Juzi nilialikwa nyumba ya jirani katika mazungumzo yanayohusu masuala ya Kishika uchumba na mahari
Hii nyumba ya jirani yetu kuna binti kama wa miaka 22 hivi ,huyu binti aliacha shule akatoroka kwao akaenda mbali huko kakutana na chemba akamtia mimba baada ya muda akamtimua yule binti.
Binti baada ya kuona maisha yamemshinda akarudi kwao akajifungua mtoto wa kike akamlea kwa Msaada wa mamake baada ya mtoto kuacha kunyonya ,binti akatoroka tena kwao akaenda machimboni
Huku akapata msela mwingine ambaye ameoa ,akamtia mimba huyu binti ,baada ya muda akaachana nae ,binti akarudi tena kwao na mimba akazaa ,akatulia baada ya muda akatoroka tena.
Sasa hivi majuzi akarudi ,na kutoa taarifa kwao kwamba anakuja mtu kujitambulisha.
Ebhana wee siku ya tukio nilimwonea Sana huruma yule jamaa jinsi alivyopigwa hela kubwa ya Kishika uchumba,jamaa akaanza kuwaza ila mpambe wake akajifanya Wana hela akatoa kile kiasi,nikamwona jamaa ni fala Sana yani demu keshazalishwa ,hana elimu yoyote,hana shughuli yoyote halafu unakubali kupigwa hela kubwa hivi ya Kishika uchumba tu.
Baada ya kumaliza hilo ukafika muda wa kujadili mahari ,ebhana eeeh jamaa kalazimishwa alipe milioni 2,jamaa kaomba omba Sana mama wa binti kakomaa lazima atoe M 2 ,hivi single mother watoto wawili unaanzaje kimlipia mahari M2?
Ikabidi jamaa akubali kishingo upande na kuahidi atarudi tena.
Sasa kumbe binti alimpanga mamake na kumwambia huyo jamaa akija mpige hela kubwa manake anaonekana ana hela,kwa maana hii huyu binti yupo kimaslahi zaidi,je akiolewa na akaanza kuonesha mapungufu yake akaachwa atalaumu kwamba wanaume wanamuacha?
Ni uboya kutoa mahari kubwa kwa single mother.