Kama humsikilzi mama yako wewe ni mpumbavu hakuna mwanamke anayekupenda duniani zaidi yake
Inategemea huyo mtoto ulimpataje.Leo single mum mnatusimanga aiseh utadhani tukibeba mimba peke yetu, ukiona tupo peke eti msidhani sisi wakorofi ila wanaume mnakataa ukisikia tu nina mimba, sasa hata kama mkimsihi huyu mleta Uzi kama chance ya kuolewa ipo ni ipo tu.Usipooa wewe wengine wataoa
Sent using Jamii Forums mobile app
Single mums wengi tunawaona wakiolewa.Mkuu umenena vyema sana ni ukweli usiopingika uyo ni mke wa mtu na ushaidi uyo mtoto aliyenae sasa kijana mwenzangu bado hata mishindo ya ndoa bado hujaijua vzur embu fikiria vzur ufanye maamuzi sahihi juu ya future yako
Sent using Jamii Forums mobile app
Inategemea huyo mtoto ulimpataje.
Wengi wa Hawa wanabeba mimba bila mpango wowote.
In return wanaanza kulazimisha wanaume wawaoe wao na watoto wao.
Bado haitoshi wanarudiana na waliowazalisha huku wakiwa na ndoa nyingine.
Mwanamke pekee ambaye utakuwa na uhakika naye Kama ana mtoto Ni yule aliyefiwa na mumewe.
Huyo Ni mjane. Hawa wengine Ni wake za watu.
Acheni kuzaa bila mpango wakati mna ndoto za kuja kuolewa na kuwa na waume zenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama humsikilzi mama yako wewe ni mpumbavu hakuna mwanamke anayekupenda duniani zaidi yake
UTAPATA LAANA
Hiyo michezo ya kitandani si lolote mbele ya radhi za mama yako na namna anavyokuonea uchungu mwanae
HAKUNA KAMA MAMA
Umri Ni no tu
Sasa kwanini aowe mke wa mwenzie?Huu ni upuuuzi first class.
Mtu kuwa mama yako haina maana anakumiliki, na wewe kuzaa mtoto haina maana unammiliki.
Huu uzwazwa wa watanganyika kudhani wanawamiliki watoto wao ndo unaokwambisha maisha ya wengine, kila mtu ana utashi na chaguzi zake.
Kwahiyo Mama yako akisema kuwa shoga unakua sababu tu kasema? Akisema usioe maisha yako yote huoi sabbau Mama kasema? Ukomo wa kukuamulia mambo yako ni upi? Ndo nyie ambao mnaoa ila kila kitu ni Hadi Mama aseme.
Hakuna cha laana wala nini kama mama sio muelewa. Hilo ni tatizo lake. Na ndoa ni zaidi ya kulalana
Wameona mbali ila fanya maamuzi kwa busaraHii ishu imekuwa ikinisumbua sana tangu mwaka jana. Kuna mwanamke mwenye mtoto nataka kumuoa, tangu siku ya kwanza nimwambie mama yangu hizo habari alionesha kwa wazi kabisa kutokukubaliana nami. Ananiambia kama yeye hakuniweka tumboni miezi tisa basi nimuoe huyu single mother. Mashangazi nao na dada zangu nao wananisema chini chini.
Mdogo wangu wa kike ndo huwa ananivujishia hizo habari kuwa shangazi huwa anasema mimi ni mwanaume niliyesoma na kukamilika inakuwaje naoa mwanamke mwenye mtoto? Mama mdogo ndiyo ameniita mimi mpumbavu, hiyo nimeinyaka kwenye group lao la Whatsapp kupitia simu ya mdogo wangu.
Baba yangu kaniambia niwe makini sana kuoa mwanamke mwenye mtoto ila uamuzi nichukue mwenyewe.
Hii inaniweka njia panda sana. Najua humu kuna wamama watu wazima na wazee wenye umri mkubwa na busara, naombeni maoni yenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna dogo kitaa alimpata mdada mwenye life yake. Yule dada alikuwa na ajira ya kueleweka na alikuwa anaendesha maisha yake vizuri tu. Watoto wake wawili wako boarding school na ada anawalipia mwenyewe.
Mama yake dogo kusikia uchumba alisema big NO. Waliamua kuzaa, siku mama anakuja kumuona mjukuu makusudi alimsalimia mzazi “shikamoo”.
Kufika hapo dogo alimwaga manyanga chini. Analea mtoto wake na likizo anakwenda kwa bibi.
Shida ni mtoto wake? kabla hamjakutana huyo mtoto alikua analelewa vipi? na je mtoto wake ataathiri vipi mahusiano yako na yake au yake na familia yako??
Shida ni umri wake? je anakua anakubeba mgongoni na kutangazia uma kua amekuzidi umri au umri wake unaathiri nini mahusiano yako na yake au yako na familia yako?
Kuna anko wangu alipingwa vikali kuoa single mom, anko akaziba masikio kaweka kitu ndani, huu ni mwaka wa 9 wapo wote, na watoto wao.
Be crazy, Be Weird, Be whatever coz life is too short to be anything but HAPPY.
Kuvaa suruali na enyewe ni kigezo eti cha kutokumuoa mtu? Labda ungesemea mengine hayo mkuu watu tumevaa suruali toka utotoni mpaka tunaolewa tuna watoto suruali tunavaa haijawai husiana na tabia ya mtu iyo
Labda nikushauri kitu embu kuwa naye kwanza usikimbilie kuoana naye kama kwenye mapenzi yenu hamjafikisha miaka mi2 jaribu kukaa mapenzi naye ata miaka4 umsome zaidi usije ingia chakike mda uwo naisi utakuwa umejua yuko vp na mahusiano na mzazi mwezie yakoje na wanawasiliana vp na kipi kilifanya watengane na familia yake ni ya watu gani maana kuna vitu ni vyakijinga sana kufatilia ila vinaumuimu sana kama mama yake kaolewa yani anaishi na baba yake kama haishi naye na hajafariki weka kiulizo? Kingine mtindo wa maisha yake akikasirika anakuaje.
Kumbuka kakupita umri usiangalie pesa na Mali alizonazo kama anazo ila upendo heshima aliyonayo kwako ila kumbuka pia wanawake ni mabingwa wa kuigiza wakiwa wanakitaka kitu
Sent using Jamii Forums mobile app
Wazazi wako Wana akili Sana. Wapo sahihi kabisa pamoja na ndugu zako. Wote hao wamakutakie mema . Ingekuwa mmoja tungeqestion . Ndugu wote wasikilize. Single mother ni wasumbufu Sana. Huyo ni mke wa mtu yaani mwenye huyo mtoto bado ana access kubwa ya kuwasiliana na single mother. Ni rahisi kupewa mzigo akihitaji . Mtoto ni connection kubwa kati ya mama na Baba. Kwani unapenda kuitwa Baba wa kambo . Mtoto hawezi kukupa full respect kwasababu anajua wewe sio Baba yake. Jinsi ya kumlea ni ngumu mno. Inajibidi kujifunga mkanda unapojitolea kumlea mtoto huyo. Mtoto akililia wembe mpe akijikata ni shauri yake
Sent using Jamii Forums mobile app