Kuoa Single Mama ni sawa na kunywa soda iliyofunguliwa na kuonjwa
Unawasikiliza watu kwenye furaha ya moyo wako?....watu ni kina nani kwako sio kila kitu cha kushaurika oa huyo single mother kama mnapendana ....
 
Mi nasoma maoni ya wadau tuu mana mi pia nna mpango wa kuoa mdada mwenye mtoto lkn yy jamaa ake alishatangulia mbele ya haki
 
Hii ishu imekuwa ikinisumbua sana tangu mwaka jana. Kuna mwanamke mwenye mtoto nataka kumuoa, tangu siku ya kwanza nimwambie mama yangu hizo habari alionesha kwa wazi kabisa kutokukubaliana nami. Ananiambia kama yeye hakuniweka tumboni miezi tisa basi nimuoe huyu single mother. Mashangazi nao na dada zangu nao wananisema chini chini.

Mdogo wangu wa kike ndo huwa ananivujishia hizo habari kuwa shangazi huwa anasema mimi ni mwanaume niliyesoma na kukamilika inakuwaje naoa mwanamke mwenye mtoto? Mama mdogo ndiyo ameniita mimi mpumbavu, hiyo nimeinyaka kwenye group lao la Whatsapp kupitia simu ya mdogo wangu.

Baba yangu kaniambia niwe makini sana kuoa mwanamke mwenye mtoto ila uamuzi nichukue mwenyewe.

Hii inaniweka njia panda sana. Najua humu kuna wamama watu wazima na wazee wenye umri mkubwa na busara, naombeni maoni yenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mshukuru Mungu, yupo mzazi ambaye anakupigania usijeingia huo mkenge wa kuoa single mother, utajuuuta!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi nasoma maoni ya wadau tuu mana mi pia nna mpango wa kuoa mdada mwenye mtoto lkn yy jamaa ake alishatangulia mbele ya haki

Wewe hakuna tatizo oa kabisa...

Mimi nataka kuoa mwenye mtoto ila yupo hai na tatizo lake mchamungu ameshaoa mke mwingine ila sina imani naye
 
Love knows no bounds.

She has a child yes, a little human being and you love her as she is.

Marry her.
Hizi story dada yangu.
Nakupa mfano mmoja.
Williams, baba yao kina Serena.
Alioa akakuta na watoto wa kufikia.
Kawalea wote Kama wake.
Ilipotokea shida tu wote wakamsusa.
Ujinga huu.
Nimetoa mfano huu kwani iko documented.
Huku kwetu ndio kila siku shida.
Kuna watoto wa kambo wamebakwa/kulawitiawa na baba wa kambo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inategemea na huyo mwanamke unayetaka kumuoa, kama hajakuzidi umri basi unaweza kumuoa. Kuwa na mtoto si tatizo, huenda ndio akawa mke bora zaidi kuliko ambaye hajawa na mtoto. Lakini cha muhimu hapa ni kuangalia jinsi maisha yenu yatakavyokuwa. Usingle mother mwingine huja outomatically tuu pasipo mtu kutegemea.
 
wewe jamaa kwa nini unataka kuoa "makombo" ya wenzako?
pili unadai kuwa amekuzidi "umri" unatafuta ni kwa huyo dadako?
tatu jifunze kutoka kwa Irene Uwoya na Dogojanja.
 
Mwanzoni unaweza kuona kama iko poa lakini kadri siku zinavyoenda ndio utaona hasara ya hiyo kitu,wazazi wanajua ndio maana wanakuonya.Unajua shida hapo ni kuwa hao watu wengi wao wanakuwa wana majeraha ya kuachwa na jamaa zao,sasa kinachofuata anajikuta anafanya malipizi bila ya kujua kuwa wewe sio muhusika wa kuachwa kwake,kichwani mwake anakuwa anaona kila mwanaume ni mtu katili,behaviour zake ni tofauti sana na mwanamke ambaye hajakutana na hiyo hali,sisemi wote ila wengi wao ni majanga na hata ukifuatilia thread nyingi hapa JF kuhusu single mothers zinawaponda sana,hawako vyema kisaikolojia..
 
Back
Top Bottom