Ndugai ni Spika asiye na sifa za kuwa spika
Kwenye nyumba za ibada hakuna kuulizana maswali na huku kanisani ukiwa ni mtu wa kuhojihoji unaweza kutengwa. Kwenye mambo ya kiimani ni utaratibu mzuri na tunaukubali kwani nyumba za ibada ziko nyingi ukishindwa kwa Kakobe utaenda kwa mzee wa upako. Sasa ni kama vile bunge ambalo ni la kimwili zaidi linatamani kuiga utaratibu huu wa ' mchungaji kutohojiwa' na kwamba wale wenye kiherehere watatengwa hadi mwisho wa uhai wa bunge. Sidhani kama ni jambo jema sana kwani kazi ya mbunge ni kusema sasa kwanini asiseme?!!! Na kama ni kumtenga kwani mbunge anachaguliwa na bunge au ' ANAPELEKWA' bungeni na kura za wananchi. Nyumba za ibada zina wenyewe anaweza kuwa Yesu, Mtume nk lakini bunge ni la wananchi. Unapomtenga mbunge X humuathiri yeye bali wananchi waliomtuma bungeni, ahsante!!
 
Mpaka sasa ni dhahiri kuwa spika kazi imemshinda. Spika amekuwa ni mtu wa tambo, majivuno na kutoa kauli ambazo hazieleweki. Ametumia cheo chake kuwapa wabunge wengine adhabu zisizo na kichwa wala miguu, na wengine kuwatishia kuwapa adhabu zisizoeleweka, kwa definition rahisi hiyo ni abuse of power tayari.

Pia tumeona jinsi ambavyo bunge hili la awamu ya tano limekuwa haliisimamii serikali ipasavyo, limekuwa kama rubber stamp tu, further cementing jinsi spika alivyo weak. Mwishowe bunge liko kwenye makaratasi tu, lakini in practise ni zero, pia spika amekuwa kama kikaragosi wa serikali.

Kwahiyo ni muda muafaka huyu spika apumzishwe aende kufanya kazi zingine.

So wabunge fanyeni juu chini mum-impeach spika, lasivyo kadri siku zinavyoenda ndo hali itazidi kuwa mbaya kabisa kwa bunge letu hili.
 
Mbunge Wa Kongwa ambaye kwa bahati (mbaya au nzuri) ndiye Spika Wa Bunge mwaka Jana aliandaa futari wakati Wa mfungo Wa Ramadhani. Lakini katika hali isiyotegemewa, wabunge wa upinzani walimsusia kwa dhana kuwa mwaliko huo hauna maana kiimani kama uliowaalika unatabia ya kuwabagua, kuwatenga na unawachukia.
Tulidhani kwa kitendo kile angekuwa kajifunza na kujirudi kwa kuwa MTU mwenye tabia njema, lakini kwa matukio ya Sikh mbili hizi ni wazi kuwa ni mtu mchafu sana katika imani na utu hasa katika jambo lililo mtokea mbunge na kiongozi mwenzake Bungeni mhe Lissu.
Hata hizi hasira za kina Lema na Msingwa ni wazi ni kwa vile wanashangaa jinsi wanavyo yaona mateso ya Lissu kisha ubwabwajaji wa Ndugai.
Alisusiwa Futari anadhani nini kitafuata kwake kwa jambo jingine? Maumivu ya kususiwa jambo lako binafsi kwa tabia zako ni fundisho kama MTU kajirekebisha.
 
Unadhani kwa nini Ndugai alililalamikia jambo hilo ndani ya Bunge? Lina maumivu ambayo mtu kama wewe unayeishi kwa fadhila huwezi kuelewa.
Mwanaume uliyekamilika unakuja na mada ya "kususia" na unajiona jasiri!? Ama kweli mmeishiwa hoja mnabakia kumwaga viroja.
 
Mbunge Wa Kongwa ambaye kwa bahati (mbaya au nzuri) ndiye Spika Wa Bunge mwaka Jana aliandaa futari wakati Wa mfungo Wa Ramadhani. Lakini katika hali isiyotegemewa, wabunge wa upinzani walimsusia kwa dhana kuwa mwaliko huo hauna maana kiimani kama uliowaalika unatabia ya kuwabagua, kuwatenga na unawachukia.
Tulidhani kwa kitendo kile angekuwa kajifunza na kujirudi kwa kuwa MTU mwenye tabia njema, lakini kwa matukio ya Sikh mbili hizi ni wazi kuwa ni mtu mchafu sana katika imani na utu hasa katika jambo lililo mtokea mbunge na kiongozi mwenzake Bungeni mhe Lissu.
Hata hizi hasira za kina Lema na Msingwa ni wazi ni kwa vile wanashangaa jinsi wanavyo yaona mateso ya Lissu kisha ubwabwajaji wa Ndugai.
Alisusiwa Futari anadhani nini kitafuata kwake kwa jambo jingine? Maumivu ya kususiwa jambo lako binafsi kwa tabia zako ni fundisho kama MTU kajirekebisha.
Mwite mchapabakora, kiboko ya wanaccm wenzake
 
Wanabodi,
Salaam;

Nimesikitishwa sana na kitendo kilichofanywa na ofisi ya spika juu ya kujiuzulu mh. Nyalandu.
Ni wazi ofisi ya Bunge imejidhalilisha mno!

Baada ya taarifa ya Nyalandu kuenea ktk mitandao ya kijamii na ktk vyombo vya habari, alijitokeza msemaji wa CCM asiye na uwezo wa nafasi yake, akimshangaa Nyalandu kukihama chama cha mapinduzi chenye itikadi ya ujamaa na kuhamia ktk chama kisichokuwa na Sera. Huyo aliyeyasema hayo ni kiongozi wa ngazi ya juu kabisa ya CCM.

Kwa taarifa tu na kwa faida ya wengine wasiofahamu, katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi, anaingia katika vikao vyote vikuu vya kikatiba kuliko hata mwenyekiti wa CCM taifa. Mwenyekiti siyo mjumbe wa sekretarieti ya chama ambayo inaundwa na watendaji tu. Yaani katibu mkuu(ambae ni mwenyekiti wa kikao), manaibu katibu wakuu, katibu wa itikadi na uenezi, katibu wa uchumi na fedha, makatibu wa jumuiya za chama yaani UWT, vijana na wazazi.

Hicho kikao ndo kinaandaa ajenda za kikao cha kamati kuu na huyo Polepole ni mjumbe pia wa kamati kuu. Kama Nyalandu alifukuzwa, ina maana Polepole angekuwa anajua na kwa sababu ni mropokaji, lazima angekuwa ameropoka tu!

Kwa hiki kilichofanywa na ofisi ya spika ni kitendo cha aibu mno na kama kitavumiliwa na wabunge, tutaonana 2020 msitufanye watanzania wote majuha..!
 
ndio maana wenye upeo wa siasa wanasema mataizo makubwa ya Tanzania ni ccm maana ukiw huko lazima ujite fahamu
 
Hovyo kuwahi kutokea.
Et alipewa cheti na Myweather na yeye kwaajili ya makinikia walopewa kanjiwa badala ya tembo.


Watanzania daini katiba mpya ccm itoke vinginevyo mtapata tabu sana
 
Kwani hamjajua kwa nini ilionekana ni jambo murua kumpa yule faru mwenye fujo nyingi jina lake?
 
Back
Top Bottom