Kwa mtu anayemwamini Mungu na aliyekuwa na uelewa wa kutosha ni wazi Job Ndugai amepotoka na anaendelea kupotoka katika suala la wabunge 19 wa viti maalum wanaodaiwa kuwa wa Chadema.
Ushahidi wa Chadema umewekwa wazi,maamuzi yaliyofanywa katika matukio kama hayo miaka ya nyuma yamewekwa wazi na kwa ushahidi usio na shaka.
Huku kubabaika kunatokana na nini?
Sasa ni wakati wa kuulizana,kubabaika huku knamnufaisha nani?
Uvurugaji wa uchaguzi 2020 haukufanyika kitaalamu na ulikuwa wa kibabe sasa inakuwa kama hadithi ya mbwa mwitu na mwana kondoo ("mwaka jana ulinichafulia maji ya kunywa na mwana kondoo alipojibu "mbona mwaka jana nilikuwa sijazaliwa"..)
 
Shangazi Fatuma kamjibu vyema

Screenshot_20210507-165151.png
 
HUKO CHADEMA NAKO KUNA SHIDA, AKINA MDEE WALIKATA RUFAA, HADI LEO CHADEMA WAMEKAA KIMYA!
 
Kwa hiyo Spika hana katiba ya CDM? Alikubalije mwakilishi wa CDM kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni na hajui kilichoandikwa kwenye katiba yao?

Kwanini alipopokea barua na akaona vigezo na masharti hayajatimizwa kwa nini hakuirudisha kuomba viambatanisho?
 
Kwa hiyo Spika hana katiba ya CDM? Alikubalije mwakilishi wa CDM kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni na hajui kilichoandikwa kwenye katiba yao?

Kwanini alipopokea barua na akaona vigezo na masharti hayajatimizwa kwa nini hakuirudisha kuomba viambatanisho?
Ndugai anazidi kujianika kuonyesha kuwa Kiti cha Spika siyo size yake. Yaani yeye anavaa kiatu no 6 wakati cha Spika ni no 11. Kutembelea lazima iwe vichekesho kama siyo majanga.
 
Hua ofisi ya Spika haina utaratibu ya kujibu barua anazoletewa? kwanini ofisi yake inashindwa kuwajibu CHADEMA kwa barua kama alivyoandikiwa.
 
Kubabaika huku si kwa kawaida na nahisi kuna jambo kubwa ambalo hatulijui.
Kwa mtu anayemwamini Mungu na aliyekuwa na uelewa wa kutosha ni wazi Job Ndugai amepotoka na anaendelea kupotoka katika suala la wabunge 19 wa viti maalum wanaodaiwa kuwa wa Chadema.
Ushahidi wa Chadema umewekwa wazi,maamuzi yaliyofanywa katika matukio kama hayo miaka ya nyuma yamewekwa wazi na kwa ushahidi usio na shaka.
Huku kubabaika kunatokana na nini?
Sasa ni wakati wa kuulizana,kubabaika huku knamnufaisha nani?
Uvurugaji wa uchaguzi 2020 haukufanyika kitaalamu na ulikuwa wa kibabe sasa inakuwa kama hadithi ya mbwa mwitu na mwana kondoo ("mwaka jana ulinichafulia maji ya kunywa na mwana kondoo alipojibu "mbona mwaka jana nilikuwa sijazaliwa"..)
kunatokana na kuwa covid 19 waliingizwa na marehemu. kama unavyojua waafrika hawavunji maagizo ya marehemu
 
Back
Top Bottom