Kuoa Single Mama ni sawa na kunywa soda iliyofunguliwa na kuonjwa
Single mother ni shida. Mimi huwa siwaonei huruma kwasababu wengi wao utakuta walikuwa wanafunzi ila kiherehere chao cha kukimbilia mapenzi wakanasa mimba. Wengine waliwakataa WASUKUMA wakakimbilia masharobaro na kuishia kutelekezwa. Na kuna baadhi jeuri na kiburi wakashindwa kulinda ndoa zao na kuishia kuzivunja. Ni single mother wachache sana chini ya jua wanaweza wasiwe na tatizo wakiolewa na mtu mwingine. Na katika hao wachache utakuta wapo huko Cambodia, Uzbekistan au Nepal... kwa Tanzania ni ngumu kupata single mother mwenye akili timamu.
Una uhakika kuwa Tz hawapo??
 
Ngoja nitoe story moja labda inaweza kumuinua somebody here. Kuna ndugu yangu flani tumpe jina Abshir. alikuaga na mdada tumpe jina Rosina. Abshir na Rosina were so in love, mahaba ya njiwa kama yote. Wakiwa mahali wanaonyesha mapenzi mpaka sisi watazamaji tunaona. Miaka miwili ikapita hapo Abshir hana pesa, mwenye kimango ni Rosina. So Rosina alikua kama bread winner kimtindo.

Baadae Abshir akampa mimba Rosina. Baada ya Rosina kubeba ujauzito, Abshir akawa kama anajiengua flani ivi. Rosina akanotice, akaja kusema nyumbani kwamba mimi siumuelewi ndugu yenu, mbona kanibadilikia. Basi Abshir akawa anasema "mimi sikupanga nimuoe huyu dada so kaamua kubeba ujauzito kwa lazima. So Abshir akaachana na Rosina. Mtu mzima mmoja tu upande wetu ndie aliekuwaga intouch na Rosina kuuliza maendeleo lakini Abshir yeye na ndugu wengne tukajikataaga completely. So basi bwana, Rosina akajifunguaga mtoto wa kiume akapambana mwenyewe mpaka mtoto akakua.

Huku nyuma Abshir alistruggle kivyake, akaja akaoa mwanamke mwingine. Wakaishi pamoja kama miaka miwili, Abshir akaanza kuugua then akaja kufariki. Kwenye msiba ndipo movie iliponoga. Abshir alikua na mtoto wa kiume mmoja tu ambae alimtelekeza kwa Rosina. Rosina alishapataga mwanaume akaolewaga. Kuna ndugu viherehere wakawa wanadai eti mtoto wa Abshir wa kiume apelekwe kwenye msiba wa baba ake. Mtu mzima yule aliekuwaga in contact nae akampigia simu Rosina na kumwambia bwana bwana. Huku wanasema A B na C. Rosina akamwambia naongea na wewe kwa sabbu weww ndo pekee ulienipa support all this time. Waambie nawaheshimu sana. Please sitaki kelele na mtu. Nina amani kwenye ndoa yangu, just leave me alone. Alishaniacha huyu mtoto ni wa huyu mume wangu. Akakata simu.

Basi mtu mzima huyu akafikisha ujumbe na akasema she is very correct. Miaka yote mmekaa kimya kama ndugu leo mnamuulizia wa nini. Mumuache mtoto wa watu kaolewa na ana amani kwenye ndoa yake. Basi bwana watu sura zikawashuka wakakituliza. Msiba ukaisha..and by the way Abshi hakuwahi kupata mtoto na huyu mwanamke mwingine and nae alikuaga single mother mwenye watoto wawili. It is what it is.

My point hasa ni kwamba, incase yameshatokea ya kutokea kila mtu ashinde mechi zake. Wewe ni mwanamke lea m/watoto wako mwenyewe. Do not try to force yourself kwenye maisha ya huyo mwanaume. Akifanya sawa asifofanya kufa na Yesu wako. Because ukizidi kujisumbua nae sanasana wewe ndo utawaste your life. Ukija kuzinduka miaka 10 imeshaisha na ulikua busy unacheza games za back and forth.

Na wewe mwanaume incase tayari yameshatokea, ni jukumu lako kulea mtoto wako. Kwanini ugongewe hodi lakini. Tuma fedha, kata bima ya mtoto wako ili kuepuka usumbufu. Kama amefika 7 years na unaona kuna drama sana kwa mama mtoto basi fata taratibu mchukue ishi nae au sort it out. Lakini msitumie hiyo nafasi ya kumlea mtoto kama chachu ya kumfanya mama mtoto sex machine. Na wewe unazidi kujipotezea muda na kukaribisha hasara na nuksi kwenye maisha yako. Maana unakuta umeshaoa mwanamke mwingine na huku mnatafunana na huyo mama mtoto sijui mnakua mnafikiria nini.

Lets all be emotionally mature and grow up. Back and forth sex games and drama ni hasara tu. Mistake zikishatokea zimetokea why tunazidi kuzipalia makaa na kuwa wapumbavu kiasi hiki? I really hope and pray kila mtu ajifunze kuwa responsible kwa choices anazozifanya kwenye maisha yake.
 
Umekuna kunako..soma huu mkasa ulionikuta itakusaidia

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Mimi ni mtu ambaye nilikuwa siamini katika kumuoa single mother ila baadaye nikajikuta nimekutana na single mother nikaona nitengue msimamo wangu ila kwa hili msimamo wangu narudi kuiheshimu.

Mnamo mwaka huu mwezi wa January, nimekutana na mdada mmoja ambaye tulimaliza naye chuo, na kwa bahati nzuri nilikuwa nasoma naye course moja na pia tulikuwa group moja kwenye discussion. Hivyo na mfahamu kwa kiasi alikuwa ni binti mwenye msimamo kwenye mahusiano.

Kipindi hicho sikuweza kumtongoza kwasababu nilikuwa nipo kwenye stress kubwa wakati nasoma university.

Ila ilikuwa namkubali kubali kiasi, ila wakati tukiwa mwaka wa tatu akakutana na jamaa alikuwa ni graduate na anakazi. Jamaa akafanikiwa kumuweka kwenye himaya yake. Kwangu haikuniumiza sana kwa kwasababu sikuwahi kumtongoza akanitoe nje.

Siku zikaenda jamaa akaenda kujitambulisha kwa binti, ikapangwa mpaka siku ya harusi na vitu kwa hivyo.

Jamaa akawa anahairisha harusi mara kwa mara ila kafanikiwa kuzaa naye mtoto, ila baadaye wakaingia kwenye misuguano wakavunja uhusiano na sababu mwanamke anasema jamaa alikuwa na mwanamke mwingine na mpaka sasa eti jamaa anaishi naye na amezaa naye mtoto, anyway mwanamke akamchukua yule mtoto aliyezaa na jamaa akampeleka kwa wazazi wake.

Mpaka nakutanane naye ameachana na jamaa na kwa takribani miaka mitatu. Anyway baada ya kunieleza hayo kwa uchungu nikaanza naye mahusiano baadaye nikaona kwasababu ni mwanamke ambaye namfahamu kitabia tokea nikiwa chuo acha nifumbe macho nifanye haraku za kuweka ndani kwa heshima.

Anyway baada ya kuanza naye mahusiano akapata ujauzito nikaona ili nisimkweze na aone nipo sereous naye ngoja nikamtambulishe, nikampeleka home kwa utambulisho.

Nikawa nimebakiza kibarua ya kwenda kwao ambaye mpaka sasa sijaenda bado.

Sasa leo akanipigia simu akaniambia amepata msiba, nikamuuliza nani akasema baba mkwe wake wa zamani na waenda na dada yake. Anyway sikutaka kumcrash.

Ila nimeona nipate muda wakutafsiri hiyo picture na kujiuliza maswali mengi.

1. Binafsi najiuliza kama ametoka misri na ameamua kwenda Caana kwanini anarudi nyuma

2. Na kama wameachana na hawakufunga ndoa na ameshatambulishwa katika familia nyingine anaenda kule kama nani...?na kwasababu gani hasa...?

Binafsi nikaona huyu anacheza na akili yangu kwasababu kama yupo sereous
Pole mkuu,haya masingle mother ya hovyo ndo yanawaharibia wengine wenye heshima na wanaojielewa, shame on them[emoji57]
 
Single maza tunawalaumu bureee,,,hivi ikiwa wewe uliyemzalisha bado unamfuatafuata na kumtamani unadhani atakataa? Wengi hufanya hivyo ili Watoto/Mototo azidi kupata mapenzi ya Baba,,,Me naamini ikiwa wewe uliyemsababishia huo usingle maza ukawa mbali naye na ukaweka mipaka siyo (minyau)baina yake na wewe sidhani kama kuna kitu kinaweza Haribika,,,ila wengi wa waluowazalisha wanakuaga na tamaa,,,kumbukeni kuna wanaume baadhi ni mara umbwa yaani tunawaita zoazoa.......
Ukiona mwanaume wa hivyo anataka tu akuharibie kwa mtu wako mwenye future na ww,hakikisha mkiachaha mnaachana kweli na sio reja reja,na single mother mnatakiwa kuwa na misimamo.
 
Habari wana jf?

Oyaaaa vijana wapanbanaji acha niwape mnara iko hivi:
Kiburi, jeuri, Nyodo, kisirani, ujuaji, Midomo na kutoridhika na wanachopewa na wanaume wao hizi ni changamoto za single mothers wa Tanzania kwa 90% ni single mothers wachache sana wasio na hizi tabia na huwezi kuwakuta wanabwatuka hovyo humu mitandaoni,,

Single mothers wa humu wote wanasema wanaume ndio chanzo Cha situation zao lakini Kuna walioachwa kwa ajili ya usaliti na umalaya na hawatakwambia na wenyewe wapo humu bila aibu nao wanatulaumu wanaume

Ukiona lijanamke linashinda mtandaoni kujisafisha makosa yake na kurusha lawama kwa wanaume ujue hilo ni jini kisirani usijichanganye mwamba utaisha vibaya,

hapa mtandaoni anajifanya ye malaika, ye ndio kaonewa sasa we jichanganye,, single mothers wa aina hiyo wengi hawanaga shukrani siku maisha yako yakiyumba halafu baba wa mtoto wake ndio kapata hela my friend utalia kichina...[emoji28]

Ni single mothers wachache sana tena wachache sana nasisitiza wachache sana wanaojielewa na huwezi kuwakuta wanachamba watu humu mitandaoni, wako busy na maisha hawana muda wa kupoteza sio hawa wawindaji haramu kijana mwenzangu kuwa makini na hawa viumbe..

Kuna wapanbanaji wenzetu wako jela sasa hivi na wengine wamekufa kwa ajili ya humiliation za hawa single mothers wa kuokota okota mitandaoni..

Mpambanaji mwenzangu ukipata single mother humu usikurupuke kuoa nenda nae taratibu hatua kwa hatua hakikisha unapata taarifa zake sio zile alizokupa bali zile ambazo hajakupa , muhimu sana kuijua familia yake anayotokea, ndugu na marafiki zake wa karibu hii itakusaidia kujua uko na mtu wa aina gani maana ndege wanaofanana huruka pamoja..

Usiamini kila story mbaya atakayokupa kuhusu baba wa mtoto wake, mama zetu huwa hawasemi mabaya yao kamwe siku zote huwa wanasema mabaya ya baba zetu tu! usibebe picha mbaya dhidi ya mwanaume mwenzio huwezi kujua nini kilimkuta kwa huyo mwanamke we kaa kwenye nafasi yako, mchunguze mtu wako utaujua ukweli tumia akili sio hisia..

Usianze mahusiano na single mother halafu ukaanza kuwekeza kwenye maisha yake moja kwa moja hilo kosa litakugharimu kumbuka nimekwambia wengi wao hawana mioyo ya kuridhika wala shukrani.. we msaidie kwenye kile ulichomkuta nacho wakati huo na wewe endelea na ratiba zako za utafutaji ulizokuwa nazo, usibadili malengo Wala mfumo wako wa utafutaji kwa ajili yake we msaidie kwa kile unachoweza ila usimuingize kwenye mifumo yako wala usiingie kwenye mifumo yake, ukiingia tu kwenye mfumo wake anakuunganisha na marejesho utaimba kikorea mwanawane,,

Kama ni single mother anayejielewa utaona siku zinavyokwenda anajiset kuendana na mfumo wako wa maisha kuanzia kwenye mambo ya fedha, nidhamu hadi chumbani yani anaacha anaji sacrifice kwa ajili yako hata kabla hujatangaza ndoa na wala hana uhakika wa hiyo ndoa ila anafurahia uwepo wako kwenye maisha yake na anafanya jitihada za ziada ili uendelee kuwepo kwenye maisha yake my brother huyo ndio single mother wa kuoa sasa sio hawa wawindaji haramu utawapa jasho lako lote na bado hawataridhika watatafuta mwingine awape zaidi kumbuka nature ya mwanamke ni kiumbe kisichoridhika,
MUNGU aliweka matunda ya kila aina bustani ya edeni lakini bado mwanamke hakuridhika akafuata lile moja alilokatazwa na bado leo wanatutupia lawama sisi kwamba haturidhiki wamesahau ndio walitufundisha kutoridhika pale bustani ya edeni [emoji28]
Tuishi nao kwa akili wanangu TUWAPENDE ila TUSIWAAMINI[emoji1666]



Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
Duh,umeandika kwa uchungu sana mkuu[emoji120]
 
Nakuibia tu siri ndogo......hao wanawake mliowaoa kwenye nyumba za ibada ndo tunawafaidi sisi sasa

Unaona jinsi ulivyo mjinga, hapa tunazungumzia umiliki, hatimiliki.
Kwani MTU ukiwa na shamba Wezi hawawezi kukuibia?

Unazungumzia mambo mawili tofauti. Ndio maana Wanawake wanawaona Vijana WA siku hizi ni vichwa panzi.
 
KWA NINI SINGLE MOTHER WANAOGOPWA KULIKO SINGLE FATHER?

Anaandika, Robert Heriel

Baadhi ya Wadada wamekuwa wakiniuliza iweje Single mother pekee Yao wanaogopwa na Vijana wakiume lakini Single father hawaogopwi na Vijana wakike? Aidha ni Kwa nini Mwanamke mwenye mtoto anapata changamoto kubwa Kupata Mwenza wa kumuoa ukilinganisha na Single father?

Kwa kuongezea, ni kwanini kijana akitaka kuoa single mother atapata upinzani mkubwa kutoka Kwa Wazazi na Ndugu zake na jamii Kwa ujumla? Maswali hayo leo tutaenda kuyajibu Kwa kifupi.

Single mother ni mwanamke mwenye mtoto au Watoto ambaye hajaolewa au aliyepewa Talaka. Huyo ndio single mother. Wakati Single Father ni Mwanaume mwenye mtoto au Watoto ambaye hajaoa au aliyekwisha kupeana Talaka.

Zifuatazo ni sababu za Kwa nini single mothers wanaogopwa zaidi kuliko Single Father;

1. Upendo
Wanawake asilimia 90 wanabeba mimba Kwa wanaume wanaowapenda iwe kwa upendo halisi au upendo wa Mali,
Mwanamke hawezi kuzaa na Mwanaume asiyempenda, Wakati Sisi wanaume suala la kuzaa halipo Chini ya maamuzi yetu.
Sisi wanaume tunaweza bebewa mimba na Mwanamke yeyote hata tusiyempenda, na bahati nzuri au Mbaya wale Wanawake tusiowapenda ndio wepesi kushika MIMBA.

Mwanaume anaweza kutelekeza Mama na mtoto Kwa sababu Hakumpenda Mama na bila Shaka mtoto hakuwa kipaombele chake. Mtoto hawezi kumfanya mwanaume ampende Mwanamke, Ila Kwa upande wa mwanamke mtoto anaweza kumfanya Mwanamke ampende Mwanaume.

Mwanamke analazimika kumpenda mzazi mwenza Kwa MASLAHI ya mtoto, Wakati Sisi wanaume hatunaga kitu kama hicho. Hatulazimiki kumpenda Mwanamke Kwa sababu ya Watoto.

Hii inafanya Single mother kuogopwa Kwa sababu bado wengi wao huwa na bond na Wanaume waliozaa nao Kwa MASLAHI ya mtoto.
Ni nadra Kwa mwanaume kumtafuta Mwanamke aliyezaa naye lakini ni Jambo la kawaida Kwa Wanawake single mother kutafuta Mababa wa watoto Kwa sababu nyingi tuu.

2. HUDUMA KWA MTOTO/WATOTO
SIngle mother wanaogopwa zaidi Kwa sababu wanakuwa wasumbufu kupiga piga simu Kwa wanaume waluowazalisha Kudai Huduma za Watoto. Lakini Hii ni tofauti na single father, mtoto akikaa na Baba yake atahudumiwa na Baba pasipo Mama yake kusumbuliwa.
Yaani haiwezekani single father adai Huduma ya mtoto Kwa mzazi mwenza.

Single mother wengi wanajua ni hasara kubwa kwao kumpa Mwanaume mtoto kwani watakosa mawasiliano na pili wapo wanaopatiemo huduma kupitia Watoto.

Wanawake wengi wanaoolewa na Single father hupendelea huwashauri Waume zao kuwachukua Watoto waishi NAO palepale nyumbani ili kukata mawasiliano baina ya mumewe na Mzazi mwenza, na kama atataka kuwasiliana na mwanae basi simu itapokelewa na atapewa simu mtoto aongee na mama yake.

3. SINGLE MOTHER WENGI KIPAOMBELE CHAO NI WATOTO.
Hii ni tofauti na Single father, wanaume wengi Watoto sio kipaombele Sana ikiwa tuu ataona Mkewe anamheshimu na kumtii. Ndio maana ni kawaida Kwa wanaume kutelekeza watoto. Hilo wala halina mjadala.
Mwanamke yupo connected na watoto wake automatically tofauti na Sisi wanaume.

Single mother wengi kipaombele Chao ni Watoto wao, kila kitu atakiangalia katika jicho la kumlinda mtoto wake, na yupo tayari kufanya lolote kwaajili ya mtoto wake. Hii ni tofauti na Single father, yeye atadili na Familia Kwa ujumla Kwa kumpenda Mkewe na kumpa kipaombele Mkewe kwani yeye ndiye mlezi wa watoto na familia Kwa ujumla.

Single mother hawezi kukupenda kama anavyompenda mtoto au Watoto wake Ila SIngle father anaweza akampenda Mwanamke/Mkewe Mpya kuliko anavyowapenda Watoto wake.

4. DRAMA
Single mother wanadrama nyingi mno ukilinganisha na Single father. Waliooa single mother wamekuwa Watu wanaoripoti visa na mikasa ya kusisimua na kushangaza, tofauti na wanawake walioolewa na single father.

Tabia ya mwanaume ni ileile haijalishi ni single father au sio single father. Haijalishi ni kijana au Mzee. Wanaume Tabia zetu ni zilezile.
Hii ni tofauti na wanawake, Wanawake wapo tofauti tofauti kulingana na umri, maumbile, Elimu, hadhi, mwenye Watoto n.k

I) Mwanamke Bikra hafanan na Mwanamke asiyebikra,
ii) Mwanamke single mother hafanani kabisa na Mwanamke asiyesingle mother, yaani ni jinsia moja lakini wapo tofauti kihisia, Kiakili, kimtizamo na kimaamuzi.
iii) Mwanamke mwenye umri wa miaka 15-25 hafanani na Mwanamke mwenye umri miaka 25-40 na pia hawafanani na Wanawake wenye miaka 41-60 linapokuja suala la mahusiano.

Lakini kijana wa miaka 15-25, 25-40, MTU mzima wa miaka 41-60 wanafanana linapokuja suala la mahusiano.

5. SINGLE MOTHER HUPENDA KUPEWA HESHIMA ILEILE UNAYOMPA MKEO HATA KAMA MMEACHANA. WAKATI SINGLE FATHER HUO MUDA HANA NA SIO AJABU AKAWATELEKEZA HATA NA WATOTO.

Ukioa single mother elewa kuwa kama aliyemzalisha anampa heshima yote kama Mkewe(Kwa jina la Mzazi mwenza) na akawa anawahudumia Watoto wake basi kazi yako kama mume Kwa huyo Mwanamke ni kubwa Sana. Utapata tabu Mno.

Elewa kuwa Mwanamke single mother ndio hulazimisha ukaribu wa mzazi mwenza naye Kwa mgongo WA mtoto. Ila ni ngumu mwanaume single father kutafuta ukaribu na Mwanamke aliyemzalisha. Hakunaga kitu kama hicho.
Ingawaje single mother wanaweza kukuambia kuwa hawasiliani na Mzazi mwenza lakini Kwa Sisi wakulungwa tunasema huo ni Uongo.

Lakini single father akikuambia hajawasiliana na Mzazi mwenza muamini kabisa Kwa sababu Sisi wanaume tunaathiriwa zaidi na MTU aliyekaribu kuliko aliyembali, sio ajabu Mwanaume anauwezo wa kukaa hata mwezi au miezi sita bila kuwasiliana na Wazazi wake lakini Kwa Mwanamke ni tofauti.
Sasa ikiwa mwanaume anauwezo wa kukaa muda mrefu bila kuwasiliana na Mzazi aliyemzaa sembuse Mwanamke aliyemzalisha au sembuse Mtoto?

Lakini Kwa Mwanamke hilo hataweza tena akijua Mwanaume aliyemzalisha anauwezo wa kiuchumi.

Eid Mubarak

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Single mother chenga mi hata sishauri kwa kijana ambaye hajaoa kuoa single mother , hao wanatakiwa wapambane na madanga ya mjini , ukioa single mother hakikisha ana pesa chafu yani weww uwe kibenten
 
Back
Top Bottom