Naomba ntakujibu kwa visa Joka maana kuishi kwingi kuona mengi:
1. Kuna polisi kaibiwa mke ambaye alimuoa akiwa vizuri tu, ila akatokea mtu huko akamuiba na mke akahamia kwake. Jamaa kaelekezwa alipo mkewe kamfata kampata ila maelezo ya mke ni kwamba, nifanye itakavyokupendeza ila sikutaki tena. Polisi sasa hivi kakubaliana na hali kaachana nae amemove on ila hakuamini kabisa kilichotokea maana mwanamke alimkuta akiwa vizuri
( Ila nina Ndugu yangu yupo tu na single mother wake hawaachani miaka na miaka)
2. Mzee mwenzangu aliwekewa mtego akanaswa, alishikiwa bastola kwa kosa la kutembea na mke wa mtu, akabebwa mkuku mkuku chini ya ulinzi na njemba mpaka dukani kwa mke wa jamaa, mke kaulizwa unamfahamu huyu akajibu namfahamu ndio na hajui kama nimeolewa ila natembea nae ndio, akamgeukia mumewe akamwambia wewe si upo busy, utajua mwenyewe. Mwenye mke akaona hapa ntaua wangapi? Mzee akaachiwa kuna siku akatafutwa akaombwa msamaha na fidia juu za usumbufu na mwenye mke akakiri mkewe hajatulia amebadilika na kuwa malaya. Tupo na mzee mtaani tukila mvinyo na jamaa mwenye mke kabla ya fumanizi alijua ana mke kweli.
(Ila nina Ndugu yangu yupo tu na single mother wake na kamwongezea mtoto hawaachani miaka na miaka)
3. Kuna mtu yupo na mwanamke aliyezaa watoto 3 alimnyang'anya jamaa huko alikuwa njaa njaa hawezi kuimudu familia.
Jamaa kazaa na mkewe watoto 3, sio kamkuta na mtoto, la ha sha, kamzalisha watoto 3 akajua ila katokea mwamba huko kamtongoza mke wake mpaka kakubali kaanza kumuhudumia mpaka mke akaona ya nn shida, akamkimbia jamaa na kuhama nyumbani.
Watoto wa jamaa wapo nje huko wanasoma kwa fedha za mume mpya.
jamaa ukimpa hii hadithi ya single mama ndo wenye tatizo hatakuelewa maana mkewe(Shemeji yake kwa sasa) ni mwanamke na nusu ila ameshawishiwa na ametulizwa na mwanaume mwingine.
(Ila nina Ndugu yangu yupo tu na single mother wake na kamwongezea mtoto hawaachani miaka na miaka)
HITIMISHO
Vijana ambao hamjaoa tafuteni ukwasi muweze kuzitunza familia na mwanamke akuheshimu lakini la muhimu ni kuomba sana usikosee kuoa.
Achana na formula, hakuna formula ingekuwepo kila mtu angeandikiwa aifuate. Sio kila mwenye matatizo ya ndoa alioa single mother.