Ndugai ni Spika asiye na sifa za kuwa spika
Kunawatu Ni ma Idd Amin dada sema tuu hawajapata nafasi!! Roho nyeusiiiiiii....
 
Ametawaliwa na jazba hafai kuongoza muhimli kubwa kama bunge na alipoteza sifa zaidi alipo mpiga mgombea mwenzake fimbo ya kichwani hadi akazimia.
 
Mlimshangilia sana kawageuka mmeanza kumtukana mtamsifia tena Tulia. Wabunge wakijiheshimu hayawezi kutokea haya
 
Kutokana na Mgogoro ambao umemhusu Mbunge wa kibamba Mhe John Mnyika nimebaini Pasipo na shaka kuwa Job Ndugai ambae ni Spika, hana uwezo kabisa wa kuongoza chambo kikuu cha maamuzi kama Bunge,

Japo kuwa ni Spika Tayari lakini tunatakiwa kujua kuna watu ni Marais lakini hawana sifa za kuvaa uhusika hivyo hivyo Ndugai hafai kuwa Spika na Wala tusitegemee jipya lolote kutoka kwenye Bunge analoliongoza yeye na msaidizi wake Tulia Ackison.

Nimesema hivyo hana sifa yoyote ambayo imetokana na Nadhalia za uongozi ususani skill model of Leadership.

Na hizi ndio sifa za Job Ndugai ambazo zinamfanya kukosa sifa za kuwa Spika japo ni Spika na kwa maana hiyo Bunge la sasa ni Dhaifu sana.

1)-Anajaziba, kutokana na hii sifa siku zote hawezi kutoka maamuzi sahihi sifa hii inaonekana pale alipompiga Mgombea mwezake wa ndani ya chama chake.

2)-Ni Mtu wa kujipendeza, na hii inafanyika ili atete kiti chake cha uspika ndio maana anatumia nguvu nyingi kuwaonea wapinzani ili amfurahishe Rais ambae ndio Mwenyekiti wa chama.

3)-Nimkurupukaji, kutokana na sifa hii inamfanya afanye maamuzi na atoe kauli za kitoto ambazo zinalifanya Bunge kuwa dhaifu sababu linaogozwa na watu dhaifu.

Mfano aliposema Lusinde wewe ni kiboko yao mpaka wote wameondoka hii nikauli ya kitoto haikupaswa kusemwa na mtu kama Spika.

4)- ni kigeu geu, sio mtu wa kuamini au kupanga nae mambo makubwa na hii inasababishwa na yeye kuwa mtu wa kujipendekeza.

5)-Anaongozwa na Mhemko, Hana Busara wala Hekima kwa Suala la Mnyika hajatumia Busara wala Hekima Mropokaji.

Kutokana na madhaifu yake yote hayo mzee Chenge ameonyesha uwezo mkubwa kuliko yeye pamoja na msaidizi wake Tulia Ackison.

Kutokana na wabunge kuonewa katika kipindi chake na Serikali au na yeye Mwenyewe pamoja na Msaidizi wake wamefanya ubunge kutokueshimaka kabisa na watu.

Nilikuwa sijawahi kusikia Kwamba Mbunge anaweza kuwekwa ndani mwezi 4 na hajaua ni kipindi cha Ndugai kwa maana hiyo pale amekaa kuziba nafasi isiwe wazi na sio kuliongoza Bunge kupitisha maamuzi sahihi kwa maslahi ya nchi yetu kama lilivyokuwa Bunge la 2005- 2010 kila mtu alitamani kuwa Mbunge.

Ni Mhere Mwita.

Ndio hata mwislamu safi atakuambia bora mbuzi kuliko nguruwe.

well said bro! Mwita
Yaani ni ngumu sana kwa wananchi kuwaelewa na kuwaamini hawa jamaa. Ni vigeugeu wa hatari..
Hata katika kesi, washinde wao tu utasikia mahakama imetenda haki, tunaimani na mahakama.
Ila wakishindwa kesi...matusi yake kwa mahakama hayasemeki.
 
Nyie jamaa huwa hamna akili!! Au kama mnazo basi mnawendawazimu... Kila siku mlikuwa mnamsifia hapa Na kumtukana hadi matusi ya nguoni naibu spika Tulia. Leo mnamgeuka Ndugai wakati mlimchagua kwa wingi wa Kura! Mkapimwe akili
 
SPIKA WA BUNGE HATOSHI; ANAWASALITI WANANCHI. HADHI NA UKUBWA WA BUNGE KUDHOOFIKA.

Kwa mujibu wa Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai, askari hawa kama waonekanavyo katika picha, walikuwa wanambembeleza MHE John Mnyika (Mb) aende nje ya ukumbi wa Bunge.

Kwa utashi wa kawaida (common sense), yawezekana askari hawa walitakiwa kutoa bastola kumnyooshea mhe. Mnyika, au kupiga risasi juu, ndiyo wangemridhisha Spika Ndugai kuwa wametekeleza amri aliyowapa, na kwa kosa la kutokufanya hivyo ameamua kuwahamisha kabisa na kuleta askari wengine.

Bunge ni chombo pekee cha kuwatetea wananchi dhidi ya serikali, lakini hivi sasa Bunge limekuwa kama wizara ya serikali au idara mojawapo ya serikali, uongozi wa Bunge hauna tofauti na uongozi wa serikali, ukubwa wa Bunge (supremacy of the parliament) haupo tena, na badala yake Kuna umoja wa Bunge na serikali, hii ni hatari kubwa kwa nchi na wananchi.

Tanzania hi inaelekea wapi? Utumwani tena?

Sasa watanzania mtakubaliana nami kwamba, tunahitaji uongozi wa Bunge usitokane na chama Cha siasa, kuanzia Spika, Naibu Spika na wenyeviti wa Bunge. Pia, tunahitaji mawaziri wasitokane na wabunge, na Mwanasheria Mkuu wa serikali asiwe sehemu ya wabunge. Bunge lifanye majukumu yake ya kibunge, na serikali iwajibike kwa upande wake. Ndipo tutakapoweza kuuondosha Ubatili huu.

tmp_8776-FB_IMG_14967235271991238003012.jpg
 
Nyie jamaa huwa hamna akili!! Au kama mnazo basi mnawendawazimu... Kila siku mlikuwa mnamsifia hapa Na kumtukana hadi matusi ya nguoni naibu spika Tulia. Leo mnamgeuka Ndugai wakati mlimchagua kwa wingi wa Kura! Mkapimwe akili
Mnachoshangaa ni nini, hata kama walimkubali mwanzo ni wao na leo wamegundua wamebugi master ni wao pia and they are right, acheni kukariri majibu.
 
Keshasahau alimtandika mwenzake bakora na akasamehewa!
 
Nyie mna matatizo kweli si mlisema bora ndugai kuliko huyo tulia ackson
Kuwa bora sio bora zaidi kuliko bora.....hata bora huweza kupoteza ubora.....co kuwa bora ukipoteza ubora ubaki kuwa bora.

Tulisema bora kulko yule mama ....lkn hatuulnganisha ubora huo ns vchwa bora vya upinzani.

Hv umeewahi kujiuliza bila upinzani maisha yako yangekuaje mtaaani!!?
 
Mfyuuuh yaani kuna comments mbili humu nimeziona zahovyo haijawahi kutokea. Sjui walikula nini Jana hao.
 
Ndugai nimemshangaa Sana, Kamati ya maadili ya bunge Nimeishangaa sana! wabunge wa CCM wanatumia Lugha chafu sana, Isiyo ya Kibunge na Isiyo faa! Hata tukio lililosababishwa Mnyika Kutupwa nje ya Bunge Kama Mbwa! Lilitokana Na Kejeli na Matusi ya Wabunge wa CCM, Kuwaita Chadema ni Wezi na Wamehogwa, Na Mnyika aliepopotaka Kuhusu utaratibu Ndugai akampa nafasi lakini Kwa Kejeli. Yeye Ndugai ailiona ni sawa Lusinde anamwambia Mnyika atamfanya ajiharibie nguo kwa maana ya kujinyea! Na kisha kuwaita Wabunge wa Upinzani wamehongwa, Wezi etc. Muda wote huo huyu Ma..ya Ndugai anatabasamu na Kufurahia.

Na wakati Mnyika anaongea Mbunge Mmoja akawasha Mic na kwa sauti ya !usikika na Kila Mtu akasema, "Mnyika ni Mwizi" Ndugai akasema hajali akina Ester. Na Halima wamtetea mbunge mwenzao aliyekuwa akidhalilkshwa kwa Double standards n Ohovyo wa Speaker!
At wanafungiwa Mwaka Mzima, Double standards nje ya Bunge Double Standards ndani ya Bunge!. Enough is Enough! My prayer is when this fellow fell sick again, that God should bring him to conclusions! His Life is suffering to others and a danger to Justice and Democracy!


Huyu jamaa hana spear kibogo ya Machadema ... wewe mtumwa wa wazungu utaendelea hivyo hivyo kuosha vitaulo mambo ya bongo tuachie wabongo. Ukoloni mambo leo peleka kwa wakimbizi wenzako.
 
Nikweli kabisa hauwezi kuongoza bunge kishabiki naupendeleo wabunge wa upinzani wanapotoa hoja za msingi wanapingwa sijapenda hakuna usawa
 
Bunge hili la sasa limejaa vituko, chuki na kufitiniana kwa kiwango ambacho hakijapata kutokea huko nyuma. Sasa imefikia wabunge wanaombeana mabaya na kufikia kutaka kuzichapa kavukavu.

Hii ni dalili mbaya kuwa uongozi umeshindwa kuliweka pamoja Bunge kwa manufaa ya wananchi. Na kitendo cha wabunge kumsusia futari spika ni salamu kuwa amekuwa adui yao.
Ndugai, toka urudi kwenye matibabu umekuwa na mambo ya ajabu ajabu jee kuna shida?

Kama hali sio nzuri sii ujipumzishe ili kulinda heshima maana haya ufanyayo hayajawahi kutokea kwa watangulizi wako.
 
Back
Top Bottom