Ndugai ni Spika asiye na sifa za kuwa spika
Wanabodi,
Salaam;

Nimesikitishwa sana na kitendo kilichofanywa na ofisi ya spika juu ya kujiuzulu mh. Nyalandu.
Ni wazi ofisi ya Bunge imejidhalilisha mno!

Baada ya taarifa ya Nyalandu kuenea ktk mitandao ya kijamii na ktk vyombo vya habari, alijitokeza msemaji wa CCM asiye na uwezo wa nafasi yake, akimshangaa Nyalandu kukihama chama cha mapinduzi chenye itikadi ya ujamaa na kuhamia ktk chama kisichokuwa na Sera. Huyo aliyeyasema hayo ni kiongozi wa ngazi ya juu kabisa ya CCM.

Kwa taarifa tu na kwa faida ya wengine wasiofahamu, katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha mapinduzi, anaingia katika vikao vyote vikuu vya kikatiba kuliko hata mwenyekiti wa CCM taifa. Mwenyekiti siyo mjumbe wa sekretarieti ya chama ambayo inaundwa na watendaji tu. Yaani katibu mkuu(ambae ni mwenyekiti wa kikao), manaibu katibu wakuu, katibu wa itikadi na uenezi, katibu wa uchumi na fedha, makatibu wa jumuiya za chama yaani UWT, vijana na wazazi.

Hicho kikao ndo kinaandaa ajenda za kikao cha kamati kuu na huyo Polepole ni mjumbe pia wa kamati kuu. Kama Nyalandu alifukuzwa, ina maana Polepole angekuwa anajua na kwa sababu ni mropokaji, lazima angekuwa ameropoka tu!

Kwa hiki kilichofanywa na ofisi ya spika ni kitendo cha aibu mno na kama kitavumiliwa na wabunge, tutaonana 2020 msitufanye watanzania wote majuha..!
Hayashangazi haya! Ikiwa "mtu" alitumwa India kutibiwa na watu hawakushangaa iweje hili la mtu kujiuzulu ikasemwa kafukuzwa pasina kikao!!!???
 
Kiukweli haingii akilini pale spika anapokuwa hayupo na kisha bunge kuendeshwa na yule mwanadada halafu wabunge wanasema huyu mwanamama hafai anawaminya na kisha kumtaka huyu mzee kifimbo cheza kuongoza!
Huyu mzee kifimbo alipokuwa ughaibuni kwa matibabu wabunge walikuwa wakichukizwa sana jinsi ambavyo huyu mwanamama alivyokuwa akiongoza, hivyo wakawa wanamuombea sana kifimbocheza apone ili aongoze!
Baada ya kifimbo kupona, yaliyotokea yamekuwa tofauti sana...
Kwa kweli hii haikubaliki wapinzani kuendelea kuwasifia hawa watu kwa matendo wanayofanyiwa...
Pia hata wabunge wa chama tawala wanaojali na kutambua demokrasia ya kweli huu ni wakati wa kuungana na wale wote wenye mapenzi mema kuinusuru demokrasia yetu!
Hawa watu wawili wanapaswa kujirekebisha, ama kuondolewa kwenye viti vyao!
 
Suluhu ni kuondolewa.

Je, nani atawaondoa?
 
Spika atakuwaje upande wenu wakati waliompa uSpika ni Wabunge wa CCM
 
Kiukweli haingii akilini pale spika anapokuwa hayupo na kisha bunge kuendeshwa na yule mwanadada halafu wabunge wanasema huyu mwanamama hafai anawaminya na kisha kumtaka huyu mzee kifimbo cheza kuongoza!
Huyu mzee kifimbo alipokuwa ughaibuni kwa matibabu wabunge walikuwa wakichukizwa sana jinsi ambavyo huyu mwanamama alivyokuwa akiongoza, hivyo wakawa wanamuombea sana kifimbocheza apone ili aongoze!
Baada ya kifimbo kupona, yaliyotokea yamekuwa tofauti sana...
Kwa kweli hii haikubaliki wapinzani kuendelea kuwasifia hawa watu kwa matendo wanayofanyiwa...
Pia hata wabunge wa chama tawala wanaojali na kutambua demokrasia ya kweli huu ni wakati wa kuungana na wale wote wenye mapenzi mema kuinusuru demokrasia yetu!
Hawa watu wawili wanapaswa kujirekebisha, ama kuondolewa kwenye viti vyao!

Kwa nafasi ya USPIKA na UNAIBU SPIKA au uenyekiti wa Bunge ukishakaa kwenye kile kiti unatakiwa kuwa very neutral na kama huwezi jiweke 75% neutral maana ukishakuwa Bungeni hatuangalii chama kule ni watanzania wanakaa kuifunga kengele serikali.

Hivyo Spika anaongoza wananachi na si serikali.Bunge si la serikali bali la wananchi bila kujali itikadi zetu.Ujinga wa kufanya upendelea matokeao yake ni kutokuenedelea kwa taifa
 
Katiba za ki Africa ktk swala la democracy ni pasua kichwa!! Na kwa Tz ni dhambi kushirikiana mtu wa chama cha upinzani. Ila inatakiwa wa upinzani yeye ashirikiane na chama tawala ajabu!!!

Ndugai analifanya bunge jumuia ya chama. Katiba zetu mbovu.
 
Kwa mfululizo wa mambo na matukio anayoyafanya mheshimiwa sana ya kujichukulia madaraka na kujigeuza yeye ndio kila kitu,nina hakika ingekuwa ni katika nchi za wenzetu wabunge wangeshachachamaa na pengine kuanza mchakato wa kikatiba kumshughulikia.

Kwa mfano,ingekuwa ni hapo Bondeni kwa mzee Madiba saa hizi pangekuwa hapatoshi na kina Julius Malema wangekuwa wameshamtolea uvivu ila hapa kwetu tumelala usingizi na yeye ana-take advantage ya uzembe wetu.

Binafsi ningekuwa mule ndani ningeshalianzisha ingawa najua ningekamwisha lakini nisingejali kwani lengo ni ujumbe ufike na umma uelewe.
 
20171113_091536.jpg
 
Kutokana na Mgogoro ambao umemhusu Mbunge wa kibamba Mhe John Mnyika nimebaini Pasipo na shaka kuwa Job Ndugai ambae ni Spika, hana uwezo kabisa wa kuongoza chambo kikuu cha maamuzi kama Bunge,

Japo kuwa ni Spika Tayari lakini tunatakiwa kujua kuna watu ni Marais lakini hawana sifa za kuvaa uhusika hivyo hivyo Ndugai hafai kuwa Spika na Wala tusitegemee jipya lolote kutoka kwenye Bunge analoliongoza yeye na msaidizi wake Tulia Ackison.

Nimesema hivyo hana sifa yoyote ambayo imetokana na Nadhalia za uongozi ususani skill model of Leadership.

Na hizi ndio sifa za Job Ndugai ambazo zinamfanya kukosa sifa za kuwa Spika japo ni Spika na kwa maana hiyo Bunge la sasa ni Dhaifu sana.

1)-Anajaziba, kutokana na hii sifa siku zote hawezi kutoka maamuzi sahihi sifa hii inaonekana pale alipompiga Mgombea mwezake wa ndani ya chama chake.

2)-Ni Mtu wa kujipendeza, na hii inafanyika ili atete kiti chake cha uspika ndio maana anatumia nguvu nyingi kuwaonea wapinzani ili amfurahishe Rais ambae ndio Mwenyekiti wa chama.

3)-Nimkurupukaji, kutokana na sifa hii inamfanya afanye maamuzi na atoe kauli za kitoto ambazo zinalifanya Bunge kuwa dhaifu sababu linaogozwa na watu dhaifu.

Mfano aliposema Lusinde wewe ni kiboko yao mpaka wote wameondoka hii nikauli ya kitoto haikupaswa kusemwa na mtu kama Spika.

4)- ni kigeu geu, sio mtu wa kuamini au kupanga nae mambo makubwa na hii inasababishwa na yeye kuwa mtu wa kujipendekeza.

5)-Anaongozwa na Mhemko, Hana Busara wala Hekima kwa Suala la Mnyika hajatumia Busara wala Hekima Mropokaji.

Kutokana na madhaifu yake yote hayo mzee Chenge ameonyesha uwezo mkubwa kuliko yeye pamoja na msaidizi wake Tulia Ackison.

Kutokana na wabunge kuonewa katika kipindi chake na Serikali au na yeye Mwenyewe pamoja na Msaidizi wake wamefanya ubunge kutokueshimaka kabisa na watu.

Nilikuwa sijawahi kusikia Kwamba Mbunge anaweza kuwekwa ndani mwezi 4 na hajaua ni kipindi cha Ndugai kwa maana hiyo pale amekaa kuziba nafasi isiwe wazi na sio kuliongoza Bunge kupitisha maamuzi sahihi kwa maslahi ya nchi yetu kama lilivyokuwa Bunge la 2005- 2010 kila mtu alitamani kuwa Mbunge.

Ni Mhere Mwita.
Binadam ni viumbe wa ajabu sana.
Mwaka jana wakati Spika alipokuwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu na nafasi yake kuchukuliwa na naibu spika, kulikuwa na malalamiko mengi sana dhidi ya N/S na wengi walikuwa wanasema ni bora mwenye kiti chake arejee mapemba maana huyo aliyekuwepo alikuwa hatoshi.
Leo hii mnaanza kusema kuwa huyo ambaye mlikuwa mnamsifia sasa naye amekuwa hafai.
 
Binadam ni viumbe wa ajabu sana.
Mwaka jana wakati Spika alipokuwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu na nafasi yake kuchukuliwa na naibu spika, kulikuwa na malalamiko mengi sana dhidi ya N/S na wengi walikuwa wanasema ni bora mwenye kiti chake arejee mapemba maana huyo aliyekuwepo alikuwa hatoshi.
Leo hii mnaanza kusema kuwa huyo ambaye mlikuwa mnamsifia sasa naye amekuwa hafai.
Hii kauli ilimkasirisha sizonje, ndio maana siku ya kupokea ripoti ya madini ya tanzanite, aliamua kumpasukia live spika kwa kuwa aliona kama anawalea lea wapinzani, akamwambia wakilopoka, i mean wakipishana kwa kauli awatoe nje na jamaa anatekeleza tu bila aibu!:,(
 
Nahisi Ndugu Ndugai Bado anapwaya sana katika nafasi yake ya uspika, ni mwaka wa tatu sasa hatujaona hata meno ya Bunge kuiwajibisha serikali katika masuala nyeti na Muhimu,

Nakumbuka kipindi cha jamaa Kikwete Bunge limewajibisha serikali Mara kibao sana na nashangaa mpaka Leo tuna mengi ya kuhoji lakin Bunge linaiogopa serikali,

Kuna masuala nyeti sana lakin Bunge Lipo kimya,

Naona viatu vya Makinda vinampwaya ndugai,

Hata wakati wa mwalimu Nyerere ambaye tunaamini ndo alikuwa mkali na ndo alikuwa rais kweli, lakin Bunge lilihoji na kuisimamia serikali ipasavyo mpaka saa nyingine kuikataa miswada na Nyerere ku surrender

Kipindi hicho Adam Sapi Mkwawa akiwa spika bunge lake lilikataa muswada wa Rais na kuurudisha na Rais akabwaga manyanga. Tena siyo hawa marais wa kuja bali ni Rais anayeheshimiwa hata miaka 200 ijayo yaani Rais Julius Nyerere. Je, ilikuwaje? Ilikuwa hivi.

Mwaka 1969 Waziri wa Elimu, Solomon Eliufoo aliugua na ikaonekana anaweza asiendelee kuwepo serikalini. Serikali kwa ku-panic ikapeleka muswada bungeni unaohusiana na mafao au maslahi ya mawaziri hasa wanaougua.

Muswada huo ulileta mgawanyiko bungeni ukizingatia kwamba ni miaka miwili tu tangu siasa ya Ujamaa na Kujitegemea itangazwe pia miiko ya uongozi.

Bunge likaukataa muswada ule likamrudishia Rais Nyerere ili ikiibidi afanye lolote na kama ni kuurudisha tena basi na iwe ili hatimaye wavunje bunge na nchi irudi kwenye uchaguzi.

Rais Nyerere mwenyewe alipohojiwa na waandishi alinywea na kusema "the parliament had a point" yaani bunge lilikuwa na hoja na hakuthubutu kuupeleka tena bungeni.

Haya, niambieni ni bunge lipi tena lililowahi kufauluujasiri kama huu. Wote waliobaki na mnaowataja wafyata mkia watupu, tena kukiwa na hatauwezekano wa kuhama vyama.

Leo hii Viatu vya Makinda ni vikubwa mno kwa ndugai
 
Nahisi Ndugu Ndugai Bado anapwaya sana katika nafasi yake ya uspika, ni mwaka wa tatu sasa hatujaona hata meno ya Bunge kuiwajibisha serikali katika masuala nyeti na Muhimu,

Nakumbuka kipindi cha jamaa Kikwete Bunge limewajibisha serikali Mara kibao sana na nashangaa mpaka Leo tuna mengi ya kuhoji lakin Bunge linaiogopa serikali,

Kuna masuala nyeti sana lakin Bunge Lipo kimya,

Naona viatu vya Makonda vinampwaya ndugai,

Hata wakati wa mwalimu Nyerere ambaye tunaamini ndo alikuwa mkali na ndo alikuwa rais kweli, lakin Bunge lilihoji na kuisimamia serikali ipasavyo mpaka saa nyingine kuikataa miswada na Nyerere ku surrender

Kipindi hicho Adam Sapi Mkwawa akiwa spika bunge lake lilikataa muswada wa Rais na kuurudisha na Rais akabwaga manyanga. Tena siyo hawa marais wa kuja bali ni Rais anayeheshimiwa hata miaka 200 ijayo yaani Rais Julius Nyerere. Je, ilikuwaje? Ilikuwa hivi.

Mwaka 1969 Waziri wa Elimu, Solomon Eliufoo aliugua na ikaonekana anaweza asiendelee kuwepo serikalini. Serikali kwa ku-panic ikapeleka muswada bungeni unaohusiana na mafao au maslahi ya mawaziri hasa wanaougua.

Muswada huo ulileta mgawanyiko bungeni ukizingatia kwamba ni miaka miwili tu tangu siasa ya Ujamaa na Kujitegemea itangazwe pia miiko ya uongozi.

Bunge likaukataa muswada ule likamrudishia Rais Nyerere ili ikiibidi afanye lolote na kama ni kuurudisha tena basi na iwe ili hatimaye wavunje bunge na nchi irudi kwenye uchaguzi.

Rais Nyerere mwenyewe alipohojiwa na waandishi alinywea na kusema "the parliament had a point" yaani bunge lilikuwa na hoja na hakuthubutu kuupeleka tena bungeni.

Haya, niambieni ni bunge lipi tena lililowahi kufauluujasiri kama huu. Wote waliobaki na mnaowataja wafyata mkia watupu, tena kukiwa na hatauwezekano wa kuhama vyama.

Leo hii Viatu vya Makinda ni vikubwa mno kwa ndugai
tatizo viongoza wetu wanatamba na gpa za 32 walizopata sua ya dom

ben.big.boss
 
Back
Top Bottom