Ndugai ni Spika asiye na sifa za kuwa spika
Kubabaika huku si kwa kawaida na nahisi kuna jambo kubwa ambalo hatulijui.
Kwa mtu anayemwamini Mungu na aliyekuwa na uelewa wa kutosha ni wazi Job Ndugai amepotoka na anaendelea kupotoka katika suala la wabunge 19 wa viti maalum wanaodaiwa kuwa wa Chadema.
Ushahidi wa Chadema umewekwa wazi,maamuzi yaliyofanywa katika matukio kama hayo miaka ya nyuma yamewekwa wazi na kwa ushahidi usio na shaka.
Huku kubabaika kunatokana na nini?
Sasa ni wakati wa kuulizana,kubabaika huku knamnufaisha nani?
Uvurugaji wa uchaguzi 2020 haukufanyika kitaalamu na ulikuwa wa kibabe sasa inakuwa kama hadithi ya mbwa mwitu na mwana kondoo ("mwaka jana ulinichafulia maji ya kunywa na mwana kondoo alipojibu "mbona mwaka jana nilikuwa sijazaliwa"..)
Ndugai
1. Mirembe member full filed
2. The most expensive patient in the world that has not been totally recovered....;;;
3. Sufferer of drugs side effects due to enormous medicine taken for years
 
Kwa hiyo Spika hana katiba ya CDM? Alikubalije mwakilishi wa CDM kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni na hajui kilichoandikwa kwenye katiba yao?

Kwanini alipopokea barua na akaona vigezo na masharti hayajatimizwa kwa nini hakuirudisha kuomba viambatanisho?
Halafu, Ndugai hatakiwi kusimama bungeni na kujiaibisha kwa kujibia barua bungeni.
Anatakiwa akiri kupokea kipeperushi kama alivyo kiita na kujibu kwa maandishi.
Chadema hawawezi kujibu kwa maneno ya kwenye bunge.
Huyu spika huyuuu... Lazima kuna shida kubwa sana.
Nasikia baadhi ya covid 19 ni vyakula vya wakubwa. Mambo ya aibu kabisa haya.
Yaani mna pindisha sheria kisa starehe zenu?? Kweli???
Halafu mnasema mna linda wanawake wasi nyanyaswe. Wakati nyie mna wanyanyasa kingono??
 
HUKO CHADEMA NAKO KUNA SHIDA, AKINA MDEE WALIKATA RUFAA, HADI LEO CHADEMA WAMEKAA KIMYA!
Na sio lazima wasikilize, na Ndugai rufaa haimhusu na kwa wakati huu hao si wanachama, hivyo ni lazima afanyie kazi hicho kipeperushi kama alivyofanyia kazi viperushi toka vyama vingine, huyu anazoea kuvunja katiba, alifanya kwa Mwambe wa ndanda baada ya kutangaza mwenyewe kujitoa kwenye chama aliendelea kumtambua bungeni!
 
Umeingia mwenye Rekodi ya kuwa Spika wa hovyo kabisa kuwahi kutokea ktk Historia ya Tanzania tangu tupate Uhuru.

Mungu ainusuru Tanzania isije kupata Spika mwingine wa hovyo Kama wewe.

Ulitoa wapi ujasiri wa kumfanyia unafiki mama yetu Suluhu asiapishwe wakati ulijua fika Katiba ilimtaka awe Rais?

Yaani wewe Mh Ndugai, ulikuwa kwenye kikosi cha kamati ya Roho mbaya iliyokuwa ikipika majungu eti Mama asiwe Rais.

Yaani hili la wabunge wasio na Chama,uliowakumbatia ni dogo sana kulinganisha na tukio ulilokuwa ukifanya na wenzako.

Yaani huoni hata aibu,hao wabunge wana faida gani na wewe au na CCM?

Yaani umeifanya Tanzania idharaulike sana kimataifa kwa Tabia zako.

Mungu huwa mkubwa mno,wewe na wenzako kina kesi eti mlitaka kubadili katiba ili mwendazake atawale milele, halafu mnajifanya mna hofu ya Mungu, Aisee,Mungu hadhihakiwi, pamoja na yote hakuna ulilojifunza,bado umeshupaza shingo.

Tanzania ilikuwa inaheshimika sana kimataifa,wewe ni mmoja wa walioharibu sifa ya Tanzania.

Yaani unapindisha sheria makusudi kabisa bila woga wala hofu,halafu eti Ulisomea sheria.

I had a dream for you,if you won't repent,bad days are coming whereas teeth will be gnashed.
 
Umeingia mwenye Rekodi ya kuwa Spika wa hovyo kabisa kuwahi kutokea ktk Historia ya Tanzania tangu tupate Uhuru.
Mungu ainusuru Tanzania isije kupata Spika mwingine wa hovyo Kama wewe.
Ulitoa wapi ujasiri wa kumfanyia unafiki mama yetu Suluhu asiapishwe wakati ulijua fika Katiba ilimtaka awe Rais?
Yaani wewe Mh Ndugai, ulikuwa kwenye kikosi cha kamati ya Roho mbaya iliyokuwa ikipika majungu eti Mama asiwe Rais.
Yaani hili la wabunge wasio na Chama,uliowakumbatia ni dogo sana kulinganisha na tukio ulilokuwa ukifanya na wenzako.
Yaani huoni hata aibu,hao wabunge wana faida gani na wewe au na CCM?
Yaani umeifanya Tanzania idharaulike sana kimataifa kwa Tabia zako.
Mungu huwa mkubwa mno,wewe na wenzako kina kesi eti mlitaka kubadili katiba ili mwendazake atawale milele, halafu mnajifanya mna hofu ya Mungu, Aisee,Mungu hadhihakiwi, pamoja na yote hakuna ulilojifunza,bado umeshupaza shingo.
Tanzania ilikuwa inaheshimika sana kimataifa,wewe ni mmoja wa walioharibu sifa ya Tanzania.
Yaani unapindisha sheria makusudi kabisa bila woga wala hofu,halafu eti Ulisomea sheria.
I had a dream for you,if you won't repent,bad days are coming whereas teeth will be gnashed.
Huyo alisomea sheria wapi wakati kasomea choo cha nyumbu Mweka
 
Kutokana na Mgogoro ambao umemhusu Mbunge wa kibamba Mhe John Mnyika nimebaini Pasipo na shaka kuwa Job Ndugai ambae ni Spika, hana uwezo kabisa wa kuongoza chambo kikuu cha maamuzi kama Bunge.

Japo kuwa ni Spika Tayari lakini tunatakiwa kujua kuna watu ni Marais lakini hawana sifa za kuvaa uhusika hivyo hivyo Ndugai hafai kuwa Spika na Wala tusitegemee jipya lolote kutoka kwenye Bunge analoliongoza yeye na msaidizi wake Tulia Ackison.

Nimesema hivyo hana sifa yoyote ambayo imetokana na Nadhalia za uongozi ususani skill model of Leadership.

Na hizi ndio sifa za Job Ndugai ambazo zinamfanya kukosa sifa za kuwa Spika japo ni Spika na kwa maana hiyo Bunge la sasa ni Dhaifu sana.

1)-Anajaziba, kutokana na hii sifa siku zote hawezi kutoka maamuzi sahihi sifa hii inaonekana pale alipompiga Mgombea mwezake wa ndani ya chama chake.

2)-Ni Mtu wa kujipendeza, na hii inafanyika ili atete kiti chake cha uspika ndio maana anatumia nguvu nyingi kuwaonea wapinzani ili amfurahishe Rais ambae ndio Mwenyekiti wa chama.

3)-Nimkurupukaji, kutokana na sifa hii inamfanya afanye maamuzi na atoe kauli za kitoto ambazo zinalifanya Bunge kuwa dhaifu sababu linaogozwa na watu dhaifu.

Mfano aliposema Lusinde wewe ni kiboko yao mpaka wote wameondoka hii nikauli ya kitoto haikupaswa kusemwa na mtu kama Spika.

4)- ni kigeu geu, sio mtu wa kuamini au kupanga nae mambo makubwa na hii inasababishwa na yeye kuwa mtu wa kujipendekeza.

5)-Anaongozwa na Mhemko, Hana Busara wala Hekima kwa Suala la Mnyika hajatumia Busara wala Hekima Mropokaji.

Kutokana na madhaifu yake yote hayo mzee Chenge ameonyesha uwezo mkubwa kuliko yeye pamoja na msaidizi wake Tulia Ackison.

Kutokana na wabunge kuonewa katika kipindi chake na Serikali au na yeye Mwenyewe pamoja na Msaidizi wake wamefanya ubunge kutokueshimaka kabisa na watu.

Nilikuwa sijawahi kusikia Kwamba Mbunge anaweza kuwekwa ndani mwezi 4 na hajaua ni kipindi cha Ndugai kwa maana hiyo pale amekaa kuziba nafasi isiwe wazi na sio kuliongoza Bunge kupitisha maamuzi sahihi kwa maslahi ya nchi yetu kama lilivyokuwa Bunge la 2005- 2010 kila mtu alitamani kuwa Mbunge.

Ni Mhere Mwita.
ok
 
Kwa ku-declare internet mimi ni katibu wa mbunge toka moja ya majimbo ya mkoa Singida, kwakweli haya nitakayonena yatatoka katika sakafu ya uvungu wa moyo wangu.

Speaker Ndungai kuendelea kukumbatia wabunge wasiokua na vyama kinyume na katiba ya nchi huku akijua kabisa ni udhalilishaji wa mhimili wake na pia ni unajisi wa kiti chake. Hili linalochangia kwa kiasi kikubwa chama chetu na wala halina maslahi kwa chama na halina maslahi kwa taifa. Kama ni wenyeviti wa kamati mbili za hesabu za serikali wapo wabunge wa ACT na CUF, Ndungai asitutie aibu yawezekana kapokea rushwa si bure, ang'ang'ania kitu gani kwa waliokua kinamama wa CHADEMA? Kama kuna semi wake kule tujue moja.

Tunamtaka spika Ndungai Aachie kiti hafai apishe watu wenye maadili wafanye kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria ya nchi siyo lazima yeye awe spika. Asitishike watu kwa sababu yeye ana kinga ya kutoshtakiwa.

Ningeomba wabunge kwa umoja wao wajipange tuweze kuondoa hii sintofahamu. Sasa amechanganyikiwa anajibishana na kina Mama wa CHADEMA kwa sababu ya kiburi chake cha hovyo. Hili suala la ubabe wake muda si mrefu linaweza kutugeukia sisi wana CCM.

Spika aliyesema kua yeye ana faili lake hospitali Mirembe maana yake yeye ni kichaa. Hawezi kufanya kazi na Mama yetu ambaye ni mchamungu. Hili hatutakubaliana nalo kamwe. Lazima apigiwe kura ya kutokuwa na imani naye na lazima wanaccm tulisimamie hili. Tukimwacha huyu mtu mbeleni atatusumbua sana.
 
Kwa ku-declere internet mimi ni katibu wa mbunge toka moja ya majimbo ya mkoa Singida, kwakweli haya nitakayonena yatatoka katika sakafu ya uvungu wa moyo wangu.

Speaker Ndungai kuendelea kukumbatia wabunge wasiokua na vyama kinyume na katiba ya nchi huku akijua kabisa ni udhalilishaji wa mhimili wake na pia ni unajisi wa kiti chake. Hili linalochangia kwa kiasi kikubwa chama chetu na wala halina maslahi kwa chama na halina maslahi kwa taifa. Kama ni wenyeviti wa kamati mbili za hesabu za serikali wapo wabunge wa ACT na CUF, Ndungai asitutie aibu yawezekana kapokea rushwa si bure, ang'ang'ania kitu gani kwa waliokua kinamama wa CHADEMA? Kama kuna semi wake kule tujue moja.

Tunamtaka spika Ndungai Aachie kiti hafai apishe watu wenye maadili wafanye kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria ya nchi siyo lazima yeye awe spika. Asitishike watu kwa sababu yeye ana kinga ya kutoshtakiwa.


Ningeomba wabunge kwa umoja wao wajipange tuweze kuondoa hii sintofahamu. Sasa amechanganyikiwa anajibishana na kina Mama wa CHADEMA kwa sababu ya kiburi chake cha hovyo. Hili suala la ubabe wake muda si mrefu linaweza kutugeukia sisi wanaccm.

Spika aliyesema kua yeye ana faili lake hospitali Mirembe maana yake yeye ni kichaa. Hawezi kufanya kazi na Mama yetu ambaye ni mchamungu. Hili hatutakubaliana nalo kamwe. Lazima apigiwe kura ya kutokuwa na imani naye na lazima wanaccm tulisimamie hili. Tukimwacha huyu mtu mbeleni atatusumbua sana
Kweli kadharau na kusigina Katiba..

Lakini alifanya hivyo kwa Baraka za utawala wa ccm kupitia hawa:--
✓Jiwe
✓Bashiru
✓Polepole
 
Ndugai anashangaa Sharia za kijinga ambazo ni kichaa tu angeweza kuzipitisha. Anajiuliza alikua wapi wakati wanapitisha sheria chafu kama hizo? Nadhani mambo mawili, moja huenda anaumwa au legacy ya mwendazake inaisha nguvu.

Hili ni Bunge la CCM...je ni sharia ngapi za kijinga zimepitishwa na kuumiza Watanzania?

IMG-20210527-WA0043.jpg
 
Back
Top Bottom